Nawaonea wivu wachaga, kwetu hatukutani pamoja nje ya misiba, mjini tuna maendeleo ila kijijini hali mbaya, watoto hawakujui kwao watapoteza asili yao

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
  • Kijijini kwetu huwa tunarudi wote kwa pamoja kukiwa na msiba tu, nje ya hapo kila mtu huwa anarudi kimpango wake, kuna ambao hawarudigi kabisa.
  • Tunaoishi mijini hatujawazoesha watoto warudi kwao, wakiwa wakubwa wanashindwa hata kurudi kwao kwasababu hawajapazoea, Nina marafiki wengi waliokulia mjini wamewahi kwenda kwao mara tatu tu, wamekuwa watu wazima hawajawahi kwenda kwasababu hawakuzoeshwa kurudi, mtoto inabidi azoeshwe kurudi kwao kila mwaka hata akiwa mtu mzima awe anarudi mwenyewe.
  • Huku mijini ndugu tunakutana wenye nafuu ya maendeleo wapo wenye biashara zao, kazi nzuri, n.k. tunaishi vizuri mjini lakini huko vijijini maendeleo ni duni, wapo wanaoendeleza kwao lakini unakuta kijiji kizima nyumba za kisasa ni asilimia 2 tu, hizo ndio huwa zinapigwa picha kudanganya kwamba kijiji kina maendeleo.
  • Imani za kishirikina nazo zinachangia watu wasirudi, Sikatai kwamba kuna matambiko na hakuna kabila lisilo na tambiko lake, hata wachaga kuna koo zenye historia za kichifu lazima watambike. Tatizo huku kwetu makabila mengi mambo ya uchawi yamesahamiri tunaogopa kurudi vijijini, stori kibao zipo vijijini watu kupigana vipapai kisa tu mtu kanunua pikipiki, kutupiana magonjwa, kutupiana majini, n.k.
Tukija kwa wachaga nawaonea wivu maana hawasahau kwao, kila mwaka wanarudi kwao "KWA PAMOJA" yani wale waliotawanyika mikoani na nje ya nchi wanarudi kwao, na hii inasaidia hata watoto wapazoee kwao na wao kuendeleza utamaduni, si tu hivyo bali huchochea maendeleo, kuikuta nyumba ya nyasi uchagani ni sawa na kutafuta punje ya mchele kwenye tope.
 
Christmas ya leo nimefanya reserve baadae tupate mtoko pamoja na familia lakini bado sina furaha,

  • Mwaka mzima huu sijarudi kwetu, Kijijini kwetu huwa tunarudi wote kwa pamoja kukiwa na msiba tu
  • watoto wangu nimewahi kuwapeleka mara mbili tu huko kwao, mara ya mwisho ilikua 2020, kwa lugha nyepesi ni kwamba hawajapazoea kwao na nahisi washasahaulika na wao wamepasahau,
  • Huku mijini ndugu tunakutana wenye nafuu ya maendeleo mtu ana nyumba yake na kausafiri lakini kule kijijini maendeleo yaliyofanyika ni kubadili bati tu.
  • Kijijini kiujumla hali za wanajikijiji ni mbaya, Ni matajiri wawili tu wamejenga nyumba zinazoeleweka lakini kuna nyumba za nyasi nyingi, barabara mbovu, maji ya bomba hakuna, n.k.
Tukija kwa wachaga nawaonea wivu maana hawasahau kwao, kila mwaka wanarudi kwao "KWA PAMOJA" yani wale waliotawanyika mikoani na nje ya nchi wanarudi kwao, na hii inasaidia hata watoto wapazoee kwao na wao kuendeleza utamaduni, si tu hivyo bali huchochea maendeleo, kuikuta nyumba ya nyasi uchagani ni sawa na kutafuta punje ya mchele kwenye tope.
Sahihi kabisa..
Huo mwezi ambao huenda huko, sio tu kukutana wale wakosefu wote ndio siku za hukumu na adhabu.

Wewe usie na maendeleo ndiyo unaitwa na wazazi na ndgu wengine kukuuliza unakwama wapi. Ole wako wajue mjini ulikuwa unapata hela na unachezea.

Kimsingi disputes zote za ukoo na familia ama majirani wa huko zinakuwa solved mbali na hayo ulioyasema
 
Kwa wahaya umefika?
Wahaya tupo nao January mpaka December mkuu, wachache sana wanaorudi kwao na hata wakirudi sio kwa pamoja ni kila mtu kivyake.

Wahaya kjiji kizima wenye nyumba za kisasa ni wachache sana maybe 2%, nyumba zingine za kale.

Huwa wanapenda kupiga picha hizo nyumba za 2% wanajisifia,
 
Wahaya tupo nao January mpaka December mkuu, wachache sana wanaorudi kwao na hata wakirudi sio kwa pamoja ni kila mtu kivyake.

Wahaya kjiji kizima wenye nyumba za kisasa ni wachache sana maybe 2%, nyumba zingine za kale.

Huwa wanapenda kupiga picha hizo nyumba za 2% wanajisifia,
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
  • Kijijini kwetu huwa tunarudi wote kwa pamoja kukiwa na msiba tu, nje ya hapo kila mtu huwa anarudi kimpango wake, kuna ambao hawarudigi kabisa.
  • Tunaoishi mijini hatujawazoesha watoto warudi kwao, wakiwa wakubwa wanashindwa hata kurudi kwao kwasababu hawajapazoea, Nina marafiki wengi waliokulia mjini wamewahi kwenda kwao mara tatu tu, wamekuwa watu wazima hawajawahi kwenda kwasababu hawakuzoeshwa kurudi, mtoto inabidi azoeshwe kurudi kwao kila mwaka hata akiwa mtu mzima awe anarudi mwenyewe.
  • Huku mijini ndugu tunakutana wenye nafuu ya maendeleo wapo wenye biashara zao, kazi nzuri, n.k. tunaishi vizuri mjini lakini huko vijijini maendeleo ni duni, wapo wanaoendeleza kwao lakini unakuta kijiji kizima nyumba za kisasa ni asilimia 2 tu, hizo ndio huwa zinapigwa picha kudanganya kwamba kijiji kina maendeleo.
  • Imani za kishirikina nazo zinachangia watu wasirudi, Sikatai kwamba kuna matambiko na hakuna kabila lisilo na tambiko lake, hata wachaga kuna koo zenye historia za kichifu lazima watambike. Tatizo huku kwetu makabila mengi mambo ya uchawi yamesahamiri tunaogopa kurudi vijijini, stori kibao zipo vijijini watu kupigana vipapai kisa tu mtu kanunua pikipiki, kutupiana magonjwa, kutupiana majini, n.k.
Tukija kwa wachaga nawaonea wivu maana hawasahau kwao, kila mwaka wanarudi kwao "KWA PAMOJA" yani wale waliotawanyika mikoani na nje ya nchi wanarudi kwao, na hii inasaidia hata watoto wapazoee kwao na wao kuendeleza utamaduni, si tu hivyo bali huchochea maendeleo, kuikuta nyumba ya nyasi uchagani ni sawa na kutafuta punje ya mchele kwenye tope.
Waha mnajuwa kuroga tu na kutia kelele mijini basi ila kwenu hamna lolote.
 
Back
Top Bottom