Waheshimiwa!
Mtu anaponunua gazeti siyo kwamba anataka kusoma habari zote, wengine Siasa, Uchumi, Nafasi za Kazi, Michezo na wengine Vikatuni ambavo mara nyingi huonekana mwishoni mwa gazeti fahamuni kuwa navyo vinawashabiki wake!
Itabidi niwe nakuja na mada katuni iliwale wataalamu wanaojua kuvisoma ujumbe wake, naamini hao watakuwa wanafaidika navyo.
Baada ya kuifuatilia mada hii kuanzia mwanzo wake mpaka hapa ilipofikia, nimegundua kunawatu wachache sana ambao ni wataalamu wakusoma vijikatuni;
Kumradhi kuwataja majina siyo vyema lakini ni vizuri nikiwataja iliwajitambue wao wana uwezo wa kusoma vikatuni.
1:Mama - huyu anauwezo wa kusoma vikatuni lakini ni mchoyo ama hapendi kuongea sana! Uwezo wake nimeuona kwenye Post 125, Pg 13
2: Kubwa Jinga- Huyu pia anauwezo wa kusoma katuni: Hata mimi kwa mara ya kwanza nilikuwa hata sitaki kusoma post zake nikiamaini ni kubwa jinga; nadhani jina ndilo linamponza mpaka watu wanafikiri hana lolote. Kwa jinsi nilivyomsoma kubwa jinga ni mtu anayevitakia Mema vya Siasa na wala siyo mshirika wa chama chochote cha Siasa, lakini hataki kuwafumbulia watu: Soma Post yake No.154, Uk.16. Mambo yote ameyaweka wazi ilikuviokoa vya vya Siasa, na ameniokolea muda sana maana nilitaka kuzungumzia kitu hicho hicho.
3: Jamco Za - huyu ni mtu mwenye malengo mema na vyama vya Siasa pinzani na SiSi-eM: Post 188;Uk 19, utatambua nia yake njema.
Tuendelee na staili yetu ya Kikatuni-katuni.
KAMA CHADEMA WANATAKA WASHUHUDIE ANGUKO KUBWA LA CHAMA CHAO...wampeleke Mh. Dr. Wilbroad Slaa akachukue FOMU ya KUGOMBEA URAISI.
Nieleweke vyema sina maana kwamba Chadema na vyama vinginevyo wasisimamishe wagombea Urais 2010..Wasimamishe lakini siyo Slaa, Zitto, Kimario..ah kumbe huyu ni wa CCM..lakini siyumo? maana hapa sizungumzii Ushabiki wa Kivyama.
Nataka niwathibitishie Wanavyama Shirika, katika vita vita waliyonayo SiSi-eM ni kumwondoa Slaa na jamii yake Bungeni, halafu ninyi wenyewe mnataka kuwasaidia kumwondoa Bungeni!!!??? Kweli ninyi ni njiti kweli..ah! samahani nimejikuta limenitoka tu haikuwa nia yangu kuwaita hivyo.
KIKATUNI:
Hawa watu mpaka wakaamua kutunga wimbo kupitia Bendi yao zamani TOT sijui leo nasikia inajina jipya ilikuhamasihana jinsi yakuwang'oa Bungeni hao jamaa wenye Siasa Chimbuzi (nadhani niwatumishi wa Umma)
Baadhi ya Mashairi yake yanasema:-
Eh,eh eh, eh!!! kitim-tim,
kitimtim umekiona leo,
Kwenye nyumba ya Starehe kijiko kimeingiaje?
Kwenye nyumba ya Starehe mwendawazimu kaingiaje?
....nakuendelea.....
