The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Mkuu ES...hakuna vigezo wazi vya kumkataa SAS....zaid ya Rangi na Asilia yake...na Ndicho alichokumbana nacho JK kule Butiama kuhusu MSETO ZNZ. Pamoja na NIA Njema ya JK, wengine hawapo tayari kuona mazuri yanafanyika kwajili ya nchi.

Tuna kazi ktk kuyafikia maendeleo ya Kweli TZ...ila mbegu tunazozipanda...zikiota vema tutakula matunda yake

Heshima mkuu,

Kwanza Salim naikubali CV yake na ninamheshimu! Pamoja na uwezo wake wa kuiongoza organisation kubwa OAU,ameshindwa kabisa kusimama kidete kuwakemea viongozi wa hapa nyumbani juu ya uozo wao.

Ananifanya niwe na mashaka nae kama kweli anajua au anaona uchungu wa hali halisi ya mtanzania.

Kwa sasa hivi tunahitaji kiongozi mwenye uchungu na hili taifa na ambae anajua watanzania tunataka nini.Ukiniambia mtu kama Slaaa,mimi namkubali zaidi kulko Salim kwani angalao ameonyesha uwezo wa kulionoza hili taifa kwani anajua matatizo mengi tulio nayo,hata matatizo ya kimfumo.Angalo ameonyesha uwezo wa kuwakaripia viongozi wetu.

Anaonekana ni mtu wa hatua tofauti na Salim ambae ataongoza kukwepa lawama,maanake hadi sasa hivi hajaonyesha kama ataweza kubadili mfumo wetu. Afadhali Slaa ataweza kutuongoza na kukabiliana na challenge zsa kiuchumi za watani wetu wa jadi.

So far,SAlim huwa sijui n nini mtazamo wake wa kiuchumi,sasa hivi tunataka kiongozi ambae atatuletea mabadiliko ya kiuchumi na sio diplomasia kusolve matatizo ya comoro au kwingineko
 
1.
Huyu nafikiri hafai ndio maana wanaokuheshimu wameamua kukaa kimya ili wasilete zogo. Lakini hebu fikiria haya;
Shule yake ni mbovu
Uongozi wake Chamani haujaridhisha wengi(ukabila kwenye uteuzi wa wabunge, matumizi ya pesa n.k.)
Zaidi ya Bilicanas, CV yake haina kingine cha kumfanya awe kiongozi bora let alone kuongoza nchi.

Mkuu KJ,

Heshima mbele, mimi ni CCM damu na so far sijasema nani nayemuona anafaa, ingawa ninaelekea kulalia sana kwa Mama Migiro, lakini baadaye nitasema nani ninayemuona anafaa, lakini hii analysis yako kwa mwenyekiti wa Chadema, sio fair kabisa na ina-amount to matusi ya nguoni, badala ya maoni binafsi kama mwananchi,

1. Shule au elimu ya Mwenyekiti wa Chadema ya form six, pamoja na experience yake nzito ya biashara, na the fact kwamba sasa yuko shule kwenye degree level, haiwezi kuwa mbovu kama ulivyosema that is below the belt bro!

2. Uongozi wake chamani hauridhishi wengi? Hivi ni wakati gani Chadema imewahi kuwika katika taifa letu toka ianzishwe na Mtei in the 90s? Unasema hauridhishi wengi kina nani hao? Zitto na Slaaa ni matunda ya uongozi wa Chadema under nani? Unafikiri ni kwa nini Slaa na Zitto hawakugombea ubunge kupitia CUF au TLP? Unasema kugombea kwao Chadema ilikuwa ni by accident na sio uongozi imara wa mwenyekiti wa sasa wa Chadema?

3. Ukabila? Zitto ni kabila gani? Wangwe ni kabila gani? Slaaa ni kabila gani? Mnyika ni kabila gani? Tundu Lissu ni kabila gani? Kitila ni kabila gani? Hawa wote ni Wachagga? Besides hawa naomba uwe mkweli wa Mungu kuna wengine wanaojulikana kwenye taifa as Chadema? Sana sana ni Ndesamburo tu!

