Prof. Muhongo: Kazi Zinazohitajika Duniani: Software developer, Data scientist, Information Security Analyst, Nurses, Management Analyst na Artif...

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,902
945

Prof. Muhongo Ataja Kazi Zinazohitajika Duniani: Software developer, Data scientist, Information Security Analyst, Nurses, Management Analyst na Artificial Intelligence Specialist.

Mbunge wa Musoma Vijijini Profesa Sospeter Muhongo kutokana na utafiti alioufanya amezitaja kazi kuu sita duniani ambazo zinahitajika zaidi.

Kazi hizo ni Software developer, Data scientist, Information Security Analyst, Nurses, Management Analyst na Artificial Intelligence Specialist.

Amesema kazi hizo zote zinategemea uchumi na ndio sababu nchi zenye uchumi mkubwa ndio zinaweza kufanya vizuri katika maeneo hayo na kuongeza kuwa kama nchi itahitaji kuwa na uchumi shindani ni lazima isomeshe watu na iheshimu tafiti na wasomi.

Profesa Muhongo ameitaja India kama nchi ya mfano ambayo amesema imeshika nafasi ya tano kwa kuwa na uchumi mkubwa duniani kwa sababu vijana wake wameweka kipaumbele katika masomo ya Data scientist, Blockchain engineering, Digital Marketing, Machine Engineering na Artificial Inteligence.
.
.
.
*Prof Sospeter Muhongo ametoa ushauri wa kuboresha elimu yetu iendane na matakwa ya ukuaji wa uchumi wa wakati huu.

*Prof Muhongo ameonyesha umuhimu wa kuwekeza kwenye masomo ya sayansi na teknolojia, na kutolea mfano nchi ya India ambayo mwaka jana (2023) pato lake la Taifa (GDP), lilikuwa la tano (5) Duniani lenye US Dollar Trilioni 3.7, sawa na 3.7% ya GDP ya Dunia.

Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa ambayo ina mchango wote wa Prof Muhongo

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumatano, 7.2.2024
profesapicmnjuh.jpg
 
Elimu lazima iendane na mazingira. Tatizo letu tunachukua elimu ya wazungu kwenye mazingira duni. Hebu niambia nani hapa bongo anahitaji mtu mwenye ujuzi wa Artificial intelligence? Labda kufundisha vyuoni.
 
Hapo vyuo viteme BA 10k tu kwa mwaka hakuna pa kuwapeleka, Wapunguze chai bana hii nchi bado sana kwa hizo ndoto tumalizane na Nurses kwanza.
 
SI MLISEMA KILIMO NDO UTI WA MGONGO NA TOKA TUKO SHULE YA MSINGI MKASISITIZA 80% TUNATEGEMEA KILIMO
 
Yuko sahihi ila sasa mifumo ya elimu ndio mibovu yaani unakuta mtu yuko pale Coict anachukua masters ya data science lakini ukija ground ni sifuri.
Tuna computer engineers kibao, computer scientists kutoka cive,coict, Hata kile chuo cha takwimu naona wameanzisha Bs in data science lakini elimu inayotolewa bora kwenda veta

Sent from my SM-A025U using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom