Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,608
- 860,789
- Thread starter
- #821
UPDATES KUTOKA MAHAKAMA KUU DAR ES SALAAM.
Leo Tarehe 20/07/2026 Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es salaam. Kesi Na. 7300/2026 iliyofunguliwa na Mawakili watatu, Paul Kisabo, Nashon Nkungu na Maduhu William baada ya kukumbana na vikwazo wakati wanaenda kumtembelea Mh. Tundu Lissu.
Vikwazo hivyo ni ikiwemo mazungumzo yao kuwa yanasikilizwa na magereza.
Kesi hii imefunguliwa mwezi March, 2026 dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kamishna Mkuu wa Magereza na Mkuu wa Gereza la Ukonga.
Mh. Tundu Lissu ni sehemu ya wajibu maombi kwenye hii kesi ambapo yeye ni mjibu maombi wa nne katika maombi haya.
Baada ya pande zote kubadilishana nyaraka. Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kiliomba kuunganishwa kwenye kesi hii kama interested party kwasababu waliofungua maombi haya ni wanachama wa TLS. Mahakama iliwakubalia.
Mara baada ya wajibu maombi kuwasilisha kiapo kinzani. Mheshimiwa Lissu aliomba kuwauliza maswali ya Dodoso mawakili waliofungua kesi pamoja na Mkuu wa Gereza la Ukonga.
Mahakama ilimkubalia ombi hilo na leo linaanza zoezi la kuulizwa maswali ya Dodoso kwa Mkuu wa Gereza la Ukonga anaitwa Andrew Shabani Ntamamiro.
Hapa maswali kwa Mkuu wa Gereza la Ukonga tutegemee ataulizwa maswali ya namna anavyotekeleza majukumu yake ikiwemo utaratibu wa mawakili kuingia na kutoka magerezaa na namna ya kuzungumza na wateja wao.
Tutapata nafasi ya kujua kama Wakuu wa Magereza nchini wanajua wajibu wao au hawajui? Wanajua sheria au hawajui sheria. Je nao akili zao zinafanana na maafisa wa jeshi la Polisi katika usimamizi wa sheria.
Muda huu saa tano na dakika 40 maombi haya yataanza kusikilizwa kwa mjibu maombi kuanza kuulizwa hayo maswali ya Dodoso.
Leo Tarehe 20/07/2026 Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es salaam. Kesi Na. 7300/2026 iliyofunguliwa na Mawakili watatu, Paul Kisabo, Nashon Nkungu na Maduhu William baada ya kukumbana na vikwazo wakati wanaenda kumtembelea Mh. Tundu Lissu.
Vikwazo hivyo ni ikiwemo mazungumzo yao kuwa yanasikilizwa na magereza.
Kesi hii imefunguliwa mwezi March, 2026 dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kamishna Mkuu wa Magereza na Mkuu wa Gereza la Ukonga.
Mh. Tundu Lissu ni sehemu ya wajibu maombi kwenye hii kesi ambapo yeye ni mjibu maombi wa nne katika maombi haya.
Baada ya pande zote kubadilishana nyaraka. Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kiliomba kuunganishwa kwenye kesi hii kama interested party kwasababu waliofungua maombi haya ni wanachama wa TLS. Mahakama iliwakubalia.
Mara baada ya wajibu maombi kuwasilisha kiapo kinzani. Mheshimiwa Lissu aliomba kuwauliza maswali ya Dodoso mawakili waliofungua kesi pamoja na Mkuu wa Gereza la Ukonga.
Mahakama ilimkubalia ombi hilo na leo linaanza zoezi la kuulizwa maswali ya Dodoso kwa Mkuu wa Gereza la Ukonga anaitwa Andrew Shabani Ntamamiro.
Hapa maswali kwa Mkuu wa Gereza la Ukonga tutegemee ataulizwa maswali ya namna anavyotekeleza majukumu yake ikiwemo utaratibu wa mawakili kuingia na kutoka magerezaa na namna ya kuzungumza na wateja wao.
Tutapata nafasi ya kujua kama Wakuu wa Magereza nchini wanajua wajibu wao au hawajui? Wanajua sheria au hawajui sheria. Je nao akili zao zinafanana na maafisa wa jeshi la Polisi katika usimamizi wa sheria.
Muda huu saa tano na dakika 40 maombi haya yataanza kusikilizwa kwa mjibu maombi kuanza kuulizwa hayo maswali ya Dodoso.