Tukiachana na wachaga, makabila mengi yana watoto wa mama, wanapajua zaidi kijijini na ndugu wa mama, Kwanini wanaume hawapeleki Watoto vijijini?

gearbox

JF-Expert Member
Apr 20, 2024
524
1,476
Ukiondoa wachaga wengi (sio wote) watanzania wengi wa makabila mengine wanapajua zaidi vijijini kwa mama zao na ndugu wa mama kuzidi upande wa baba hivyo wanakidhi kigezo cha kuitwa WATOTO WA MAMA.

Kwa wachaga naona wapo tofauti, watoto wanarudi mara kwa mara vijiji vya baba zao na kuzoeleka na ndugu wa baba, hii inawapa sifa ya kuwa WATOTO WA BABA

unakuta mtoto hajawahi kufika kabisa kijijini kwa baba yake, kujuana na ndugu upande wa baba ni mpaka waje mjini, Hata wale wanaopelekwa vijijini unakuta ni mara chache sana hawapati muda wa kuvijua vijiji vyao vizuri na kuzoeana na ndugu wa huko, watoto wanaenda msibani wanakuwa kama wageni mbele ya ndugu za baba zao.

Pia nachoona japo sina ushahidi naamini kwamba mtoto akiwa karibu zaidi na asili ya baba, inachangia kuleta mafanikio kuliko akiwa mtoto wa mama, mfano ni wahindi, waarabu, wasomali wanaoishi Tz na kwa makabila ya Tanzania wapo wachaga ambao kimaendeleo mbali ukilinganisha na makabila mengine.
 
Mtoto wa mama ni yule ambae ana connection kubwa zaidi ya mama kuzidi baba, yupo karibu zaidi ya ndugu zake mama na kujulikana zaidi kijijini kwa mama.
 
Hii naona pia sana kwa waliooa uchagani kwa mtu asie mchaga watoto wanavutwa sana kwa mama
Ni kila sehemu mkuu, wewe kama baba usipozoesha watoto kijijini kwenu na kwa ndugu zako, watoto watazoea zaidi upande wa mama, watoto wa hivi mara nyingi ndio wanakuwa mstari wa mbele kusema "hakuna kama mama", "nani kama mama", n.k. wana asili ya mama zaidi kuzidi baba.
 
Makabila mengi watoto ni mali ya mama na humthamini zaidi mama kwasababu wapo karibu zaidi na asili ya mama, ndio maana ni kawaida kukuta wengi wakisifia "nani kama mama". "hakuna kama mama", n.k. ni dalili ya kwmba mtu huyu ni mtoto wa mama, ni ngumu kukuta mtoto wa baba akimsifia mama tu, atamsifia pia baba kama anavyofanya kwa mama tena inaweza kuzidi.
 
ukiondoa wachaga watanzania wengi wanapajua zaidi vijijini kwa mama zao na ndugu wa mama kuzidi upande wa baba hivyo wanakidhi kigezo cha kuitwa WATOTO WA MAMA.

Kwa wachaga naona wapo tofauti, watoto wanarudi mara kwa mara vijiji vya baba zao na kuzoeleka na ndugu wa baba, hii inawapa sifa ya kuwa WATOTO WA BABA

unakuta mtoto hajawahi kufika kabisa kijijini kwa baba yake, kujuana na ndugu upande wa baba ni mpaka waje mjini, Hata wale wanaopelekwa vijijini unakuta ni mara chache sana hawapati muda wa kuvijua vijiji vyao vizuri na kuzoeana na ndugu wa huko, watoto wanaenda msibani wanakuwa kama wageni mbele ya ndugu za baba zao.
Huna lolote zaidi ya kutaka kutaja ukabila! Shwaini!
 
