The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Kitila,Alnabady,Wembe-mkali,Bongolander,

I would prefer a scenario when the President and the Prime Minister are from different political parties.

Our constitution stipulates that the Prime Minister will be appointed from the majority party in the Parliament.
 
Yes Upinzani has no financial capital, but it has Watu!The opposition needs to start investing in people and do what Kingunge used to do Mass Mobilization.

Focus should not be in airing uozo na ufisadi kila siku (I am pissed of with new barage from Slaa on BOT and Balali), watanzania ni wepesi kushangilia gumzo na vitendo ni vingine!

Problem ya Upinzani ni kusubiri 2009, kuanza kujijenga. the question I have been asking myself, why didn't they start on December 19th 2005 their trip to topple CCM?

Hivi ukiondoa zile sehemu nyeti za Upinzani ambazo ni mkao wa ukabila na udini (Uchagani, Usukumani, Pemba, Dar) do they have anything in Ruvuma, Iringa, Rukwa or Dodoma?

Utafutaji wao wa mageuzi utafanikiwa vipi ikiwa kila siku wao wanananyemelea jimbo moja moja?

2010 will be 15 years since mageuzi came to Tanzania, jee watatuambia kama Kikwete kuwa wameanza kujenga msingi na kuweka tofali moja moja na hivyo 2010 tutaona matokeo?

Mnyika, umesema niwasiliane nawe, sawa hilo sina shida! Je ni mipango gani mliyo nayo zaidi ya kujaza magazeti na kulalama kuhusu ufisadi?

You have no political capital but gossip and rumours! Nothing can ever be resolved through press confrences everyday!

You do not win or secure mandate of trust from Wananchi by sounding like Alasiri. That is why none of the issues raised by you (opposition) will ever be resolved.

Mara kumi na Mtikila anayefungua kesi mahakamani, angalau hata kama shauri litatupwa, there is a record that he brought ushahidi credible mahakamani and wananchi can decide, yes kaonewa or well ushahidi ulikuwa hautoshi!

What Chadema, CUF, TLP, NCCR need to do is to sit down with the other camp ya Makaidi na Mtikila and come with a game plan.

Slandering and smear does not equate into votes! Opposition need to sit down and strategies and even reach muafaka wa kugawanyana majimbo so that they can get at least near majority on parliament.

So what happens if Mrema, Lipumba, Marando , Mtikila or Mbowe wins Ikulu and CCM has 90% seats in the parliament? will President Mtikila dissolve the parliament everytime they stall his budget?
 
Rev.Kishoka said:
So what happens if Mrema, Lipumba, Marando , Mtikila or Mbowe wins Ikulu and CCM has 90% seats in the parliament? will President Mtikila dissolve the parliament everytime they stall his budget?

..the President will have to be very careful before he dissolves the Parliament. It has to be for reasons that the voters will agree with.

..hao CCM watakuwa na ujasiri of taking on the someone who has won the Presidency even with CCM winning 90% of parliamentary seats?

..i believe a very close election is the one that will bring the President and PM from different parties.
 
..the President will have to be very careful before he dissolves the Parliament. It has to be for reasons that the voters will agree with.

..hao CCM watakuwa na ujasiri of taking on the someone who has won the Presidency even with CCM winning 90% of parliamentary seats?

..i believe a very close election is the one that will bring the President and PM from different parties.

1. Kikatiba Raisi ana nguvu na mamlaka kuvunja Bunge!
2. CCM ni jasiri (manipulative)watasema Raisi hana muelekeo na sera zinaangamiza nchi hivyo impeachment!
 
Kila linalohitajika kufanywa na vyama vya upinzani ili kuleta mabadiliko katika mstakabali wa nchi yetu limekwishazungumziwa katika michango iliyomo humu.

How I wish these people (wapinzani)would heed the call and 'fanya' kweli!

Rev. kudosfor this topic.
Kitila Mkumbo - tunatarajia kuyaona hayo ya Mwenyekiti akitoa msimamo na mwelekeo wa chama katika vikao vizito, sio kukalia ulalamishi tuuuu, kuhusu mambo ambayo yanafanywa na CCM. It is high time they set their own agenda; isiwe mambo ya ku-react tu kila mara.

