Tulionusurika kufa maji tukutane hapa

Tulionusurika kufa maji tukutane hapa

Nikiwa Olevel tulifukuzwa ada tukaenda kudiba mtoni, sasa kuna msela angu alikua ajui kuogelea kimasiara masiara watu wakamtosa kina kirefu mara kikombe cha kwanza mara chapili, mi nkajitia ufundi nkamuokoe jamaa alikua mbavu alinipiga roba anapanda mwilin mwangu awe juu apumue mi niwe chini, kila nkitoa wap piga ngumi wap, mpaka nkapanic, thank to God nkapata akili ya kuzama chini ndo kuniachia nkapita chin kwa chini nkatoka njee tukamrushia mgomba ndo kumvuta nao......! nkuanzia siku iyo ukitaka ugonvi naewe zungumizia mambo ya kuogea
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119]
 
Namsubiri yule jamaa aliepona mv iliyozama juzijuzi.
 
Nilinusurika Mto Ruaha siku hiyo, hua natafakari sana lile tukio, nakumbuka pia ndo siku ambayo mtoto mmoja alibebwa na maji mpaka kwenye shimo kubwa lililochimbwa Kwa ajili ya kufyatulia tofali akafia humo
 
Aiseee... nimeponea scenario 2. Sitakaa nisahau.
Sisi wachagga mito yetu ilivyo na mawe kuogolea wapi na wapi kwamfano?

1. Enzi hizo tukienda moshi likizo bwana kila actuvity hutaki kumiss. Kuna vibarua walikua wanaenda shamba Ibukoni huko. Sina hata kilo za nyama enzi hizo kadogo tu. Bibi alibikataza sana kwani naelewa. Nataka nikale maembe huko mwai. Wooi, tukaenda na binamu yangu haooo tukafika shamba. Miye nahangaika tu huku na huku. Binam yangu alikua na mdogo wake pia mdogooo tena kunizidi. Binamu alikua mkubwa na ana mwili. Muda wa kurudi ukafika. Uuwuuii, mvua iliyokuja utasema huko mbinguni malaika wa zamu alibet mkeka ukachanika. Barabara zote zimejaa maji. Kumbuka hiyo ni kupanda. Nikawa naona kizunguzungu. Tukafika mahali kuna mfereji unaenda kuunganisha na bonde ni kama mto hivi linapeleka maji kenya. Mdogp wake binamu akavuka kwanza, huyoo akachukuliwaa, nikawa nayadharau yale maji. Na mimi nikavukaa. Weeee, nikajikuta hata kusema maa siwezi napambana kujiokoa. Aisee yule binam yangu kwa hofu alirukia kwenye maji akaanza nitoa mimi, then later akamtoa mdogo wake. Yaan angechelewa tukafija kwenye lile bonde ndo basi wangesubiria miili yetu kenya iletwe tena tz kutuzika.

2. Hii nilienda marangu mtoni kwa mamdogo wangu ameolewa huko. Ule mto na kwake pamepakana. Hata maji enzi hizo wanachota huko kuna mifereji ndo huchota maji yake. Siku moja wakawa wanaenda kuogelea. Watu woote wanaogelea. Mimi peke yangu ndo nimebaki kwenye jiwe nawaangalia wanavyodive. Hapo pia kadogo kweli. Nikasema jaman si na mimi naweza? Wooiii si na mimi nikajidumbukiza1[emoji23][emoji23][emoji23] nilikunywa maji apaaaa womii[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] sasa kuna binamu akiwa yuko ndani ya maji akahisi kama ameshika mtu maana miye hapo nasubiria kukata roho tuu[emoji23][emoji23] ila akawa anasita asije akamtoa nguva bure ila akajikaza kisabuni akasema liwalo na liwe, akaninyakua paaaap, kufika nje ya maji si huyu hapa fulani mungu wangu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] msaada wa chap chap. Since then sitaki tabia mbaya na maji. Yaan hata uniue. Lama ni kuogelea natbeaga tu kwenye yale maji mafupu ya wet en world ama popote mahi mafupi
 
Nakumbuka niko Advance Tanga.... Friends zangu wapenda maji kama samaki, sisi most of week end days tunatoroka shule kwenda kuogelea, tukiwa na ela tunaenda Raskazone tukifulia tunaingia deepsea.......!

Ilikua kawaida tukiwa Raskazone tunaogealea mpaka meli zilipotia nanga, pana umbali kidogo sasa siku moja tunatoka kwenye nanga turud nchi kavu misuli ikakaza, kila nikistrech wap, dooohhh nilitoa macho nkaomba Mungu aniepushe na kifo cha maji ila kwaushirikiano ya washkaji na mabaharie wengine nilirud salama......!

Kuanzia siku iyo nkawa nikitakakupiga zoez la kuogelea nnaenda parallel na bahari....
Hahaha ni epamiss tangaaa, ila yale mawe ya raskazoni yanakata miguu hapana aisee[emoji23][emoji23]
 
  • Thanks
Reactions: Oxx
Pole sana Mkuu ila nimecheka sana 😂😂😂

Duuh huu Uzi umenikumbusha mbali Sana

Ilikuwa mwaka 2011 nikiwa form six huko mwanga Kilimanjaro ,alikuja dada mzungu jirani na shule basi nikaja kumshobokea na viinglish vyangu vya broken.

Mtoto akaja kukolea akawa anakuja school asiponiona analia basi masela wananisaka Kila chimbo kwamba mzungu wako analia huko.

Basi siku moja kaja na wazungu wenzake Kama watatu wakasema tukaogelee, nikawabeba washkaji zangu Kama kumi ivi..

Kufika bwawa lenyewe la umwagiliaji limejengwa kwa sakafu,basi watu wakapunguza nguo wakaanza kuruka kwenye maji ,kiukweli mi sijui kuogelea nkabaki mwenyewe nje nawashangaa Mara wakaanza come on men sio parefu
Nkaona itakuwa aibu niende na watasha alafu wajue sijui kupiga mbizi Mara nkapunguza nguo nkasogea nyuma umbali wa Kama mita kumi nkakimbia nkajitosa kwenye bwawa bwaaaaa
Watu ohhh oyeeee hiooo ....Mara naibuka nazama ,naibuka nazama nikaona ndo mwisho tayari sasa

Ikafika hatua sasa nikiibuka kidogo nanyoosha mikono kuomba msaada tatizo sasa wenzangu wakajua ni manjojo daah nlikunywa maji machafu Kama Lita tano ivi nahisi

Basi akaja malaika wa mungu ,jamaa mmoja akatambua nimezidiwa akaja akaniokoa daaah

Niliumwa U.T.I Kama mwezi mzima ivi
"Ukitaka kujua maji sio uhai we Zama tu utapata mrejesho"

Kwa sasa ata maji ya beseni tu nayaogopa ..
 
Duuh huu Uzi umenikumbusha mbali Sana

Ilikuwa mwaka 2011 nikiwa form six huko mwanga Kilimanjaro ,alikuja dada mzungu jirani na shule basi nikaja kumshobokea na viinglish vyangu vya broken.

Mtoto akaja kukolea akawa anakuja school asiponiona analia basi masela wananisaka Kila chimbo kwamba mzungu wako analia huko.

Basi siku moja kaja na wazungu wenzake Kama watatu wakasema tukaogelee, nikawabeba washkaji zangu Kama kumi ivi..

Kufika bwawa lenyewe la umwagiliaji limejengwa kwa sakafu,basi watu wakapunguza nguo wakaanza kuruka kwenye maji ,kiukweli mi sijui kuogelea nkabaki mwenyewe nje nawashangaa Mara wakaanza come on men sio parefu
Nkaona itakuwa aibu niende na watasha alafu wajue sijui kupiga mbizi Mara nkapunguza nguo nkasogea nyuma umbali wa Kama mita kumi nkakimbia nkajitosa kwenye bwawa bwaaaaa
Watu ohhh oyeeee hiooo ....Mara naibuka nazama ,naibuka nazama nikaona ndo mwisho tayari sasa

Ikafika hatua sasa nikiibuka kidogo nanyoosha mikono kuomba msaada tatizo sasa wenzangu wakajua ni manjojo daah nlikunywa maji machafu Kama Lita tano ivi nahisi

Basi akaja malaika wa mungu ,jamaa mmoja akatambua nimezidiwa akaja akaniokoa daaah

Niliumwa U.T.I Kama mwezi mzima ivi
"Ukitaka kujua maji sio uhai we Zama tu utapata mrejesho"

Kwa sasa ata maji ya beseni tu nayaogopa ..
Hahahahhahahahah!!! Kweli kwa hali hiyo maji si uhai aisee!
 