Wenzenu walishafanya Bungeni ni Sehemu ya Starehe,sasa wakashangaa kuona kunakijiko kimeingia kuwatibulia starehe zao (UFISADI na matendo mengine yafananayo na hayo)- ambayo ndiyo akina Dr. Slaa na wenziwake!Cha ajabu ninyi wenyewe mnataka kuwasaidia kutoa kijiko kwenye nyumba ya starehe:
Naapa: HAKI YA MUNGU TENA VILE! CHADEMA WASIFANYE KOSA LA KUMUONDOA DR. SLAA BUNGENI!! ninaukakika asilimia 90,Siku tu Dr. Slaa atakapochukua FOMU YA KUGOMBEA URAISI kwenye radio vijijini, lazima huu wimbo utapigwa:
Oh! oh! MCHIMBA KISIMA, KATUMBUKIA MWENYEWE!!!!KAINGIAA!!
Nakisha Mkuu wa Kaya atakuwa na safari ya Kiserikali Ulaya..lengo lake itakuwa nikwenda kupumzika baada ya kazi ngumu inayosababishwa na Kijiko!! Asomaye na afahamu.
Tatitito watu wa humu wanapenda Ushahidi,sasa mimi nisiyekuwa nao nitafanya je sasa?
Ngoja nijaribu kupanga kama KJ:
1: Kwa wale walifuatilia kampeni kwa ajili ya Uchaguzi wa '05,Karatu nadhani kwenye bajeti ya SiSi-eM walitumia garama kubwa sana ilikuhakikisha Slaa harudi Bungeni.
2: FAIDA ZA SLAA KUWA BUNGENI - ndipo mahali pekee ambapo Chama Kinajitangaza kwa garama Nafuu kutokana na hoja zitolewazo na mbunge husika.
3: HASARA ZA SLAA KUGOMBEA URAISI- hili liko wazi, na nikubwa saana!,,Sina maana kwamba hafai, ila ukweli hatopata kura stahiliki (50%)ilikuweza kumuingiza Ikulu, halafu atakuwa amepoteza Ubunge, dhen atakapokuwa akitoa maoni watu watasema..ah! huyo si alishindwa Uraisi ndiyo maana anasema hivyo!
4: Mwl. ama Mzee haambiliki, japo alikataa asitwe kwa jina hilo na kuahidi kuwa litakwenda mtu. Alimshauri Mh. Lyatonga, aache kugombea Uraisi akagombee Ubunge watu wakajua, SiSi-eM imeshaona itashindwa! kwa vile wazo hilo lilitolewa na Mzee wa CCM, lakini angelifuata Ushauri wake NCCR ya Mrema ingekuwa wapi sasa hivi?..lakini baada ya kukataa ushauri bila kufikiria unakimbilia itikadi za kichama, nadhani ndiko kulikuja sababisha anguko la NCCR..sasa hivi, ALM akizungumza nani anamsikiliza tena?..hata kama hoja yake inaukweli ndani yake!
Namalizia kwa Kusema,
Sipendi kuwapa Ki-bri, ila tumeambiwa kwenye ukweli tuseme.
Huku Kijijini kwetu,ambako ndiyo wapiga kura wengi tupo Ukisema CUF tunajua ni Maalimu Self, hawa akina Lipumba na wengine mnawajua nyie, Ukisema CHADEMA tunajua ni Dr. Slaa mbuge wa Karatu, Mbowe, sijui nani hao mnawajua nyie, Pia ukitaja NCCR-MAGEUZI, haki yanani vile siyo utani bado tunajua ni Augustine Mrema, sasa kwa vile mimi ndiyo nimetoka Mjini naanza kuwaelimisha!
Ee! Mwenyezi Mungu sijui hawa wanadamu wamenielewa??? ..umenipa kazi ngumu sana kuwaelimisha.
Umeme umekaribia kukatika naomba nitoe ONYO: kwa Wanachadema na Wote wenye Mapenzi mema na nchi hii, naomba sana tusijekosea kukiondoa kijiko kwenye Nyumba ya Starehe; Kama ikiwezekane Dr. Slaa afie Bungeni, hata akifikisha umri wa Mugabe (84) asikubali kung'atuka, labda aje mwenye kasi yake.
MAWAZO MEMA YA HAWA JAMAA:
Mama
Yah, sipingi mada, napinga Dr Slaa kugombea urais 2010. Nimekupata kabisa
Jamco Za
Your right man, tunamhitaji zaidi Dr. Siraa bungeni na sio kwenye uraisi, ambako atazungukwa na mafisadi wa kila aina.