Vyama haviweki wala havijadili 'malengo' wanayotarajia kuyafikia; na wala hakuna 'evaluation and assessment' ya malengo hayo.
Wekeni na jadilini malengo mnayotaka kuyafikia, malengo mnayoweza kuyapima utekelezaji wake katika muda mliouweka wa kuyafikia hayo malengo. Kama hamkuyafikia, changanueni sababu zilizowazuia kuyafikia na kufanya marekebisho.

Tulishasema humu, vyama vya upinzani kila mara wanasubiri uchaguzi ndipo waonekane wanafanya kazi. Mtindo huu hausaidii kabisa. Nendeni vijijini; viongozi wenu huko vijijini wapeni agenda ya mambo mnayotaka yatimizwe na kuwafikia wananchi, bila ya kusubiri uchaguzi utakapokuwa karibu, au HELIKOPTA itakapokuwa tayari kufika hko (what a joke?)

Hii 'myth' ya viongozi wazuri walipo CCM, lakini wasiotaka waonekane is driving me crazzy - They need to come out and be counted, vinginevyo hawana uzuri wowote hawa.
 
Tunapaswa kuifukuza CCM madarakani kama tunaamini imeshindwa kazi na kutuchosha, tusilete vizingizio, la sivyo tutamke tu kuwa CCM bado haijatuchosha!

Mkuu bado tuna kazi nzito sana kwenye taifa hili na who is best for us, mimi nilisha kata tamaa siku nyingi sana, viongozi wetu ni sisi wenyewe tu wananchi, waongo, wanafiki, wezi, uwezekano wa kuibadili CCM haupo kwenye hii generation yetu,

I mean mimi ninajua mijitu chungu nzima hapa JF, ambayo ni minafiki mikubwa kujifanya upinzani hapa ipate kupewa thanks tu kumbe ndio ya kwanza kujiweka sawa na viongozi mafisadi, yaani kuna limoja hata lilitaka kumtapeli majuzi kiongozi mmoja wa CCM na ni lijumbe hapa JF, what a shame? Eti ndio wataleta mabadiliko hawa? Mijitu miongo kazi kutafuta ujiko tu nyama kabisaa!

Hivi hili taifa tulimfanya nini Mungu?
 
Mzee ES,

Si ututajie hawa mahaini ambao wanadai ni wazaledo kama sisi huku wao ni masubiani ili tuanze kuwaepuka?

Mwanzo wa mageuzi uanzie humu ndani na ndipo tutafanikiwa ndani ya CCM na Chadema.
 
Miye nimechoka kusubiri ajizi na danganya toto za kila siku. JK katamka, sifukuzi mtu, hakuna mwizi au fisadi. Mambo ni murua, sisi ni masikini hatuna mtaji, waacheni wawekezaji wavune dhahabu ingalawa twapata hata hiyo 3% ni win win situation.

Sasa twajua yeye shabiki wa Chelsea ingawa alipewa jezi ya New Castle! Kadai Dodoma ni lazima tuhamie katika miaka miwili.

Sasa najiuliza, wakati tunamshupalia koo Balali atoe siri kabla ya kwufwa, kwa nini tusiache yaliyopita aykijipika tartibu, tukaganga kwa yanayokuja 2010?

Ni mipango gani tuliyonayo kama Taifa kuhakikisha kuwa Uchaguzi wa 2010 utaleta mageuzi ya kweli kwa Taifa na si win win situation?

Mfano, Kwa nini Upinzani usimsimamishe Zimbwe kama mgombea Uraisi wao?

Kwa nini Upinzani unazubaa kujijenga kutwa japo 40% ya Bunge ili kulazimisha zile Kura za Theluthi Mbili za CCM kuwa batili kwa kushindwa?

Je katia CCM, ni nani wako tayari kuachana na Chama Cha Mafisadi na kuwa Watekelezaji wa Chama cha Mapinduzi?

We have 3 years to be constructive, otherwise February 2011, we will be talking about Ushindi wa Elnino na kusubiri Wafadhili watusaidie kuung'oa unyang'au wa CCM (Mafisadi) ambao umeboresha Umasikini, Ujinga, Njaa na Maradhi!

Kheri ya Krismas, Hannuka na Eid Mubarak!

Rev Kishoka

Lazima tushapalie yaliyopita kwa kuwa yatatusadia kuamua yajayo 2010.

