ya Lissu imeanza lakini upande wa mashataka, wanasheria wanaiomba Mahakama ihairishe kwa sababu shahidi wao amepata dharura. Wanaomba Jumatatu wataleta mashahidi wao wote.
Lissu amesimama na kupinga hoja hiyo.
Lissu: "Kulikua na amri mliyoitoa mwaka jana siwezi kukumbuka tarehe, kwamba upande wa mashitaka ulete mashahdi wawili kila kesi inaposikilizwa, na hii amri mmeirudia tena juzi jumatano mmeirudia jana, kwamba upande wa mashitaka walete mashahidi wengi.
Lissu: Sasa waheshimiwa Majaji upande wa Mashitaka hautekelezi amri za Mahakama kwa sababu hamuwachukulii hatua, wanajua mtawakubalia. Lissu: Waheshimiwa majaji kusema maneno haya sio kitu chepesi kwangu ila mmeachia amri zenu kupuuzwa.
Lissu: Sasa kwa vile mlisema jana na hawajaleta mashahidi naomba msikubali Mahakama kuu ya Tanzania ikageuzwa kama ile iliyomuhukumu Jomo Kenyatta, ikiwakubalia waleta mashitaka kila kitu na kuukatalia upande wa utetezi kila kitu.
Lissu: Kwanini hawapo tayari kuheshimu amri ya Mahakama. Kama pumzi imekata wafunge ushahidi twende hatua inayofuata. Kama hawako tayari kuendelea wafunge kesi. Msikubali kugeuzwa kama hiyo mahakama niliyoisema.
Lissu: Again for the record (kwa kumbukumbu) hii ndio kesi kubwa zaidi kwa Jamuhuri ya Muungano kwa mujibu wa Katiba, lazima Mahakama ioneshe umuhimu kwa namna inavyosimamia amri zake na maamuzi inayofanya. Hatutembelei njia ambayo haijafagiliwa, kesi ya uhaini ya kwanza ilichukua miezi sita na siku 17 miaka ya 1970. Na ikasafishwa tena miaka ya 1982 na 1983 kesi ilichukua mwaka mmoja na siku 17 chumba hiki hiki.
Lissu: Leo ni siku ya 495, mwaka mmoja na zaidi ya miezi minne hatujamaliza mashahidi wa upande wa mashitaka nikija kusema aitwe Samia si itachukua miaka mitano, na Philip Mpango na IGP Wambura mtakuwa mmestaafu hawajaitwa. Naomba msiwakubalie walete mashahidi tuendelee na kesi.
Mshirikishe mwenzako, "Nikija kusema aitwe Samia si itachukua miaka mitano?" - Lissu