Bora Wachina wa Bandari ya Bagamoyo kuliko Waarabu wa DP World

Burkinabe

JF-Expert Member
Feb 12, 2023
1,893
3,200
Baada ya kudodosa dodosa mikataba ya makampuni ambayo yamejikita katika uwekezaji wa Bandari, nimeona na nimejiridhisha kabisa kwamba, masharti ya Wachina kwa Bandari ya Bagamoyo, yalikuwa nafuu kuliko hawa jamaa wa DP World.

Zifuatazo ni baadhi ya sababu zilizonifanya nifikie maamuzi haya:

1. Mkataba wa Wachina wa Bagamoyo ulikuwa na ukomo wa miaka 99, huu wa DP World hauna ukomo (ni wa milele na milele)

2. Wachina wa Bagamoyo hawakutaka kutupoka bandari zetu Tanzania Bara, hawa jamaa wa DP World wana "njaa kali" wanataka bandari zote za Tanzania bara (Tanganyika) isipokuwa Zanzibar. Tena DP World wanataka bandari hadi za kwenye mito na mabwawa, achilia mbali bahari na maziwa makuu tuliyo nayo.

3. Wachina wa Bagamoyo walitaka kuja kujenga na kuendeleza bandari ya Bagamoyo, hawa Waarabu wanakuja tu na tu-mitambo twao ambatwo hata hatuna uhakika kama wanatwo hutwo tu mitambo au la! Bandari ya Dar Es Salaam ni Bandari kongwe ambayo ipo tayari na serikali imekuwa ikitumia mabilioni ya fedha kuiboresha. Leo hii eti tu kwa sababu waarabu wana mitambo tuwapatie tena kwa masharti ya kijinga kijinga.

Zingine, wana jamvi mtaendelea kuziweka.

Asalaam Aleykum..
 
Mnahangaika
Ndiyo, tunahangaikia uhuru wetu kama nchi.
Hatutaki kurudishwa utumwani. Tena utumwa kwa waarabu waliokuwa wanawaasi mababu zetu kipindi kile cha utumwa.
Ngoja tuendelee kuhangaika.
 
Wachina walishika bandari huko Ugiriki na kuifanya kuwa moja ya bandari kubwa duniani. Kwanza China ni mzalishaji namba moja duniani, ni afadhali yeye ashike bandari. Dubai ni dalali tu wa bidhaa zinazozalishwa kwingine, hasa China. Tumeruka mkojo tumekanyaga......
 
Wachina walishika bandari huko Ugiriki na kuifanya kuwa moja ya bandari kubwa duniani. Kwanza China ni mzalishaji namba moja duniani, ni afadhali yeye ashike bandari. Dubai ni dalali tu wa bidhaa zinazozalishwa kwingine, hasa China. Tumeruka mkojo tumekanyaga......

Nenda kawalete Israel basi wachukue bandari,Taifa teule
 
Wachina walishika bandari huko Ugiriki na kuifanya kuwa moja ya bandari kubwa duniani. Kwanza China ni mzalishaji namba moja duniani, ni afadhali yeye ashike bandari. Dubai ni dalali tu wa bidhaa zinazozalishwa kwingine, hasa China. Tumeruka mkojo tumekanyaga......
Ukweli ni afadhali Wachina. Wao walitaka kujenga bandari mpya. Hawa wanatupokonya bandari yetu ambayo inafanya kazi, halafu sisi hatutapata chochote kutoka kwenye faida watakayotengeneza.
 
Hapo ukitazama kwa makini utaona wazi kabisa, kilichofanya waarabu wapewe hizo bandari milele ni sababu ya ujomba tu, hakuna akili yoyote ya maana iliyotumika kuwapa wale mafedhuli wenye kesi kila nchi walikowekeza bandari zetu.

Samia ni msaliti wa ardhi ya Tanganyika na watu wake.
 
Hapo ukitazama kwa makini utaona wazi kabisa, kilichofanya waarabu wapewe hizo bandari milele ni sababu ya ujomba tu, hakuna akili yoyote ya maana iliyotumika kuwapa wale mafedhuli wenye kesi kila nchi walikowekeza bandari zetu.

Samia ni msaliti wa ardhi ya Tanganyika na watu wake.
 

Attachments

  • 5394886-774acdfc87d3afa8f4140ab87cefff5c.mp4
    1.1 MB
Nafikiria kwa kuandika

Hivi bandari ya bagamoyo ndio basi tena? Na tukitaka kuendeleza lazima tumwambie DP?

Na ikiendelezwa ina bakia kuwa yake?

