NAMBA MOJA AJAYE NCHINI
JF-Expert Member
- Oct 29, 2019
- 8,525
- 17,434
Wakuu
Binafsi sielewi ni nani HASA alieamua kuwa kazi ya siasa ndio iwe na malipo na posho kubwa sana kuliko taaluma nyingine yeyote hapa nchini.
Wataalamu wa taaluma mbali mbali wameacha kada zao na kukimbilia siasa kuliko kujikita kwenye taaluma zao na kutuhudumia wananchi!
maprofesa wa vyuo, madaktari, mainjinia na n.k wamekimbilia kwenye siasa HASA ubunge ILI kufata malipo makubwa kuliko kutuhudumia jamii.
Siasa imezalisha rushwa, uchawa, mauaji, ulozi, migogoro hata umafia kutokana na malipo makubwa yaliyopo siasani.
Ipo haja ya kupunguza malipo na posho hizo kuwa za kawaida kama taaluma nyingine nchini na hiyo iwe kikatiba kabisa kuliko sasa mambo yalivyo.
Kuna familia zimeacha kujikita kwenye taaluma zenye tija KWA jamii na kukimbilia siasa tu na vyeo vya serikali na kusababisha u Mungu mtu KATIKA NCHI yetu!piga chini malipo makubwa ya siasa ILI watu wajikite kwenye taaluma na shughuli za kiuchumi kuliko Sasa mambo yalivyo.
Jaribuni kuifikiria Tanzania ninayo zungumzia hapa muone Namna ambavyo mtakuwa mmetatua Matatizo makubwa Sana yaliyopo!
Angalau mishahara na posho za wanasiasa Bungeni ziwe sawa na madaktari, Walimu, wanasheria, maafisa kilimo na mifugo na wengineo tena kawaida Sana posho isizidi 50000/= na mishahara isizidi MILIONI tatu tu kwa wote.
Tuepuke ubadhirifu unaoendelea na Vifo kibao vinavyotokea wakati wa chaguzi kwasababu ya migogoro ya kusaka vyeo vya siasa na kuifanya siasa iwe kazi ya kawaida Sana.
Someni, tafakarini na mfanyie kazi Haya kwa mstakabali wa Tanzania ijayo.
Asanteni kwa kusoma
Binafsi sielewi ni nani HASA alieamua kuwa kazi ya siasa ndio iwe na malipo na posho kubwa sana kuliko taaluma nyingine yeyote hapa nchini.
Wataalamu wa taaluma mbali mbali wameacha kada zao na kukimbilia siasa kuliko kujikita kwenye taaluma zao na kutuhudumia wananchi!
maprofesa wa vyuo, madaktari, mainjinia na n.k wamekimbilia kwenye siasa HASA ubunge ILI kufata malipo makubwa kuliko kutuhudumia jamii.
Siasa imezalisha rushwa, uchawa, mauaji, ulozi, migogoro hata umafia kutokana na malipo makubwa yaliyopo siasani.
Ipo haja ya kupunguza malipo na posho hizo kuwa za kawaida kama taaluma nyingine nchini na hiyo iwe kikatiba kabisa kuliko sasa mambo yalivyo.
Kuna familia zimeacha kujikita kwenye taaluma zenye tija KWA jamii na kukimbilia siasa tu na vyeo vya serikali na kusababisha u Mungu mtu KATIKA NCHI yetu!piga chini malipo makubwa ya siasa ILI watu wajikite kwenye taaluma na shughuli za kiuchumi kuliko Sasa mambo yalivyo.
Jaribuni kuifikiria Tanzania ninayo zungumzia hapa muone Namna ambavyo mtakuwa mmetatua Matatizo makubwa Sana yaliyopo!
Angalau mishahara na posho za wanasiasa Bungeni ziwe sawa na madaktari, Walimu, wanasheria, maafisa kilimo na mifugo na wengineo tena kawaida Sana posho isizidi 50000/= na mishahara isizidi MILIONI tatu tu kwa wote.
Tuepuke ubadhirifu unaoendelea na Vifo kibao vinavyotokea wakati wa chaguzi kwasababu ya migogoro ya kusaka vyeo vya siasa na kuifanya siasa iwe kazi ya kawaida Sana.
Someni, tafakarini na mfanyie kazi Haya kwa mstakabali wa Tanzania ijayo.
Asanteni kwa kusoma