Tunayofanya yote kwa pamoja, na kwa kweli hilo suala la kuweka nguvu katika kuongeza viti bungeni tunalifanya. Tofauti ni kwamba ya ufisadi yanaanikwa hadharani, lakini ya mikakati ya kuongeza majimbo si ya kuanikwa hadharani. Ingawa ukienda majimbo tuliyoyafikia mpaka sasa kwenye mkakati wa kujenga oganizesheni utanilewa nasema nini. Otherwise, nilikuomba tuwasiliane chemba

JJ
 
CCM has two camps, Mapinduzi na Mafisadi. Mafisadi have had an upper hand for the last 20 years. If CCM will lose the power to use 2/3 power of votes to pass Mswaada, you will see CCM Mapinduzi crossing the lines and join opposition to put the government in a check.

If opposition will work united and secure 40% of parliament seats, then the political dynamics will change and Mafisadi will have to use udikteta au whatever to continue to rule!

With 40% secured to opposition, there could be constitutional changes that will strip the president the absolute powers, Special seats will be eliminated, government expenditure will be tight and most of ills that are due to incompetence or malice will b e addressed.

In CCM, at least 35% of its Wabunge are anti-establishment, however they live in fear of Kikao cha Kamati Kuu na Kutengwa because there are no alternative options for them.

If opposition will build a a solid structure that it's focus is on good governance and delivery of hope (not preaching), then the 35% of Wabunge wa CCM who have morals and passion for their country will cross the line and vote with opposition or even join opposition.

This will only happen if Mbowe, Lipumba, Mrema, Cheyo and Mtikilla, will agree to step aside from running to Ikulu and focus on Halmashauri, Kata, Vijiji, Wilaya and Ubunge!

They need to have an agreement to field one candidate in Zanzibar (not Sefu Hamad anymore) and one candidate for Union presidency. Focus for 2010 should be to secure 40% of elected seats in the parliament!

Naamini kwa ushirikiano ulioko hivi sasa kati ya CHADEMA, CUF, TLP na NCCR Mageuzi hili la kuachiana maeneo litawezekana.

Na kwa wale ambao hawatagombea urais ni wazi watakamata majimbo! Kinachohitajika ni watanzania wengi zaidi kujitokeza kugombea kupitia upinzani ama kuunga mkono hizi harakati za mabadiliko ya kweli.

JJ
 
For the opposition to acquire 40% of the seats in the parliament we need a miracle.We are talking of an electorate of which 80% is not aware of what is going on in the country.The rest which is 20% is divided.
What can be possibly be done to change the situation which has been deliberately been put in place by the first phase government?The people are ignorant and poor.They can be easily be manipulated by the rich because they are ignorant and poor.
Kabwe and company and the likes have no power of money and CCM has alot of it.The poor ignorant voter has no agenda,he is ready to be bought at a very awkward price.
Even the once powerful opposition leaders like Amani Kabourou,Tambwe Hiza and Ngawaiya realized that it is impossible to win an election in the present situation and decided to join CCM.
In a few years time I will not be surprised if Zitto himself joins CCM.You fight where you see the possibility of winning.Tanzania is not like Kenya,Zambia or Malawi.

The opposition in our country is lacking what a party like ODM has in Kenya i.e the financial muscle.

The people lack civic education and comprehension of national issues.The peole are scared in their hearts...a Nyerere ghost is haunting them.

What can be done to arouse their minds? A miracle from heaven.

Kutoka kwa kaborou Kigoma hakujaathiri CHADEMA, kule chama ni taasisi sio mtu. Hivyo ndivyo tunapaswa kuwa kote

Karatu, Tarime, Pemba nk upinzani umeshinda-sijui unazungumziaje elimu ya uraia ya watu wa maeneo hayo? Ama mzimu wa Nyerere ulilala?

Mi naamini watu wakiamua nguvu ya umma inashinda, wachache wakiamua watatoa elimu ya Uraia na kuutumia mzimu wa Nyerere kuwahukumu CCM

JJ
 
Tunapaswa kuifukuza CCM madarakani kama tunaamini imeshindwa kazi na kutuchosha, tusilete vizingizio, la sivyo tutamke tu kuwa CCM bado haijatuchosha!

