Tofauti kati ya Yesu na Nabii Issa
Watu wengi hujiuliza: Je, Nabii Issa bin Maryam (Yesu) alikuwa Mkristo?
Swali hili linahitaji kufafanuliwa kwa elimu, mantiki na ushahidi wa kweli kutoka katika Qur-aan na hata maandiko yanayohusishwa na Wakristo.

Ukweli ni kwamba:
Issa bin Maryam (Yesu) hakuwa Mkristo, bali alikuwa Muislamu aliyemwabudu Allah Mmoja pekee na aliwaita watu kwenye Tawhiid.
Kwa sababu:
Ukristo ulianza baada ya kunyanyuliwa kwa Issa عليه السلام.
Issa mwenyewe hakuwahi kusema “Mimi ni Mungu”.
Hakuwahi kusema “Niabuduni”.
Hakuwahi kufundisha Utatu (Trinity).

Maana ya “Muislamu”
“Muislamu” maana yake ni:
Mtu anayejisalimisha kwa Allah kwa Tawhiid na kumtii.
Hivyo Mitume wote walikuwa Waislamu:
Adam
Nuh
Ibrahim
Musa
Issa
Muhammad ﷺ
Wote walikuja na ujumbe mmoja:
“Mwabuduni Allah peke yake.”

Ushahidi Kutoka Qur-aan
1. Issa Aliwaita Watu Wamwabudu Allah
Allah amesema:
إِنَّ اللَّهَ رَبِّي وَرَبُّكُمْ فَاعْبُدُوهُ ۚ هَٰذَا صِرَاطٌ مُسْتَقِيمٌ
“Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na Mola wenu, basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo njia iliyonyooka.”
— Surat Aal Imraan 3:51
Hapa Issa anasema wazi:
Allah ni Mola wake.
Allah ni Mola wa watu wengine.
Watu wamwabudu Allah, si yeye.
Mtu anayesema:
“Muabuduni Allah”
hawezi kuwa Mungu.

2. Issa Hakudai Uungu
Allah amesema:
مَا الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ إِلَّا رَسُولٌ
“Masihi mwana wa Maryam si chochote ila ni Mtume.”
— Surat Al-Maaidah 5:75
Qur-aan imesema wazi:
Issa ni Mtume.
Si Mungu.
Si mwana wa Mungu.

3. Mitume Wote Walikuwa Waislamu
Allah amesema kuhusu Ibrahim:
مَا كَانَ إِبْرَاهِيمُ يَهُودِيًّا وَلَا نَصْرَانِيًّا وَلَٰكِن كَانَ حَنِيفًا مُّسْلِمًا
“Ibrahim hakuwa Myahudi wala Mkristo, bali alikuwa mcha Mungu Muislamu.”
— Surat Aal Imraan 3:67
Kama Ibrahim hakuwa Mkristo, basi hata Issa hakuwa Mkristo, kwa sababu Ukristo haukuwepo kabla yake.

Je, Ukristo Ulianza Lini?
Neno “Mkristo” lilianza baada ya Issa kunyanyuliwa.
Katika Biblia yenyewe imeandikwa:
“Wanafunzi wakaanza kuitwa Wakristo kwanza huko Antiokia.”
— Matendo 11:26
Hii inaonyesha:
Issa hakuwahi kujiita Mkristo.
Wala hakuwaita wafuasi wake Wakristo.
Jina hilo lilikuja baadaye.

Je, Issa Alihubiri Utatu?
Hakuna sehemu Issa aliposema:
Mungu ni watatu.
Mimi ni sehemu ya Utatu.
Niabuduni mimi.
Badala yake alisema:
“Msikie Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja.”
— Marko 12:29
Huu ndio ujumbe wa Tawhiid.

Issa Aliswali Kama Waislamu
Katika Biblia:
Alikuwa akisujudu.
Alifunga.
Aliomba kwa Allah.
Alisema:
“Si mapenzi yangu bali yako yatimizwe.”
Mungu haombi kwa Mungu mwingine.

Je, Issa Ni Mwana wa Mungu?
Allah amesema:
لَقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّهَ هُوَ الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ
“Kwa yakini wamekufuru wale wanaosema Mwenyezi Mungu ndiye Masihi mwana wa Maryam.”
— Surat Al-Maaidah 5:72

Na Issa mwenyewe alisema:
“Ninakwenda kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
— Yohana 20:17
Kama Issa ana “Mungu wangu”, basi yeye si Mungu.
Ujumbe wa Kweli wa Issa
Ujumbe wa Issa ulikuwa:
Muabuduni Allah mmoja.
Acheni shirk.
Fuateni Mitume.
Tubu kwa Allah.
Jiandaeni kwa Akhera.
Na hata alimtabiri kuja kwa Mtume Muhammad ﷺ.
Allah amesema:
وَمُبَشِّرًا بِرَسُولٍ يَأْتِي مِن بَعْدِي اسْمُهُ أَحْمَدُ
“Na mwenye kutoa bishara ya Mtume atakayekuja baada yangu jina lake Ahmad.”
— Surat As-Saff 61:6

Hitimisho
Issa bin Maryam:
Hakuwa Mungu.
Hakuwa mwana wa Mungu.
Hakuwa Mkristo.
Alikuwa Mtume mkubwa wa Allah.
Alikuwa Muislamu mwenye kumwabudu Allah mmoja.
Na dini ya Mitume wote ilikuwa moja:
Tawhiid — kumuabudu Allah peke yake bila kumshirikisha.
Mwisho
Allah amesema:
إِنَّ الدِّينَ عِندَ اللَّهِ الْإِسْلَامُ
“Bila shaka dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu.”
— Surat Aal Imraan 3:19

Isa bin Maryam. Hakuzaliwa kwa uwezo wa Kibinadamu. Jiulize kwa nini anaitwa Bin Maryam jina la mamaye? Ni sababu hakutungwa mimba kwa njia ya Kawaida. Hakuwa na Baba wa Duniani. Maana yake nini?

