Tulionusurika kufa maji tukutane hapa

Tulionusurika kufa maji tukutane hapa

Aisee, mwaka fulani nikiwa form 1 nilitaka kuagana na ugali kimasihara hivi.
Ilikuwa boarding skul, jioni tulikuwa na kawaida ya kwenda kuogelea ziwa Victoria..Nakumbuka hiyo siku ziwani kulikuwa kumechafuka sana, maji ya jirani tulipokuwa twaogelea hayakutamanika kwa uchafu, hivyo tukaamua kusonga mbele zaidi ili tupate maji masafi, sikuwa mzuri sana katika kuogelea hivyo nikawa natumia dumu ya litre 5 kupata support (boya) nimefika umbali mrefu nikajaribu kupima kina cha maji, aisee nilihisi kama maji yananinyonga vile, kina kilikuwa kirefu nikakosa pumzi nikipiga yowe nakunywa vikombe vya kutosha, nikakata tamaa ya kuokoka, giza likatanda, nikaanza kujutia dhambi zangu, nikamkumbuka mamangu nyumbani, ndgu zangu, nikaikumbuka hadi ile siku naletwa shule kuripoti machozi yakanitoka nakufa kizembe[emoji22].

Kumbe katika purukushani zile wanafunzi wenzangu waliokuwa nchi kavu waliniona wakawa wanaduwaa hawajui wafanye nini, kuna sister mmoja (alikuwa form 2 alikuwa fundi wa kuogelea) kajitosa kuja kuniokoa....Kafanikiwa kuniokoa ingawa kwa mbinde maana kila alikuwa akijaribu kunipa mkono nimshike naambulia vikombe, ikabidi anyooshe mguu wake nikafanikiwa kuudaka, kafanya machachari yake mara niko mgongoni kwake[emoji120][emoji120][emoji120]

JACQUELINE popote ulipo Mwenyezi Mungu akujalie kila lililo jema. Bila roho mtakatifu kukuongoza giza lingetanda siku hiyo hiyo..
Mkuu ww ulikuwa ushakufa na sijui kama ulikumbuka kutoa sadaka! Duuh! Visa vya maji noma sana aisee
 
Humu kuna watu inabd watuamkie kila uchao, 2011 ulikuwa fomu siks!!?
Ni kweli mkuu inawezekana Ni mdogo lakini +8 years ahead , sasa naweza kukaa na wazee tukashauriana..
Pia inawezekana nilikuwa form six na umri mkubwa.
 
Kuna siku naogolea coco kumbe Sasa jioni maji Yana kuja na yanarudi yakanipeleka mbali bila kujua nakuja kushtuka Niko mbali Seema uzuri palikuwa na watu wengi ilibidi nimshike braza mwenye tairi..WANAWAKE wanapelekwa mbali halafu wanabakwa utafanyaje jamaa anataka kukuacha anakwambia mpe kidogo akuokoe??[emoji1787]
Kwa hiyo na wewe ulimpa kidogo!!
 
Nikiwa Olevel tulifukuzwa ada tukaenda kudiba mtoni, sasa kuna msela angu alikua ajui kuogelea kimasiara masiara watu wakamtosa kina kirefu mara kikombe cha kwanza mara chapili, mi nkajitia ufundi nkamuokoe jamaa alikua mbavu alinipiga roba anapanda mwilin mwangu awe juu apumue mi niwe chini, kila nkitoa wap piga ngumi wap, mpaka nkapanic, thank to God nkapata akili ya kuzama chini ndo kuniachia nkapita chin kwa chini nkatoka njee tukamrushia mgomba ndo kumvuta nao......! nkuanzia siku iyo ukitaka ugonvi naewe zungumizia mambo ya kuogea


Hhahahaa nimecheka had kulia .dah jaman..maisha haya
 
Nilipia msukosuko wa maji ambapo sitakuja kusahau ila baada ya apo nikaambiwa ushajua kuogelea
Na kwel nachezea maji kama kambale[emoji2][emoji2] [emoji2]
 
Nilishuhudia Mara tatu pale raskazone tanga kuna mshikaji yeye anawafundisha kuogelea anawapeleka mbali then anaomba abatizwe Maji mengi Demu akikataaaaa jamaa anatishia kumwachia aisee.demu anaamua ambatize tuu mshkaji...na alisema yeye akitaka papuch anashuka beach
Vipi khs maradhi? Yeye haogopi?
 
Maji yalimuua rafiki yangu Tomas tukiwa f1 huku tukiwa tupo pembeni hii kitu wakati mwingine haina ujuzi..