Kubwa Jinga
Mimi napingana na hilo wazo la kumpendekeza Dr. Slaa kuwa mgombea uraisi. Ku-focus kwenye uraisi pekee ni moja ya sababu kubwa ya wapinzani kushindwa kwenye kila uchaguzi. Ufumbuzi wa matatizo ya mtanzania hautatokana na upinzani kuingia ikulu, bali kwa kubadilisha mfumo mzima wa kiutawala. Ni vema tukaelewa yafuatayo;
1. Nchi haijengwi na mtu mmoja na ndio maana Nyerere yalimshinda. Kwa hiyo kama mfumo wa kiutawala hautabadilishwa na kuondoa madaraka makubwa aliyonayo raisi na serikali yake hivi sasa, na kuyahamishia bungeni, mahakamani na kwa wananchi, yeyote yule atakayeingia anaweza akaifuja nchi bila kipingamizi.
2. Hadi hivi sasa hakuna dalili zozote zinazoonyesha uwezekano wa CCM kushindwa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi 2010, hata baada ya kulipuliwa kwa mafisadi wote wakiwa wanaCCM. Uchaguzi wa hivi karibuni Kiteto inatoa picha ya ugumu uliopo.
3. Mgawanyiko na tamaa katika kambi ya upinzani ni kikwazo kikubwa sana kwao kupata ushindi. Hata kama Nyerere angefufuka na kuwa mgombea wa chama kimojawapo cha upinzani, bado ingekuwa vigumu kwao kuunganisha nguvu zao kuing'oa CCM.
4. Uongozi mbovu ndani ya vyama vya upinzani nao ni kikwazo kikubwa katika kuwavutia wasomi na wafanyabiashara wengi ambao wanakerwa na CCM. Ni muhimu kutatua masuala kama ya udini, ukabila na umungu-mtu ndani ya vyama ili kuondoa hali ya hivi vyama kuwa na ushabiki wa kimajimbo na wenye upeo mwembamba.
5. Nyerere alisema upinzani wa kiukweli TZ utatoka ndani ya CCM, na mimi nakubaliana naye kabisaa hata baada ya kufariki. Hili litawezekana kwa CCM wenyewe kupingana au kwa wapinzani kuwa na vyama ambavyo vitawavutia walioCCM kuhamia kwao. Hivi sasa la awali la CCM kupingana linakaribia linalohitajika ni kwa wapinzani kuunda mazingira yatakayoweza kuwavutia wanaCCM kuhamia kwao.
6. Msisitizo kwa upinzani uwe katika kuandaa wabunge wengi iwezekanavyo. Na hii ndio sababu kubwa ya kupinga kumuingiza Dr. Slaa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi. Uwezekano wa yeye kushinda ubunge ni mkubwa kuliko uraisi na isingekuwa vema akakosekana kwenye ulingo wa kisiasa kwa miaka 5, kama ilivyokuwa kwa Mrema, na kushindwa kufanya yale tuliyoona anaweza kuyafanya akiwa bungeni. Kila mpinzani aliye na uwezo wa kushinda ubunge, aanze kujengwa hivi sasa kwenye majimbo yao ili agombee ubunge na kuimarisha upinzani bungeni.
7. Upinzani wapunguze hili la ku-focus zaidi kwenye uraisi, na kutumia rasilimali zao kwenye ubunge. Kwa mfano CHADEMA walitumia zaidi ya TShs 220millioni (30% ya pesa waliyokuwa nayo) kwenye kukodisha helicopter tu. Lakini jumla ya pesa yote walizowapa wagombea wa ubunge wao ilikuwa ni TShs. 59 millioni tu (8% tu). Kama wangewekeza zaidi kwenye wabunge labda watu kama Bob Makani wangekuwa wabunge hivi sasa.
Changamoto langu kwa vyama vya upinzani ni kuungana na kuwekeza zaidi kwenye ubunge maana kwa hali ilivyo hivi sasa, sio rahisi kuing'oa CCM in 2010.
