The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
SAS kwa wakati ule na kwa akili yake ya kupindukia ndio vilivyompeleka India. Walikuwapo vijana wengi lakini hawakuweza kufanya aliyoweza kuyafanya SAS.

Kwa Mbowe kama ingekuwa ni 1964, elimu yake ingekuwa sawa, lakini yeye alienda shule miaka ya 80s. Mbowe alikuwa na nafasi nzuri kuliko waTZ wengi kwenda mbali kishule kwani wazazi wake walikuwa na uwezo, lakini hakuweza kusonga mbele. Hivi sasa, 2008, tunategemea viongozi wetu, hasa walio vijana, kuwa na elimu ya kutosha. Nafasi za kusoma hivi sasa zipo sio kama ilivyokuwa 60s.




SAS amesomea Columbia University, an Ivy League University. Ina rank 1-5 kwenye vyuo siku zote US. Hiyo ya Cuba ni news kwangu. Ya Mongela na akina DeNiro hayaondoi ukali wa shule ya SAS. Wengine waliosomea Columbia ni kijana Barack Obama.



Kiwango cha Mbowe cha elimu ni hatari kwa yeye kupewa nchi. Dr. Slaa, Zitto, Halima, Lucy wote wana shule zinazofaa zaidi ya Mbowe. Form Six yake sio ya zamani, ni ya miaka ya 80s, na hii excuse ina-apply tu kwa akina Mwinyi, Kawawa na wengine wa marika yao. Mbowe hakufanya jitihada kujiendeleza kielimu mpaka alipogombea uraisi licha ya kuwa na uwezo wa kifedha.



Hata na mimi pia naiheshimu kazi yake Mbowe hasa kwa mazingira ya kisiasa anayofanyia kazi. Lakini hii haimuepushi kuto kukosolewa.

____________________

Hapana Kubwa Jinga hapa sasa naona ni too much!

Mbona unalazimishia Freeman hafai bana na ndio maana mpaka sasa watu wanadhani una chuki kwasababu hakuna vipimo vya maana unavotoa hapa kuwa eti Freeman hawezi kuwa rais mzuri?!

Freeman hata yeye nchi anaweza kuingoza bana acha hizo!

Contribution yake kwenye upinzani inampa nafasi kubwa kwenye coalition!
 
1.
SAS kwa wakati ule na kwa akili yake ya kupindukia ndio vilivyompeleka India.

Unajua mkuu hoja zingine ni way too low kwa standards za hapa JF, leave alone kutoka kwako, this is just too low!

Just think kwamba alikuwa na akili ya kupindukia bila ya kwenda shule, akapewa pewa alipogombea UN akashindwa, urais wa Tanzania mara tatu hamna kitu, na akili za ke nyingi za kupindukia

2.
Walikuwapo vijana wengi lakini hawakuweza kufanya aliyoweza kuyafanya SAS.

Lakini hao hao vijana wakaja kumpiga bao kwenye urais kule Dodoma mpaka kumfanya alie na kuacha siasa na kukimbilia Abuja! Sasa mwenye akili ya kupindukia hapa ni yupi? Yeye au vijana waliompiga bao!

Mwenyekiti wa Chadema, as a matter of fact politically ana more convincing record hapa bongo kuliko Salim, kwa sababu wengi waliokuwepo enzi za Salim walishazeeka, kwa hiyo mimi ninafikiri huu ni wakati wa vijana kama mwenyekiti wa Chadema, wakati wa Salim umepita sana.
 
SAS amesomea Columbia University, an Ivy League University. Ina rank 1-5 kwenye vyuo siku zote US. Hiyo ya Cuba ni news kwangu. Ya Mongela na akina DeNiro hayaondoi ukali wa shule ya SAS. Wengine waliosomea Columbia ni kijana Barack Obama.


Hiyo shule mkuu hata Fisadi Mkapa, amesoma pia ila kuna tofauti kubwa ya kusoma pale ukiwa kijana mdogo mwanafunzi, na mtu mzima balozi wa Tanzania kwenye umoja wa mataifa(UN), otherwsie hata Mkapa alisoma hapo bro! Na kama ranking hapana haishiki namba 1-5, the matter of fact haijawahi kutokea, mara ya mwisho majuzi ilishika rank namba 11,

1-5 never kabisaaaa!
 