4. Unasema zaidi ya Billicanas, hivi mkuu unajua maana ya kuwa mmiliki wa Bilicanas bongo? Mbona unaiandika kimzaha mzaha tu as if ni soko la samaki mkuu? Huyu si alishawahi kuwa mbunge wa kuchaguliwa na wananchi, je Salim aliwahi kuchaguliwa kuwa mbunge wa wapi? Hivi mwenyekiti wa chadema angepelekwa na Mwalimu ubalozini nje akiwa na miaka 22 je leo asingekuwa na elimu suspect kama ya Salim? Hivi ni shule gani ya wazungu huko majuu unayoijua inayoweza kumnyima Degreee balozi wa any nation katika UN akiomba kusoma hata online?

Tunapowachambua viongozi wetu tuwe wakweli kuliko kujali kujaribu ku-balance mijadala hapa JF, kwa sababu mijadala mingi inashambulia CCM, basi dawa ni kushambulia Chadema hata kama hakuna hoja wala ishu that is low, mkuu binafsi katika sababu zako zote ulizoweka hapa against mwenyekiti wa Chadema na urais, siiioni hata moja ya muhimu, na ninasema wazi kuwa he does not deserve this kind of analysis.

Ahsante Mkuu!
 
hakuna vigezo wazi vya kumkataa SAS....zaid ya Rangi na Asilia yake

Mkuu chuma,

Heshima yako kaka baada ya kupotea sana, lakini si nimesikia hapa JF kuwa sauti ya umma kama iliyomkataa Salim, huwa ni ya Mungu! au?
 
Mkuu Heshima mbele, Salim amepitwa na wakati Mwalimu amejaribu kila njia mwaka 1985 kumpitisha huko ndani ya CCM akashindwa, Mwalimu akajaribu tena mwaka 1995 kumpitisha huko CCM akashindwa tena, mwaka 2005 akajaribu mwenyewe huko CCM tena akashindwa vibaya sana, na this time akakubali yaishe kuwa hataki tena,

Kweli CV yake ni nzito sana na kazi za nje ya taifa letu, amejaribu huko UN ambako ndiko hasa CV yake inakodai na ku-fit sana, lakini nako pia wakamtupa chini, hata unaibu nao hawakumpa, unless kuna something unakijua kuhusu Salim na urais ambacho hata yeye binafsi hakijui, lakini otherwise the record is very clear kuwa wananchi wa Tanzania wamemkataa kabisa kuwa hafai na vigezo vimetolewa wazi!

nakazia tu je kama kwenye chama haaminiwi na hapitishwi je ataweza vipi kuwa rais?
na hili swala la vijisenti halioni? mbona yupo kimya? hiyo elimu yake tuliyoorodheshewa kwenye CV yake anaitumia vp?...HAFAI
 
Kwani mimi sifai au nawafaa??
Mwenye sifa zangu azimwage hapa ili wanabodi wanichambue

With that name "Msanii", hutufai kabisa, utatuletea USANII.

Yeah, I am judging the book by its cover.

CV yako imeishia hapo.
 
Nakubaliana na wewe mkuu kuwa, ukilinganisha na Mbowe au Zitto, huyu bwana anafaa zaidi. Lakini ukilinganisha na Salim A. Salim, tofauti zao zinakuwa ni kubwa mno. Kwangu mimi SAS anafaa zaidi. Sababu nilizimwaga hapo awali.



________..................________________

"Kwenye hilight" umeshindwa ku consider hii quote hapo chini ambayo ndio wakati wa kunijibu uliitumia!