Nikiwa Olevel tulifukuzwa ada tukaenda kudiba mtoni, sasa kuna msela angu alikua ajui kuogelea kimasiara masiara watu wakamtosa kina kirefu mara kikombe cha kwanza mara chapili, mi nkajitia ufundi nkamuokoe jamaa alikua mbavu alinipiga roba anapanda mwilin mwangu awe juu apumue mi niwe chini, kila nkitoa wap piga ngumi wap, mpaka nkapanic, thank to God nkapata akili ya kuzama chini ndo kuniachia nkapita chin kwa chini nkatoka njee tukamrushia mgomba ndo kumvuta nao......! nkuanzia siku iyo ukitaka ugonvi naewe zungumizia mambo ya kuogea
Hahahahah
 
hahahaaha huu uzi..... nimecheka sana aisee... hasa huyo mkuu alieleta mbwembwe kwenye bwawa la umwagiliaji. . eti wanajua ni mbinu tu za kuogelea anavorusha rusha mikono juu...
 
Mkuu ushawah kuogelea pale kigogoni kwny daraja la ruaha?
Nilinusurika Mto Ruaha siku hiyo, hua natafakari sana lile tukio, nakumbuka pia ndo siku ambayo mtoto mmoja alibebwa na maji mpaka kwenye shimo kubwa lililochimbwa Kwa ajili ya kufyatulia tofali akafia humo
 
Hahaha ni epamiss tangaaa, ila yale mawe ya raskazoni yanakata miguu hapana aisee[emoji23][emoji23]
Tanga raha....... Kama umeshika jembe maeneo ya Ibukoni yale mawe ni smooth kabisa[emoji16][emoji16] (jokes).

Ulikua KO au St C.?
 
Tanga raha....... Kama umeshika jembe maeneo ya Ibukoni yale mawe ni smooth kabisa[emoji16][emoji16] (jokes).

Ulikua KO au St C.?
Hahaha

Ko mzee baba. Kohogweeee
Shule yetu nzuri ya korogweee... kule st. C mashost kama wote tuition cilos enzi hizo.
Niligoma kbs kutoka government. Nilionja raha maisha yalivyokua huru[emoji23][emoji23] na vile nikawa waziri wa menu kwa ubabe wangu baasii sikua na tatizo la chakula. Mawe hayafai ya raskazone aisee. Hayafai hata kidogooo
 
  • Thanks
Reactions: Oxx
Hiyo kipindi niko forn one makoko
Sem. Sijajua kuogelea fresh nikaingia kwenye maji nafuata jiwe flani hivi ambalo tulikua tunatumia kusimama halafu lipo kwenye kina kirefu kidogo,
Nikakosea target kuweka miguu chini haifiki,sijakaa vizuri naibuka juu na wimbi linapita,nikazama chini kurudi juu wimbi hiloo.Nikaona hapa kuna kufa halafu washkaji wako mbali wana mishe zao.Ikabidi nizamie,nilipotoka nimeshapiga na vikombe kadhaa,sikumuongelesha mtu yoyote ni kuchukua nguo zangu na kusepa,halafu nikapitisha week nzima bila kukanyaga ziwani.Mpaka leo mimi na kuogelea hata sitaki kusikia.👀👀
 
Kuna siku naogolea coco kumbe Sasa jioni maji Yana kuja na yanarudi yakanipeleka mbali bila kujua nakuja kushtuka Niko mbali Seema uzuri palikuwa na watu wengi ilibidi nimshike braza mwenye tairi..WANAWAKE wanapelekwa mbali halafu wanabakwa utafanyaje jamaa anataka kukuacha anakwambia mpe kidogo akuokoe??[emoji1787]
du, na madada wanatoa kwenye maji kimya kimya nahisi akirudi wala hawaambii mashoga zake
 
Hahaha

Ko mzee baba. Kohogweeee
Shule yetu nzuri ya korogweee... kule st. C mashost kama wote tuition cilos enzi hizo.
Niligoma kbs kutoka government. Nilionja raha maisha yalivyokua huru[emoji23][emoji23] na vile nikawa waziri wa menu kwa ubabe wangu baasii sikua na tatizo la chakula. Mawe hayafai ya raskazone aisee. Hayafai hata kidogooo
naona umeongea tofauti na mada, mambo ya menu tena
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] tatizo hatupendagi kusema hatuwezi kuogelea, na maji hayajaribiwi lazima yakuumbue tu
Nyagi ndio ilikusababisha upaniki, ukiingia kwenye maji hakikisha upo ok na nati hazijalegea kila sehemu ziwe zimekaza, maji ninayoyaheshimu mie ni ya mtoni aisee, yale hayana utaalamu, ile speed yake, lakini ziwani na baharini, tunafukuzana na samaki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom