Tukikubaliana na dhana za kuikejeli elimu kisa Profesa Muhongo kakejeliwa tutapotea kama Taifa

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,608
Mheshimiwa Msukuma amepata umaarufu mkubwa siku za karibuni haswa kwa kumkejeli Profesa Muhongo mwenye kuamini kwamba umeme wa gesi ni suluhisho la suala zima la nishati hiyo. Ni mawazo ya Profesa Muhongo na anao uwezo wa kuyatetea kwa hoja kila anaposimama na kuongea bungeni.

Naona kama Msukuma anakwenda mbali sana anapoamua kumkejeli Profesa na akawaweka katika kundi moja maprofesa wote kwa kigezo cha kutokubaliana tu na mitazamo yake. Ujinga ni mzigo mzito sana na upo uhakika hao mabilionea na mamilionea wanaojulikana kila kona wanawategemea wasomi wenye elimu za juu.

Tutakuwa tunapotea kama Taifa tukianza kukubaliana na dhana hizi za darasa la saba kuwa na manufaa na mafanikio kiasi cha wenye elimu kubwa kuanza kuonekana hawana maana. Ni kosa kubwa sana tutakuwa tunalifanya.

Wanaokesha usiku ndani ya maabara kubwa za mataifa yaliyoendelea wakitafuta kila aina ya chanjo dhidi ya Covid19 ni wasomi wa viwango vya juu. Na matokeo ya elimu zao wameanza kuzaa matunda kwani miezi michache ijayo dunia kwa maana ya ile ya watu kuchanganyika wakifanya shughuli mbalimbali itaanza kurudi kama ilivyokuwa zamani.

Wanaoandika ilani na kuwawezesha wagombea wanaopanda majukwaani ni wataalam wa fani mbalimbali. Hivyo Msukuma kuwepo kwake mle bungeni ni matunda ya hao hao wasomi anaowakejeli kisa tu ametofautiana kimtazamo na Prof Muhongo.

Ujinga kama alivyowahi kusema Hayati Mwalimu Julius Nyerere pale Karimjee miaka ya nyuma ni sawa na uchi wa akili. Ndio sababu hata wanamichezo ambao wanafanikiwa wakiwa na elimu ndogo, wakishapata pesa za kutosha huamua kutafuta elimu ambayo waliikosa hapo kabla, lengo ni kuuvalisha nguo ubongo.

Wenye elimu ya darasa wanaoweza kufika alipofika Mheshimiwa mbunge Msukuma ni wachache sana. Na sekta zetu nyingi zimekuwa zikikwama kwa kukosa maarifa sahihi ya wakati husika. Uendeshaji wa taasisi zetu nyingi ukiuchunguza kwa undani unagundua upungufu mwingi unaotokana na elimu kuwa ni ndogo pamoja na wahusika kukosa ufahamu mpana wa kitu wanachokifanya, wanakosa exposure.

Nimemuelewa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kumkabidhi wizara ya mambo ya nje Mama Liberata Mulamula, anataka aitumie exposure yake kubwa katika kujenga taswira chanya ya Tanzania kimataifa. Inakuwa ni aibu unapomsikia mbunge anakejeli elimu wakati ndio silaha namba moja ya mataifa yaliyoendelea.

Kejeli anazokutana nazo Prof Muhongo zinawahusu pia maprofesa wengi ambao wamefanya mengi ya maana na yenye kuonekana kwa faida ya taifa. Ni mawazo fulani duni kuiponda elimu eti kwa sababu ya kutofautiana mitazamo na msomi mmoja
 
Maadui wakuu wa taifa:
(1) Ujinga
(2)Umasikini na
(3)Maradhi.
Adui namba moja hapo juu ndo anamsibu Mh. Msukuma. Pia hakana staha kale kajamaa ni ka kupuuza tu.
Yeye kuwa tajiri asiye na elimu zaidi ya ile ya darasa la saba sio sifa kama anavyodhani. Wapo watu wengi tu wanaoshindwa kufika popote kimaisha sababu ya elimu zao ndogo.
 
Niambieni kosa la Profesa Muhongo ni nini?

Profesa anataka tuwe na energy mix, yaani vyanzo vingi vya nishati ikiwemo gesi

Profesa anaeleza kuwa ili umeme wa maji uwe bei chini ni mpaka kwanza urudishe pesa yako uliyoitumia kuinvest kisha ndo mbeleni buko unaweza kuufanya cheap na it takes time
 
Niambieni kosa la Profesa Muhongo ni nini?

Profesa anataka tuwe na energy mix, yaani vyanzo vingi vya nishati ikiwemo gesi

Profesa anaeleza kuwa ili umeme wa maji uwe bei chini ni mpaka kwanza urudishe pesa yako uliyoitumia kuinvest kisha ndo mbeleni buko unaweza kuufanya cheap na it takes time
Kosa lake ni kuwa mkweli kwa nchi yake. Mataifa makubwa yana vyanzo vingi vya umeme, hawana siasa kwenye masuala yenye maslahi ya muda mrefu ya uchumi.
 
Bado tuna sisitiza, Wasomi waongee Kama waelevu na waweze kueleweka in simple terms, mfano hapa Tanzania tuna umeme wa Gas, wa Hydropower, wa Solar, Wa upepo na wa mafuta.

Ivi katika mazingira ya uwepo wa hizi project ilishindikanaje hoja ya Muhongo kutetewa kwa tafiti ili asionekane muongo?
 
Msukuma ni mgonjwa wa akili, kutoelewa kwake hoja ya Prop Mhongo ndiko kulikosababisha personal attack zake..

Speaker naye ni wakuaumiwa kwa kuruhusu bunge kufanya personal attacks na sio kujikita kwenye hoja. Speaker ndio msimamizi wa hii mijadala sasa kama anashindwa kusimamia na kuwa mshabiki kwa maslahi yake binafsi mbeleni huko tutapata shida..

Kuruhusu elimu inakejeliwa ndani ya Bunge na bunge linashangilia maana yake ni kuiambia jamii iachane na shule maana haina umuhimu wala msaada...effect yake ni kubwa kuliko tunavyodhania.

Awamu ya tano nayo ni ya kulaumiwa kwa kulazimisha watu watumie fikra za mtu mmoja na ukipingana naye basi wewe msaliti, sio mzalendo, mpiga dili, kibaraka nk.

Prop Mhongo aliwakilisha fikra zake na kuzitetea kwa ufahamu wake bila kumkejeli mtu, Msukuma kama hakubaliana alipaswa kuweka hoja zake mezani tupime na sio kufanya personal attack.
 
Mimi nina degree tatu ukijumlisha degree ya falsafa na ni mwalimu wa vyuo vikuu mbalimbali wewe na darasa lako la saba utanishauri nini mimi? Nilimskia mwana Mbeya mmoja akiwapasha darasa la saba. Sheria ibadilishwe ili mbunge au diwani awe na si chini ya degree moja.
 
Gas ya Mtwara siyo yakwetu bado turudie huu upuuzi tukimaliza umeme wa maji tutaenda kwenye gas tena kwa pesa zetu za ndani.
 
Msukuma ni mgonjwa wa akili, kutoelewa kwake hoja ya Prop Mhongo ndiko kulikosababisha personal attack zake..

Speaker naye ni wakuaumiwa kwa kuruhusu bunge kufanya personal attacks na sio kujikita kwenye hoja...Speaker ndio msimamizi wa hii mijadala sasa kama anashindwa kusimamia na kuwa mshabiki kwa maslahi yake binafsi mbeleni huko tutapata shida..

Kuruhusu elimu inakejeliwa ndani ya Bunge na bunge linashangilia maana yake ni kuiambia jamii iachane na shule maana haina umuhimu wala msaada...effect yake ni kubwa kuliko tunavyodhania..

Awamu ya tano nayo ni ya kulaumiwa kwa kulazimisha watu watumie fikra za mtu mmoja na ukipingana naye basi wewe msaliti, sio mzalendo, mpiga dili, kibaraka nk..

Prop Mhongo aliwakilisha fikra zake na kuzitetea kwa ufahamu wake bila kumkejeli mtu, Msukuma kama hakubaliana alipaswa kuweka hoja zake mezani tupime na sio kufanya personal attack....
Inaonekana wawili hawa wanao ugomvi wao wa miaka mingi. Tetea hoja kwa kujenga hoja sio kumdhalilisha mtu.
 
Yeye kuwa tajiri asiye na elimu zaidi ya ile ya darasa la saba sio sifa kama anavyodhani. Wapo watu wengi tu wanaoshindwa kufika popote kimaisha sababu ya elimu zao ndogo.
Sasa kama msomi anaenda bungeni kwa wizi wa kura, sawa sawa na yule asiye na elimu, unataka huyo asiye na elimu amuheshimu ili iweje?

Mikataba mibovu na sheria za kijinga huwa zinapitishwa humo humo bungeni kishabiki wakiwemo na wasomi. Hapo unatarajia hao ambao hawajasoma waache kuwakejeli wasomi? Wasomi wajipambanue kwa kufanya mambo ya kisomi na sio kuendekeza uganja njaa.
 
Sisi ni Taifa ambalo ..Mganga wa kienyeji ambae ana tangaza dawa hadi za kufuta kesi.

Kitu ambacho ni Sawa na kutangaza kulinda wahalifu... Mganga huyo anagombea hadi ubunge na kushinda.

Taifa ambalo waziri wa afya anaunga mkono kuacha kupima corona na kuita media kutangaza chachandu ya ndimu kama dawa ya Corona.

Msukuma ni zao la jamii ambayo tunayo.
Upumbavu wa halaiki
 
Shida ilianzia pale wasomi walipokubali mambo ya kienyeji yakiwamo ya kupigishwa pigishwa hadi nyungu huku wao wakiwa wameuchuna.

Wasomi uchwara waliposhindwa kuongea lugha walizopaswa kuzijua kwa usomi wao, ikasemekana ni kukuza kiswahili, hali wao wakiwa wameuchuna tu.

Wasomi waliporuhusu njaa za matumbo yao kufunika akili vichwani kwao kufanana tu na za akina msukuma.

Usaka fursa kwa gharama yoyote umewagharimu sana bandugu hawa.
 
Mheshimiwa Msukuma amepata umaarufu mkubwa siku za karibuni haswa kwa kumkejeli Profesa Muhongo mwenye kuamini kwamba umeme wa gesi ni suluhisho la suala zima la nishati hiyo. Ni mawazo ya Profesa Muhongo na anao uwezo wa kuyatetea kwa hoja kila anaposimama na kuongea bungeni.

Naona kama Msukuma anakwenda mbali sana anapoamua kumkejeli Profesa na akawaweka katika kundi moja maprofesa wote kwa kigezo cha kutokubaliana tu na mitazamo yake. Ujinga ni mzigo mzito sana na upo uhakika hao mabilionea na mamilionea wanaojulikana kila kona wanawategemea wasomi wenye elimu za juu.

Tutakuwa tunapotea kama Taifa tukianza kukubaliana na dhana hizi za darasa la saba kuwa na manufaa na mafanikio kiasi cha wenye elimu kubwa kuanza kuonekana hawana maana. Ni kosa kubwa sana tutakuwa tunalifanya.

Wanaokesha usiku ndani ya maabara kubwa za mataifa yaliyoendelea wakitafuta kila aina ya chanjo dhidi ya Covid19 ni wasomi wa viwango vya juu. Na matokeo ya elimu zao wameanza kuzaa matunda kwani miezi michache ijayo dunia kwa maana ya ile ya watu kuchanganyika wakifanya shughuli mbalimbali itaanza kurudi kama ilivyokuwa zamani.

Wanaoandika ilani na kuwawezesha wagombea wanaopanda majukwaani ni wataalam wa fani mbalimbali. Hivyo Msukuma kuwepo kwake mle bungeni ni matunda ya hao hao wasomi anaowakejeli kisa tu ametofautiana kimtazamo na Prof Muhongo.

Ujinga kama alivyowahi kusema Hayati Mwalimu Julius Nyerere pale Karimjee miaka ya nyuma ni sawa na uchi wa akili. Ndio sababu hata wanamichezo ambao wanafanikiwa wakiwa na elimu ndogo, wakishapata pesa za kutosha huamua kutafuta elimu ambayo waliikosa hapo kabla, lengo ni kuuvalisha nguo ubongo.

Wenye elimu ya darasa wanaoweza kufika alipofika Mheshimiwa mbunge Msukuma ni wachache sana. Na sekta zetu nyingi zimekuwa zikikwama kwa kukosa maarifa sahihi ya wakati husika. Uendeshaji wa taasisi zetu nyingi ukiuchunguza kwa undani unagundua upungufu mwingi unaotokana na elimu kuwa ni ndogo pamoja na wahusika kukosa ufahamu mpana wa kitu wanachokifanya, wanakosa exposure.

Nimemuelewa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kumkabidhi wizara ya mambo ya nje Mama Liberata Mulamula, anataka aitumie exposure yake kubwa katika kujenga taswira chanya ya Tanzania kimataifa. Inakuwa ni aibu unapomsikia mbunge anakejeli elimu wakati ndio silaha namba moja ya mataifa yaliyoendelea.

Kejeli anazokutana nazo Prof Muhongo zinawahusu pia maprofesa wengi ambao wamefanya mengi ya maana na yenye kuonekana kwa faida ya taifa. Ni mawazo fulani duni kuiponda elimu eti kwa sababu ya kutofautiana mitazamo na msomi mmoja
Hawa maprofesa walijidharaulisha wenyewe waliposema wameokotwa barabarani wakati walikuwa chuo kikuu mlimani hapo acha wasemwe akili ziwakae sawa warudi kufundisha
 
Back
Top Bottom