1.
Mbowe hakufanya jitihada kujiendeleza kielimu mpaka alipogombea uraisi licha ya kuwa na uwezo wa kifedha.

Alipomaliza Form Six, aliingia kwenye biashara kama vile Salim alivyoingia kazini, Salim hakufika Form Six kama Mwenyekiti wa Chadema, kwa hiyo hata kwa msingi wa elimu yetu bado Salim hawezi kukaa meza moja na mwenyekiti wa Chadema, na kama nilivyosema huko nyuma sio watu wote Tanzania waliomaliza Form Six, wanamiliki the likes of Billicanas, kwa hiyo ni vyema ukampa heshima na hasa kwa kazi yake kubwa ya kuwaamsha wananchi wa Tanzania na hasa na ufisadi, ambao Salim hajawahi hata kuutamka wazi kwa public na sina uhakika hata kama anajua kuwa upo!

2.
Hata na mimi pia naiheshimu kazi yake Mbowe hasa kwa mazingira ya kisiasa anayofanyia kazi. Lakini hii haimuepushi kuto kukosolewa.

Kumkosoa ni one thing, na kumshusha hadhi kama ambavyo umekuwa ukifanya ni another thing, lakini haibadili ukweli kuwa anaweza kugombea any position in Tanzania, na yeye kama Salim, aliwahi kugombea urais wa Tanzania akashindwa, tena yeye ni nafuu zaidi maana aliweza kuwa mgombea wa chama chake Chadema, Salim hata hiyo nafasi hajawahi kuipata na hatakuja inavyoonekana, au?
 
1.
Sijasema ninampa Mama Migiro, full support lakini ninasema kuwa ninaelekea huko, angekuwa hayuko out of touch basi asingelia kuhusu kampeni chafu za kugombea urais, na pia asingewachukua Warioba na Butiku kuwa wapiga debe wake hizo zote ni dalili za kuwa out of touch na bongo na wananchi wake, kama ni kuomba omba Salim, ndiye aliyekuwa akitumwa na Mwalimu kila wakati kuomba omba nje kwa hiyo kuomba omba haikuanza leo mkuu, Mama Migiro alikuwa waziri wa nje akaitwa UN kuwa Mwafrika wa kwanza Mwanamke kushika nafasi hiyo nzito sana ya dunia, ambayo Salim na CV yake hakuweza kupata, kama ni usomi sidhani kama unaweza kuwalinganisha Salim na Mama Migiro not even close yaaani ni mbali sana, Salim hayuko nyumbani alirudi tu kuvizia urais, alipokosa tu akakimbia yuko Abuja mkuu hayuko nyumbani, lakini najua kuwa atasubiri tena uchaguzi wa rais na kurudi tena avizie!

Mkuu FMES,
Hizi ndio siasa anazozikataa Obama. Siasa za kushushana chini badala ya kuwa wakweli kwa nia ya kujenga nchi. Ni vema ukamsifia yule unayemtaka, say Dr. Migiro, na kuacha kumchafulia jina mtu anayeheshimika na ulimwengu wote.

Kwa wewe kusema kuwa Migiro ni zaidi ya SAS, sio tu kuwa ni kichekesho, bali inaonyesha tunapokuwa na upendeleo huwa na dira zetu hupotea. Migiro hakustahili hata hiyo nafasi maana hakuwahi hata kuwa diplomat let alone kufahamu shughuli za UN. Ndio maana hata waandishi wa habari walimshikia bango sana katibu mkuu wa UN na mama migiro kuwa kwa nini alipewa hiyo nafasi. Yeye ni mwanasheria aliyefaulu vizuri sana lakini hajashika madaraka yeyote zaidi ya ya le ya UDSM, Wizara ya Akina Mama na Watoto na muda kiduchu MOFA.

Ukilinganisha na SAS ambaye sio tu kuwa amesomea mambo ya diplomasia, pia amekuwa ubalozini tokea akiwa na miaka 21 (CUBA). Aliendelea kuwa balozi Egypty, India, China, UN n.k., na wakati huo huo aliteuliwa kwenye jumuiya kibao za kimataifa, zote hizi akiwa na umri chini ya miaka 40.

