Tofauti kati ya Yesu na Nabii Issa
Hawa watu waliishi karne ipi?
Kwani unataka kusema hata hujui chochote kuhusu karne ipi waliishi?
Jee kujua kama ni sawa au tofauti itatusaidia nini?
Haiwezekani wakawa sawa na wala haisaidii chochote?
Nani ana authority wa kutoa kauli ya mwisho katika kuthibitisha hili?
Kuthibitisha hili ili iweje?
Tungepata mabaki yao labda DNA analysis ingeondoa utata au vipi?

Anyway, ni historia...kama ya Nyerere na muungano wake!
 
Nimekuwa nikisikia mijadala mingi mtaani na hata mitandaoni kuhusu Yesu na Nabii Isa. Wengine wanasema ni mtu mmoja kwa majina tofauti, wengine wanadai kuna tofauti kubwa sana.

Katika Ukristo, Yesu anatajwa kama Mwana wa Mungu, alizaliwa na Bikira Maria, alifanya miujiza mingi, alisulubiwa msalabani kwa ajili ya dhambi za wanadamu, akafa, akafufuka na kupaa mbinguni. Ana nafasi ya kipekee kama Mwokozi wa ulimwengu.

Kwa upande wa Uislamu, Nabii Isa bin Mariam naye alizaliwa kwa muujiza bila baba, pia alifanya miujiza mingi (kama kuponya wagonjwa na kufufua wafu), lakini haaminiki kama Mwana wa Mungu bali Nabii wa Mwenyezi Mungu. Waislamu huamini hakuuliwa msalabani bali alinyakuliwa na Mungu, na atarudi tena kabla ya Siku ya Kiyama.

Swali langu kwa wana Jamii Forums:

Hivi tunaposema Yesu na Nabii Isa ni mtu mmoja, ni sahihi kihistoria na kiimani?

Je, tofauti hizi za kiimani zinaathiri vipi maelewano ya kidini?

Na kwa wale wanaopenda kuchimba zaidi, kuna maandiko yanayofanana kwenye Biblia na Qur’an kuhusu maisha yake?


Naomba tujadili kwa heshima, kueleweshana, siyo mihemko
 
Nimekuwa nikisikia mijadala mingi mtaani na hata mitandaoni kuhusu Yesu na Nabii Isa. Wengine wanasema ni mtu mmoja kwa majina tofauti, wengine wanadai kuna tofauti kubwa sana.

Katika Ukristo, Yesu anatajwa kama Mwana wa Mungu, alizaliwa na Bikira Maria, alifanya miujiza mingi, alisulubiwa msalabani kwa ajili ya dhambi za wanadamu, akafa, akafufuka na kupaa mbinguni. Ana nafasi ya kipekee kama Mwokozi wa ulimwengu.

Kwa upande wa Uislamu, Nabii Isa bin Mariam naye alizaliwa kwa muujiza bila baba, pia alifanya miujiza mingi (kama kuponya wagonjwa na kufufua wafu), lakini haaminiki kama Mwana wa Mungu bali Nabii wa Mwenyezi Mungu. Waislamu huamini hakuuliwa msalabani bali alinyakuliwa na Mungu, na atarudi tena kabla ya Siku ya Kiyama.

Swali langu kwa wana Jamii Forums:

Hivi tunaposema Yesu na Nabii Isa ni mtu mmoja, ni sahihi kihistoria na kiimani?

Je, tofauti hizi za kiimani zinaathiri vipi maelewano ya kidini?

Na kwa wale wanaopenda kuchimba zaidi, kuna maandiko yanayofanana kwenye Biblia na Qur’an kuhusu maisha yake?


Naomba tujadili kwa heshima, kueleweshana, siyo mihemko
Hapana ni Watu wawili tofauti .na Pia Mungu wa Waislam sio yule Mungu wake Yesu Kristu- Ni Miungu miwili tofauti
 
Iko wazi kwamba Qur'an tukufu inapo mzungumzia Issa ina refer kwa Yesu Kristo kulingana na ilivyomsimulia kuanzia kuzaliwa mpaka huko kunyakuliwa.

Tofauti kubwa ni kuwa kwenye Biblia Yesu amezungumzwa kwa namna ya pekee sana toka kwenye kitabu cha mwanzo hadi ufunuo.

Kuhusu kuchengana kwa masimulizi sina uhakika Quran kama inapinga mambo ambayo haijayasema kama swala la Yesu kufa msalabani, au haijayasimulia tu. Kama inapinga basi tatizo linaanzia hapo.

Ukisoma Biblia kwenye injili, Alichosimulia Mathayo sio Extactly the same na kile cha Yohana na hawapingani maana kila mmoja ameandika alichokiona au kukisikia.
 
Tatizo kwenye hili suala ni wakristo kujimilikisha Yesu, yani hapo ndio mzizi wa tatizo kwa maana wao wanataka vile wanavyomuelezea na kumtambua wao basi ndio iwe hivyo hivyo kinyume na hivyo basi huyo sio Yesu. Lakini cha ajabu wakristo na waislamu wanapozungumzia majini huwa wote pamoja wanakusudia kitu kimoja japokuwa ukitizama maelezo ya uislamu majini ni tofauti na wakristo ila hukuti wakristo wakisema majini wanaoelezwa na waislamu ni majini tofauti na majini wenye kuelezwa na wakristo.
 
Tatizo kwenye hili suala ni wakristo kujimilikisha Yesu, yani hapo ndio mzizi wa tatizo kwa maana wao wanataka vile wanavyomuelezea na kumtambua wao basi ndio iwe hivyo hivyo kinyume na hivyo basi huyo sio Yesu. Lakini cha ajabu wakristo na waislamu wanapozungumzia majini huwa wote pamoja wanakusudia kitu kimoja japokuwa ukitizama maelezo ya uislamu majini ni tofauti na wakristo ila hukuti wakristo wakisema majini wanaoelezwa na waislamu ni majini tofauti na majini wenye kuelezwa na wakristo.

Swali Dogo : Issa alisulubiwa?
 
Yesu huyo huyo wengine wanasema ni Mungu na wengine wanasema sio Mungu, kwahiyo hata Yesu hayupo mmoja.
Sio kila swali linajibu la moja kwa moja(illusion)

Kusema Yesu sio MUNGU ni sawa na kusema alikuja kwa mapenzi yake mwenyewe
Pili UMUNGU ni kama U-raisi:- umekamilishwa na Raisi mwenyewe, Makamu Raisi na Waziri Mkuu
Nako kwenye Umungu kuna Mungu Baba, Mungu mwana(Yesu) na Roho mtakatifu
Na utasemaje kama Yesu sio Mungu kama kila kitu kili umbwa na yeye?
 
Nimekuwa nikisikia mijadala mingi mtaani na hata mitandaoni kuhusu Yesu na Nabii Isa. Wengine wanasema ni mtu mmoja kwa majina tofauti, wengine wanadai kuna tofauti kubwa sana.

Katika Ukristo, Yesu anatajwa kama Mwana wa Mungu, alizaliwa na Bikira Maria, alifanya miujiza mingi, alisulubiwa msalabani kwa ajili ya dhambi za wanadamu, akafa, akafufuka na kupaa mbinguni. Ana nafasi ya kipekee kama Mwokozi wa ulimwengu.

Kwa upande wa Uislamu, Nabii Isa bin Mariam naye alizaliwa kwa muujiza bila baba, pia alifanya miujiza mingi (kama kuponya wagonjwa na kufufua wafu), lakini haaminiki kama Mwana wa Mungu bali Nabii wa Mwenyezi Mungu. Waislamu huamini hakuuliwa msalabani bali alinyakuliwa na Mungu, na atarudi tena kabla ya Siku ya Kiyama.

Swali langu kwa wana Jamii Forums:

Hivi tunaposema Yesu na Nabii Isa ni mtu mmoja, ni sahihi kihistoria na kiimani?

Je, tofauti hizi za kiimani zinaathiri vipi maelewano ya kidini?

Na kwa wale wanaopenda kuchimba zaidi, kuna maandiko yanayofanana kwenye Biblia na Qur’an kuhusu maisha yake?


Naomba tujadili kwa heshima, kueleweshana, siyo mihemko
waislamu wanasema Nabii Issa hakuzaliwa kwa njia ya kibaolojia i.e alizaliwa na bikra kwa neno la Mungu,

swali, ikiwa alizaliwa kwa neno na roho ya Mungu, huyu anakuaje sio mtoto wa Mungu?

ukifuatilia kwa makini namna Quran inamsema Nabii Issa, utagundua hawana tofauti yoyote na Biblia, wanaongea kitu kile kile ila kwa lugha tofauti,
 
Tatizo kwenye hili suala ni wakristo kujimilikisha Yesu, yani hapo ndio mzizi wa tatizo kwa maana wao wanataka vile wanavyomuelezea na kumtambua wao basi ndio iwe hivyo hivyo kinyume na hivyo basi huyo sio Yesu. Lakini cha ajabu wakristo na waislamu wanapozungumzia majini huwa wote pamoja wanakusudia kitu kimoja japokuwa ukitizama maelezo ya uislamu majini ni tofauti na wakristo ila hukuti wakristo wakisema majini wanaoelezwa na waislamu ni majini tofauti na majini wenye kuelezwa na wakristo.
Hata kwenye majini Kuna tofauti kubwa wakristo hakuna sehemu wanakwambia Kuna majini wazuri na kwenye uislam **** majini wazuri pia. Sasa kwa Yesu na Isa ipo tofauti uislam unasema hakufa ukristo amekufa na kufufuka. Hapo wanazungumziwa watu wawili tofauti.
 
Sio kila swali linajibu la moja kwa moja(illusion)

Kusema Yesu sio MUNGU ni sawa na kusema alikuja kwa mapenzi yake mwenyewe
Pili UMUNGU ni kama U-raisi:- umekamilishwa na Raisi mwenyewe, Makamu Raisi na Waziri Mkuu
Nako kwenye Umungu kuna Mungu Baba, Mungu mwana(Yesu) na Roho mtakatifu
Na utasemaje kama Yesu sio Mungu kama kila kitu kila umbwa na yeye?
Mimi nimeonyesha tu kwamba kuna Yesu tofauti pia.
 
Issa gani?
Isa wa kwenye Quran

Jibu ni Isa hakusulubiwa
Quran 4:157 "the Jews did not kill or crucify Jesus, but rather, it was made to appear that way to them"

Na mtu aliyesema Isa hakusulubiwa amezaliwa miaka 500 baada ya kifo chake.

Kuna sababu zingine za maeneo waliozaliwa nitofauti , jinsi walivyozaliwa ni tofauti, ukuaji wao ni tofauti, mpaka kazi waliyoitiwa Duniani n.k
 
Swali Dogo : Issa alisulubiwa?
majuzi nilikua nasoma mtandaoni, what does the Quran say about Jesus, it seems kuna school of thought kadhaa zinaamini alisulubiwa (

kwenye quran baadhi wanasema mstari unaopinga kusulubiwa kwa Yesu ni ule unaosema "wao walidhani wamemsulubisha,.......", sasa, some scholars wana-argue kwamba huu mstari hausemi hakusulubiwa, ila unadai wao hawakumsulubishwa kwa kutaka wao (bali waliyatimiza matakwa ya Mungu, which is actually the same na bible, Yesu anaposema "hakuna mtu anaenipokonya uhai wangu,...... nautoa mwenyewe"


binafsi nilihitimisha kwa kusema Quran ipo sahihi pia kwa namna inavyomwongelea Yesu, ila tu namna ya kuyatafsiri yale maandiko inakua ngumu kama ambavyo wakristo wanapata tabu kuyatafsiri maandiko ya ufunuo........mpk wengime wanayapinga!


NB/
as bizarre as it goes, Qur'an inasema Yesu ndiye atauhukumu ulimwengu, na ndiye atakayekuja kumshinda shetani katika siku za mwisho (same as the bible), hapo ndio utajua hizi dini zinaongea kitu kimoja ila wahuni wameamua tuendelee kuishi kwenye migawanyiko na magomvi kwa interest zao!
 
Back
Top Bottom