Pfizer
JF-Expert Member
- Mar 25, 2021
- 304
- 518
Jumapili Machi 03, 2024 kupitia mitandao ya kijamii na makundi sogozi, zilisambaa taarifa za kudorora kwa utendaji kazi ya kuhudumia Meli na Shehena katika Bandari ya Dar es Salaam kunakohusishwa na mgomo wa wafanyakazi wenye madai mbalimbali likiwemo kufutiwa mikataba yao ya kazi.
Kufuatia taarifa hiyo, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inapenda kutoa ufafanuzi ufuatao, Kwanza, hakuna mgomo wala hujuma zozote katika Bandari ya Dar es Salaam na badala yake kazi za uhudumiaji Meli na Shehena zinaendelea kutekelezwa ipasavyo katika Magati yote kwa mujibu wa taratibu za shughuli za Bandari.
Pili, hakuna Mtumishi yeyote wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA). (Mtumishi wa ajira ya kudumu au Mtunishi wa ajira za muda maalum) aliyesitishiwa mkataba wake kwa sababu zozote zile. Watumishi wote Wanatimiza majukumu yao kikamilifu kwa kuzingatia ratiba za sehemu zao za kazi.
Tatu, Menejimenti ya TPA inatimiza ipasavyo jukumu lake la kusimamia kikamilifu utendaji wa ldara na Vitengo vyote vya operesheni za kibandari katika Bandari ya Dar es Salaam kwa saa 24 ili kuhakikisha kuwa, huduma zinatolewa kwa Weledi, kasi na ufanisi wa hali ya juu wakati wote huku Mkurugenzi wa Bandari na Wakuu wa ldara na Vitengo wakipatikana muda wote katika sehemu zao za kazi na kupitia Mawasiliano ya Simu.
Nne, Mamlaka imejiwekea utaratibu wa kuchapisha taarifa za mwenendo wa uhudumiaji Meli Bandarini ili kuwapa Wateja na Wadau taarifa sahihi wakati wote. Taarifa hizi zinaeleza idadi ya Meli zinazohudumiwa gatini, Meli zilizo nje zikisubiri kuingia (Outer Anchorage) na Meli zilizokwisha hudumiwa na kuondoka. Hakuna Meli zinazohudumiwa kinyume na utaratibu huu.
Tano, kutokana na tabia iliyojengeka siku za hivi karibuni ya Watu wasio na nia njema kuzua taharuki kwa kusambaza Habari za uongo zinazochafua taswira njema ya TPA mbele ya Wateja, Wadau na Umma kwa ujumla, Mamlaka imejjpanga kuanza kuchukua hatua kali za kisheria kwa wale wote watakaobainika kuhusika na upotoshaji huu.
TPA inawasihi Wateja na Wadau wake wote kuendelea kutumia huduma za Bandari ya Dar es Salaam na Bandari zote za TPA bila shaka yoyote kwa kuwa Mamlaka imejipanga vyema kuendelea kutoa huduma bora wakati Wote na kutatua kwa haraka changamoto zote zinazojitokeza kwa kushirikiana na Wadau wote wanaohusika na uondoshaji wa Shehena Bandarini.
Aidha, TPA inaendelea kukaribisha taarifa zote kuhusiana na huduma zake kupitia njia rasmi za Mawasiliano za Mamlaka ambazoni Kituo cha Huduma kwa Wateja kilichopo ghorofa ya 6 katika Jengo la Makao Makuu ya TPA (One Stop Centre). Mawasiliano pia yanapokelewa kupitia simu ya bure kwa namba 0800-110032, Barua pepe kwa anuani ya customercare@ports.go.tz, Tovuti www.ports.go.tz na kurasa rasmi za Mitandao ya kijamii ya Instagram, X (Twitter) na facebook kwa jina @tpa_tz, kwa saa 24.
Imetolewa na; Kurugenzi ya Masoko na Uhusiano; TPA-Makao Makuu.