Salim pia alifanikiwa kuwa mwafrika wa kwanza kugombea ukatibu mkuu wa UN 1981 na kufanikiwa kupata kiasi cha kura kinachohitajika dhidi ya katibu mkuu wa wakati ule Kurt Walheim, lakini veto tu ya wamarekani ndio iliyomkosesha. Mama Migiro hakugomebea nafasi yake, alipewa hiyo nafasi tu kama shukrani na Korea kwa TZ, ambao pia wakati huo huo walituhonga pesa za kujenga daraja Kigoma, ili tu tuwapigie kampeni Africa, maana sisi tulikuwa tunaongoza UN Security Council. Hivi sasa inasemekana mama Migiro anapata upinzani mkubwa kutoka kwa watumishi wengine wa UN ambao wanaona kuwa hakustahili kupewa hicho kiti.

Kwa hiyo usimpake SAS matope, tunachotakiwa tumuombee mama Migiro naye afanikiwe. Kama una sababu za kiukweli na ni vema kuziweka wazi tuzijadili lakini uchochezi na uzushi hautakusaidia wala wasomaji wengine maana mambo mengi ya hawa wakuu yanajulikana.


2.
Mkuu siasa nyingi za dunia zinasema kuwa ukishagombea urais mara tatu ukashindwa, ni vyema kuacha tu ili wengine nao wajaribu, Salim has his time, sasa ni wakati wa wengine, na wapo wengi sana mkuuu!

Kikwete aligombea uraisi mara mbili, SAS amegombea uraisi hadi hivi sasa mara moja tu. Kwa hiyo hata kwa mizengwe hiyo unayotaka kumuwekea, bado ana-qualify. Salim ndie mtu pekee Kikwete anayemuogopa katika kinyang'anyiro cha uraisi, ulizia utaambiwa.
 
Hapana Kubwa Jinga hapa sasa naona ni too much!

Mbona unalazimishia Freeman hafai bana na ndio maana mpaka sasa watu wanadhani una chuki kwasababu hakuna vipimo vya maana unavotoa hapa kuwa eti Freeman hawezi kuwa rais mzuri?!

Freeman hata yeye nchi anaweza kuingoza bana acha hizo!

Contribution yake kwenye upinzani inampa nafasi kubwa kwenye coalition!

Mkuu Mushi,
Sio chuki, kiwango cha elimu cha Mbowe ni cha chnini sana kuweza kumuamini kuendesha nchi. Kisheria ana haki ya kugombea maana nafikiriana tertiary eduction kutokea CBE, lakini mimi siwezi kumpendekeza maana wapo wengi wenye uwezo na elimu kuliko yeye wanaofaa kuiongoza nchi.

Tusisahau hii ni karne ya 21 sio enzi za akina Kawawa.
 
1.

Unajua mkuu hoja zingine ni way too low kwa standards za hapa JF, leave alone kutoka kwako, this is just too low!

Just think kwamba alikuwa na akili ya kupindukia bila ya kwenda shule, akapewa pewa alipogombea UN akashindwa, urais wa Tanzania mara tatu hamna kitu, na akili za ke nyingi za kupindukia

2.

Lakini hao hao vijana wakaja kumpiga bao kwenye urais kule Dodoma mpaka kumfanya alie na kuacha siasa na kukimbilia Abuja! Sasa mwenye akili ya kupindukia hapa ni yupi? Yeye au vijana waliompiga bao!

Mwenyekiti wa Chadema, as a matter of fact politically ana more convincing record hapa bongo kuliko Salim, kwa sababu wengi waliokuwepo enzi za Salim walishazeeka, kwa hiyo mimi ninafikiri huu ni wakati wa vijana kama mwenyekiti wa Chadema, wakati wa Salim umepita sana.

Mkuu FMES, SAS kabla ya kupewa kazi ubalozini, alikuwa mkuu wa gazeti kubwa kuliko lote Zanzibar tokea akiwa na miaka 18 hivi. Niambie ni vijana wangapi leo hii walio na uwezo au vipaji vya aina hii katika umri mdogo kama wake?