Makabila mengi watoto ni mali ya mama na humthamini zaidi mama kwasababu wapo karibu zaidi na asili ya mama, ndio maana ni kawaida kukuta wengi wakisifia "nani kama mama". "hakuna kama mama", n.k. ni dalili ya kwmba mtu huyu ni mtoto wa mama, ni ngumu kukuta mtoto wa baba akimsifia mama tu, atamsifia pia baba kama anavyofanya kwa mama tena inaweza kuzidi.
Una miaka mingapi kijana!
 
ukiondoa wachaga watanzania wengi wanapajua zaidi vijijini kwa mama zao na ndugu wa mama kuzidi upande wa baba hivyo wanakidhi kigezo cha kuitwa WATOTO WA MAMA.

Kwa wachaga naona wapo tofauti, watoto wanarudi mara kwa mara vijiji vya baba zao na kuzoeleka na ndugu wa baba, hii inawapa sifa ya kuwa WATOTO WA BABA

unakuta mtoto hajawahi kufika kabisa kijijini kwa baba yake, kujuana na ndugu upande wa baba ni mpaka waje mjini, Hata wale wanaopelekwa vijijini unakuta ni mara chache sana hawapati muda wa kuvijua vijiji vyao vizuri na kuzoeana na ndugu wa huko, watoto wanaenda msibani wanakuwa kama wageni mbele ya ndugu za baba zao.
Ukiwapeleka watoto kwenu utawachanganya ndugu zako, mtaa mmoja umezaa na wanawake wanne ambao mkeo hawajui, kazini kwako saluni umezaa na wawili, katika hawa kuna Mkurya, Mzaramo, Mmwera, Msukuma, Mnyaturu na mwingine jina wala kabila haulijui! Hii ni ajali kwa mamantilie. Acha mambo yajiseti yenyewe kwani hawahitaji kunyonya.
 
Ukiwapeleka watoto kwenu utawachanganya ndugu zako, mtaa mmoja umezaa na wanawake wanne ambao mkeo hawajui, kazini kwako saluni umezaa na wawili, katika hawa kuna Mkurya, Mzaramo, Mmwera, Msukuma, Mnyaturu na mwingine jina wala kabila haulijui! Hii ni ajali kwa mamantilie. Acha mambo yajiseti yenyewe kwani hawahitaji kunyonya.
kwa ndugu zako hata ukipeleka watoto wa mama tofauti ni sawa tu, Vijijini mtu kuoa mitaala ni jambo la kawaida tu hivyo watoto wa mama tofauti kwao si jambo geni wanachojua ni mbegu yako.....damu ni nzito kuliko maji
 
kwa ndugu zako hata ukipeleka watoto wa mama tofauti ni sawa tu, Vijijini mtu kuoa mitaala ni jambo la kawaida tu hivyo watoto wa mama tofauti kwao si jambo geni wanachojua ni mbegu yako.....damu ni nzito kuliko maji
Si kwa idadi hiyo, huoana hapohapo kijijini kwao au cha karibu.
 
Oeni makabila yenu kidogo inasaidia hampotezi watoto lakini we mkurya unaoa mtu wa mbeya na mnaishi dom au dar hao watoto kupajua kwenu ni ngumu ila watapajua mbeya na vijiji vyake
 
Oeni makabila yenu kidogo inasaidia hampotezi watoto lakini we mkurya unaoa mtu wa mbeya na mnaishi dom au dar hao watoto kupajua kwenu ni ngumu ila watapajua mbeya na vijiji vyake
Wakurya wamewakosea nini aisee 🤣🤣, naona ni mara ya pili mnawataja kwenye uzi huu
 
Oeni makabila yenu kidogo inasaidia hampotezi watoto lakini we mkurya unaoa mtu wa mbeya na mnaishi dom au dar hao watoto kupajua kwenu ni ngumu ila watapajua mbeya na vijiji vyake
Wengi wanakutana mjini na kuanzisha familia wanavurugana na kuachana mjini mjini! Kwao na wazazi kubaya mafukara wanaogopa aibu
 
Back
Top Bottom