Wenzetu wana usemi kuwa..We gonna judge you based on your character and nothing else.. Wanakusilkiliza kwanza kwamba utawafanyia nini na si assumption tulizozizoea za
kutajana majina based na nafasi za kifisadi walizokuwa nazo before!
Ni lazima tuaminiane sisi wenyewe kwa wenyewe...Kuondokana na fikra kuwa viongozi wanazaliwa viongozi!
Kwamba no matter what they do or say wao bado watakuwa viongozi tu!
Hii ni risk ambayo watanzania tuna kila haki ya kuichukua!

Its time to now think outside the box!
 
Kwa vile hajakamata madaraka makubwa yoyote zaidi ya kanisani, angalau ingekuwa vema akapewa uenyekiti wa CHADEMA (kama ilivyo UK) ili apate nafasi ya kuipandisha CHADEMA chati, kuondoa madukudu ndani yake, kuongeza wanachama, kuweka dira zinazoeleweka za kila suala n.k., n.k.

Yale yale tuliyoyazoea..Think outside the box ma man! Watu hawazaliwi na sifaza uongozi...Huwa wanazipata kutokana na wananchokifanya mbele za watu wao! Kuwa wako upande wao!

Na si mtu ama group la watu flani flani kukaa chini somewhere na kupiga ramli ama kujadili ni nani apokezwe kijiti!


Huoni yanayomkumba muungwana?


Outside the box ma man!


Nakubaliana na hoja ya wengi kuwa Salim yeye naye maybe ana upinga ufisadi kwa siri kama anavyoelekea kufanya Muungwana!


Tunataka wale wanaoupinga ufisadi out on the open!


Kauli mbiu hapa ni.."Ufisadi ni Ukimwi wa Maendeleo"-Jmushi1


Tukicapitalize kwenye hilo then Slaa anafaa kutupitisha kwenye wakati huu!


Kumbuka urais si wa maisha...so tutaona what he's going to do!

Tumpe muda na uwezo wa kumaliza kile alichoanza!


Baada ya miaka minne tutakuwa tumejua kama direction ni right!

WE'VE GOT TO GIVE THIS MAN A SHOT!

For he deserves to take us on the next level in this historical battle!
 
ni mapema mno kubashiri kwanitunasubiri ripoti za ufisadi

HATUTAKI RIPOTI ZA UFISADI TUNATAKA HATUA DHIDI YA MAFISADI!

Hivi ndugu yangu JF huijui vizuri wewe huh?

Nenda kajipange then come back tuanze mjadala!

Pia naomba utembelee thread ya "Mafisadi wakamatwe-wasiruhusiwe kuligawa Taifa" kabla hujaja kunijibu ili tusirudishe mjadala huu nyuma!

Ahsante!
 
Anayetufa 2010 ni yule anayeweza kumkoma Nyani Giladi, kama Levi Mwanawasa wa Zambia dhidi ya Chiluba, Yaradua wa Nigeria Dhidi ya Obasanjo, Wa Malawi dhidi ya Bakili Muluzi etc.

Sasa Yupo wa Kutoka ChiChiemu anayeweza kufanya Hivyo?
Kama Yupo Basi na ajitokeze au itakapofika Siku ajitokeze tuone hiyo Sera yake.
 
ni mapema mno kubashiri kwanitunasubiri ripoti za ufisadi

Selwin kama hiyo statement hapo juu ni honest...Basi inatia huruma mno na machozi karibia yanitoke!

Yani umesound kama jinsi sisi watanzania tulivyo: Kwa utulivu, moyo mmoja,uaminifu, unyenyekevu na uvumilivu! Yani inatia HURUMA kweli!


Lakini viongozi wetu they take this for granted! Wakichukulia kuwa yote hayo ni umbumbumbu!

Yale ambayo hata mzungu aliya take for granted! Ukarimu unenyekevu na uvumilivu..Yani Tanzania inatia huruma!


Naamini kuna wale ninaoshare nao view hii!


Huruma pia kwa wale wananchi wanaokubali again and again kuwa patient!


Is patience gonna pay this time around?
 
Huyu bwana amewatumikia wananchi kwa namna zote zenye kumfanya aqualify kuendelea kuwatumikia kwenye ngazi yoyote ile provided anakuja na plan ya ni kwavipi atauzika ufisadi for once and for all!

Wenzetu wana usemi kuwa..We gonna judge you based on your character and nothing else.. Wanakusilkiliza kwanza kwamba utawafanyia nini na si assumption tulizozizoea za kutajana majina based na nafasi za kifisadi walizokuwa nazo before!
Ni lazima tuaminiane sisi wenyewe kwa wenyewe...Kuondokana na fikra kuwa viongozi wanazaliwa viongozi!
Kwamba no matter what they do or say wao bado watakuwa viongozi tu!
Hii ni risk ambayo watanzania tuna kila haki ya kuichukua!

Its time to now think outside the box!


Kwa hilo ulilosema hapo juu nakubaliana na wewe kabisaa. SAS anatakiwa ajitokeze na kutoa mwelekeo anaotaka kuipeleka nchi.

Msimamo juu ya ufisadi anaweza pia akauweka wazi ingawa hilo linaweza likamletea upinzani mkubwa kutoka kwa wafuasi walionao mafisadi.
 
Kwa hilo ulilosema hapo juu nakubaliana na wewe kabisaa. SAS anatakiwa ajitokeze na kutoa mwelekeo anaotaka kuipeleka nchi. Msimamo juu ya ufisadi anaweza pia akauweka wazi ingawa hilo linaweza likamletea upinzani mkubwa kutoka kwa wafuasi walionao mafisadi.

But i also mentioned Dk Slaa!
 
Mkuu Heshima mbele, Salim amepitwa na wakati Mwalimu amejaribu kila njia mwaka 1985 kumpitisha huko ndani ya CCM akashindwa, Mwalimu akajaribu tena mwaka 1995 kumpitisha huko CCM akashindwa tena, mwaka 2005 akajaribu mwenyewe huko CCM tena akashindwa vibaya sana, na this time akakubali yaishe kuwa hataki tena,

Kweli CV yake ni nzito sana na kazi za nje ya taifa letu, amejaribu huko UN ambako ndiko hasa CV yake inakodai na ku-fit sana, lakini nako pia wakamtupa chini, hata unaibu nao hawakumpa, unless kuna something unakijua kuhusu Salim na urais ambacho hata yeye binafsi hakijui, lakini otherwise the record is very clear kuwa wananchi wa Tanzania wamemkataa kabisa kuwa hafai na vigezo vimetolewa wazi!


Mkuu FMES, Salim ndio yuko kwenye umri unaofaa kabisa kuwa raisi. Akiwa na umri wa miaka 66, yuko kwenye wakati muafaka ambao busara ndio iko katika kilele chake.

Ni kweli wapo ndani ya CCM wanaomuogopa kwa vile yuko very serious wakati wa kazi na hapendi majungu au upendeleo, lakini nafikiri hizi ndio sifa tunazozitaka hivi sasa. Lakini pia sio kweli kuwa Mwalimu aliwahi kumteua SAS akapingwa, maana Mwalimu alikuwa hana mpinzani kwenye teuzi zake. Ila inaeleweka wazi kuwa Mwalimu hakutaka afuatiwe na mtu mwenye uwezo na jina kubwa duniani kama lake, kwa hofu ya kumwekea kivuli.

Sidhani kama zipo sababu za wazi za kumkataa SAS zaidi ya zile zilizopikwa, majungu, na wapinzani wake wanaoogopa msimamo wake mkali katika kazi. Kama zipo, jama ningeomba tuzi-list na kuzijadili badala ya kumpakazia majungu ya kisiasa.
 
Heshima mkuu,

Kwanza Salim naikubali CV yake na ninamheshimu! Pamoja na uwezo wake wa kuiongoza organisation kubwa OAU,ameshindwa kabisa kusimama kidete kuwakemea viongozi wa hapa nyumbani juu ya uozo wao.