SAS ni muona mbali na mchapa kazi wa hali ya juu ndio maana alifanikiwa sana kila alipopewa nafasi. Alipoenda India hakubwetekea madaraka kama walivyofanya vijana wengi wa enzi zake, bali alipandisha shule na shule ikamkubali. Alipopata tena hiyo bahati akiwa NYC, akaongezea degree nyingine. Waulize wabongo wangapi wanaenda kufanya kazi balozini na kuamua kwenda shule badala ya kuanzisha vimiradi vyao?

Mkuu, huwezi kumlinganisha SAS na either Mbowe au Migiro, wanatakiwa kujifunza kutoka kwake maana wao sio saizi yake ingawa Migiro kidogo anakaribia. Ila kama unataka kuendelea kumpaka matope, yale waliyotumia mwaka 2005, endlea tu kumpaka, lakini leo hii akiamua kuingia kwenye kinyang'anyiro cha uraisi, tutakuwepo wengi wa kumtetea maana wakati umefika wa kuwa na raisi anayetufaa, sio hawa wanaopigiwa debe halafu wanauza nchi. Kila mtu ajiuze kulingana na sifa na uwezo wake aliokwishaonyesha na sio kumnyima mtu nafasi kwa kumpaka matope.


_______________________
 
rais awe na meno,kama nyerere ya kumfunga mtu yoyote atayechezea pesa za umma....hakuna kuleana ndani ya serikali.
 
mhhhh

hao waliokuwa na elimu zote wametufikisha wapi?


GT,
Ni kweli wasomi wetu wengi wametuangusha sana, lakini ni kwa vile tumewapa wale wasomi wasiofaa. Wapo wachache ambao wanafaa, kama Dr. Idrisa wa TANESCO, ni mfano mzuri wa wasomi wanaohitajika kuokoa nchi. Kinachokosekana zaidi ni kinara muadilifu.

Lakini hii haina maana tuchague mtu ambae shule haitoshi kwa vile wenye shule wametuangusha. Wa aina hii wakiamua kula, wanaingiza na udikiteta kabisa kama Amini.

____________
 
Hiyo shule mkuu hata Fisadi Mkapa, amesoma pia ila kuna tofauti kubwa ya kusoma pale ukiwa kijana mdogo mwanafunzi, na mtu mzima balozi wa Tanzania kwenye umoja wa mataifa(UN), otherwsie hata Mkapa alisoma hapo bro! Na kama ranking hapana haishiki namba 1-5, the matter of fact haijawahi kutokea, mara ya mwisho majuzi ilishika rank namba 11,

1-5 never kabisaaaa!

Mkuu FMES,

Naomba tusimshushie SAS hadhi yake kwa kumpaka matope. Sasa amesoma BA na Masters yake akiwa na miaka ya 23 to early 30s. Huu ni umri wa kawaida wa wanafunzi hata hivi sasa. Iikiwa chuo chake ni cha 11, kati ya zaidi ya 15,000, hiyo ina maana ni chuo bora. Google Ivy League uone ni vyuo gani viko huko ni kuna ugumu kiasi gani kujiunga. Achilia mbali ile ya Sumaye ambayo ni maalum kwa wazee kama yeye.

Salim A.S is probably the best leader TZ had ever had. Watu wanatucheka tunapompiga madongo.
 
1.
Alipomaliza Form Six, aliingia kwenye biashara kama vile Salim alivyoingia kazini, Salim hakufika Form Six kama Mwenyekiti wa Chadema, kwa hiyo hata kwa msingi wa elimu yetu bado Salim hawezi kukaa meza moja na mwenyekiti wa Chadema, na kama nilivyosema huko nyuma sio watu wote Tanzania waliomaliza Form Six, wanamiliki the likes of Billicanas, kwa hiyo ni vyema ukampa heshima na hasa kwa kazi yake kubwa ya kuwaamsha wananchi wa Tanzania na hasa na ufisadi, ambao Salim hajawahi hata kuutamka wazi kwa public na sina uhakika hata kama anajua kuwa upo!

