The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Mkuu kampeni yako inaonekana kuwa nzuri na una dhamira kabisa. Jaribu kuwasiliana na Slaa uone kama analo lengo hilo. Unaweza kumsaidia sana.

By the way, mimi naamini humu humu JF kwa wale ambao tumejisajili na hata wale wasomaji tu wamo wanaotarajia kugombea nafasi flani kisiasa. Tafadhali choteni mawazo ya watanzania hapa na mkayafanyie kazi. Taifa linawahitaji na uzalendo wenu unahitajika sana.

Mkipata kuitumia busara katika kusoma mawazo ya wengi humu mtagundua kuwa system ya sasa imewachosha sana. Hawa wenye bahati ya kuingia mtandaoni ni wachache wa wale wengi wenye vilio vya namna hii. Mkiamua (hata mimi) basi kila kitu kinawezekana.

Ahsante kwa mwanzisha mada na wote mnaoendelea kuchangia. Maoni yangu kwa kifupi yalikuwa hayo. Niko tayari kumuunga mkono yule atakayejitokeza hapa na kuthibitisha dhamira yake ya kugombea aidha Ubunge ama Urais ili mradi kwa kauli yake ama maandishi yake adhihirishe kuwa amedhamiria kufanya yaliyo mema kwa jamii ya watanzania husika ili baadaye tumbane kwa kauli hizo.

Mac
 
Mac,

Kama ulivyosema ni kweli wengi tumechoshwa sana na mambo yanayoendelea nchini mwetu.

Mimi siku zote sipendi kujihusisha na siasa na huona siasa ni kama mchezo mchafu lakini nadhani imefika kikomo sasa. Naamini kabisa ni sisi wenyewe Watanzania ndio tutakaoweza kubadilisha hali inayoendelea nyumbani, Ni sisi wenyewe wenye moyo wa uzalendo na nchi yetu ndio tunaoweza kubadilisha mweleko wa nchi yetu.

Tanzania inadidimia kila siku baada ya siku, wananchi wanazidi kuwa masikini, hali ya maisha inazidi kuwa ngumu kila siku ilhali kundi la watu wachache pale nchini linazidi kujitayarisha kwa kutumia migongo ya watanzania wote. Siasa za Tanzania zimekuwa mahali pa kuchumia na kujilimbikizia utajiri, unyonyaji na ufisadi ndio umekithiri.

Ni sisi wenyewe ndio tunaoweza kuitoa nchi hii kwenye hili dimbwi la matatizo. Muda ndio huu na hakuna kungoja. CCM Has to Go, Kikwete Has to Go !!
 
Mheshimiwa Kuongoza ni tofauti na Kukosoa. Kukosoa ni rahisi kuliko kuongoza. Unaweza kuwa bingwa wa kukosoa, lakini tabaan ukawa tobwe katika mkuongoza. Jee una hakika na Waheshimiwa (ma-champion wako) hao ambao umebaini kuwa ni mabingwa wa Kukosoa?

Msikilize Dr. Ricky akichambua fotball katika luninga lakini siku moja alipewa mpira aonyeshe jinsi ya upigaji mzuri wa penalti na hata golini hakuelekeza na badala yake aliwambia wachezaji "nyinyi ndio mnapiga kama hivi - hebu Masha waonyeshe penalti inavyopigwa"

Nakubaliana na wewe kuwa kila mtu ana wito wake unaweza kuwa mkosoaji na mchangiaji mzuri usiwe Kiongozi Bora.
 
Dr Slaa alikuwa katibu wa Baraza la Maaskofu(TEC) kwa nafasi yake alisimamia vizuri sana mipango na miradi ya kanisa katoliki. Na kwa yoyote anayejua hairakia ya kanisa hilo atajua kwamba huyu jamaa ameshaongoza na kuratibu mtandao karibu sawa na uwaziri mkuu wa nchi ama hata urais.

