Mimi sipingani nahilo, ila Je, Elimu imeshawafikia wapiga kura wengi walioko vijijini??? kwetu sisi tunaojua ku-internet tunafahamu maovu mengi sana yanayofanywa na Chama Cha Mfisadi mpaka ukaona hivi:-
SLAA/SALIM NDIO TICKET YA KUWAKOMBOA WATANZANIA WOTE!
Kumbuka Kwamba, wengi wetu humu, siyo wapiga kura japo tumejiandikisha na kadi tunazo. Sidhani kama siku yakwenda kupiga kura ukawa na dili eti ukaiacha ukaenda kujipanga mstari juani kisa unasubiri kupiga kura! natena tumejifunza "time is money"
Msimamo wangu mimi kama SAVIMBI, Dr. Slaa abakie BUNGENI na DR. SALIM muda wake ulishapita wala asitupotezee muda kumjadili!..hii ni sawa na kuanza kujadili eti Mzee Ruksa agombee uraisi tena ina maana wagombea wengine hamtuoni ama hatuna sifa??
Nimekaa Kimya lakini nalazimika kusema "Ninakosa imani kabisa na hawa watu wanaoendelea kushawishi eti Dr. Slaa aachie Ubunge, agombee Urais 2010.....nahisi kama vile ni miongoni mwa wale jamaa wa Green Guard, walipelekwa China, Cuba na Urusi ile ya wakati ule wakajifunza juu ya kuua vyama vya kisiasa, maana wale hutumia muda wao mwingi kujifanya ni wanachama hai na wenye ushawishi mkubwa kwa chama husika, watu wengi humsikiliza na kumwamini na kukubaliana na maneno yake kumbe anawatumbukiza kwenye moto!
1: Hapa kitu kipo wazi 2010 Dr. Slaa hawezi kupata 50% ya kura zote za Urais zitakazo pigwa,sababu mpaka sasa hakuna maandalizi yaliyokwishaanza kumwandaa Dr. Slaa for President 2010!!!!
2: CCM shabaha yao kubwa nikumwondoa Dr. Slaa Bungeni maana huko ndiko anakowamaliza na pia kupitia yeye Chadema ndiyo inaanza kufahamika Tanzania Bara, eti tena mtu unataka kumtoa Bungeni!
Sasa labda...ninyi Wenyechama mtupe maoni yenu mnaona je kuhusiana na hilo!
3: Maoni ni haki ya kila mtu, kupendekeza hivyo siyo vibaya, lakini kama unalengo na nia njema Mwacheni Slaa Bungeni, Chama kijengeke na mtakuwa mmejiwekea Nguvu ya Ushindani 2015 kuelekea White House.
4: Jamani, narudia tena japo nilishaeleza; Karatu hakuna mafuta wala mgodi, lakini ni Jimbo ambalo CCM wanalitaka kwa udi na uvumba, iwe hata kwa kupitia mgombea toka Chama Chochote kile Cha Upinzani, ilikuhakikisha Dr. Slaa anapoteza Ubunge, kwani kuwepo kwake Bungeni imekuwa nikikwazo kikubwa kwa Utawala wa CCM,sababu anafichua uchafu wao bila woga: Ndiyo maana mimi siungi mkono Dr. Slaa kugombea Urais 2010, acha afie Bungeni!!