Mkuu FMES,.
Mbowe anastahili heshima kubwa kwa kusaidia kudumisha mageuzi. Lakini kumiliki night club ni tofauti na kuongoza nchi, hasa kwenye karne hii ya kisomo. Ndio maana mimi siwezi kumpendekeza Mbowe. Wanaoridhika naye wanaweza wakampigia debe.

2.
Kumkosoa ni one thing, na kumshusha hadhi kama ambavyo umekuwa ukifanya ni another thing, lakini haibadili ukweli kuwa anaweza kugombea any position in Tanzania, na yeye kama Salim, aliwahi kugombea urais wa Tanzania akashindwa, tena yeye ni nafuu zaidi maana aliweza kuwa mgombea wa chama chake Chadema, Salim hata hiyo nafasi hajawahi kuipata na hatakuja inavyoonekana, au?

Mbowe kupata uteuzi CHADEMA ni rahisi. Mzee Mtei ni baba mkwe wake na kwa udogo wa CHADEMA kiuongozi, vyeo vinaweza kupewa wahusika kama kampuni binafsi. Wazee Ndesamburo na Mtei tunaweza kuwaita kama wamiliki wa hiyo kampuni hadi leo. Kwa hiyo ukitaka kufananisha uteuzi wa mwaka 2005 CHADEMA na wa CCM, inakuwa ni kichekesho kikubwa.
 
I think this is the best analysis so far!

Ninaelekea kutaka kujua CV yako, wakati haujafika bado ninaendelea kukusoma kupitia threads zako na jinsi unavyo-comment.

I am still doubtful with your credibility!

Nimemaliza na sitarudi tena hapa.
 
1
. Hizi ndio siasa anazozikataa Obama.

Obama has nopthing to do na siasa za urais wa bongo, na besides hata yeye huko naye anachafua wenziwe kwa mfano aliposmea kuwa "Bearings" za Makeni zinaanza kuharibika, na jana Liberman amesema amezi-check zinaonekana hazina kasoro, kwa hiyo mkuu siasa chafu hata huko majuu zipo sio bongo tu!

2.
Kwa wewe kusema kuwa Migiro ni zaidi ya SAS, sio tu kuwa ni kichekesho, bali inaonyesha tunapokuwa na upendeleo huwa na dira zetu hupotea.

Mama Migiro, hakusoma akiwa mtu mzima yaani balozi, mama Migiro ana historia pale Mlimani, wewe you know better on this sasa nashangaa hata kujaribu ku-argue ont this elimu ya Mama Migiro haiwezi kulinganishwa na ya Salim ya utu uzima bro tena akiwa ofisini, watu vichwa husoma kuaniza wakiwa watoto, sio watu wazima tena ofisini, ndio maana yangu hiyo mkuu!

3.
Migiro hakustahili hata hiyo nafasi maana hakuwahi hata kuwa diplomat let alone kufahamu shughuli za UN. Ndio maana hata waandishi wa habari walimshikia bango sana katibu mkuu wa UN na mama migiro kuwa kwa nini alipewa hiyo nafasi. Yeye ni mwanasheria aliyefaulu vizuri sana lakini hajashika madaraka yeyote zaidi ya ya le ya UDSM, Wizara ya Akina Mama na Watoto na muda kiduchu MOFA.

Mama Migiro, sasa hivi ni naibu katibu wa UN, Salim hajawahi kushika hiyo nafasi, that is what counts usije ukachekesha mbele ya watu walioenda shule, kinachojali ni nani amewahi kushika madaraka makubwa zaidi ya dunia kati yao, halafu unaonekana eti unayajua sana mambo ya ndani ya UN huku ukiwa bongo, Duh hiyo kali sana!

3.
Ukilinganisha na SAS ambaye sio tu kuwa amesomea mambo ya diplomasia, pia amekuwa ubalozini tokea akiwa na miaka 21 (CUBA). Aliendelea kuwa balozi Egypty, India, China, UN n.k., na wakati huo huo aliteuliwa kwenye jumuiya kibao za kimataifa, zote hizi akiwa na umri chini ya miaka 40.

Salim alipelekwa ubalozini akiwa na miaka 22 na hana elimu kabisaa hata ya Form Six, lakini Mama Migiro ameenda huko huko akiwa Doctor tayari, hiyo ni maoja ya tofauti zao!

