Nakumbuka 2016 July , nikiwa naogelea pale kipepeo beach. Nikiwa deep nilimwona jamaa mmoja kaja na Mke wake jamaa akakaa ktk vile viti vya karibu na mwanzo wa maji, ilikuwa ni msimu wa mawimbimbi makubwa. Yule mke wake ni wa umri kidogo, nikamwona anaingia kwenye maji
Kama bahati tu yule mama alifika maji ya kina cha kifuani kwake Mimi nikawa namwangalia bila sababu yoyote, Mara akaingia ndani ya maji. Nikawa najaribu kuangalia ili nione uzoefu wake,cha ajabu sioni akiibuka Juu, Kama dk 1 nzima hivi. Kwa sababu Mimi najua ni vigumu mtu kukaa ndani ya maji kwa dk 1 Kama siyo mzoefu, nikawa na Mashaka, nikapiga kelele kumstua Yule jamaa yake jamaa hasikii, na Mimi nilikuwa mbali kidogo deep sea. Ikabidi niyakate maji kwa kasi sana.
Nikafika pale alipozama namuita jamaa yake ndiyo anastuka. Alikuwa anachat. Nikazama ndani nikamuibua. Cha ajabu hapa alipozama ni maji ya kifuani tu. Nikamtoa alikuwa keshazimia. Nikamlaza ufukweni na jamaa yake sasa akawa anasaidia nikampamp kuifuani aka rushwa maji mdomoni Kama bomba la dawasco limepasuka. Akazinduka. Jamaa alinishukuru sana, alinipa Laki 3, Nilikataa zile pesa lakini jamaa alinisisitiza sana, nikachukua. Nilimwokolea mke wake. Kumbe Yule mama tangu azaliwe hajawahi kuongelea, ilikuwa Mara ya kwanza kwake.
Angalizo.
Maji Kama hujui kuogelea ni hatari sana, yanaweza kukua ndani ya dk 3 tu