GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,542
- 108,877
"Ninachojua tu ni kwamba Rafiki yangu Haji Manara ni Mwanachama Hai wa Simba SC na anaipenda Klabu ya Simba kuliko Kitu kingine chochote isipokuwa ujio wake huku Kwetu Yanga SC ni kutokana tu Hasira pamoja na kutafuta Ridhiki ila nina uhakika Siku isiyo na Jina Hasira zake zikiisha au Yanga SC Pesa zikiisha atarejea Simba SC ambako anakupenda zaidi" amesema Mkuu wa Wilaya ya Ikungi na mwana Yanga SC 'Kindakindaki' na aliyewahi pia kuwa Msemaji wa Yanga SC Jerry Cornelius Muro.
Nami GENTAMYCINE natamani sana tu Siku moja Wachezaji 'Wazawa' wa Simba SC akina Mkude, Boko, Manula, Kapombe na Kocha Msaidizi wa Simba SC Matola watoke hadharani waseme jinsi gani Msemaji wa sasa wa Yanga SC Haji Manara ambavyo huwa anawapigia Simu 'Kuwashutumu' hasa pale Simba SC inapofungwa kama Manara 'alivyokasirika' mno tu ile Siku Simba SC ilipofungwa na Mbeya City Uwanja wa Sokoine Mkoani Mbeya.
Endeleeni kuamini ni mwana Yanga SC!!!
Nami GENTAMYCINE natamani sana tu Siku moja Wachezaji 'Wazawa' wa Simba SC akina Mkude, Boko, Manula, Kapombe na Kocha Msaidizi wa Simba SC Matola watoke hadharani waseme jinsi gani Msemaji wa sasa wa Yanga SC Haji Manara ambavyo huwa anawapigia Simu 'Kuwashutumu' hasa pale Simba SC inapofungwa kama Manara 'alivyokasirika' mno tu ile Siku Simba SC ilipofungwa na Mbeya City Uwanja wa Sokoine Mkoani Mbeya.
Endeleeni kuamini ni mwana Yanga SC!!!