The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Nadhani sio haki kuwaachia wapinzani peke yao kueleza mabaya ya MAFISADI hawa waliotuzunguka. Ni wajibu wetu sisi waTZ kusimama kidete kuikomboa nchi yetu. Saa ya ukumbozi inakaribia kwa TZ na ni sisi watanzania ndio tutakaoifanya saa hiyo itufikie kwa haraka.. jamani ni lazima tujuwe kwamba kila mTZ anahaki ya kuyafikisha haya kwa jamii zetu kwa kiasi cha uwezo wetu.

Tusiishie tu kusoma na kupiga makelele humu lazima tutoke na tuieleweshe jamii. Hubu tufikirie gharama za UFISSDI huu kwa watoto wetu na vizazi vijavyo.....ni jukumu letu watanzania kuwatokomeza mafisadi kwa gharama zote kwani tukikaa kimnya hatuwatendei haki wale ndugu zetu walioko vijijini[/QUOTE
]

...hapa sioni cha kupinga, zaidi ya kukuongezea nguvu!!!
Tusiishie kwenye Forum ya JF tu, kwani huku Kijijini kwetu hizi mada hazitufikii wala hatujui haya yanayoendelea kwa undani.

Kwani mpaka leo tunaletewa zile Cinema za vitambaani na kuonyeshwa mauaji ya Kimbari ya Rwanda mwaka 1994, na zile t-shirt za A to Z zenye maandishi chagua SiSi-eM, ambapo ukiifua mara moja shingo yake inavutika na kufikia kifuani, mpaka siku moja nikamuuliza mama kayaii kwanini alivaa t-shirt yangu wakati ananyonyesha?...amesababisha ivutike shingo: kumbe nilimsingizia kwani hata ya mdogo wangu nayo ilikuwa vivyo hivyo.

Nisitoke kwenye Mada sana; NJOOONI KIJIJINI kwetu mtuelimishe..tusiwahi sana kuitaka nafasi ya Ikulu,kwani tukiwahi sana huko..tutashindwa kung'oa visiki vya Ufisadi, tutakuwa tumekata Matawi kwa Juu baadae mvua zikinyesha yanachipua tena!

Nahisi ni busara tuanze kujipanga chini, TUFANYE MWAKA 2010 NI WAKUPELEKA WABUNGE WENGI BUNGENI...ikiwezekana 50% ama ZAIDI itoke kwetu, asilimia hiyo naamini kabisa itatuwezesha kung'oa Visiki...maana haya majitu yalishaanzisha hadi Bendi na kutuimbia nyimbo za Mafumbo wa Tz...et! Mimi Kisiki cha Mpingo, unakuja na panga, wenye shoka wamenishindwa, unajisumbua.....teh! teh! teh! huku kijijini kuna mengi sana!

Slaa, Zitto, Hamadi Rashid, nguvu zao pekee haziwezi kushinda ile alisimia kubwa ya Mafisadi yaliyojiotea Mizizi!!Huku kwetu mti ukikomaa sana huwa unaota ndevu kila mahali...sijui ninyi uzunguni kama ipo. Halafu sasa hapo 2015..tutakuwa tunaelekea Head Office....et! mtu anajiita Kingung..!!teh..teh

Tuacheni utani, msisahau kuja kijijini kwetu...
 
Contd.....

UBUNGE
Lakini ukiangalia kwenye ubunge, zaidi ya wagombea 20 wa Chadema walipata zaidi ya 30% ya kura. CUF wao wanao wagombea wengi zaidi waliopata zaidi ya 30%. That means, with additional efforts na mazingira ya sasa ya siasa TZ yaliyo mazuri kwa wapinzani, sehemu kubwa ya hawa wagombea, kama wakipewa resources zaidi wanaweza wakawa wabunge. Ukiongezea majimbo ya mafisadi kama akina Basil Mramba, Chenge n.k., uwezekano wa kuibuka na wabunge wengine say 10-40 kutoka kwenye hii mizoga unaongezeka.

Then kuna kundi la akina Mnyika n.k., ambao walipata between 10% to 20%. Hawa nao wako wengi sana. Chadema peke yake ina kama 17 hivi. Hawa watahitaji mtaji mkubwa zaidi kuwafanya wawe competitive. Lakini kwa vile hawatakuwa wanashindana na JK, bado nguvu ya ushindani watakuwa nayo na wanaweza wakashinda.

Hoja yako ni ya Kikubwa Jinga Jinga kweli. Unashangaa kwanini CUF inawagombea wengi zaidi. Umesahau kwamba CUF ilisimamisha idadi kubwa ya wagombea kuliko CHADEMA. Umesahau kuwa toka uchaguzi wa 1999 wa vijiji na mitaa CUF ilipata mtandao mkubwa na ilikuwa na ruzuku mara kumi ya kiwango ambacho CHADEMA imekuwa ikipata kati ya 2000 na 2005?

Hiki ni chama kilichokuwa na mafedha mengi na mtandao. Si jambo la ajabu, na ukifanya uchambuzi wa kina utoana kuwa kwa milioni 700 za CHADEMA ukilinganisha na takribani milioni 2000 za CUF, CHADEMA ilifanya vizuri zaidi kwa kuwa walau imeambulia viti vitano bara wakati CUF haikushinda mwaka 2005 hata kiti kimoja huku.

Kumbuka CUF Zanzibar ilikuwa na bajeti yake seperate, mi nilikuwa huko wakati wote wa uchaguzi. Toka 2005 mpaka sasa, ukiangalia peformance ya CUF na CHADEMA unaweza kuilinganishaje? By the way, Sasa kwanini hutaki kuamini kwamba hiyo 30 ya CUF na 20% ya CHADEMA zikiiungana CCM haitoki?

Kwa taarifa yako, vyama vya upinzani vinashirikiana katika hili.


Asha
 
Contd.....

UBUNGE
Lakini ukiangalia kwenye ubunge,
Then kuna kundi la akina Mnyika n.k., ambao walipata between 10% to 20%. Hawa nao wako wengi sana. Chadema peke yake ina kama 17 hivi. Hawa watahitaji mtaji mkubwa zaidi kuwafanya wawe competitive. Lakini kwa vile hawatakuwa wanashindana na JK, bado nguvu ya ushindani watakuwa nayo na wanaweza wakashinda.


We Kubwa Jinga Jinga unakaa nchi gani? We hujui kwamba haya matokeo ya Ubunge ni pamoja na uwizi waliufanya kule kwa Balozi Ngaiza,Mbogoro, Pesha nk(CHADEMA); Lwakatare CUF nk, Lema(TLP Arusha) nk? Hivi CCM wasingeiba wangepoteza majimbo mangapi kwa staili hii?

Umetoa mfano wa Mnyika wa CHADEMA, si umeona hapa jinsi ambayo aliyalalamikia matokeo yake kwamba yamepikwa?

"Kwa hali iliyodhihirisha wazi kuwa matokeo yalipikwa, waliopiga kura za Ubunge walikuwa 185,684 wakati waliopiga kura za Rais walikuwa 152,525 na hivyo kufanya tofauti ya kura za Ubunge na urais kufikia 33,159. Katika hali ya kawaida na katika uchaguzi uliofanyika kwa wakati mmoja ilikuwa ni vigumu kwa tofauti kubwa ya kura kiasi hiki.

Na hata kama wananchi wangekuwa hawapendi kupiga kura za rais kwa kuwa mpiga kura alikuwa akipewa karatasi zote tatu kura hizi zilipaswa kuwepo katika kura zilizoharibika kitu ambacho hakikutokea.

Kimsingi, hujuma za kimfumo na kimkakati za chama tawala ndiyo hasa vilivyofanya uchaguzi kutokuwa huru na haki. Kabla ya uchaguzi wajumbe wa nyumba kumi waliandikisha kadi za wapiga kura kwa lengo la kuwakosesha kupiga kura wale walioelekea kupigia kura upinzani na pia kuweza kuwapa rushwa wengine ili kupigia CCM.

Wananchi wengi walizuiwa kupiga kura licha ya kuwa na kadi kutokana na ama majina yao kutoonekana kwenye orodha au kuwa tofauti na kwenye daftari. Kulikuwa na kampeni za vitisho kwa wapiga kura hususani katika kata za vijijini. Wananchi wengi walihongwa kukipigia kura chama tawala hii ni pamoja na wengi kujifanya hawajui kusoma na kuandika ingawa baadhi yao vitambulisho vyao vya kupigia kura vilionekana kuwa na saini.