Mkuu bado tuna kazi nzito sana kwenye taifa hili na who is best for us, mimi nilisha kata tamaa siku nyingi sana, viongozi wetu ni sisi wenyewe tu wananchi, waongo, wanafiki, wezi, uwezekano wa kuibadili CCM haupo kwenye hii generation yetu,

I mean mimi ninajua mijitu chungu nzima hapa JF, ambayo ni minafiki mikubwa kujifanya upinzani hapa ipate kupewa thanks tu kumbe ndio ya kwanza kujiweka sawa na viongozi mafisadi, yaani kuna limoja hata lilitaka kumtapeli majuzi kiongozi mmoja wa CCM na ni lijumbe hapa JF, what a shame? Eti ndio wataleta mabadiliko hawa? Mijitu miongo kazi kutafuta ujiko tu nyama kabisaa!

Hivi hili taifa tulimfanya nini Mungu?

Duh, mimi nakwambia kuna kitu kwenye huu utanzania sio bure. Maana hizi sifa za uongo, unafiki na woga zimezagaa sana, yaani kila mtu unayeongea naye lazima uwe makani sana.

Mimi mwenyewe kuna mijitu haishi kunitumia PM hapa inajifanya eti inanipa ushauri niwe makini na post zangu maana natumia jina langu! Mioga na minafiki tu haina chochote.Yaani hii ina-cut across hadi kwa viongozi wa dini. Hapa duniani nafikiri hakuna viongozi wa dini waoga kama wale watanzania, hasa wakristo, yaani wanapenda kuuma na kupuliza.

Kote palipotokea mabadiliko na mageuzi kuchangamka viongozi wadini wali-play a very active role-Kenya, Zambia, Malawi, Sierra Leone, Uganda, n.k. Lakini njoo Tanzania, viongozi wa dini watasema hiki kwenye jukwaa hili kesho wakikutana na Rais au Waziri Mkuu ndo wa kwanza kumwagia misifa-tunarudi hukohuko: unafiki, woga na uongo.

Kama kuna jambo la kuomba Mungu atusaidie sisi watanzania hasa hiki kizazi chetu ni kutuondole roho ya woga, uongo na unafiki na badala yake atupandikizie roho ya ujasiri, hekima, ukweli na uhalisia.
 
Tuendelee kuwalaani wote waliowafanya wana CCM wakamwamini Kikwete badala ya Salim, hao ndio waliotuletea matatizo yote haya. Hawa ni pamoja na maaskofu uchwara waliosema eti Kikwete ni chaguo la Mungu-si ajabu idadi ya waende kanisani inazidi kupungua
 
Unafiki unaanzia kwa hao wanaotuwekea mafumbo tu hapa bila kututajia hao wanafiki wanaowasema.

Sasa tunafanya nini:
Tajeni majina sasa, tuache huu upuuzi hata hapa JF. Sema Kalamu, au whatever, alini-PM kunionya nisiwaseme wakubwa vibaya, n.k.
Au Kada tulimwona D.C. akining'inia kwenye makoti ya wakubwa, n.k.

Mtu kukataa unafiki ni pamoja na kuamua ukiwa katika kila chumba cha kupigia kura, tena peke yako, kupiga kura itakayoleta mabadiliko.
 
Mnyika,

Si lazima mtamke hadharani mipango ya utandawazi wenu kwa Taifa ili tujue mnafanya nini. Vitendo vyenu vitajitangaza.

Kinacho niudhi ni huku kukimbilia majukwaani kulaumu CCM na kuanika Uozo usiosafishika bila na kuwa na nguvu ya dola(majority rule)!

You (Chadema and alliance) are wasting time to keep up with headlines to air dirty laundry of CCM! What Slaa and Zitto have become is like tablid publicists!

What you need is to demonstrate effectivelly that your plans to lead the country can work even without being in power.

Je ni miradi gani ambayo mmekuwa mbele kusaidia kuvunja umasikini, ujinga na maradhi? are your plans and utendaji better than CCM?

You need to start preaching what you can activelly demonstrate to Wananchi to gain their trust and respect which will translate to acceptance when time comes!

As of now, you all look like Mtikila! Walalamishi wasio na mbele wala nyuma na mwasubiri 2009 kuamka ndipo taifa lijue kuwa Chadema ina sera kadhaa ambazo hazifanani na CCM na zinaweza kuaminika.