Pia, woma; Tetesi: - Kuna mashaka Bandarini. Serikali itoe tamko ya kinachoendelea ili kama yanayoripotiwa ni tetesi yasilete taharuki
Kufuatia taarifa hiyo, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inapenda kutoa ufafanuzi ufuatao, Kwanza, hakuna mgomo wala hujuma zozote katika Bandari ya Dar es Salaam na badala yake kazi za uhudumiaji Meli na Shehena zinaendelea kutekelezwa ipasavyo katika Magati yote kwa mujibu wa taratibu za shughuli za Bandari.
Pili, hakuna Mtumishi yeyote wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA). (Mtumishi wa ajira ya kudumu au Mtunishi wa ajira za muda maalum) aliyesitishiwa mkataba wake kwa sababu zozote zile. Watumishi wote Wanatimiza majukumu yao kikamilifu kwa kuzingatia ratiba za sehemu zao za kazi.
Tatu, Menejimenti ya TPA inatimiza ipasavyo jukumu lake la kusimamia kikamilifu utendaji wa ldara na Vitengo vyote vya operesheni za kibandari katika Bandari ya Dar es Salaam kwa saa 24 ili kuhakikisha kuwa, huduma zinatolewa kwa Weledi, kasi na ufanisi wa hali ya juu wakati wote huku Mkurugenzi wa Bandari na Wakuu wa ldara na Vitengo wakipatikana muda wote katika sehemu zao za kazi na kupitia Mawasiliano ya Simu.
Nne, Mamlaka imejiwekea utaratibu wa kuchapisha taarifa za mwenendo wa uhudumiaji Meli Bandarini ili kuwapa Wateja na Wadau taarifa sahihi wakati wote. Taarifa hizi zinaeleza idadi ya Meli zinazohudumiwa gatini, Meli zilizo nje zikisubiri kuingia (Outer Anchorage) na Meli zilizokwisha hudumiwa na kuondoka. Hakuna Meli zinazohudumiwa kinyume na utaratibu huu.
Tano, kutokana na tabia iliyojengeka siku za hivi karibuni ya Watu wasio na nia njema kuzua taharuki kwa kusambaza Habari za uongo zinazochafua taswira njema ya TPA mbele ya Wateja, Wadau na Umma kwa ujumla, Mamlaka imejjpanga kuanza kuchukua hatua kali za kisheria kwa wale wote watakaobainika kuhusika na upotoshaji huu.
TPA inawasihi Wateja na Wadau wake wote kuendelea kutumia huduma za Bandari ya Dar es Salaam na Bandari zote za TPA bila shaka yoyote kwa kuwa Mamlaka imejipanga vyema kuendelea kutoa huduma bora wakati Wote na kutatua kwa haraka changamoto zote zinazojitokeza kwa kushirikiana na Wadau wote wanaohusika na uondoshaji wa Shehena Bandarini.
Aidha, TPA inaendelea kukaribisha taarifa zote kuhusiana na huduma zake kupitia njia rasmi za Mawasiliano za Mamlaka ambazoni Kituo cha Huduma kwa Wateja kilichopo ghorofa ya 6 katika Jengo la Makao Makuu ya TPA (One Stop Centre). Mawasiliano pia yanapokelewa kupitia simu ya bure kwa namba 0800-110032, Barua pepe kwa anuani ya customercare@ports.go.tz, Tovuti www.ports.go.tz na kurasa rasmi za Mitandao ya kijamii ya Instagram, X (Twitter) na facebook kwa jina @tpa_tz, kwa saa 24.
Imetolewa na; Kurugenzi ya Masoko na Uhusiano; TPA-Makao Makuu.
Pia, woma; Tetesi: - Kuna mashaka Bandarini. Serikali itoe tamko ya kinachoendelea ili kama yanayoripotiwa ni tetesi yasilete taharuki