Ananifanya niwe na mashaka nae kama kweli anajua au anaona uchungu wa hali halisi ya mtanzania.

Kwa sasa hivi tunahitaji kiongozi mwenye uchungu na hili taifa na ambae anajua watanzania tunataka nini.Ukiniambia mtu kama Slaaa,mimi namkubali zaidi kulko Salim kwani angalao ameonyesha uwezo wa kulionoza hili taifa kwani anajua matatizo mengi tulio nayo,hata matatizo ya kimfumo.Angalo ameonyesha uwezo wa kuwakaripia viongozi wetu.

Anaonekana ni mtu wa hatua tofauti na Salim ambae ataongoza kukwepa lawama,maanake hadi sasa hivi hajaonyesha kama ataweza kubadili mfumo wetu. Afadhali Slaa ataweza kutuongoza na kukabiliana na challenge zsa kiuchumi za watani wetu wa jadi.

So far,SAlim huwa sijui n nini mtazamo wake wa kiuchumi,sasa hivi tunataka kiongozi ambae atatuletea mabadiliko ya kiuchumi na sio diplomasia kusolve matatizo ya comoro au kwingineko


Mkuu Ben, Nafikiri ni muhimu kuelewa ukubwa wa chochote atakachosema SAS ulimwenguni. Watu wote wataanza kuingalia TZ kwa jicho la udadisi au hata kuathiri imani ya TZ, kisiasa na kibiashara.

Kwa wanasiasa wanaoipinga serikali ya JK, wangependa kuona hilo, lakini kwa wale ambao bado wana matumaini na CCM kuwa bado inao uwezo wa kujisafisha, kama SAS, sio rahisi kwake kutoa tamko ambalo litaiumiza nchi na serikali ya JK.

SAS ni mtu muhimu duniani, na wengi wanadhani kwa JK kumshinda SAS ina maana ni bora sana. Ndio maana hawakuacha kumtaka akamate AU mara tu baada ya kuchaguliwa 2005, ingawa alikataa.

Tunaowajua tunabaki kusikitikia tu waTZ kwa kufuata siasa za maangamizi na kumkataa mtu ambaye nchi nyingine wasingefikiria mara mbili mbili kumuweka kinarani.
 
mwandosya?usitake kuleta utani plisss...mwandosya single handesly destroyed mawasiliano
he made sure amefilisi ttcl na kuwapa celtel international total control.
hafai
 
1.

Mkuu KJ,

Heshima mbele, mimi ni CCM damu na so far sijasema nani nayemuona anafaa, ingawa ninaelekea kulalia sana kwa Mama Migiro, lakini baadaye nitasema nani ninayemuona anafaa, lakini hii analysis yako kwa mwenyekiti wa Chadema, sio fair kabisa na ina-amount to matusi ya nguoni, badala ya maoni binafsi kama mwananchi,

1. Shule au elimu ya Mwenyekiti wa Chadema ya form six, pamoja na experience yake nzito ya biashara, na the fact kwamba sasa yuko shule kwenye degree level, haiwezi kuwa mbovu kama ulivyosema that is below the belt bro!

2. Uongozi wake chamani hauridhishi wengi? Hivi ni wakati gani Chadema imewahi kuwika katika taifa letu toka ianzishwe na Mtei in the 90s? Unasema hauridhishi wengi kina nani hao? Zitto na Slaaa ni matunda ya uongozi wa Chadema under nani? Unafikiri ni kwa nini Slaa na Zitto hawakugombea ubunge kupitia CUF au TLP? Unasema kugombea kwao Chadema ilikuwa ni by accident na sio uongozi imara wa mwenyekiti wa sasa wa Chadema?

3. Ukabila? Zitto ni kabila gani? Wangwe ni kabila gani? Slaaa ni kabila gani? Mnyika ni kabila gani? Tundu Lissu ni kabila gani? Kitila ni kabila gani? Hawa wote ni Wachagga? Besides hawa naomba uwe mkweli wa Mungu kuna wengine wanaojulikana kwenye taifa as Chadema? Sana sana ni Ndesamburo tu!

