Kichwamaji,
Ni mimi ambaye unaniandikia hasira yako na hitimisho lako ni kutamka maneno niliyosema "I am pissed off"! Sasa kama wafikiri nampotezea wakati Mnyika, unapotoka!
Mrema na Mtikila, walitumia "tabloid" politics 1995, 2000 na 2005, je Watanzania walichiukua hatua gani? Nothing they made CCM to be the party of choice.
Sijakataa kuanika mafisadi, lakini kutumia kutafuta uchafu na kuanika uozo wa CCM kama turufu ya kushinda uchaguzi si nja ya makini kushinda uchaguzi. Ndio maana nimesema kwa sisis tunaoelewa Siasa za Kitanganyika na uelewa wa Siasa kwenye Demokrasia ya kweli, political smear campaign inaachwa kwenye vijiwe na opposition kuweka nguvu zao katika mkondo wa kisheria unaofanya kazi (Bunge hata Mahakama).
Je ni wangapi wamejiunga na Mtikila katika kesi zake anazopeleka Mahakamani ambazo ni za msingi kabisa kuhusiana na Katiba na Utendaji (Wagombea Huru) ili kuonekana kuna mshikamano? Hakuna, sana sana tunamuona Mtikila ni taahira fulani wakati anayofanya, ndiyo yanayopaswa kufanywa na Wapinzani wote kwa pamja ili kuonyesha mshikamano wa kudai mambo ya msingi ingawa kila chama kina sera zake!
Suala la Muafaka Zanzibar, BOT, Madini, Kiwira, Richmond na ufisadi mwingine hata kama umepita mfano IPTL, Radar, Ndege na kadhalika ni masuala ambayo ni nyeti kuishia katika mikutano ya waandishi wa habari pekee!
Mambo kama haya yanapaswa yashinikizwe Bungeni na wapinzani kwa kupitia kanuni na sheria zilizopo. Kuwasilishwa kwa hoja za kudai kuundiwa kwa kamati za bunge za kuchunguza niliyoyataja hapo juu, ndiyo nja sahihi ya kujenga imani kwa watu, hata kama CCM na Bunge lao la kiimla watapinga (mfano wa Zitto na Karamagi)!
Suala la Zitto kuhusu Karamagi, lilipotea njia awali kutokana na udhaifu wa hoja na ushahidi kuwakilishwa Bungeni ambako kungeshinikiza uchunguzi wa Suala la Buzwagi ufanywe na Bunge na si kuundia Kamati Kibogoyo ya Rais ambayo haitakaa kamwe kutoa suluhisho na tathmini ya maana ambayo itapelekea watuhumiwa kushitakiwa.
Sawasawa na uchunguzi wa BOT, badala ya kushinikiza kuundwa kwa kamati ya Bunge au kuipa madaraka Kamati ya Fedha ya Bunge kupeleleza na kuchunguza ubadhirifu huu kwa kutumia mamlaka yake kisheria (Bunge), kazi imepewa kwa kampuni binafsi na matokeo yake yanaenda kwa Waziri na Ikulu kwanza, yafanyiwe uhariri ndipo Taifa lipewe nakala ambayo imechujwa!
Ndio maana, nimesema " I am pissed off" with technics ambazo zinatumika na wapinzani kuelimisha umma kutumia habari ambazo zinaonekana kuwa ni za udaku na si za kweli!
Solution ni kuongeza uwakilishi wa vyama hivi katika Bunge ili miswaada ya kuchunguza ishu ikifika, basi kura zao zitafanya kazi!
Kuhusiana na urais, nimeuliza, kwa nini wasitafute mtu mmoja mahiri na popular awawakilishe wapinzani wote? Jibu ni kuwa kila mmoja wao anautaka Urais na zaidi, wengine wao ni makuwadi wa CCM. Tayari kuna mgawanyiko katika upinzani ambao unaonyesha wazi kuwa kamwe ufa wao hautaweza kuzibika.
Ni kwa nini kina Shayo, Mtikila na Makaidi wamekimbilia mbali, Cheyo yupo pekee halafu Mbowe, Lipumba, Mrema na Marando upande mmoja?
Will this work?