Kulikuwa na mapungufu kadhaa katika mpangilio na idadi ya vituo vya kupigia kura. Halikadhalika, kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa kanuni na sheria katika ujumlishaji wa kura za ubunge. Kwa kiasi kidogo mtandao hafifu wa chama katika maeneo machache na udhaifu wa baadhi ya mawakala navyo vilichangia kushindwa katika vituo vichache ambavyo visingeathiri matokeo kwa kiasi kikubwa kwa ujumla.

Na mwisho matokeo ya ubunge jimbo la Ubungo yakatangazwa kwa shuruti bila kutangaza na kujumlisha kwa pamoja matokeo ya kituo hadi kituo hali iliyoashiria kuwa matokeo ya Ubunge yalikuwa na utata. Kutangaza huku kwa nguvu ilikuwa ni mkakati wa kutaka matokeo hayo yasihojiwe kama ilivyokuwa katika matokeo ya urais ambayo yalichelewa kutangazwa kutokana na kukutwa na mapungufu mengi.

Kwa hali iliyodhihirisha wazi kuwa matokeo yalipikwa, waliopiga kura za Ubunge walikuwa 185,684 wakati waliopiga kura za Rais walikuwa 152,525 na hivyo kufanya tofauti ya kura za Ubunge na urais kufikia 33,159. Katika hali ya kawaida na katika uchaguzi uliofanyika kwa wakati mmoja ilikuwa ni vigumu kwa tofauti kubwa ya kura kiasi hiki. Na hata kama wananchi wangekuwa hawapendi kupiga kura za rais kwa kuwa mpiga kura alikuwa akipewa karatasi zote tatu kura hizi zilipaswa kuwepo katika kura zilizoharibika kitu ambacho hakikutokea.

http://www.chadema.net/hotuba/mnyika/hotuba_4.html

Lakini unadhani wapinzani watakubali tena kuibiwa 2010? Wewe badala ya kujadili jinsi ya watu kulinda hizo kura za Urais wewe kazi yako ni kusema kwama wasigombee, amakweli ukistaajabu ya Mussa utaona ya Firauni

Asha
 
Contd.....
MUUNGANIKO WA VYAMA
Pia **** maeneo ambayo wapinzani walipigana wenyewe kwa wenyewe ngwara wakawaachia CCM ubunge. Kwa mfano jimbo la Vunjo, Chadema ilipata kura (11.9%), TLP (31.2%), NCCR (11.5%) jumla 54.6%. Halafu CCM wakapata 43.8% tu, kwa hiyo kwa rule ya simple majority wakajichukulia ubunge kiulaini.

Ndio maana nasisitiza kuwa, kama wapinzani wanataka ushindi wa maana, na hata kumtoa mtu ambaye angeshinda ubunge kafara, say Dr.Slaa, ni vema wakafanya hivyo tu baada ya kuungana na wala sio kama walivyo vipande-vipande hivi sasa, maana odds za ushindi as Chadema au CUF hazipo.


To be Contd.....

Kwani we hujui kuwa wanashirikiana na walishatoa tamko la pamoja kuwa wataweka mgombea mmoja wa Urais?

Asha
 
Contd.....

UMAARUFU WA MGOMBEA
Mbowe alipoacha jimbo lake na kugombea uraisi, jimbo likachukuliwa na CCM, licha ya kuwa yeye, ambaye ni mgombea uraisi wa Chadema, alikuwa maarufu sana hapo awali. Baada ya kushindwa uraisi, umaarufu wake nje ya Chadema nao ukapungua kitu ambacho kinaweza kikawa tatizo kwake kama akiamua kurudi kugombea ubunge Hai.

Hivyo ni wazi kuwa, kama ilivyokuwa kwa Mbowe, wapiga kura wengi wanapopiga kura hutofautisha kura za ubunge na uraisi. Ndio maana vyama vya upinzani vilipata kura nyingi kwenye ubunge kuliko uraisi.