Mtu anaponunua gazeti siyo kwamba anataka kusoma habari zote, wengine Siasa, Uchumi, Nafasi za Kazi, Michezo na wengine Vikatuni ambavo mara nyingi huonekana mwishoni mwa gazeti fahamuni kuwa navyo vinawashabiki wake!
Itabidi niwe nakuja na mada katuni iliwale wataalamu wanaojua kuvisoma ujumbe wake, naamini hao watakuwa wanafaidika navyo.
Baada ya kuifuatilia mada hii kuanzia mwanzo wake mpaka hapa ilipofikia, nimegundua kunawatu wachache sana ambao ni wataalamu wakusoma vijikatuni;
Kumradhi kuwataja majina siyo vyema lakini ni vizuri nikiwataja iliwajitambue wao wana uwezo wa kusoma vikatuni.
1:Mama - huyu anauwezo wa kusoma vikatuni lakini ni mchoyo ama hapendi kuongea sana! Uwezo wake nimeuona kwenye Post 125, Pg 13
2: Kubwa Jinga- Huyu pia anauwezo wa kusoma katuni: Hata mimi kwa mara ya kwanza nilikuwa hata sitaki kusoma post zake nikiamaini ni kubwa jinga; nadhani jina ndilo linamponza mpaka watu wanafikiri hana lolote. Kwa jinsi nilivyomsoma kubwa jinga ni mtu anayevitakia Mema vya Siasa na wala siyo mshirika wa chama chochote cha Siasa, lakini hataki kuwafumbulia watu: Soma Post yake No.154, Uk.16. Mambo yote ameyaweka wazi ilikuviokoa vya vya Siasa, na ameniokolea muda sana maana nilitaka kuzungumzia kitu hicho hicho.
3: Jamco Za - huyu ni mtu mwenye malengo mema na vyama vya Siasa pinzani na SiSi-eM: Post 188;Uk 19, utatambua nia yake njema.
Tuendelee na staili yetu ya Kikatuni-katuni.
KAMA CHADEMA WANATAKA WASHUHUDIE ANGUKO KUBWA LA CHAMA CHAO...wampeleke Mh. Dr. Wilbroad Slaa akachukue FOMU ya KUGOMBEA URAISI.
Nieleweke vyema sina maana kwamba Chadema na vyama vinginevyo wasisimamishe wagombea Urais 2010..Wasimamishe lakini siyo Slaa, Zitto, Kimario..ah kumbe huyu ni wa CCM..lakini siyumo? maana hapa sizungumzii Ushabiki wa Kivyama.
Nataka niwathibitishie Wanavyama Shirika, katika vita vita waliyonayo SiSi-eM ni kumwondoa Slaa na jamii yake Bungeni, halafu ninyi wenyewe mnataka kuwasaidia kumwondoa Bungeni!!!??? Kweli ninyi ni njiti kweli..ah! samahani nimejikuta limenitoka tu haikuwa nia yangu kuwaita hivyo.
KIKATUNI:
Hawa watu mpaka wakaamua kutunga wimbo kupitia Bendi yao zamani TOT sijui leo nasikia inajina jipya ilikuhamasihana jinsi yakuwang'oa Bungeni hao jamaa wenye Siasa Chimbuzi (nadhani niwatumishi wa Umma)
Baadhi ya Mashairi yake yanasema:-
Eh,eh eh, eh!!! kitim-tim,
kitimtim umekiona leo,
Kwenye nyumba ya Starehe kijiko kimeingiaje?
Kwenye nyumba ya Starehe mwendawazimu kaingiaje?
....nakuendelea.....
Wenzenu walishafanya Bungeni ni Sehemu ya Starehe,sasa wakashangaa kuona kunakijiko kimeingia kuwatibulia starehe zao (UFISADI na matendo mengine yafananayo na hayo)- ambayo ndiyo akina Dr. Slaa na wenziwake!Cha ajabu ninyi wenyewe mnataka kuwasaidia kutoa kijiko kwenye nyumba ya starehe:
Naapa: HAKI YA MUNGU TENA VILE! CHADEMA WASIFANYE KOSA LA KUMUONDOA DR. SLAA BUNGENI!! ninaukakika asilimia 90,Siku tu Dr. Slaa atakapochukua FOMU YA KUGOMBEA URAISI kwenye radio vijijini, lazima huu wimbo utapigwa:
Oh! oh! MCHIMBA KISIMA, KATUMBUKIA MWENYEWE!!!!KAINGIAA!!