Maana mkataba una mpa haki ya bandari zote za bara kwa mujibu wa walio soma hiyo mikataba

Au swala la bandari ya Bagamoyo ndio imekufa kifo cha mende?

Vipi fidia ya lile shamba la bagamoyo tukawapa eneo tulilo tenga kuwa bandari kama fidia ndugu zetu wa damu (Zenjibar)

Nqjaribu kuwaza nikiwa kanisani
 
Nafikiria kwa kuandika

Hivi bandari ya bagamoyo ndio basi tena? Na tukitaka kuendeleza lazima tumwambie DP?

Na ikiendelezwa ina bakia kuwa yake?

Maana mkataba una mpa haki ya bandari zote za bara kwa mujibu wa walio soma hiyo mikataba

Au swala la bandari ya Bagamoyo ndio imekufa kifo cha mende?

Vipi fidia ya lile shamba la bagamoyo tukawapa eneo tulilo tenga kuwa bandari kama fidia ndugu zetu wa damu (Zenjibar)

Nqjaribu kuwaza nikiwa kanisani
Kuhusu hilo shamba la Wazanzibar, halihusiki kabisa na mapatano yetu na DP World.
Huenda ndiyo sababu Charles Hilary akatutahadharisha mapema, kana kwamba alijua tunakwenda kuuza na eneo lao!
 
Baada ya kudodosa dodosa mikataba ya makampuni ambayo yamejikita katika uwekezaji wa Bandari, nimeona na nimejiridhisha kabisa kwamba, masharti ya Wachina kwa Bandari ya Bagamoyo, yalikuwa nafuu kuliko hawa jamaa wa DP World.

Zifuatazo ni baadhi ya sababu zilizonifanya nifikie maamuzi haya:

1. Mkataba wa Wachina wa Bagamoyo ulikuwa na ukomo wa miaka 99, huu wa DP World hauna ukomo (ni wa milele na milele)

2. Wachina wa Bagamoyo hawakutaka kutupoka bandari zetu Tanzania Bara, hawa jamaa wa DP World wana "njaa kali" wanataka bandari zote za Tanzania bara (Tanganyika) isipokuwa Zanzibar. Tena DP World wanataka bandari hadi za kwenye mito na mabwawa, achilia mbali bahari na maziwa makuu tuliyo nayo.

3. Wachina wa Bagamoyo walitaka kuja kujenga na kuendeleza bandari ya Bagamoyo, hawa Waarabu wanakuja tu na tu-mitambo twao ambatwo hata hatuna uhakika kama wanatwo hutwo tu mitambo au la! Bandari ya Dar Es Salaam ni Bandari kongwe ambayo ipo tayari na serikali imekuwa ikitumia mabilioni ya fedha kuiboresha. Leo hii eti tu kwa sababu waarabu wana mitambo tuwapatie tena kwa masharti ya kijinga kijinga.

Zingine, wana jamvi mtaendelea kuziweka.

Asalaam Aleykum..
Asilimia kubwa ya wanaopinga mkataba (IGA) Hawapingi mkataba (IGA) wa bandari, kwakua ili kupinga mkataba, ni lazima uanze na sheria zitakazo ongoza mkataba kwanza, kabla ya yaliyomo, kwakua yaliyomo ni lazima yafuate sheria. Hii ni kama tu unataka kupinga kwa nia njema ya taifa. Usipofanya hivyo nisawa na kuchukua maneno, na mistari miwili kwenye vitabu vitakatifu ili iendane na haja zako. Waingereza wanaita hali kama hiyo “ulterior motives”

Kuna msukumo mkubwa kwa wanaopinga lengo Lao kuu ni wanapinga Jamhuri ya Muungano ya Tanzania 🇹🇿 kuwa HURU kimapato kwa mara ya kwanza. Usione ajabu, Kaskazini wanakua na mtazamo tofauti wa mambo na sio dhambi. Hata Mangi Mkuu Mangi Marialle alipingana na Mwl kuhusu Tz kupata uhuru 09 Dec 1961, aliona muda haijafika kwanza, hatuna uwezo wa kujiongoza Bado.

Lakini Uhuru uliletwa na TANU, ambayo leo inaitwa CCM, baada ya kuugana na Afro Shirazi (ambacho likua na wapini Znz) 1977, na Kila mtu amefaidika kutokana na hilo.

unaweza kuiangalia South Africa 🇿🇦 Kijuju ukadhania bora tungechelewa kidogo kupata uhuru kama ulivyokua mtazamo wa Mangi Mkuu Mangi Marialle, japo alikua hapatani na mmoja wa mangi wadogo, mangi Shangali.
Laking Uhuru ni sasa, alisisitiza Mwl, na njia aliyofanikisha kutupitisha ndio tunaendelea nayo Leo.

