We Kubwa Jinga Jinga unakaa nchi gani? We hujui kwamba haya matokeo ya Ubunge ni pamoja na uwizi waliufanya kule kwa Balozi Ngaiza,Mbogoro, Pesha nk(CHADEMA); Lwakatare CUF nk, Lema(TLP Arusha) nk? Hivi CCM wasingeiba wangepoteza majimbo mangapi kwa staili hii?
Umetoa mfano wa Mnyika wa CHADEMA, si umeona hapa jinsi ambayo aliyalalamikia matokeo yake kwamba yamepikwa?
"Kwa hali iliyodhihirisha wazi kuwa matokeo yalipikwa, waliopiga kura za Ubunge walikuwa 185,684 wakati waliopiga kura za Rais walikuwa 152,525 na hivyo kufanya tofauti ya kura za Ubunge na urais kufikia 33,159. Katika hali ya kawaida na katika uchaguzi uliofanyika kwa wakati mmoja ilikuwa ni vigumu kwa tofauti kubwa ya kura kiasi hiki. Na hata kama wananchi wangekuwa hawapendi kupiga kura za rais kwa kuwa mpiga kura alikuwa akipewa karatasi zote tatu kura hizi zilipaswa kuwepo katika kura zilizoharibika kitu ambacho hakikutokea.
Kimsingi, hujuma za kimfumo na kimkakati za chama tawala ndiyo hasa vilivyofanya uchaguzi kutokuwa huru na haki. Kabla ya uchaguzi wajumbe wa nyumba kumi waliandikisha kadi za wapiga kura kwa lengo la kuwakosesha kupiga kura wale walioelekea kupigia kura upinzani na pia kuweza kuwapa rushwa wengine ili kupigia CCM.Wananchi wengi walizuiwa kupiga kura licha ya kuwa na kadi kutokana na ama majina yao kutoonekana kwenye orodha au kuwa tofauti na kwenye daftari. Kulikuwa na kampeni za vitisho kwa wapiga kura hususani katika kata za vijijini. Wananchi wengi walihongwa kukipigia kura chama tawala hii ni pamoja na wengi kujifanya hawajui kusoma na kuandika ingawa baadhi yao vitambulisho vyao vya kupigia kura vilionekana kuwa na saini. Kulikuwa na mapungufu kadhaa katika mpangilio na idadi ya vituo vya kupigia kura. Halikadhalika, kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa kanuni na sheria katika ujumlishaji wa kura za ubunge. Kwa kiasi kidogo mtandao hafifu wa chama katika maeneo machache na udhaifu wa baadhi ya mawakala navyo vilichangia kushindwa katika vituo vichache ambavyo visingeathiri matokeo kwa kiasi kikubwa kwa ujumla. Na mwisho matokeo ya ubunge jimbo la Ubungo yakatangazwa kwa shuruti bila kutangaza na kujumlisha kwa pamoja matokeo ya kituo hadi kituo hali iliyoashiria kuwa matokeo ya Ubunge yalikuwa na utata. Kutangaza huku kwa nguvu ilikuwa ni mkakati wa kutaka matokeo hayo yasihojiwe kama ilivyokuwa katika matokeo ya urais ambayo yalichelewa kutangazwa kutokana na kukutwa na mapungufu mengi. Kwa hali iliyodhihirisha wazi kuwa matokeo yalipikwa, waliopiga kura za Ubunge walikuwa 185,684 wakati waliopiga kura za Rais walikuwa 152,525 na hivyo kufanya tofauti ya kura za Ubunge na urais kufikia 33,159. Katika hali ya kawaida na katika uchaguzi uliofanyika kwa wakati mmoja ilikuwa ni vigumu kwa tofauti kubwa ya kura kiasi hiki. Na hata kama wananchi wangekuwa hawapendi kupiga kura za rais kwa kuwa mpiga kura alikuwa akipewa karatasi zote tatu kura hizi zilipaswa kuwepo katika kura zilizoharibika kitu ambacho hakikutokea.
http://www.chadema.net/hotuba/mnyika/hotuba_4.html
Lakini unadhani wapinzani watakubali tena kuibiwa 2010? Wewe badala ya kujadili jinsi ya watu kulinda hizo kura za Urais wewe kazi yako ni kusema kwama wasigombee, amakweli ukistaajabu ya Mussa utaona ya Firauni
Asha