Nakisha Mkuu wa Kaya atakuwa na safari ya Kiserikali Ulaya..lengo lake itakuwa nikwenda kupumzika baada ya kazi ngumu inayosababishwa na Kijiko!! Asomaye na afahamu.
Tatitito watu wa humu wanapenda Ushahidi,sasa mimi nisiyekuwa nao nitafanya je sasa?
Ngoja nijaribu kupanga kama KJ:
1: Kwa wale walifuatilia kampeni kwa ajili ya Uchaguzi wa '05,Karatu nadhani kwenye bajeti ya SiSi-eM walitumia garama kubwa sana ilikuhakikisha Slaa harudi Bungeni.
2: FAIDA ZA SLAA KUWA BUNGENI - ndipo mahali pekee ambapo Chama Kinajitangaza kwa garama Nafuu kutokana na hoja zitolewazo na mbunge husika.
3: HASARA ZA SLAA KUGOMBEA URAISI- hili liko wazi, na nikubwa saana!,,Sina maana kwamba hafai, ila ukweli hatopata kura stahiliki (50%)ilikuweza kumuingiza Ikulu, halafu atakuwa amepoteza Ubunge, dhen atakapokuwa akitoa maoni watu watasema..ah! huyo si alishindwa Uraisi ndiyo maana anasema hivyo!
4: Mwl. ama Mzee haambiliki, japo alikataa asitwe kwa jina hilo na kuahidi kuwa litakwenda mtu. Alimshauri Mh. Lyatonga, aache kugombea Uraisi akagombee Ubunge watu wakajua, SiSi-eM imeshaona itashindwa! kwa vile wazo hilo lilitolewa na Mzee wa CCM, lakini angelifuata Ushauri wake NCCR ya Mrema ingekuwa wapi sasa hivi?..lakini baada ya kukataa ushauri bila kufikiria unakimbilia itikadi za kichama, nadhani ndiko kulikuja sababisha anguko la NCCR..sasa hivi, ALM akizungumza nani anamsikiliza tena?..hata kama hoja yake inaukweli ndani yake!
Namalizia kwa Kusema,
Sipendi kuwapa Ki-bri, ila tumeambiwa kwenye ukweli tuseme.
Huku Kijijini kwetu,ambako ndiyo wapiga kura wengi tupo Ukisema CUF tunajua ni Maalimu Self, hawa akina Lipumba na wengine mnawajua nyie, Ukisema CHADEMA tunajua ni Dr. Slaa mbuge wa Karatu, Mbowe, sijui nani hao mnawajua nyie, Pia ukitaja NCCR-MAGEUZI, haki yanani vile siyo utani bado tunajua ni Augustine Mrema, sasa kwa vile mimi ndiyo nimetoka Mjini naanza kuwaelimisha!
Ee! Mwenyezi Mungu sijui hawa wanadamu wamenielewa??? ..umenipa kazi ngumu sana kuwaelimisha.
Umeme umekaribia kukatika naomba nitoe ONYO: kwa Wanachadema na Wote wenye Mapenzi mema na nchi hii, naomba sana tusijekosea kukiondoa kijiko kwenye Nyumba ya Starehe; Kama ikiwezekane Dr. Slaa afie Bungeni, hata akifikisha umri wa Mugabe (84) asikubali kung'atuka, labda aje mwenye kasi yake.
MAWAZO MEMA YA HAWA JAMAA:
Mama
Yah, sipingi mada, napinga Dr Slaa kugombea urais 2010. Nimekupata kabisa
Jamco Za
Your right man, tunamhitaji zaidi Dr. Siraa bungeni na sio kwenye uraisi, ambako atazungukwa na mafisadi wa kila aina.