Ushahidi kutoka Qur’an
Surat Maryam (19:16–21):

“Na mtaje Mariamu katika Kitabu, alipoweka pembeni sehemu ya mashariki.
Akajitenga nao kwa pazia, nasi tukampelekea roho yetu (Jibril), akamtokea kama mwanaume mkamilifu.
Akasema: ‘Hakika mimi najilinda kwa Mwenyezi Mungu dhidi yako, ikiwa unamcha Mungu.’
Akasema: ‘Mimi ni mjumbe wa Mola wako, ili nikupatie mwana safi.’
Akasema: ‘Nitakuwaje na mwana hali mimi sijaguswa na mwanaume yeyote?’
Akasema: ‘Ndio hivyo; Mola wako amesema: Hayo ni mepesi kwangu, ili tumfanye kuwa ni ishara kwa watu na rehema itokayo kwetu.’”
(Maryam 19:16–21)

Lakini unaona kuwa huyu Mjumbe anajitambulisha yeye ni nani. Hakumkaba Maryam hamutia kashkash. Alijitambulisha.

🔹 Hapa tunajifunza wazi kuwa:
Mariamu (Maryam) alibeba mimba bila kuguswa na mwanaume.




Quran inasema ISA alibebwa kwenda Mbinguni. Itaje pia mtu mwingine ambaye hakufa alipaa na pia hakuzaliwa kwa mume na mke

Surah An-Nisā (4:157–158)
وَمَا قَتَلُوهُ وَمَا صَلَبُوهُ وَلَـٰكِن شُبِّهَ لَهُمْ ... بَل رَّفَعَهُ ٱللَّهُ إِلَيْهِ ۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَزِيزًا حَكِيمًا

“Wala hawakumuuwa, wala hawakumsulibisha, bali iliwadhihirikia hivyo tu. Bali Mwenyezi Mungu alimnyanyua kwake...”

🔹 Maana: Isa hakuuliwa wala kusulubiwa — Mwenyezi Mungu alimnyanyua kwake.
Hii inaonyesha kwamba yuko hai, si kwamba alikufa.

Quran inaposema Isa ni alama ya Kiyama maana yake nini? Na kwa nini yeye ashuke na si Muhamad? Kati ya Muhamad na Isa nani Mkubwa? Je kwa nini umfuate mdogo badala ya mkubwa wake? Je isa imetajwa mara ngapi katika Quran? Muhamad mara ngapi? Je kuna maelezo ya kuzaliwa Muhamad ya kina kama ya Isa?

Surah Az-Zukhruf (43:61)
وَإِنَّهُ لَعِلْمٌ لِلسَّاعَةِ فَلَا تَمْتَرُنَّ بِهَا وَاتَّبِعُونِ ۚ هَٰذَا صِرَاطٌ مُّسْتَقِيمٌ
“Na hakika yeye (Isa) ni alama ya Saa (Kiyama), basi msitilie shaka, na nifuateni; huu ndio njia iliyo nyoofu.”

Tafsiri:
Neno “عِلْمٌ لِلسَّاعَةِ” (alama ya Saa) linafasiriwa na wanazuoni wengi (Ibn ‘Abbas, Mujahid, Qatadah, na wengine) kwamba:
“Kurudi kwa Isa bin Mariamu duniani ndiyo mojawapo ya alama za Kiyama.”

Utagundua kuwa Waislamu walijichanganya pakubwa sana kuhusu kuichukua story ya Isa kuiweka kwenye Quran. Inaonesha ukubwa wa Isa kuliko wa Muhamad.
 
Watu wengi hujiuliza: Je, Nabii Issa bin Maryam (Yesu) alikuwa Mkristo?
Swali hili linahitaji kufafanuliwa kwa elimu, mantiki na ushahidi wa kweli kutoka katika Qur-aan na hata maandiko yanayohusishwa na Wakristo.

Ukweli ni kwamba:
Issa bin Maryam (Yesu) hakuwa Mkristo, bali alikuwa Muislamu aliyemwabudu Allah Mmoja pekee na aliwaita watu kwenye Tawhiid.
Kwa sababu:
Ukristo ulianza baada ya kunyanyuliwa kwa Issa عليه السلام.
Issa mwenyewe hakuwahi kusema “Mimi ni Mungu”.
Hakuwahi kusema “Niabuduni”.
Hakuwahi kufundisha Utatu (Trinity).

Maana ya “Muislamu”
“Muislamu” maana yake ni:
Mtu anayejisalimisha kwa Allah kwa Tawhiid na kumtii.
Hivyo Mitume wote walikuwa Waislamu:
Adam
Nuh
Ibrahim
Musa
Issa
Muhammad ﷺ
Wote walikuja na ujumbe mmoja:
“Mwabuduni Allah peke yake.”

Ushahidi Kutoka Qur-aan
1. Issa Aliwaita Watu Wamwabudu Allah
Allah amesema:
إِنَّ اللَّهَ رَبِّي وَرَبُّكُمْ فَاعْبُدُوهُ ۚ هَٰذَا صِرَاطٌ مُسْتَقِيمٌ
“Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na Mola wenu, basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo njia iliyonyooka.”
— Surat Aal Imraan 3:51
Hapa Issa anasema wazi:
Allah ni Mola wake.
Allah ni Mola wa watu wengine.
Watu wamwabudu Allah, si yeye.
Mtu anayesema:
“Muabuduni Allah”
hawezi kuwa Mungu.

2. Issa Hakudai Uungu
Allah amesema:
مَا الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ إِلَّا رَسُولٌ
“Masihi mwana wa Maryam si chochote ila ni Mtume.”
— Surat Al-Maaidah 5:75
Qur-aan imesema wazi:
Issa ni Mtume.
Si Mungu.
Si mwana wa Mungu.

3. Mitume Wote Walikuwa Waislamu
Allah amesema kuhusu Ibrahim:
مَا كَانَ إِبْرَاهِيمُ يَهُودِيًّا وَلَا نَصْرَانِيًّا وَلَٰكِن كَانَ حَنِيفًا مُّسْلِمًا
“Ibrahim hakuwa Myahudi wala Mkristo, bali alikuwa mcha Mungu Muislamu.”
— Surat Aal Imraan 3:67
Kama Ibrahim hakuwa Mkristo, basi hata Issa hakuwa Mkristo, kwa sababu Ukristo haukuwepo kabla yake.

Je, Ukristo Ulianza Lini?
Neno “Mkristo” lilianza baada ya Issa kunyanyuliwa.
Katika Biblia yenyewe imeandikwa:
“Wanafunzi wakaanza kuitwa Wakristo kwanza huko Antiokia.”
— Matendo 11:26
Hii inaonyesha:
Issa hakuwahi kujiita Mkristo.
Wala hakuwaita wafuasi wake Wakristo.
Jina hilo lilikuja baadaye.

Je, Issa Alihubiri Utatu?
Hakuna sehemu Issa aliposema:
Mungu ni watatu.
Mimi ni sehemu ya Utatu.
Niabuduni mimi.
Badala yake alisema:
“Msikie Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja.”
— Marko 12:29
Huu ndio ujumbe wa Tawhiid.

Issa Aliswali Kama Waislamu
Katika Biblia:
Alikuwa akisujudu.
Alifunga.
Aliomba kwa Allah.
Alisema:
“Si mapenzi yangu bali yako yatimizwe.”
Mungu haombi kwa Mungu mwingine.

Je, Issa Ni Mwana wa Mungu?
Allah amesema:
لَقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّهَ هُوَ الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ
“Kwa yakini wamekufuru wale wanaosema Mwenyezi Mungu ndiye Masihi mwana wa Maryam.”
— Surat Al-Maaidah 5:72

Na Issa mwenyewe alisema:
“Ninakwenda kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
— Yohana 20:17
Kama Issa ana “Mungu wangu”, basi yeye si Mungu.
Ujumbe wa Kweli wa Issa
Ujumbe wa Issa ulikuwa:
Muabuduni Allah mmoja.
Acheni shirk.
Fuateni Mitume.
Tubu kwa Allah.
Jiandaeni kwa Akhera.
Na hata alimtabiri kuja kwa Mtume Muhammad ﷺ.
Allah amesema:
وَمُبَشِّرًا بِرَسُولٍ يَأْتِي مِن بَعْدِي اسْمُهُ أَحْمَدُ
“Na mwenye kutoa bishara ya Mtume atakayekuja baada yangu jina lake Ahmad.”
— Surat As-Saff 61:6

Hitimisho
Issa bin Maryam:
Hakuwa Mungu.
Hakuwa mwana wa Mungu.
Hakuwa Mkristo.
Alikuwa Mtume mkubwa wa Allah.
Alikuwa Muislamu mwenye kumwabudu Allah mmoja.
Na dini ya Mitume wote ilikuwa moja:
Tawhiid — kumuabudu Allah peke yake bila kumshirikisha.
Mwisho
Allah amesema:
إِنَّ الدِّينَ عِندَ اللَّهِ الْإِسْلَامُ
“Bila shaka dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu.”
— Surat Aal Imraan 3:19
Kumekucha
 
Nyie Waislamu wenyewe ndo mnatufanya tuwaone nyie hamna akili timamu.

Yesu hakuwa mkristo wala hakuwa muislamu, bali alikuwa myahudi.
Hakuna Mwislamu anayesema Yesu alikuwa Mkristo. Neno "Mkristo" lilianza kutumiwa baadaye huko Antiokia (Matendo 11:26), wakati Yesu alikuwa tayari ameshapanda mbinguni.

Pia ni kweli kihistoria kwamba Yesu alikuwa Myahudi kwa kuzaliwa, alitahiriwa, alifuata Sheria ya Musa na aliishi katika jamii ya Kiyahudi.

Lakini swali ni hili: Je, Yesu aliwahi kusema "Mimi ni Mkristo"? Hakuwahi. Je, aliwahi kufundisha watu wamwabudu yeye? Hilo ndilo eneo ambalo tunatofautiana.

Kwa hiyo unaposema Yesu alikuwa Myahudi, husemi jambo ambalo Waislamu wanalikataa. Hata Qurani inamtaja kuwa ni Masihi kutoka kwa wana wa Israeli. Hoja ya mjadala ni mafundisho yake na nafasi yake, si kama alikuwa Myahudi au la.

Kwa hiyo badala ya kusema waislamu hawana akili timamu, ni bora tujadili hoja kwa ushahidi na maandiko.
 
Kwa kutumia Qurani pekee:

  1. Isa alizaliwa mji gani?
    Qurani haikutaja jina la mji.
  2. Majina ya wafuasi wa Isa ni yapi?
    Qurani haikutaja majina yao, imewaita tu Al-Hawariyyun (wanafunzi/wasaidizi).
  3. Wafuasi wa Isa walikuwa wangapi?
    Qurani haikutaja idadi yao.
Sasa swali langu ni hili:

Kutokutajwa kwa mji, majina au idadi kunathibitishaje kwamba Isa si Yesu?

Qurani inasema Isa ni:

Masihi
Mwana wa Mariamu
Alizaliwa na bikira
Alifanya miujiza kwa idhini ya Mungu
Je, unamjua mtu mwingine katika historia mwenye sifa zote hizo isipokuwa Yesu mwana wa Mariamu?

Kuhusu screenshot ya Biblia ya Kiarabu, huo si ushahidi wa Qurani bali wa Biblia ya Kiarabu. Hoja yako ilikuwa nijibu kwa Qurani, na nimejibu kwa Qurani. Sasa wewe jibu: huyo Isa mwana wa Mariamu ambaye ni Masihi ni nani kama si Yesu?
Wakristo wote duniani hatumtambui Isa ndiyo Yesu kwasababu
1. Jina Isa siyo jina la kiarabu kwasababu hata ukichukua Biblia ya Kiarabu huwezi kukuta jina Isa. Uislamu umekuwa ukijetengenezea majina yao wenyewe ili upate huruma kutoka kwenye ukristo. Angalia majina kama Yesu, Daudi, Samson, Yakobo n.k
2. Isa hajulikani mji aliozaliwa. Nikisema Isa alizaliwa chini ya mtende Tanga, utabisha?
3. Idadi ya wafuasi wa Isa hawajulikani
4. Majina ya wafuasi wa Isa hawajulikani
5. Kigezo cha masihi siyo uhalali wa kusema Isa ni Yesu😃😃😃😃
Isa ni nabii wa waislamu ila kwenye ukristo hajulikani maana Biblia Takatifu imejitosheleza
 
Wakristo wote duniani hatumtambui Isa ndiyo Yesu kwasababu
1. Jina Isa siyo jina la kiarabu kwasababu hata ukichukua Biblia ya Kiarabu huwezi kukuta jina Isa. Uislamu umekuwa ukijetengenezea majina yao wenyewe ili upate huruma kutoka kwenye ukristo. Angalia majina kama Yesu, Daudi, Samson, Yakobo n.k
2. Isa hajulikani mji aliozaliwa. Nikisema Isa alizaliwa chini ya mtende Tanga, utabisha?
3. Idadi ya wafuasi wa Isa hawajulikani
4. Majina ya wafuasi wa Isa hawajulikani
5. Kigezo cha masihi siyo uhalali wa kusema Isa ni Yesu😃😃😃😃
Isa ni nabii wa waislamu ila kwenye ukristo hajulikani maana Biblia Takatifu imejitosheleza


Kijana, hoja zako hazithibitishi kwamba Isa na Yesu ni watu wawili tofauti, bali zinaonyesha kwamba Qurani haikutoa maelezo yote ambayo Biblia imetoa.

Hebu tuangalie mantiki:

Qurani inamtaja Isa kuwa Masihi.
Qurani inamtaja kuwa mwana wa Mariamu.
Qurani inamtaja kuzaliwa na bikira.
Qurani inamtaja kufanya miujiza kwa idhini ya Mungu.
Qurani inamtaja kutumwa kwa wana wa Israeli.

Sasa taja mtu mwingine katika historia mwenye sifa hizo zote isipokuwa Yesu mwana wa Mariamu.

Kuhusu kutotajwa kwa mji wa kuzaliwa, idadi ya wanafunzi au majina yao, hiyo haithibitishi kuwa ni mtu mwingine. Ni sawa na kusema Biblia haijataja tarehe ya kuzaliwa Yesu, sura yake, urefu wake au maandishi yoyote aliyoyaandika kwa mkono wake; je, kwa sababu hiyo Yesu hajulikani?

Pia hoja ya "Wakristo wote duniani hatumtambui Isa" si hoja ya kihistoria wala ya kielimu. Ukweli wa jambo hauamuliwi kwa kura. Muhimu ni ushahidi.

Au wewe unaamini kama ilivyoandikwa kwenye biblia kuwa Bwana Yesu haonekani hata mtu mwenye ukoo safi, bali tunalazimika kumtafautisha Isa a.s. na Yesu. Biblia inasema kwamba:

1. Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi mwana wa Ibrahim. (Mathayo 1:1).

2. Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu. (Mathayo 1:5) Rahabu alikuwa kahaba (Yoshua 2:1).

3. Yuda alimzaa Peresi na Zera kwa Tamari (Mathayo 1:3). Tamari alikuwa kahaba na mzinifu. (Mwanzo 38:13-18).

4. Daudi alimzaa Sulemani kwa yule mke wa URIA (Mathayo 1:6). Beth Sheba mkewe URIA alipata mimba ya zinaa. (2 Samuel 11:2-5).

Hawa mabibi wote wa Yesu Kristo walikuwa makahaba na wazinifu. Lakini sisi hatukubaliani na Biblia bali tunaona kwamba ni taka taka zilizoongezwa katika Biblia. Na kama Wakristo mnang’ang’ania usahihi wa Biblia, basi mjuwe kwamba Biblia inasema:

“Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa Bwana; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa Bwana. (Kumb. la Torati 23:2).

Kwa hiyo bado swali linasimama: Kama Isa mwana wa Mariamu, Masihi aliyezaliwa na bikira na kutumwa kwa wana wa Israeli si Yesu, basi ni nani huyo mwingine katika historia?
 
Kijana, hoja zako hazithibitishi kwamba Isa na Yesu ni watu wawili tofauti, bali zinaonyesha kwamba Qurani haikutoa maelezo yote ambayo Biblia imetoa.

Hebu tuangalie mantiki:

Qurani inamtaja Isa kuwa Masihi.
Qurani inamtaja kuwa mwana wa Mariamu.
Qurani inamtaja kuzaliwa na bikira.
Qurani inamtaja kufanya miujiza kwa idhini ya Mungu.
Qurani inamtaja kutumwa kwa wana wa Israeli.

Sasa taja mtu mwingine katika historia mwenye sifa hizo zote isipokuwa Yesu mwana wa Mariamu.

Kuhusu kutotajwa kwa mji wa kuzaliwa, idadi ya wanafunzi au majina yao, hiyo haithibitishi kuwa ni mtu mwingine. Ni sawa na kusema Biblia haijataja tarehe ya kuzaliwa Yesu, sura yake, urefu wake au maandishi yoyote aliyoyaandika kwa mkono wake; je, kwa sababu hiyo Yesu hajulikani?

Pia hoja ya "Wakristo wote duniani hatumtambui Isa" si hoja ya kihistoria wala ya kielimu. Ukweli wa jambo hauamuliwi kwa kura. Muhimu ni ushahidi.

Au wewe unaamini kama ilivyoandikwa kwenye biblia kuwa Bwana Yesu haonekani hata mtu mwenye ukoo safi, bali tunalazimika kumtafautisha Isa a.s. na Yesu. Biblia inasema kwamba:

1. Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi mwana wa Ibrahim. (Mathayo 1:1).

2. Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu. (Mathayo 1:5) Rahabu alikuwa kahaba (Yoshua 2:1).

3. Yuda alimzaa Peresi na Zera kwa Tamari (Mathayo 1:3). Tamari alikuwa kahaba na mzinifu. (Mwanzo 38:13-18).

4. Daudi alimzaa Sulemani kwa yule mke wa URIA (Mathayo 1:6). Beth Sheba mkewe URIA alipata mimba ya zinaa. (2 Samuel 11:2-5).

Hawa mabibi wote wa Yesu Kristo walikuwa makahaba na wazinifu. Lakini sisi hatukubaliani naBiblia bali tunaona kwamba ni taka taka zilizoongezwa katika Biblia. Na kama Wakristo wanang’ang’ania usahihi wa Biblia, basi wajuwe kwamba Biblia inasema:

“Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa Bwana; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano
wa Bwana. (Kumb. la Torati 23:2).

Kwa hiyo bado swali linasimama: Kama Isa mwana wa Mariamu, Masihi aliyezaliwa na bikira na kutumwa kwa wana wa Israeli si Yesu, basi ni nani huyo mwingine katika historia?
Biblia unaijua ila Quran huijui ndiyo maana umeshindwa kuthibitisha Isa ni Yesu.
Isa na Yesu ni watu wawili tofauti na hawana uhusiano wowote ndiyo maana hata waislamu wenyewe wa Saudia Arabia ukiwauliza watakimbilia kwenye Biblia Takatifu maana Quran ina mapungufu makubwa na haijitoshelezi.
Hakuna sehemu yoyote kwenye Quran imeandika kuhusu Yesu, kurejea Yesu ni kwamba Isa ni wa kubumba ndiyo maana hana maelezo ya kutosha na Quran ina mapungufu makubwa.
Kwa kudhihirisha Isa ni wa kubumba, nitumie screenshot ya Biblia ya Kiarabu yenye jina Isa😃😃😃😃😃
 
Watu wengi hujiuliza: Je, Nabii Issa bin Maryam (Yesu) alikuwa Mkristo?
Swali hili linahitaji kufafanuliwa kwa elimu, mantiki na ushahidi wa kweli kutoka katika Qur-aan na hata maandiko yanayohusishwa na Wakristo.

Ukweli ni kwamba:
Issa bin Maryam (Yesu) hakuwa Mkristo, bali alikuwa Muislamu aliyemwabudu Allah Mmoja pekee na aliwaita watu kwenye Tawhiid.
Kwa sababu:
Ukristo ulianza baada ya kunyanyuliwa kwa Issa عليه السلام.
Issa mwenyewe hakuwahi kusema “Mimi ni Mungu”.
Hakuwahi kusema “Niabuduni”.
Hakuwahi kufundisha Utatu (Trinity).

Maana ya “Muislamu”
“Muislamu” maana yake ni:
Mtu anayejisalimisha kwa Allah kwa Tawhiid na kumtii.
Hivyo Mitume wote walikuwa Waislamu:
Adam
Nuh
Ibrahim
Musa
Issa
Muhammad ﷺ
Wote walikuja na ujumbe mmoja:
“Mwabuduni Allah peke yake.”