WaTZ wengi wako radhi kumpa ubunge mgombea wa upinzani kama anawavutia, lakini ni wagumu kufanya hivyo kwenye uraisi. Hii ina maana kuwa hata Slaa akigombea, umaarufu wake sio kweli kuwa utasaidia kuleta kura. Hivi ni nani maarufu zaidi, Dr. Slaa wa 2010 au Mrema wa 1995?? Mrema aliingia ulingoni, sio tu baada ya kulipua mabomu na kukamata dhahabu airport, bali nchi nzima ilikuwa inamtambua maana alikuwa kiongozi wa ngazi ya juu na maarufu zaidi ya wengine wote. Lakini bado alipigwa chini kiulaini na Mkapa. Hivi sasa sidhani kama Dr.Slaa ana even 1/2 ya umaarufu alioingia nao Mrema kwenye kinyang'anyiro.

Lakini nina uhakika hii inaweza kubadilika kama major oppostion parties zikiamua kuungana. Faida ziko wazi;
  1. Watakuwa na Resources nyingi zaidi kwenye ubunge, na kwenye uraisi.
  2. Wananchi watakuwa wanacompare qualities za watu wawili tu na sio utitiri.
  3. Hata kama hawatashinda uraisi, lakini bado wanaweza wakawa na majority bungeni, badala ya kupoteza wabunge, maana chaguo la wananchi litakuwa wazi either CCM au upinzani.
Lakini wakiendelea na huu mchezo wa kila mtu na vyake, au hata kushirikiana tu bila kuvivunja vyama, kama ilivyokuwa Vunjo,
  1. Watashindwa kushindana na CCM sababu ya mgawanyiko
  2. Overheads zao zitakuwa kubwa na
  3. Sio ajabu wataishia kutapanya vipesa vichache walivyo navyo kwenye uraisi, maana kila mmoja wao atakuwa na mgombea, badala ya kuzipeleka kwenye ubunge.

We Kubwa Jinga Jinga, hujui kwamba Sheria za Uchaguzi na Ya VYama vya Siasa zilizowekwa na CHama Cha Mafisadi zinazuia Muungano wa vyama? Hujui kwamba CUF leo wakitaka kuungana na CHADEMA kuwa chama kimoja wanapoteza viti vya Ubunge, Udiwani nk? Hujui kwamba msajili ambae ni mtumishi wa serikali ya CCM chini ya Waziri Mkuu anaweza kukataa kukisajili cha hicho kipya?

Kuna ubaya gani katika kushirikiana na kuachiana maeneo? Wewe unazungumza hadithi za mwaka 2005. Toka mkataba wa ushirikiano usainiwe wapinzani wameshaanza kuachiana maeneo. Huko vunjo unaposema NCCR, TLP na CHADEMA zote zina nguvu, lakini kwenye uchaguzi wa udiwani wa marudio wa hivi karibuni mbona waliachia chama kimoja tu? Si umeona pia Kiteto. Hebu grow mentallly tafadhali, au ndio maana hali ya kuwa Kubwa Jinga?

Asha
 
Lakini nina uhakika hii inaweza kubadilika kama major oppostion parties zikiamua kuungana. Faida ziko wazi;

Watakuwa na Resources nyingi zaidi kwenye ubunge, na kwenye uraisi.

Wananchi watakuwa wanacompare qualities za watu wawili tu na sio utitiri.

Hata kama hawatashinda uraisi, lakini bado wanaweza wakawa na majority bungeni, badala ya kupoteza wabunge, maana chaguo la wananchi litakuwa wazi either CCM au upinzani.

Sawa sawa mkuu, hapa tupo ukurasa mmoja, kwamba tatizo lililopo kwa upinzani ni muungano, wakiungana na kuwapa wananchi chaguo la either CCM, au Dr. Slaaa basi kuna uwezekano mkubwa sana akafanya vizuri sana, kuliko akigombea kutoka chama kimoja cha upinzani. Hapa tupo wote the same page!
 
Hayo ya ukabila na udini tunayaonea kwa wanaKilimanjaro ndani ya Chadema na CUF kwenye misikiti.

Tokea Mrema apate almost 30% ya kura mwaka 1995, hakujatokea mgombea mwingine aliyekaribia hata 20%. This is a fact.
JINA LAKO NA POST YAKO VINAFANANA SANA.
 