Sasa tumpime kwa ufanisi wake huko. Lakini mimi nina wasiwasi kwamba kutokana na kuwa alikuwa padri wa kanisa katoliki lazima atakuwa Rais mdini anayependelea zaidi wagalatia!

PM
 
Mac,

Kama ulivyosema ni kweli wengi tumechoshwa sana na mambo yanayoendelea nchini mwetu. Mimi siku zote sipendi kujihusisha na siasa na huona siasa ni kama mchezo mchafu lakini nadhani imefika kikomo sasa. Naamini kabisa ni sisi wenyewe Watanzania ndio tutakaoweza kubadilisha hali inayoendelea nyumbani, Ni sisi wenyewe wenye moyo wa uzalendo na nchi yetu ndio tunaoweza kubadilisha mweleko wa nchi yetu. Tanzania inadidimia kila siku baada ya siku, wananchi wanazidi kuwa masikini, hali ya maisha inazidi kuwa ngumu kila siku ilhali kundi la watu wachache pale nchini linazidi kujitayarisha kwa kutumia migongo ya watanzania wote. Siasa za Tanzania zimekuwa mahali pa kuchumia na kujilimbikizia utajiri, unyonyaji na ufisadi ndio umekithiri. Ni sisi wenyewe ndio tunaoweza kuitoa nchi hii kwenye hili dimbwi la matatizo. Muda ndio huu na hakuna kungoja. CCM Has to Go, Kikwete Has to Go !!

Geeque

Umewahi kusoma hapa:http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php

Kuna matumaini ya mabadiliko

Asha
 
Dr Slaa alikuwa katibu wa Baraza la Maaskofu(TEC) kwa nafasi yake alisimamia vizuri sana mipango na miradi ya kanisa katoliki. Na kwa yoyote anayejua hairakia ya kanisa hilo atajua kwamba huyu jamaa ameshaongoza na kuratibu mtandao karibu sawa na uwaziri mkuu wa nchi ama hata urais. Sasa tumpime kwa ufanisi wake huko. Lakini mimi nina wasiwasi kwamba kutokana na kuwa alikuwa padri wa kanisa katoliki lazima atakuwa Rais mdini anayependelea zaidi wagalatia!

PM


Tukianza na udini tutataja na ukabila. Mie ninadhani Slaa angebaki kuwa mbunge aendelee.
 
Dr Slaa alikuwa katibu wa Baraza la Maaskofu(TEC) kwa nafasi yake alisimamia vizuri sana mipango na miradi ya kanisa katoliki.

Na kwa yoyote anayejua hairakia ya kanisa hilo atajua kwamba huyu jamaa ameshaongoza na kuratibu mtandao karibu sawa na uwaziri mkuu wa nchi ama hata urais. Sasa tumpime kwa ufanisi wake huko.

Lakini mimi nina wasiwasi kwamba kutokana na kuwa alikuwa padri wa kanisa katoliki lazima atakuwa Rais mdini anayependelea zaidi wagalatia!

PM

Siamini hivyo kuwa kutokana na Upadri wake atakuwa ni Mdini. Dr. Slaa amekuwa akipigania watanzania bila kujali dini zao. Dr. Slaa alisimama kidete kutetea rasilimali zetu bila kujali itikadi za dini zetu. Dr. Slaa amewaumbua MAFISADI na WANYONYAJI wa CCM ilihali viongozi wa Kikristo na Kiislamu walikuwa wamezubaa wakiendelea kumpigia vigelegele na kumkumbatia Rais Kikwete.

Viongozi wa dini wamekuwa kimya kwa muda mrefu bila kusimama kidete kutetea haki za watanzania. Naamini Dr. Slaa anaweza na atasimamia haki kwa wote. Dr. Slaa for President.
 