4. Unasema zaidi ya Billicanas, hivi mkuu unajua maana ya kuwa mmiliki wa Bilicanas bongo? Mbona unaiandika kimzaha mzaha tu as if ni soko la samaki mkuu? Huyu si alishawahi kuwa mbunge wa kuchaguliwa na wananchi, je Salim aliwahi kuchaguliwa kuwa mbunge wa wapi? Hivi mwenyekiti wa chadema angepelekwa na Mwalimu ubalozini nje akiwa na miaka 22 je leo asingekuwa na elimu suspect kama ya Salim? Hivi ni shule gani ya wazungu huko majuu unayoijua inayoweza kumnyima Degreee balozi wa any nation katika UN akiomba kusoma hata online?

Tunapowachambua viongozi wetu tuwe wakweli kuliko kujali kujaribu ku-balance mijadala hapa JF, kwa sababu mijadala mingi inashambulia CCM, basi dawa ni kushambulia Chadema hata kama hakuna hoja wala ishu that is low, mkuu binafsi katika sababu zako zote ulizoweka hapa against mwenyekiti wa Chadema na urais, siiioni hata moja ya muhimu, na ninasema wazi kuwa he does not deserve this kind of analysis.

Ahsante Mkuu!


Mkuu FMES,
Naelewa kuwa una mapenzi makubwa na hao wakuu walioko hapo NYC, akina Dr. Migiro, Balozi wetu UN, n.k. Maana nakumbuka uliwahi pia kumpendekeza balozi kuwa awe PM.

  1. Ukweli ni kuwa hao wote wanafaa sana, kwani wana elimu na wameonyesha kuwa wana uwezo wa kukabiliana na makubwa yanayoikabili nchi na jumuiya za kimataifa. Pia wamepata upeo wa mwelekeo wa dunia na wapi TZ inatakiwa kwenda ili nayo isonge mbele. Kosa lao ni kuwa wote wako karibu sana na Kikwete na kwahiyo hawawezi kujitosa kupambana naye, wanachoweza kufanya tu ni kumrithi. Urithi huu pia unaweza usiwe mzuri sana kwani wanaweza wakashindwa kukemea aliyofanya JK. This is not the case kwa SAS.
  2. Salim ni msomi wa madarasa na vitendo tusimpakazie kwa vile alisoma akiwa ofisini. Ameweza kuitumia elimu yake kisomi katika kiwango cha juu kabisa na akiwa na umri mchanga sana. Hii ni kuonyesha kuwa hakupewa vyeti. Zaidi ya hayo, vyeti vya kupewa havitoki Columbia University, hiki ni kati ya vyuo bora duniani na SAS akitokea 3rd world, hawezi kuwa na jina la kumfanya apewe degree. Kitengo chake cha international affairs hapo Columbia Unv., ni kati ya vilivyo bora zaidi duniani. Baadhi ya Alumni wanaojivunia ni pamoja na Madeline Albright.
  3. Binafsi yangu, siko tayari kuongozwa na raisi aliyeishia form six katika karne hii ya 21, ingawa nafikiri Mbowe ana some other certificates. Mbowe ameishia hapo baada ya kusoma kwenye the best schools primary na secondary. Hii ni dalili ya upungufu fulani ambao hata pesa haikuweza kuuondoa. Hizi degree za kutafuta wakati tunataka uongozi, hazitufai maana shule sio darasa tu, ni pamoja na kupata muda wa kutosha kutumia ulivyosomeshwa katika ulimwengu halisi. Kwa hiyo kama Freeman akimaliza shule kesho, anahitaji afanyie kazi aliyofundishwa kwa angalau miaka 10 hivi ili tumtambue kuwa aliyaelewa aliyofundishwa. Tuko karne ya 21, ni muhimu tukaheshimu nguvu ya elimu. Hii haina maana ya PhDs, bali angalau a good first degree ni mwanzo mzuri wa kupima uwezo wa mtu.
  4. La uongozi na ukabila chamani tumeshaliongelea sana. Kama yeye akiwa mwenyekiti ameweza kuruhusu wabunge 5 kati ya 6 kutokea mkoani kwake bila kuliona kuwa lina ualakini, then hafai kabisa kukamata nchi. Hili pia ni swali kwa viongozi wengine wa CHADEMA hasa wale waliopo humu mtandaoni watueleze msimamo wao kuhusiana na hili jambo. Zitto, Mnyika na wengine tutashukuru kama mtatujibu kwa nini mmelikalia hili kimya?
Kwa hiyo, ukikata ukatavyo, SAS kwa mawazo yangu ana nafasi kubwa ya kumuondoa JK in 2010 kuliko wengi tulionao, tatizo ni kwa yeye tu kukubali kuuchukua huu mzigo mkubwa.