..wakubwa!

Mimi ni mgeni kabisaa! na sibingwa wa uandishi maana nina mwezi tangu nitoke kijijini kwetu, lakini kitu kilichonishangaza, ni ule usemi wa Jogoo wa shamba hawiki mjini...ninavyokumbuka yule jogoo niliyekuja naye kama zawadi aliwika tena saa mbili usiku baada ya kuona ule mwanga wa umeme..sijui alijua kumekucha ama vipi...lakini nataka kusema Ukweli jogoo wa shamba huwika mjini pia...

Napenda nikueleze Dada'angu kuwa haya mambo ya % (fulani alipata asilimia ngapi..na fulani ngapi ni mazuri kwenu ninyi mnaojua kutofautisha kati ya Phillips TV na Phillips Computer..huku kwetu sisi TV na Computer zote ni TV..remote ya Radio aina ya Sumsung na Mobile ya Sumsung kwetu zote ni simu za mkononi. Kama mimi nasema uongo naomba Mzee mwanakijiji akuelezee! maana anaifahamu hali yetu hapa kijijini..mfano zaidi ni hiyo T-shirt yake aliyoivaa ndiyo maisha yetu yalivyo.

Sasa kama tutaletewa hizo kofia na t-shirt na kanga tutaacha kuwapigia kura mafisadi?..maana hamtaki kuja kutuelimisha huku kijiini kwetu, mnang'ang'ana na %!!!! shauri yetu..tutachelewa kufikia lengo

Huku kwetu pia mtu akipanda ndege Swiss Air, Emirates, Gulf Air na nyinginezo, tunajua ameenda Ulaya..iwea kaenda Asia ama America, Africa Kusini .. tunasema kaenda Ulaya tu, hatujatofautisha kati ya Ulaya, Asia na Marekani..zote ni Ulaya!

Sasa kitu ambacho nataka kuwaeleza Maswahiba zangu wa TLP, CUF, CHADEMA, NCCR na Wengineo wenye Mapenzi Mema na Nchi hii..tuacheni kubishania asilimia zinatupotezea muda!!! Asha!! tutumie POINT yako ..ya KUANDAA MAZINGIRA MAZURI MAPEMA KABLA YA 2010 IKIWEMO KUJENGA MTANDAO WA VYAMA VYA SIASA WASHIRIKA NCHI NZIMA...nadhani hapo ndiyo uwezo wangu wakufikiri umeishia hapa, ilikuweza kuushinda Ufisadi.

.... Sasa Mbowe, Dr Slaa na wengine kama wanataka kugombea uchaguzi 2010 wataanza kuaandaa mazingira mapema kabla ya 2010 ikiwemo kujenga mtandao wa chama nchi nzima.
Asha

..Mwisho; sijisikii vyema kuviita vyama vyetu vitukufu vya siasa kuwa Vyama vya Upinzani..naona kama tunawajengea kapepo kadogo hawa akina SiSi-eM; kwanini wao wasiitwe kwa domain hiyo hiyo ya Chama Cha Upinzani Cha CCM? si wanapinzana na wenzao wa vyama vingine?...Kazi kwako Mch. Kishoka!ila nakupa onyo ukienda A-town/City usitumie jina hilo la Kishoka, maana kama utapita karibu na Ofisi za Tanesco unaweza kupata matatizo..

Mkitaka Kuja Kijijini nitumieni barua C/O.Mwl. Mkuu, Shule ya Msingi...., ambaye atampa Katibu Kata, kwani yeye anafahamiana na Mjomba'angu ambaye ni Mjumbe wa Shina, ili nije niwapokee...kisha niwapeleke nikawatafsirie kwa wanavijiji kama mtaenda wenyewe wanavijiji watabakia kushangaa hizo nywele zenu mlizo tia dawa ama kusuka rasta na suruari za kubana kwa wanawake..hivyo hawatawasikiliza zaidi ya kuwashangaa!

Massege Send!
 
Hii ni mesage ninayoisema kila siku ila mkulu umeileta katika mtindo ambao nafikiri watakuelewa zaidi, tuache kupiga kelele mjini twende vijijini, juzi kwenye taharifa ya habari wamesema kuna sehemu wilaya ya kyela mkoa wa mbeya hawajawai kuona pikipiki maana hakuna hata kinjia cha pikipiki, lakini hawa watu wanalima mpunga, wanamabalozi wa nyumba kumi wa CCM, hawa sifikiri kama wanajua kuwa kuna TLP, CUF, au CHADEMA hachilia mbali kujua kuwa CCM ni mafisadi.

hawa bila kuwafikia na kuwaeleza kuwa CCM ni mafisadi watawapigia kura CCM tena na itashinda kwa kishiondo maana huko CCM haina haja ya kuiba kura kwa kuwa wanajua kijiji kizima watawapigia wao kura.

Hizi taasisi zinazotoa elimu ya uraia wanaishia mjini tu na kugawana posho na kurudi dar, twebde vijijini huko ndo kuna wapiga kura wetu, tunajua kuwa resources ni muhimu na ndo maana CCM wanaiba mamilioni kutoka BOT ili washinde uchaguzi lakini tukiamua atleast tutaweza kuongeza idadi ya wabunge wa upinzania mjengoni.
 
I am not sure whether this gentleman has what it takes to be the President. Nadhani kuwa rais ni zaidi ya kulipua mabomu. Mrema alilipua mambomu lakini wengi tuliona hafai kuwa rais.
 
Nadhani wengi wetu mnalijua jina la Dr. Wilbroad Slaa Mbunge wa Karatu kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA. Mimi ni Mtanzania ambaye sifungamani na chama chochote lakini mwenye kuamini kabisa ya kwamba, miongoni mwetu kuna Watanzania ambao wanaweza kuleta mabadiliko makubwa katika njanja mbalimbali kama za kisiasa, kiuchumi na kijamii. Nchi yetu iko kwenye wakati mgumu sana hivi sasa na tunahijati kiongozi bora na sio bora kiongozi ambaye ataweza kuleta mabadiliko makubwa na ya kweli katika kuiendeleza nchi yetu kiuchumi.

Kama mjuavyo tatizo la ufisadi na rushwa limekithiri sana na imeshajionyesha wazi ya kwamba, Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameshindwa kwa kiasi kikubwa kutekeleza majukumu yake aliyopewa na watanzania kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Naamini huu ni muda thabiti kabisa kumtafuta mtu atakayefaa kukichukua kiti chake itakapofika wakati wa Uchaguzi wa mwaka 2010. Binafsi ningependa Kikwete aondoke hata leo hii na arudi kijijini kwao Bagamoyo akalime Mananasi yake na huku akiendelea kujichekesha mbele ya ndugu zake. Naamini kabisa Dr. Slaa ndio mtu anaefaa kuwa Rais wa nchi yetu na mwenye uwezo mkubwa wa kulianzisha gurudumu la maendeleo nchini. Mimi niko tayari kulipia gharama zote za kutengeneza tovuti ya Dr. Slaa na kulipia hosting charges kutoka hivi sasa mpaka wakati wa uchaguzi mwaka 2010. Kwa hiyo ningeomba watanzania wenzangu tumhamasishe Dr. Slaa agombee hiki kiti cha Urais mwaka 2010. Tumebakisha miaka miwili na nadhani huu ni muda muafaka kuanza kujiandaa ili kuhakikisha Kikwete na CCM hawarudi tena kwenye uongozi.

Ahsanteni.

(Haya ni maoni yangu binafsi hayaingiliani kabisa na maamuzi ya CHADEMA) www.drwilbroadslaa2010.com

Jamani, jamani. Ni kweli mawazo binafsi umeleta na bila shaka ulitegemea watu kuchangia hoja yako.

Naomba Nikuulize ni kweli Unamaaanisha kwa kuaangalia Alama za Nyakati? Kwanini isiwe Mbowe au Zitto Kabwe.

Elewa kuna Kukubalika kwa Wananchi na Kukubalika Bungeni na wabunge wenzio na wasomi walio wachache wenye kuelewa maana ya siasa na nchi inapoelekea. Ukiniambia aje kuwa WAZIRI MKUU nitakubaliana na wewe ila sio Uraisi(Maoni yangu haya)
 
Bongolander,
Dr Slaa ni zaidi ya mlipua mabomu. Ukipita jimboni kwake nadhani kuna mambo mengi ambayo ameyafanya na yanadhihirisha uwezo wake kama kiongozi,
 
I am not sure whether this gentleman has what it takes to be the President. Nadhani kuwa rais ni zaidi ya kulipua mabomu. Mrema alilipua mambomu lakini wengi tuliona hafai kuwa rais.