Kubwa Jinga
Mimi napingana na hilo wazo la kumpendekeza Dr. Slaa kuwa mgombea uraisi. Ku-focus kwenye uraisi pekee ni moja ya sababu kubwa ya wapinzani kushindwa kwenye kila uchaguzi. Ufumbuzi wa matatizo ya mtanzania hautatokana na upinzani kuingia ikulu, bali kwa kubadilisha mfumo mzima wa kiutawala. Ni vema tukaelewa yafuatayo;
1. Nchi haijengwi na mtu mmoja na ndio maana Nyerere yalimshinda. Kwa hiyo kama mfumo wa kiutawala hautabadilishwa na kuondoa madaraka makubwa aliyonayo raisi na serikali yake hivi sasa, na kuyahamishia bungeni, mahakamani na kwa wananchi, yeyote yule atakayeingia anaweza akaifuja nchi bila kipingamizi.
2. Hadi hivi sasa hakuna dalili zozote zinazoonyesha uwezekano wa CCM kushindwa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi 2010, hata baada ya kulipuliwa kwa mafisadi wote wakiwa wanaCCM. Uchaguzi wa hivi karibuni Kiteto inatoa picha ya ugumu uliopo.
3. Mgawanyiko na tamaa katika kambi ya upinzani ni kikwazo kikubwa sana kwao kupata ushindi. Hata kama Nyerere angefufuka na kuwa mgombea wa chama kimojawapo cha upinzani, bado ingekuwa vigumu kwao kuunganisha nguvu zao kuing'oa CCM.
4. Uongozi mbovu ndani ya vyama vya upinzani nao ni kikwazo kikubwa katika kuwavutia wasomi na wafanyabiashara wengi ambao wanakerwa na CCM. Ni muhimu kutatua masuala kama ya udini, ukabila na umungu-mtu ndani ya vyama ili kuondoa hali ya hivi vyama kuwa na ushabiki wa kimajimbo na wenye upeo mwembamba.
5. Nyerere alisema upinzani wa kiukweli TZ utatoka ndani ya CCM, na mimi nakubaliana naye kabisaa hata baada ya kufariki. Hili litawezekana kwa CCM wenyewe kupingana au kwa wapinzani kuwa na vyama ambavyo vitawavutia walioCCM kuhamia kwao. Hivi sasa la awali la CCM kupingana linakaribia linalohitajika ni kwa wapinzani kuunda mazingira yatakayoweza kuwavutia wanaCCM kuhamia kwao.
6. Msisitizo kwa upinzani uwe katika kuandaa wabunge wengi iwezekanavyo. Na hii ndio sababu kubwa ya kupinga kumuingiza Dr. Slaa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi. Uwezekano wa yeye kushinda ubunge ni mkubwa kuliko uraisi na isingekuwa vema akakosekana kwenye ulingo wa kisiasa kwa miaka 5, kama ilivyokuwa kwa Mrema, na kushindwa kufanya yale tuliyoona anaweza kuyafanya akiwa bungeni. Kila mpinzani aliye na uwezo wa kushinda ubunge, aanze kujengwa hivi sasa kwenye majimbo yao ili agombee ubunge na kuimarisha upinzani bungeni.
7. Upinzani wapunguze hili la ku-focus zaidi kwenye uraisi, na kutumia rasilimali zao kwenye ubunge. Kwa mfano CHADEMA walitumia zaidi ya TShs 220millioni (30% ya pesa waliyokuwa nayo) kwenye kukodisha helicopter tu. Lakini jumla ya pesa yote walizowapa wagombea wa ubunge wao ilikuwa ni TShs. 59 millioni tu (8% tu). Kama wangewekeza zaidi kwenye wabunge labda watu kama Bob Makani wangekuwa wabunge hivi sasa.
Changamoto langu kwa vyama vya upinzani ni kuungana na kuwekeza zaidi kwenye ubunge maana kwa hali ilivyo hivi sasa, sio rahisi kuing'oa CCM in 2010.