Tulikuwa tunavua kwa kutumia ndoano ziwani, mshkaji akasema aogelee aamie jiwe jingine kama mita 5 tu kutoka jiwe tulilokuwepo mwanzo na alikuwa mjuzi mzuri tu wa kuogelea.

Kaingia tu majini kumbe pale chini kuna tope zote akanasa ile sisi tunafikiria anaogelea chinichini kwenda upande mwingine maana tulikuwa tunaona kama mtikisiko wa maji chini...

Kumbe ndo safari iliwadia.. kwenye maji dkk 3 ni nyingi sana ukizama. RIP
 
Hii imewahi kunikuta..Nilikuwa sijui vizuri kuogelea..Uogeleaji wangu ilikuwa siangalii ninapokwenda..Kichwa kipo ndani ya maji macho nimefumba..Nikaanza kwenda wrong direction naelekea kwenye kina kirefu bila kujijua..

Imefika stage nataka nisimame miguu haifiki chini then naanza kuzama..Nilidata..Nikianza kupiga mbizi kwa kasi huku sijui naelekea wapi..Hapo nishapanic..Mungu alikuwa upande wangu,nilikuwa naelekea kwenye kina kifupi..

Baada ya kuchoka kabisa na kuona siwezi tena kuendelea nikaamua nisimamame..Nikagusa chini..Maji yapo kifuani..Nilitembea hadi nje nikabeba nguo zangu na kusepa bila kuaga washkaji...

Hii siku siji kuisahau kamwe..

exactly this happened to me UDSM pool. aisee it was terrible experience. mwaka huu lazima nijue kuogelea, kufa maji kubaya
 
pole, what happened ?
hahaha asante,
ilikuwa coco beach 2011 wakati huo maji yalikuwa yamejaa sasa pale coco maji yakijaa mpaka kule kwenye ile mimawe mikubwa (rocks) kote maji yanakuwa full pia.
sasa watu wanajirusha kutokea juu ya yale mawe wanazama baharini hapo ndo tamaa iliponiingia, kumbuka sijui kuogelea hapo (yani sina uwezo kukaa kwenye kina kirefu) sasa ile najitupa kutokea juu ya mawe nikazama mpaka baharini baada ya kuona haya maji si size yangu nikapanic niwahi kutoka nje hapo ndo picha linaanza sasa.
ndo maana nikasema siku zangu zilikuwa bado, baada ya kutapatapa kupiga mbizi nikachoka na pale pale nika give up tena nilishahadia kabisa nikasema kwaheri ya kuonana hiyo.
bahati nzuri sasa, nikayaona yale mawe makubwa ambayo juu yake watu ndo wanaruka kuingia kwenye maji nikayafata ikawa kama boya langu nikaenda nalo kwa kulishika mpaka namefika ufukweni.
niliponea hivyo, ila nilipiga lita kadhaa ya maji ya chumvi acha mdomo upasuke.
 
nimenusurika kufa na maji twice ni dhairi siku zangu zilikuwa bado hazijafika, sifa za kijinga zilitaka kuniua.
Uliposema sifa za kijinga umenikumbusha kisa kimoja jamaa yangu nae alitaka kufa kisa sifa za kijinga..

Tulikuwa hotel kuna swimming pool sasa jamaa yangu alikuwa yuko pembeni akituangalia sisi tukipiga michomo, pembeni yake wako mabinti kumbe wale madada walikuwa wanzungumzia kuhusu sisi tunavyopiga michomo na kuogelea kwa madaha!! Sasa alivyo mwendawazimu na kutaka sifa nae akavua kofia, akaweka simu na vitu vingine pembeni bila kujua kina cha maji kurupu akaiingia majini kuja kutahamaki mtu anenda juu anarudi chini, mie nikajua huyu mjomba maji hayawezi, nikajitoma kwenye maji kumpa msaada kufika lilivyojinga likanikumbatia, nikaona nikijikaza kufosi nimtoe kwa nguvu ataning'ang'ania na tutakufa wote, mie nikajilegeza tukazama woote mpaka chini likaniachia, ikabidi mie nije juu nikawa nampush taratibu kuelekea maji ya kina kifupi ambayo haikuwa mbali, mpaka nikamtoa maji marefu.
Kichekesho baada ya kumuokoa eti anajidai mkono wake unamsumbua alipata ajali kwao shinyanga huko so kuna wakat mkono unamgomea kuogelea..
Tukacheka akaendela na kazi yake ya ulinzi wa mizigo yetu..

Kupenda sifa kubaya saana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom