Patandi
JF-Expert Member
- Oct 10, 2015
- 401
- 374
Wabunge wakiwa bungeni wanajiona kuwa wako sawa katika kila kitu. Tofauti zao (ikiwemo elimu) huachwa getini. Ndiyo maana hoja zao huwa zinaungwa mkono kwa kishindo. Endapo mmoja hutaka kwenda tofauti hupondwa kwa kudharauliwa, kuzodolewa na kuzomewa kwa nguvu zote!Sasa kama msomi anaenda bungeni kwa wizi wa kura, sawa sawa na yule asiye na elimu, unataka huyo asiye na elimu amuheshimu ili iweje?
Mikataba mibovu na sheria za kijinga huwa zinapitishwa humo humo bungeni kishabiki wakiwemo na wasomi. Hapo unatarajia hao ambao hawajasoma waache kuwakejeli wasomi? Wasomi wajipambanue kwa kufanya mambo ya kisomi na sio kuendekeza uganja njaa.
by the way huyu mheshimiwa si ndiye yule aliyetua uwanja Sheikh Amri Abeid pale Arusha kwa mbwembwe nyingi akiwa na helicopter yake 2015 au majina yafanana?!!!