__________________________________
 
1.
Salim ndio yuko kwenye umri unaofaa kabisa kuwa raisi. Akiwa na umri wa miaka 66, yuko kwenye wakati muafaka ambao busara ndio iko katika kilele chake.

Umri haujawahi kuwa important ishu kwenye uchaguzi wa rais wetu kwa hii mkuu ni none ishu au skill, na sio muhimu sana kama sio kabisaa.

2.
Ni kweli wapo ndani ya CCM wanaomuogopa kwa vile yuko very serious wakati wa kazi na hapendi majungu au upendeleo, lakini nafikiri hizi ndio sifa tunazozitaka hivi sasa.

Unajua kurudia rudia neno moja bila ushahidi ni kupoteza muda wa wasomaji, CCM haiwezi kumuogopa mgombea urais anayeomba kugombea kupitia chama chake, kama sifa tunazozitaka sasa hivi ni kiongozi anayeweza kusimamia ufisadi na Salim hana record yoyote ya hata kukemea ufisadi, sasa huo u-serious wake uko wapi hasa?

Halafu hii habari kuwa Salim hapendi majungu, inatokea wapi? Ni lini Salim aliwahi kukemea majungu, au upendeleo ndani ya taifa letu?

3.
Lakini pia sio kweli kuwa Mwalimu aliwahi kumteua SAS akapingwa, maana Mwalimu alikuwa hana mpinzani kwenye teuzi zake. Ila inaeleweka wazi kuwa Mwalimu hakutaka afuatiwe na mtu mwenye uwezo na jina kubwa duniani kama lake, kwa hofu ya kumwekea kivuli.

Unajua imefika wakati mkuu ukubali tu kuwa unampenda sana huyu jamaa, lakini huna hoja zaidi za kumtetea, kwa sababu hii sina hata sababu ya kuijibu!

4.
Sidhani kama zipo sababu za wazi za kumkataa SAS zaidi ya zile zilizopikwa, majungu, na wapinzani wake wanaoogopa msimamo wake mkali katika kazi. Kama zipo, jama ningeomba tuzi-list na kuzijadili badala ya kumpakazia majungu ya kisiasa.

Salim aligombea urais, na wagombea wengine, ili ashinde ilibidi awashinde wagombea wengine, lakini akashindwa na kulia sana na kuapa kuwa hatarudia tena siasa za bongo, sasa hapa anyewaogopa wenziwe ni nani hasa? Siasa ni siasa ni mchezo mchafu na unachezwa na watu wachafu wachache, kwa bahati mbaya huwa Tanzania hatutoi urais tu bure bure,

amegombea ameshindwa urais, amekubali yaishe sasa mmetokea mnaojua better kuliko anavyojijua mwenyewe, kwa sababu kwangu mimi ni kwamba Salim amejiangalia vizuri na kukubali kuwa hana uwezo wa kushinda urais wa Tanzania, sasa sielewi hizi filimbi ni za nini hasa!
 
Back
Top Bottom