Hili Jambo ni kubwa kiasi kwamba haliwezi kuwa na mkataba (IGA) mmoja wenye kurasa 38 tu, lazima iwepo mengine, pia ya kupenda na na makubaliano kati ya Tanzania 🇹🇿 na Dubai. Kuku, mbuzi, nguruwe, ngombe, ni nyama, kama vile IGA, HGA, na PA(s) yote ni mikataba, lakini nyama zote ziko Sawa? Mikataba yote iko Sawa?
Watu wanajua tofauti Za nyama, ila kutokana na shughuli zao Za Kila siku sio wote wanajua tofauti ya tofauti ya IGA, HGA, na PA(s).
Kutokua kwao usikutumie kwa faida yako kama wewe ni kiongozi wa kweli.

ukiiangalia kipengele cha 21, kipengele pekee pekee kinachoelezea sheria zitakazo ongoza mkataba, kwakua yaliyomo yote lazima yaendane na sheria.

Kimsingi tafsiri ya mkataba ni makubaliano yanayoweza kulazimishwa na sheria.

Sheria gani sasa zinaweza kulazimisha hayo makubaliano?

Jibu liko kipengele cha 21, kwamba IGA itafuata sheria Za uingereza ambazo tunazifuata tayari, zinafanana na Sheria zetu, kwakua tumezirithi kutoka serikali iliyokuwepo kabla ya 09 Dec 1961. Kipengele cha 21 pia kinasema HGA na makubaliano ya mradi yatafuata sheria Za Jamhuri ya muungano ya Tanzania. Na sheria Za Tanzania tunaweza kuzibadilisha tunavyotaka bila na mkataba (IGA) inatambua hilo, na kukiri hilo. Hii inakua muhimu kwenye mapato. Ndio maana mapato hayamo kwenye IGA, yatakuwepo kwenye HGA ili yafuate sheria Za Tanzania, na hapo ndipo Prof Mbarawa, wanalinda maslahi, ya wa Tanzania, kwamba mapato yangekuwepo kwenye IGA, tusingekua na control nayo. Badala ya kufurahia hilo wanaliruka, hakuna anayepinga anaweza kukataa ukweli huu.
 
Baada ya kudodosa dodosa mikataba ya makampuni ambayo yamejikita katika uwekezaji wa Bandari, nimeona na nimejiridhisha kabisa kwamba, masharti ya Wachina kwa Bandari ya Bagamoyo, yalikuwa nafuu kuliko hawa jamaa wa DP World.

Zifuatazo ni baadhi ya sababu zilizonifanya nifikie maamuzi haya:

1. Mkataba wa Wachina wa Bagamoyo ulikuwa na ukomo wa miaka 99, huu wa DP World hauna ukomo (ni wa milele na milele)

2. Wachina wa Bagamoyo hawakutaka kutupoka bandari zetu Tanzania Bara, hawa jamaa wa DP World wana "njaa kali" wanataka bandari zote za Tanzania bara (Tanganyika) isipokuwa Zanzibar. Tena DP World wanataka bandari hadi za kwenye mito na mabwawa, achilia mbali bahari na maziwa makuu tuliyo nayo.

3. Wachina wa Bagamoyo walitaka kuja kujenga na kuendeleza bandari ya Bagamoyo, hawa Waarabu wanakuja tu na tu-mitambo twao ambatwo hata hatuna uhakika kama wanatwo hutwo tu mitambo au la! Bandari ya Dar Es Salaam ni Bandari kongwe ambayo ipo tayari na serikali imekuwa ikitumia mabilioni ya fedha kuiboresha. Leo hii eti tu kwa sababu waarabu wana mitambo tuwapatie tena kwa masharti ya kijinga kijinga.

Zingine, wana jamvi mtaendelea kuziweka.

Asalaam Aleykum..
mara mia wachina na Oman walikuwa na faida sana na walikuwa washindani wakubwa wa dp world, sasa dp world watafanya kazi bila kuwa na mshindani yeyote na kwa muda usiojulikana.
 
Marekani alijitolea kuwa mshauri asiyelipwa kwa serikali ya Tanzania kwenye maswala ya bandari.

Hadi hapo China akawa keshapigwa teke.

Uwepo wa DP world maana yake China hawezi wekeza Bagamoyo
 
Back
Top Bottom