4.
Salim pia alifanikiwa kuwa mwafrika wa kwanza kugombea ukatibu mkuu wa UN 1981 na kufanikiwa kupata kiasi cha kura kinachohitajika dhidi ya katibu mkuu wa wakati ule Kurt Walheim, lakini veto tu ya wamarekani ndio iliyomkosesha. Mama Migiro hakugomebea nafasi yake, alipewa hiyo nafasi tu kama shukrani na Korea kwa TZ, ambao pia wakati huo huo walituhonga pesa za kujenga daraja Kigoma, ili tu tuwapigie kampeni Africa, maana sisi tulikuwa tunaongoza UN Security Council. Hivi sasa inasemekana mama Migiro anapata upinzani mkubwa kutoka kwa watumishi wengine wa UN ambao wanaona kuwa hakustahili kupewa hicho kiti.

Alimshinda kura huyo M-Austria baada ya kugundulika kuwa ni former NAZI, lakini Salim hakushinda ukatibu, Ghali wa Egypt ndiye Muafrika wa kwanza kushinda ukatibu wa UN, sio Salim, Korea kwa nini ilishindwa kumpa nafasi Salim, lakini ikampa Mama Migiro? Hayo yako ni maneno ya kawaida bongo hasa kwa wapenzi wa Yanga na Simba, kuwa isingekluwa kipa wao tungewafunga wale as if kazi ya kipa ni kulala golini!

5.
Kwa hiyo usimpake SAS matope, tunachotakiwa tumuombee mama Migiro naye afanikiwe. Kama una sababu za kiukweli na ni vema kuziweka wazi tuzijadili lakini uchochezi na uzushi hautakusaidia wala wasomaji wengine maana mambo mengi ya hawa wakuu yanajulikana.

Sina sababu ya kumpaka Salim, aliyelia machozi ndani na mkewe wiki nzima baada ya kupigwa kipigo kwenye ule uchaguzi wa rais Dodoma, na kuamua kuacha kabisa siasa, na ninaheshimu uamuzi wake kuwa hawezi siasa za bongo, sasa abaki tu huko nje maana siasa za bongo ni kwa wanaume wa shoka mkuu!

6.
Kikwete aligombea uraisi mara mbili, SAS amegombea uraisi hadi hivi sasa mara moja tu. Kwa hiyo hata kwa mizengwe hiyo unayotaka kumuwekea, bado ana-qualify. Salim ndie mtu pekee Kikwete anayemuogopa katika kinyang'anyiro cha uraisi, ulizia utaambiwa.

Eti did I get it right? Umesema kuwa Kikwete anamuogopa Salim? You must be kidding me bro! Salim hakatazwi kugombea tena aje tu kama anataka, ila one thing ni hawezi kupewa urais bure kama ule ubalozi, kama Kikwete anamuogopa aje basi mkuu kugombea urais next time, hiyo ni haki yake hakatazwi!

Anyways, ninaona niishie hapa mkuu, maana naona una mpango wa kujaza hii forum na none hojas, naona nikutakie ugombeaji mwema na upigaji debe pia wa Salim, great debate, ingawa bado umeshindwa kusema ukweli kuhusu kumpendekeza Mahiga kuwa PM, na nashangaa umelkikwepa kabisa hilo, next time hakikisha unaandika ukweli mkuu, wengine huwa hatupendi hadithi na huwa tuna kumbu kumbu ya kila tunachoandika hapa,

Tukutane tena mkuu next topic!
 
SAS kabla ya kupewa kazi ubalozini, alikuwa mkuu wa gazeti kubwa kuliko lote Zanzibar tokea akiwa na miaka 18 hivi.

Mkuu vipi ukiiweka elimu yake mpaka kufikia miaka 18? Gazeti mbona hata Muhogo mzchungu aliwakuwa akiandika, lakini sio vijana waliokuwa na elimu ya Form Six kama Mwenyekiti wa Chadema, wakiwa na huo umri,

Hebu kuwa mkweli weka hapa elimu ya Salim mpaka miaka 18!
 
Mkuu Ben,
Nafikiri ni muhimu kuelewa ukubwa wa chochote atakachosema SAS ulimwenguni. Watu wote wataanza kuingalia TZ kwa jicho la udadisi au hata kuathiri imani ya TZ, kisiasa na kibiashara. Kwa wanasiasa wanaoipinga serikali ya JK, wangependa kuona hilo, lakini kwa wale ambao bado wana matumaini na CCM kuwa bado inao uwezo wa kujisafisha, kama SAS, sio rahisi kwake kutoa tamko ambalo litaiumiza nchi na serikali ya JK.

SAS ni mtu muhimu duniani, na wengi wanadhani kwa JK kumshinda SAS ina maana ni bora sana. Ndio maana hawakuacha kumtaka akamate AU mara tu baada ya kuchaguliwa 2005, ingawa alikataa. Tunaowajua tunabaki kusikitikia tu waTZ kwa kufuata siasa za maangamizi na kumkataa mtu ambaye nchi nyingine wasingefikiria mara mbili mbili kumuweka kinarani.


_________________________

Asante mkuu,ila....

Sasa mkuu mbona hakutumia umaarufu wake kurekebisha mambo hapo serikalini?
Basi kama dunia inajali atakachosema,kwanini asikemee nchi zinazotoa makampuni yanayosaini mikataba haramu ya kunyonya watanzania?

Kama ana mtazamo chanya juu ya uchumi wa Tanzania,kwa nini basi sakata la Rada lilipopamba moto huko Uk asiongee chochote kitakachofanya dunia ione kweli Tanzania pamoja na umaskini wake bado serikali ya uingereza inajihusisha kuhujumu uchumi wake?

Pia,kwanini basi asingeibuka na kukemea ufisadi?Hata kama nchi hisani zingetishia kutoa misaada,huoni mkuu utakua ndio mwanzo wa serikali yetu kuwa adilifu kitu ambacho kitatupa faida in the long run?

Au kwa wewe kusema kwamba SAS asingetaka kutamka jambo ambalo lingeumiza Tanzania,kwa maoni yako unaona kwamba alitusaidia sisi watanzania na vizazi vijavyo au ni lipi unalotaka kutuambia mkuu?
 
Dr. Slaa anafaa, lakini ni kwa ticket ya chama/vyama vipi?




__________________________

Nimeshaweka wazi kuwa atafute wazalendo wengine ambao wameonyesha kuupinga ufisadi hadharani then waunde coalition ya maana!

Vyama visiangaliwe hapa!

UTU NA CHARACTER! vipewe kipaumbele!

Cha muhimu na hao watu wawe na uhuru wa kumu endorse yule wanayefikiri atalifaa taifa kutupitisha kwenye wakati huu mgumu kupindukia!

Its a defining moment throughout the world so is our country!

Nimeshaweka baadhi ya majina kwenye previous posting! Kadri muda unavyokwenda, tunazidi kuwagundua wale wazalendo!
 
Nimeshaweka wazi kuwa atafute wazalendo wengine ambao wameonyesha kuupinga ufisadi hadharani then waunde coalition ya maana!

Vyama visiangaliwe hapa!

UTU NA CHARACTER! vipewe kipaumbele!

Cha muhimu na hao watu wawe na uhuru wa kumu endorse yule wanayefikiri atalifaa taifa kutupitisha kwenye wakati huu mgumu kupindukia!

Its a defining moment throughout the world so is our country!

Nimeshaweka baadhi ya majina kwenye previous posting! Kadri muda unavyokwenda, tunazidi kuwagundua wale wazalendo!


mkuu wangu umeongea point.Cha mihimu ni kuangalia wazalendo wa kweli na kuunda coalition.Full stop!
 
Nadhani inabidi tuunde bodi, nchi iongozwe na bodi labda kutakuwa na tofauti.

Kusema kwelie niliamini JK atakuwa tie braker lakini what happened ni kwamba amekuwa the worse nightmare tangu uhuru 1961. Amekuwa kama kisiki kisochosikia vishindo vya mpita njia.

Labda upinzani wafanye muungano ambao utachagua wawili wenye enough skills, kisha watumiwe hao wawili kuwapa pressure CCM. Hata CCM wakishinda kwa 51% will make alot of difference.
 
Back
Top Bottom