Mkuu FMES et al,
Nakubaliana na wewe kuwa bila kujaribu huwezi kujua matokeo. Lakini ni vema kutumia uzoefu wa awali na data zilizopo kujaribu kuangalia future (forecasting) na sio kufanya mambo kienyeji-enyeji au kwa jazba kama watu wasioenda shule au kwa ushabiki kama Mwafrika wa Kike na bibie Asha.
URAISI
Katika uchaguzi uliopita, Kikwete alipata 80.3% (9,123,952), Lipumba 11.7% (1,327,125) na Mbowe alipata 5.9% (668,756). Kwa Chadema ni mikoa 4 ambayo walipata zaidi ya 10%, Kilimanjaro, Arusha, Mara na Manyara. Kigoma walikaribia kidogo na kupata 9.4%. Kilimanjaro peke yake ndio walipata zaidi ya 20% (ambayo ilikuwa 20.6%). Kwenye hizo kura alizopata Mbowe, karibu 40% zimetoka mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Mara with Kilimanjaro having almost 25%. Kwa hiyo kwa mtu mwenye akili yake, hata ukiweka factor za EPA, Chenge, Richmond, Mkapa n.k., unless kama JK naye akaguswa moja kwa moja kama Chenge, sidhani kama huku kuzomea kunakoongelewa kuna ukubwa wa kutosha kubadilisha mawazo ya hata say 20% ya waliompigia JK kura. Tusisahau pia kuwa, hawa wanaojiuzulu bado waTZ wengi wanaona kama vile Kikwete ndie anayewashughulikia.
Unaweza kukagua matokeo ya uchagusi kwenye attachment, Nimeyatoa NEC website au www ya Chadema
To be Contd.....
Wewe unamlaumu Mbowe na CHADEMA kwa kutumia milioni 700(kati ya hizo milioni 200 kwa helikopta) na kupata kura hizo; unajua Lipumba na CUF walitumia kiasi gani kupata kura hizo? Si unakumbuka mwenyewe walisema wametumia takribani bilioni mbili?Hii ni sawa na milioni 2000. Sasa piga mahesabu, nani amemefanikiwa zaidi kwa fedha alizotumia.
Haya sasa sema Chama Cha Mafisadi kilitumia bei gani kutoka BOT, EPA nk kwenye hizo kampeni za 2005. Tshirt na Kofia pekee ziliwagharimu bilioni 20(milioni 20,000). Si ajabu nikaambiwa walitumia bilioni 200 kwenye zile kampeni kwa ujumla. Si ajabu kwa kuwa najua majimbo ambayo jimbo moja ilitumika bilioni 1(milioni 1000) Eti 'kulikomboa'. Sasa hao nao waliotumia mapesa yote hayo wakapata 80% nao utawesemaje?
Na kwa kuwa hawakufanya 'uamuzi wa kijinga' wa kutumia helikopta kama CHADEMA kwanini wasingepata 100% kwa mapesa yote hayo?
Soma tena nilichokwambia mwanzo: Hoja yako haina uzito. Mrema alipata kura hizo wakati huo kwa kuwa CCM ilikuwa haijajiandaa kikamilifu kuiba na kulikuwa na wave kubwa ya upinzani nchi nzima. Mwaka 2000 Mkapa alikuwa amejizatiti wakati huo huo NCCR ilikuwa imeanguka, mwaka 2005 kulikuwa na ujio wa Kikwete kama Tumaini lililorejea wakati huo huo TLP na CUF zilikuwa zinaelekea kushuka.
Mwaka 2010 Kikwete atakuwa ameporomoka wakati huo huo hamasa ya upinzani na CHADEMA inazidi kuendelea nchi nzima na kuna ushirikiano wa vyama. Ufisadi umetamalaki na watanzania wameelewa zaidi. Sasa unategemea nini?
Siasa ni kitu cha ajabu, lolote laweza kutokea wakati wowote. Kwa hiyo usijidanyanye eti kwa kuwa Kikwete amepata 80 ya kura upinzani 20 basi kibao hakiwezi kugeuka upinzani ukapata 80 Kikwete 20!
Nikupe mfano mdogo tu, hebu angalia matokeo ya Urais Tarime na Karatu mwaka 2000 halafu angalia yalivyokuwa ghafla mwaka 2005 mpaka Mbowe amepata 30-40 percent! Kutokana na ufisadi uliokithiri, sitashangaa kama maeneo yote yakawa zaidi ya Tarime na Karatu mwaka 2010.
Umeona jinsi watu wa Kiteto mijini walivyobadilika na kutoa kura nyingi kwa upinzani kuliko CCM. Umeona jinsi ambavyo CCM ilibidi ipeleke nguvu yote. Umeona yule mbunge wa Kiteto jinsi ambavyo anazomewa hivi sasa akipita kule. Sasa jua kwamba hataweza hayo nchi nzima, by election ni tofauti na election nchi nzima.
Halafu, kura za upinzani sivyo kama unavyoziona kwenye matokeo- CCM walijiokotea kura nyingi tu kama sio kuiba, tazama matokeo ya udiwani na ubunge.
Utakufata maeneo mengi sasa CHADEMA haikuwa na wagombea hivyo hapakuwa na mtu wa kulinda kura ama palikuwa na wagombea dhaifu kupindukia ambao hawakuwa na mawakala. Lakini 2010 kwa muamka uliokuwepo hali itakuwa tofauti CCM itabanwa kila mahali. Pia jiulize 2005 CHADEMA ilikuwaje?
Iliingia ikiwa haina nguvu, hata uchaguzi wa 2004 imeshinda vijiji na mitaa michache sana. Sasa subiri uone mwaka 2009 kabla ya kumaliza kazi 2010. CHADEMA kabla ya Mbowe kugombea Urais ilikuwa ni chama cha kawaida sana.Urais umesaidia sana kukiamsha chama.
Mwaka 2003 CHADEMA haikuwa ikijadiliwa kama hivi, lakini sasa tunaanza kujadili toka 2008 kuhusu mgombea wa CHADEMA wa mwaka 2010 hii inamaanisha kuwa kuna watu wanafanya maamuzi leo ya kumpigia mgombea wa CHADEMA tofauti na Mbowe alivyoibuka kwa ghafla tu wakati wa uchaguzi 2010.
Sasa Mbowe, Dr Slaa na wengine kama wanataka kugombea uchaguzi 2010 wataanza kuaandaa mazingira mapema kabla ya 2010 ikiwemo kujenga mtandao wa chama nchi nzima.
Sasa hiki ndicho kinachokuuma Kubwa Jinga Jinga, Chama Cha Mafisadi kuondoka katika Urais.
Hebu angalia haya matokeo ya Urais hapa linganisha na mwaka 2000 utoana jinsi ambavyo kuna maeneo yamebadilika ghafla ya kupigia upinzani na mengi ya majimbo hayo sio ya Kilimanjaro kabisa:
http://www.chadema.net/uchaguzi/matokeo/urais_1.php
Halafu urudi tena
Asha