Ushahidi Kutoka Qur-aan
1. Issa Aliwaita Watu Wamwabudu Allah
Allah amesema:
إِنَّ اللَّهَ رَبِّي وَرَبُّكُمْ فَاعْبُدُوهُ ۚ هَٰذَا صِرَاطٌ مُسْتَقِيمٌ
“Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na Mola wenu, basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo njia iliyonyooka.”
— Surat Aal Imraan 3:51
Hapa Issa anasema wazi:
Allah ni Mola wake.
Allah ni Mola wa watu wengine.
Watu wamwabudu Allah, si yeye.
Mtu anayesema:
“Muabuduni Allah”
hawezi kuwa Mungu.

2. Issa Hakudai Uungu
Allah amesema:
مَا الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ إِلَّا رَسُولٌ
“Masihi mwana wa Maryam si chochote ila ni Mtume.”
— Surat Al-Maaidah 5:75
Qur-aan imesema wazi:
Issa ni Mtume.
Si Mungu.
Si mwana wa Mungu.

3. Mitume Wote Walikuwa Waislamu
Allah amesema kuhusu Ibrahim:
مَا كَانَ إِبْرَاهِيمُ يَهُودِيًّا وَلَا نَصْرَانِيًّا وَلَٰكِن كَانَ حَنِيفًا مُّسْلِمًا
“Ibrahim hakuwa Myahudi wala Mkristo, bali alikuwa mcha Mungu Muislamu.”
— Surat Aal Imraan 3:67
Kama Ibrahim hakuwa Mkristo, basi hata Issa hakuwa Mkristo, kwa sababu Ukristo haukuwepo kabla yake.

Je, Ukristo Ulianza Lini?
Neno “Mkristo” lilianza baada ya Issa kunyanyuliwa.
Katika Biblia yenyewe imeandikwa:
“Wanafunzi wakaanza kuitwa Wakristo kwanza huko Antiokia.”
— Matendo 11:26
Hii inaonyesha:
Issa hakuwahi kujiita Mkristo.
Wala hakuwaita wafuasi wake Wakristo.
Jina hilo lilikuja baadaye.

Je, Issa Alihubiri Utatu?
Hakuna sehemu Issa aliposema:
Mungu ni watatu.
Mimi ni sehemu ya Utatu.
Niabuduni mimi.
Badala yake alisema:
“Msikie Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja.”
— Marko 12:29
Huu ndio ujumbe wa Tawhiid.

Issa Aliswali Kama Waislamu
Katika Biblia:
Alikuwa akisujudu.
Alifunga.
Aliomba kwa Allah.
Alisema:
“Si mapenzi yangu bali yako yatimizwe.”
Mungu haombi kwa Mungu mwingine.

Je, Issa Ni Mwana wa Mungu?
Allah amesema:
لَقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّهَ هُوَ الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ
“Kwa yakini wamekufuru wale wanaosema Mwenyezi Mungu ndiye Masihi mwana wa Maryam.”
— Surat Al-Maaidah 5:72

Na Issa mwenyewe alisema:
“Ninakwenda kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
— Yohana 20:17
Kama Issa ana “Mungu wangu”, basi yeye si Mungu.
Ujumbe wa Kweli wa Issa
Ujumbe wa Issa ulikuwa:
Muabuduni Allah mmoja.
Acheni shirk.
Fuateni Mitume.
Tubu kwa Allah.
Jiandaeni kwa Akhera.
Na hata alimtabiri kuja kwa Mtume Muhammad ﷺ.
Allah amesema:
وَمُبَشِّرًا بِرَسُولٍ يَأْتِي مِن بَعْدِي اسْمُهُ أَحْمَدُ
“Na mwenye kutoa bishara ya Mtume atakayekuja baada yangu jina lake Ahmad.”
— Surat As-Saff 61:6

Hitimisho
Issa bin Maryam:
Hakuwa Mungu.
Hakuwa mwana wa Mungu.
Hakuwa Mkristo.
Alikuwa Mtume mkubwa wa Allah.
Alikuwa Muislamu mwenye kumwabudu Allah mmoja.
Na dini ya Mitume wote ilikuwa moja:
Tawhiid — kumuabudu Allah peke yake bila kumshirikisha.
Mwisho
Allah amesema:
إِنَّ الدِّينَ عِندَ اللَّهِ الْإِسْلَامُ
“Bila shaka dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu.”
— Surat Aal Imraan 3:19
YESU ni YESU na uyo issa ni issa since they are too different

Note: YESU hakuwai kuwa na dini jina na hatakuja kuwa nayo pia kumbuka kuwa yeye mwenyewe anajitosheleza na ndiye mwanzilishi wa ukristo ambao ni zaidi ya dini ukimjua YESU kisawasawa utaelewa HAYA.
Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa. Biblia Yakobo 1:27

YESU ndiye chanzo Cha dini yaani Ukristo waiyo kuuliza dini yake ni kumdharorisha labda jibu elewa hiyo kauli.

Nakazia
Isa bin Mariam ni jina la kutengenezwa Ili kuwadanganya watu kuwa ata waislamu wanamwamini ingawa ibada ya kweli wameikataa na Kila anayemwamini YESU wanamuita kafiri....

