1.
Umri haujawahi kuwa important ishu kwenye uchaguzi wa rais wetu kwa hii mkuu ni none ishu au skill, na sio muhimu sana kama sio kabisaa.
2.
Unajua kurudia rudia neno moja bila ushahidi ni kupoteza muda wa wasomaji, CCM haiwezi kumuogopa mgombea urais anayeomba kugombea kupitia chama chake, kama sifa tunazozitaka sasa hivi ni kiongozi anayeweza kusimamia ufisadi na Salim hana record yoyote ya hata kukemea ufisadi, sasa huo u-serious wake uko wapi hasa?
Halafu hii habari kuwa Salim hapendi majungu, inatokea wapi? Ni lini Salim aliwahi kukemea majungu, au upendeleo ndani ya taifa letu?
3.
Unajua imefika wakati mkuu ukubali tu kuwa unampenda sana huyu jamaa, lakini huna hoja zaidi za kumtetea, kwa sababu hii sina hata sababu ya kuijibu!
4.
Salim aligombea urais, na wagombea wengine, ili ashinde ilibidi awashinde wagombea wengine, lakini akashindwa na kulia sana na kuapa kuwa hatarudia tena siasa za bongo, sasa hapa anyewaogopa wenziwe ni nani hasa? Siasa ni siasa ni mchezo mchafu na unachezwa na watu wachafu wachache, kwa bahati mbaya huwa Tanzania hatutoi urais tu bure bure,
amegombea ameshindwa urais, amekubali yaishe sasa mmetokea mnaojua better kuliko anavyojijua mwenyewe, kwa sababu kwangu mimi ni kwamba Salim amejiangalia vizuri na kukubali kuwa hana uwezo wa kushinda urais wa Tanzania, sasa sielewi hizi filimbi ni za nini hasa!