My passion and opinions are for the sake of Taifa and I am not a stooge who is trying to figure the upinzani best next move. I learn by observation and reading simple details and analyze them and try to provide alternatives that can work on the best interest of opoosition to make sure that the Political Dominance and Un-Accountability of CCM comes to an end!
Hivyo basi kama waona nampotezea wakati Mnyika, huo ni uhuru wa maoni yako, na mtazamo wako na nitauheshimu kwa maana weye na mimi hatujuani!
Rev. Kishoka
Kuhusu BOT, mkondo wa bunge ulijaribiwa na Dr Slaa alishaandika Hoja Binafsi lakini dalili zilionyesha wazi kabisa kwamba walitaka kuifanyia mizegwe isiingie, umesoma ripoti ya usalama wa taifa ikimshauri Waziri Mkuu Lowasa ahakikishe Kashfa ya BOT kama alivyoiandika Dr Slaa haiingii bungeni?
Katika mazingira hayo, unaweza kumlaumu vipi Dr Slaa kuichomoa hoja yake na kuiwasilisha kwenye mahakama ya wananchi ama bunge la umma? Dr Slaa ni mbunge, kama angeiwasilisha ile hoja mule, kuna baadhi ya mambo angebanwa na kanuni za bunge(naomba niseseme kwa nini ingawa najua kwaninini). Kwa hiyo, alifanya uamuzi wa busara kabisa.
Kuhusu EPA, hili ni tone dogo sana kati ya bahari ya yanayohitaji kuchunguzwa kuhusu BOT na kwa maoni yangu mimi limefanyika ili watu waghilibike kwamba uchunguzi umeshafanyika.
Kura serikali duniani zimewahi kuanguka kwa sababu ya mambo ya ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka tu; kuna upinzani umewekwa madarakani kwa sababu ya chuki ya watawaliwa dhidi ya watawala wa kiimla fisadi!. Sisi hatujafika huko bado, ndio maana nimesema- tunafanya yote, tunaanika ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka, wakati huo huo, chini kwa chini tunaendelea kujijenga kama chama mbadala na kutoa sera mbadala. Bado tuna safari ndefu kutokana na ukubwa wa nchi.
Lakini watu kama wewe mkibadili mawazo yenu, mkawa na mtazamo chanya juu ya upinzani na kuchukua hatua- hakika tutafika.
Umetaja orodha ndefu ya viongozi wa upinzani! Kumbuka si kila anayesema bwana bwana bwana ndio atayeuona ufalme wa Mungu(natumai unaelewa mantiki ya maneno yangu).
Ndio maana kama ulitazama kipindi cha TVT This Week Perspective kuhusu utafiti wa REDET nimewakosoa sana kwa ku-lump vyama vyote pamoja na kuita upinzani badala ya pamoja na kufanya hivyo, walipaswa kutafuta pia maoni ya wananchi kuhusu Ushirikiano wa Vyama(CHADEMA, TLP, NCCR na CUF) kama entity, na pia walipaswa kutafuta maoni kuhusu individual parties!.
Hata huko ulaya, kuna vyama vingine ni vya kiunamazingira tu(the greens) sasa ulitika ajenda zao ziwe sawa na waende mkondo mmoja na wakue(kwa maana ya kiasi cha kukubalika) sawa sawa na social democrats, socialists, conservatives au liberals? Huwezi kuihukumu CHADEMA kwa yanayofanywa na kila chama kingine kimoja kimoja!
Hilo la kuiongeza wabunge nimeshalizungumza umuhimu wake bila kuondoa haja pia ya kuweka nguvu katika Urais. Kama kuna wanaona uongozi wa Kikwete una mapungufu, unadhani suluhisho litapatikana vipi bila kuigusa na taasisi ya Urais? Yes, wabunge ni priority, but Yes, Urais ni lazima pia.
Cha msingi ni kwamba, chini ya ushirikiano wa vyama- akipatikana mgombea mmoja wa Urais, naamini wengine watakwenda majimboni kuongeza nguvu zaidi.
Mimi nitaendelea kuwa nawe mpaka kieleweke ndugu yangu. Endeleeni na mjadala
JJ