Siamini hivyo kuwa kutokana na Upadri wake atakuwa ni Mdini. Dr. Slaa amekuwa akipigania watanzania bila kujali dini zao. Dr. Slaa alisimama kidete kutetea rasilimali zetu bila kujali itikadi za dini zetu. Dr. Slaa amewaumbua MAFISADI na WANYONYAJI wa CCM ilihali viongozi wa Kikristo na Kiislamu walikuwa wamezubaa wakiendelea kumpigia vigelegele na kumkumbatia Rais Kikwete. Viongozi wa dini wamekuwa kimya kwa muda mrefu bila kusimama kidete kutetea haki za watanzania. Naamini Dr. Slaa anaweza na atasimamia haki kwa wote. Dr. Slaa for President.

Agreed Mazee!

Dr Slaa amefanya makubwa kuliko hao viongozi wa dini wanaofumbia macho madudu
 
WAPI PAPAA KADA MPINZANI?

Jamani KADA ametimua kweli nini maana watu wamempamba kwenye hii threads lakini kakaa kimya dah, WE MISS YOU, WE LOVE YOU WE NEED YOUR COMMETS ingawa some times unaboaga lakini bado tunahitaji chalenges zako mheshimiwa sana, pls come on sir...........
 
WAPI PAPAA KADA MPINZANI?

Jamani KADA ametimua kweli nini maana watu wamempamba kwenye hii threads lakini kakaa kimya dah, WE MISS YOU, WE LOVE YOU WE NEED YOUR COMMETS ingawa some times unaboaga lakini bado tunahitaji chalenges zako mheshimiwa sana, pls come on sir...........

Kada angekuwepo hapa pangependeza sana naona amemua kukimbia maana mashambulizi yamemzidi, sisi tunaangalia upande mmoja ndo maana nasema kama kada angekuwepo hali ingekuwa nzuri sana.
 
Ni vigumu sana kuwashinda hawa Mafisadi kwa sasa katika post ya Upresident, ukizingatia watatumia pesa za BOT kuwadanganya watanzania, na ikibidi za kina Chenge na lowassa.

Ninachoweza kushauri ni kuwa pale ambapo wapinzani wanaweza kufika inabidi wafanye nchini juu kuwaelimisha wananchi wa maeneo hayo na kushinda ubunge, hii itasaidia sana ukikuta sehemu nyingi zina upinzani, itawasaidia pia wao kuweza kupata nguvu pia za kuweza kucompete zaidi next time

Nadhani sio haki kuwaachia wapinzani peke yao kueleza mabaya ya MAFISADI hawa waliotuzunguka. Ni wajibu wetu sisi waTZ kusimama kidete kuikomboa nchi yetu.

Saa ya ukumbozi inakaribia kwa TZ na ni sisi watanzania ndio tutakaoifanya saa hiyo itufikie kwa haraka.. jamani ni lazima tujuwe kwamba kila mTZ anahaki ya kuyafikisha haya kwa jamii zetu kwa kiasi cha uwezo wetu.

Tusiishie tu kusoma na kupiga makelele humu lazima tutoke na tuieleweshe jamii. Hubu tufikirie gharama za UFISSDI huu kwa watoto wetu na vizazi vijavyo ni jukumu letu watanzania kuwatokomeza mafisadi kwa gharama zote kwani tukikaa kimnya hatuwatendei haki wale ndugu zetu walioko vijijini
 
Ulivyosema huna habari zake nikaingia kwenye google search kwa kuangika maneno dr Wlbroad Slaa, angalia ana blogspot lakini hajapost kitu,http://www.chadema.net/blogu/slaa/
Google search yangu nimeieneleza kwa jina la manaJF aliyenikuna kwa itikadi yake aliyoipost humu JF,nimesearch kwa jina la kahangwa,nikagundua yawezekana ndio George Kahangwa,naona naye ana blogspot kwa jina hilo hilo.samahani kama sio yeye,but I see something in this JF member by that name

Waridi,
Ndimi,lakini please ebu endelea kulitafakari pendekezo la ugombea wa Dr.Slaa. Namfahamu kwa karibu.Ni mtu aliyejaliwa hekima nyingi,anayo aiba ya kuwa kiongozi wa ngazi tajwa, ni mjuvi wa mambo kwa kiwango kikubwa na uzoefu wake katika siasa unatosha kabisa.
Achana na sisi amabao licha ya umri kutotosha,bado tuko masomoni.
 
Tanzania tunahitaji kiongozi mtendaji na si kiongozi wa kuongea siasa siasa na kutoa misamiati migumu migumu isiyoweza kueleweka kwa wananchi wa kawaida.

Nikiangalia kwa mbali tunahitaji kiongozi asiye mwoga asiyehitaji kubebwa ndipo awe RAiS.

Asiyehitaji majambazi(MAFISADI) kuingia ikulu. Tunahitaji mtu asiyehitaji kushauriwa shauriwa ndipo atoe maaamuzi.

Tunahitaji Siasa isiwe silaha ya kuangamizia wananchi. Tunahitaji RAis wa kuangamiza MAFiSADi na kukubali kuwepo na marekebisho ya katiba(kuandikwa upya) ili kutoa mstakabali wa Taifa masikini sana duniani kama Tanzania.
 
JJ unaoppose au unasupport mada ya Dr Slaa kugombea Urais 2010?

Mama

Naunga mkono mada kuendelea kujadiliwa na mawazo ya pande zote kuendelewa kutolewa; ama kuhusu maoni yangu, naomba nisiyatoe kwa sasa.

JJ
 
Nimekusikia mdogo wangu, Mimi naoppose mada.

Natumaini hupingi mada kujadiliwa; unapinga suala la yeye kugombea. Ni nzuri, hayo ni maoni yako-unaweza kuyakubali kwa upande wako lakini wenzako wasiyakubali kwa upande wao. Ndio maana nikasema naunga mkono huu mjadala uendelee.

Mpaka siku, tutakubaliana au tutakubaliana kutokubaliana. Wakati mwafaka ukifika nami nitatoa maoni yangu kama mwanachama.

JJ
 
Natumaini hupingi mada kujadiliwa; unapinga suala la yeye kugombea. Ni nzuri, hayo ni maoni yako-unaweza kuyakubali kwa upande wako lakini wenzako wasiyakubali kwa upande wao. Ndio maana nikasema naunga mkono huu mjadala uendelee. Mpaka siku, tutakubaliana au tutakubaliana kutokubaliana. Wakati mwafaka ukifika nami nitatoa maoni yangu kama mwanachama.

JJ



Yah, sipingi mada, napinga Dr Slaa kugombea urais 2010. Nimekupata kabisa
 
Dr Slaa alikuwa katibu wa Baraza la Maaskofu(TEC) kwa nafasi yake alisimamia vizuri sana mipango na miradi ya kanisa katoliki. Na kwa yoyote anayejua hairakia ya kanisa hilo atajua kwamba huyu jamaa ameshaongoza na kuratibu mtandao karibu sawa na uwaziri mkuu wa nchi ama hata urais. Sasa tumpime kwa ufanisi wake huko. Lakini mimi nina wasiwasi kwamba kutokana na kuwa alikuwa padri wa kanisa katoliki lazima atakuwa Rais mdini anayependelea zaidi wagalatia!

PM

So far so good. Ni michango kama hii ndio itatusaidia wengi kumfahamu Dr. Slaa ni mtu wa aina gani hasa!

Upadre ilikuwa ni kazi kama kazi zingine, na haukumuondolea u-Tanzania wake. Kama ni mzalendo kwa Taifa la Tanzania, atakuwa tayari kuwatumikia watanzania wenzake bila kujali dini zao.
Mtu mdini, sio lazima awe alishakuwa padre au mchungaji au shekh.
 
Back
Top Bottom