Bongolander

Ukiwa unalinganisha watu huwepia unajaribu kupitia CV zao, halafu wakati wa kutoa michango bungeni huwe unafuatilia sana ikibidi tafuta na za Mzee Lyatonga uangalie wana tofauti gani.

Halafu msiwe mna complicate mambo, by the way hakuna kozi ya kuwa rais duniani.
 
Tunachoitaji Watanzania sasa sio kumpeleka strong man kama yule ikilu, tutakuwa hatujafanya la maana kama tunataka maendeleo ya kweli na kule haendi peke yake, sisi wananchi tutampeleka kule lakini atakao wateua je watajali masirahi ya wananchi?
We need those strong men in the parliament waweze kusaidia kuchange system iliyopo ambayo sasa hivi ni kifisadi, hata JK anaodoka leo hali itabakia ile ile maan system yote ni ya kifisadi na inaweza kubalidilishwa bungeni tu, watu waogope na kueshimu bunge badala ya sasa linaoneka kana kwamba ni sehemu ya kwenda kuchulia poso tu.

NA MAHALI PAKUALIKA VIMADA WAO PALE BUNGENI
 
Jamani, jamani. Ni kweli mawazo binafsi umeleta na bila shaka ulitegemea watu kuchangia hoja yako.

Naomba Nikuulize ni kweli Unamaaanisha kwa kuaangalia Alama za Nyakati? Kwanini isiwe Mbowe au Zitto Kabwe.

Elewa kuna Kukubalika kwa Wananchi na Kukubalika Bungeni na wabunge wenzio na wasomi walio wachache wenye kuelewa maana ya siasa na nchi inapoelekea. Ukiniambia aje kuwa WAZIRI MKUU nitakubaliana na wewe ila sio Uraisi(Maoni yangu haya)

Nadhani haujatoa sababu ni kwa nini unadhani Dr. Slaa hafai kuwa President ukilinganisha na Zitto,Mbowe au mtu mwingine yeyote. Mimi kama wengi wetu hapa naamini kabisa Dr. Slaa ni mtu mwenye judgement nzuri na ambaye ni competent kuwa President wa nchi yetu.

Pia ni kiongozi mahiri mpenda nchi yake na mwenye kujitoa mhanga kuhakikisha anatetea maslahi ya nchi kwa njia zote zile. Tunachokiona hivi sasa ni jinsi viongozi wa CCM wanavyoweka mbele maslahi ya matumbo yao kuliko nchi yetu. CCM inanuka na haifai kuiongoza Tanzania.

Tumeshavumilia vya kutosha na kilichobaki ni jukumu letu watanzania kuwafukuzia mbali hawa watu wa Chama Cha Mafisadi na Majambazi (CCM). Tusije kujilaumu tukiendelea kuwachagua makanyaboya kutoka CCM.
 
Nadhani haujatoa sababu ni kwa nini unadhani Dr. Slaa Slaa hafai kuwa President ukilinganisha na Zitto,Mbowe au mtu mwingine yeyote. Mimi kama wengi wetu hapa naamini kabisa Dr. Slaa ni mtu mwenye judgement nzuri na ambaye ni competent kuwa President wa nchi yetu. Pia ni kiongozi mahiri mpenda nchi yake na mwenye kujitoa mhanga kuhakikisha anatetea maslahi ya nchi kwa njia zote zile. Tunachokiona hivi sasa ni jinsi viongozi wa CCM wanavyoweka mbele maslahi ya matumbo yao kuliko nchi yetu. CCM inanuka na haifai kuiongoza Tanzania. Tumeshavumilia vya kutosha na kilichobaki ni jukumu letu watanzania kuwafukuzia mbali hawa watu wa Chama Cha Mafisadi na Majambazi (CCM). Tusije kujilaumu tukiendelea kuwachagua makanyaboya kutoka CCM.