YESU ni jina kutoka kwa Mungu yaani jina tulilopewa kutoka kwa Mungu.
Ona hapa...
Biblia-Wafilipi 2:9-10
Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
Mathayo 1:21
Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.(Mathayo 1:21)
asante
 
Ubatizo:

Hii pia ni ibada kuu na ya msingi katika dini ya Kikristo ambayo hata watoto wachanga nao huusishwa nayo pia! Kwa ujumla wake, ibada hii (ya ubatizo) imeshamiri sana katika Ukristo.

Hata hivyo, pamoja na kuwemo katika orodha ya ibada za Kikristo, lakini kwa mujibu wa maelezo ya Biblia tukufu, asili ya ibada hiyo (ya ubatizo) imetokana na dini ya kipagani (Mithraism). Uthibitisho wa hayo tunaupata katika maelezo ya Biblia yafuatayo:

"Ibada ya (ubatizo) kutosa mwili majini ni mfano wa utakaso au wakujitengeneza upya. Ibada kama hiyo ilijulikana na kutendeka katika dini za kale za kipagani na dini ya Kiyahudi pia (kama ubatizo wa waongofu Mdo 2:10; Waesseni)'.

(Tazama Biblia ya Wakatoliki, Imprimatur M. Mihayo Archbishop of Tabora, February, 1967, kwenye maelezo ya Mathayo 3:6 uk. 879).

Maelezo hayo ya Biblia hapo juu yanathibitisha wazi kwamba ibada hiyo ya ubatizo inatokana na dini za kale za kipagani na kamwe haitokani na dini ya Yehovah. Nasema ibada hiyo (ya ubatizo ya kipagani) katu haitokani na Yehovah, kwa sababu tangu mapema Yehovah alikwishawakataza na kuwaonya wanadamu kutenda ibada yoyote (kama hiyo ya ubatizo) ya watu wa mataifa (yaani wapagani) kama asemavyo (Yehovah) katika maandiko yafuatayo:

"Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako, usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale".
(Kumbukumbu la Torati 18:19)

Mkristo anaweza kutaka kuutetea ubatizo kuwa ndio ondoleo la dhambi. Lakini wakrito wote wanakiri kuwa Bw. Yesu hakuwa na dhambi, je iweje asiye na dhambi kama bw. Yesu abatizwe? Huu kama si uzushi ni kitu gani?
Isa alibatizwa?
 
YESU ni YESU na uyo issa ni issa since they are too different

Note: YESU hakuwai kuwa na dini jina na hatakuja kuwa nayo pia kumbuka kuwa yeye mwenyewe anajitosheleza na ndiye mwanzilishi wa ukristo ambao ni zaidi ya dini ukimjua YESU kisawasawa utaelewa HAYA.
Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa. Biblia Yakobo 1:27

YESU ndiye chanzo Cha dini yaani Ukristo waiyo kuuliza dini yake ni kumdharorisha labda jibu elewa hiyo kauli.

Nakazia
Isa bin Mariam ni jina la kutengenezwa Ili kuwadanganya watu kuwa ata waislamu wanamwamini ingawa ibada ya kweli wameikataa na Kila anayemwamini YESU wanamuita kafiri....

YESU ni jina kutoka kwa Mungu yaani jina tulilopewa kutoka kwa Mungu.
Ona hapa...
Biblia-Wafilipi 2:9-10
Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
Mathayo 1:21
Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.(Mathayo 1:21)
asante

Ahsante kwa maelezo yako. Hata hivyo, hoja kwamba “Yesu” na “Isa” ni watu wawili tofauti haina ushahidi wa kihistoria. Tofauti iliyopo ni ya lugha, si ya mtu.

Jina la Yesu katika Kiebrania lilikuwa “Yeshua”, katika Kigiriki likawa “Iesous”, na katika lugha nyingine likapata matamshi tofauti. Vivyo hivyo, Qurani inamtaja kama Isa bin Maryam. Kwa hiyo tofauti ya jina pekee haithibitishi kuwa ni watu wawili tofauti.

Pia si sahihi kusema kwamba Waislamu wamekataa Isa/Yesu. Uislamu unafundisha kwamba Isa bin Maryam alizaliwa kwa muujiza, alikuwa Masihi, alifanya miujiza kwa idhini ya Mungu, na ni miongoni mwa Mitume wakubwa. Kumkataa Isa ni kutoka katika imani ya Kiislamu.

Kuhusu nani yuko sahihi kati ya Ukristo na Uislamu, hilo ni suala la kuchunguza mafundisho na ushahidi, si suala la jina pekee. Swali muhimu ni: Yesu mwenyewe alifundisha nini kuhusu Mungu, ibada, na wokovu? Hapo ndipo mjadala unapaswa kuelekezwa.

Ninakubaliana kwamba kuwasaidia yatima, wajane na wenye shida ni jambo jema sana. Tofauti yetu ni katika kuelewa nafasi ya Yesu/Isa, si katika umuhimu wa kufanya mema.
 
Yesu siyo Isa.
Asante kwa kujibu
Sisi Waislamu tunaamini kwamba Bwana Yesu a.s. alikuwa Nabii wa Mungu. Na manabii wote ni watukufu na wapendwa wa Mwenyezi Mungu. Wanatoka kutoka koo takatifu.

Kuhusu ukoo wa Bwana Yesu Kristo Masihi Mwana wa Mariamu a.s. Qur'an Tukufu inaeleza kwamba:

A. Masihi bin Mariamu siye ila ni Mtume tu, bila shaka mitume wote wamekwisha fariki kabla yake, na mama yake ni mwanamke mkweli. (Qur'an 5:76).

B. (Ewe Mariam) baba yako hakuwa mtu m’baya wala mama yako hakuwa asherati. (Qur'an 19:29).

Kwa hiyo sawa na mafundisho ya dini ya Kiislamu tunamheshimu Nabii Isa a.s. (Yesu Kristo) na vile vile wazee wake.

Sisi tunashangaa sana wakati tunaposoma Biblia, tunaona Biblia inamfedhehesha Yesu Kristo vibaya sana.

Licha ya kuwa Mtume wa Mungu sawa na Biblia, Bwana Yesu haonekani hata mtu mwenye ukoo safi, bali tunalazimika kumtafautisha Isa a.s. na Yesu. Biblia inasema kwamba:

1. Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi mwana wa Ibrahim. (Mathayo 1:1).

2. Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu. (Mathayo 1:5) Rahabu alikuwa kahaba (Yoshua 2:1).

3. Yuda alimzaa Peresi na Zera kwa Tamari (Mathayo 1:3). Tamari alikuwa kahaba na mzinifu. (Mwanzo 38:13-18).

4. Daudi alimzaa Sulemani kwa yule mke wa URIA (Mathayo 1:6). Beth Sheba mkewe URIA alipata mimba ya zinaa. (2 Samuel 11:2-5).

Hawa mabibi wote wa Yesu Kristo walikuwa makahaba na wazinifu. Lakini sisi hatukubaliani na Biblia bali tunaona kwamba ni taka taka zilizoongezwa katika Biblia. Na kama Wakristo wanang’ang’ania usahihi wa Biblia, basi wajuwe kwamba Biblia inasema:

“Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa Bwana; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa Bwana. (Kumb. la Torati 23:2).

Enyi Wakristo! Kama mnaona kwamba Biblia bado ni sahihi basi mjue kwamba Yesu ni kizazi cha wazinifu, hawezi kuingia katika mkutano wa Mungu. Kama hawezi hata kuingia katika mkutano wa Mungu, ninyi mnamtegemea nani?
 
Ni Kwanini mnalazimisha Isa awe Yesu ?
Kwani Isa hajitosherezi kwenye hicho kitabu Cha Majini ?
 
Ahsante kwa maelezo yako. Hata hivyo, hoja kwamba “Yesu” na “Isa” ni watu wawili tofauti haina ushahidi wa kihistoria. Tofauti iliyopo ni ya lugha, si ya mtu.

Jina la Yesu katika Kiebrania lilikuwa “Yeshua”, katika Kigiriki likawa “Iesous”, na katika lugha nyingine likapata matamshi tofauti. Vivyo hivyo, Qurani inamtaja kama Isa bin Maryam. Kwa hiyo tofauti ya jina pekee haithibitishi kuwa ni watu wawili tofauti.

Pia si sahihi kusema kwamba Waislamu wamekataa Isa/Yesu. Uislamu unafundisha kwamba Isa bin Maryam alizaliwa kwa muujiza, alikuwa Masihi, alifanya miujiza kwa idhini ya Mungu, na ni miongoni mwa Mitume wakubwa. Kumkataa Isa ni kutoka katika imani ya Kiislamu.

Kuhusu nani yuko sahihi kati ya Ukristo na Uislamu, hilo ni suala la kuchunguza mafundisho na ushahidi, si suala la jina pekee. Swali muhimu ni: Yesu mwenyewe alifundisha nini kuhusu Mungu, ibada, na wokovu? Hapo ndipo mjadala unapaswa kuelekezwa.

Ninakubaliana kwamba kuwasaidia yatima, wajane na wenye shida ni jambo jema sana. Tofauti yetu ni katika kuelewa nafasi ya Yesu/Isa, si katika umuhimu wa kufanya mema.
Hayo mengine nitakueleza badae ukinijibu hili. Kwanini waislamu wanawaita waKristo makafiri???
 
Umeandika wayahudi wana dini yao , ni dini gani hiyo ??
Quran imeandika msiwafanye mayahudi kuwa marafiki zenu maana wao wana dini yao.
Kwanini kwenye dini ya uislamu kuna manabii mayahudi?😃😃😃😃
 
Kwanza issa sio Yesu ni watu wawili tofauti,sijui kwanini waislam hulazimisha hilo🙄🙄🙄🙄 issa sio Yesu
Kwasababu Quran haina maelezo ya kutosha kuhusu Isa ili kuifanya Quran kuwa halali hulazimisha Isa kuwa Yesu.
Ukisoma kuhusu habari za Isa kwenye Quran utagundua aliyeandika alikuwa hajui alichokuwa anaandika kwasababu neno Isa siyo jina la Kiarabu. Tafuta Biblia ya Kiarabu kama utakuta jina Isa. Hata ukisoma Quran kwa kiswahili hautakuta neno Yesu
Isa na Yesu ni watu wawili tofauti na hawana uhusiano wwte, maelezo yao yanapishana pakubwa. Isa alizaliwa chini ya mtende.
Waislamu ili kuficha madhaifu ya maelezo ya Isa watakuambia Isa ni Yesu😃😃😃😃 wakati hakuna mahali popote kwenye Quran pameandikwa Yesu
Waislamu wamechakachua majina mengi sana kutoka kwenye Biblia Takatifu kama Daudi, Samsom, Nuhu, Eva n.k
 
Back
Top Bottom