Geeque,

Leo ni 25/04/2008. Bado hapaonekani dalili zozote kwamba wapinzani wana(me)jiandaa kuikabili CCM hapo 2010.

Mawazo mengi na mazuri yamekwishachambuliwa hapa JF, katika mjadala huu, na ule wa Rev. Kishoka unaozungumzia kujiandaa kwa 2010.

Mimi ninapendekeza, kama inawezekana, (kwa hisani ya Invisible na wenzake) nakala za mijadala yote hii miwili, au zaidi ipelekwe kwenye ofisi za vyama vya upinzani ili yaliyomo humu yajadiliwe na kuchambuliwa huko na wanachama wao.

Zaidi ya hivyo, tujiandae tu kuendelea na CCM yetu na uozo wote tunaoupigia kelele hapa.
 
Geeque,

Leo ni 25/04/2008. Bado hapaonekani dalili zozote kwamba wapinzani wana(me)jiandaa kuikabili CCM hapo 2010.

Mawazo mengi na mazuri yamekwishachambuliwa hapa JF, katika mjadala huu, na ule wa Rev. Kishoka unaozungumzia kujiandaa kwa 2010.

Mimi ninapendekeza, kama inawezekana, (kwa hisani ya Invisible na wenzake) nakala za mijadala yote hii miwili, au zaidi ipelekwe kwenye ofisi za vyama vya upinzani ili yaliyomo humu yajadiliwe na kuchambuliwa huko na wanachama wao.

Zaidi ya hivyo, tujiandae tu kuendelea na CCM yetu na uozo wote tunaoupigia kelele hapa.
Kalamu nakubaliana nawe kabisa kuhusiana na hilo na nadhani kutokana na kwamba kuna baadhi ya wanachama na viongozi kutoka vyama vya upinzani ambao wanakuja hapa, ni bora wachukue maoni yetu.

Unajua mwaka 2010 sio mbali kabisa na mikakati ya ushindi inabidi ianze sasa na sio kuongojea hadi inapokaribia muda wa kampeni.

Tatizo la vyama vyetu vinakuwaga havina long term plans za mambo yao mbalimbali. Wakati ni huu na wakiamua kufanya ngoja ngoja itawapa nafasi zaidi CCM.
 
I am not sure whether this gentleman has what it takes to be the President. Nadhani kuwa rais ni zaidi ya kulipua mabomu. Mrema alilipua mambomu lakini wengi tuliona hafai kuwa rais.
Ni kwasababu kuna watu wanachagua viongozi kama vile wanavyoenda kuchagua malapa dukani!
 
I am not sure whether this gentleman has what it takes to be the President. Nadhani kuwa rais ni zaidi ya kulipua mabomu. Mrema alilipua mambomu lakini wengi tuliona hafai kuwa rais.
THE MAN HAS CREDENTIALS BANA ACHA HIZO!WE HAVE TO LOOK BEYOND THE MABOMU AND WE THEN CAN SEE IF HE QUALIFIES NA SIO VIJEMBE!HOJA BANA!
 
Kalamu nakubaliana nawe kabisa kuhusiana na hilo na nadhani kutokana na kwamba kuna baadhi ya wanachama na viongozi kutoka vyama vya upinzani ambao wanakuja hapa, ni bora wachukue maoni yetu. Unajua mwaka 2010 sio mbali kabisa na mikakati ya ushindi inabidi ianze sasa na sio kuongojea hadi inapokaribia muda wa kampeni. Tatizo la vyama vyetu vinakuwaga havina long term plans za mambo yao mbalimbali. Wakati ni huu na wakiamua kufanya ngoja ngoja itawapa nafasi zaidi CCM.

GQ,

viongozi wa upinzani wameaanza long term plan na kama ulisoma ile thread ya Mnyika alikuwa anauliza maoni ya wana JF kwa chama ili ijulikane cha kufanya.

Kuna ile thread ya Rev Kishoka ya focus 2010 pia ilikuwa na very good insight ya what to do. Mambo mengine though yanafanyika in private na kuna wengi tu wamemtumia Mnyika mapendekezo yao kwenye PM.

Tusife moyo kwani nchi hii ni sisi ndio tutaingoa toka makucha ya mafisadi.
 
Back
Top Bottom