I can not stand the incompetence syndrome that is spreading in opposition taking great lessons from CCM.

Opposition needs to look and act differently from CCM. One step for them to achieve that is to be open minded to Ideas of new political structure that are in the world today.

Naomba uende kwenye mada yangu ya kuomba Chadema ifanye reform. Nia ya kuanzisha ule mjadala tofauti na huu ni kwa kuwa malengo ni tofauti na njia ni tofauti ingawa end result ni kuingoa CCM.

Hapa nawauliza, mnajiandaa vipi kuchukua uongozi wa Serikali (not Ikulu) 2010? Je mwaaminiana hata huko kuachiana majimbo? mna mtaji mkubwa kiasi gani?

Je sera zenu collectivelly ni kumkomboa Mtanzania na matatizo yake kwanza au ni Kuing'oa CCM tu?

Je wote mna msimamo gani kuhusu Zanzibar na hatima ya muungano?
 
Tuendelee kuwalaani wote waliowafanya wana CCM wakamwamini Kikwete badala ya Salim, hao ndio waliotuletea matatizo yote haya. Hawa ni pamoja na maaskofu uchwara waliosema eti Kikwete ni chaguo la Mungu-si ajabu idadi ya waende kanisani inazidi kupungua

Binti Maria,

Tatizo si Kikwete pekee bali system nzima.Ukiongelea kumchagua Salim instead of Kikwete labda ungeweza kupunguza makali ya uozo, lakini kimsingi tungekuwa pale pale maana sera za chama ni zile zile na bunge ni lile lile.Hii ni moja ya udhaifu wa siasa za Afrika na Latin America, siasa zinawazunguka "certain strongmen" instead ya kuwa about policies and manifesto.

CCM imeshindwa kumuadibisha Kikwete ala Thabo Mbeki sina confidence nayo kabisa.Tatizo upinzani umejiandaaje?
 
Mnyika,

Si lazima mtamke hadharani mipango ya utandawazi wenu kwa Taifa ili tujue mnafanya nini. Vitendo vyenu vitajitangaza.

Kinacho niudhi ni huku kukimbilia majukwaani kulaumu CCM na kuanika Uozo usiosafishika bila na kuwa na nguvu ya dola(majority rule)!

You (Chadema and alliance) are wasting time to keep up with headlines to air dirty laundry of CCM! What Slaa and Zitto have become is like tablid publicists!

What you need is to demonstrate effectivelly that your plans to lead the country can work even without being in power.

Je ni miradi gani ambayo mmekuwa mbele kusaidia kuvunja umasikini, ujinga na maradhi? are your plans and utendaji better than CCM?

You need to start preaching what you can activelly demonstrate to Wananchi to gain their trust and respect which will translate to acceptance when time comes!

As of now, you all look like Mtikila! Walalamishi wasio na mbele wala nyuma na mwasubiri 2009 kuamka ndipo taifa lijue kuwa Chadema ina sera kadhaa ambazo hazifanani na CCM na zinaweza kuaminika.

I can not stand the incompetence syndrome that is spreading in opposition taking great lessons from CCM.

Opposition needs to look and act differently from CCM. One step for them to achieve that is to be open minded to Ideas of new political structure that are in the world today.

Naomba uende kwenye mada yangu ya kuomba Chadema ifanye reform. Nia ya kuanzisha ule mjadala tofauti na huu ni kwa kuwa malengo ni tofauti na njia ni tofauti ingawa end result ni kuingoa CCM.

Hapa nawauliza, mnajiandaa vipi kuchukua uongozi wa Serikali (not Ikulu) 2010? Je mwaaminiana hata huko kuachiana majimbo? mna mtaji mkubwa kiasi gani?

Je sera zenu collectivelly ni kumkomboa Mtanzania na matatizo yake kwanza au ni Kuing'oa CCM tu?

Je wote mna msimamo gani kuhusu Zanzibar na hatima ya muungano?

Rev. Kishoka:

Kukimbilia majukwaani kukosoa si kupoteza muda-ni kutimiza wajibu wa upinzani wa kuwajibisha serikali iliyoko madarakani. It's a watch dog function. So far we have succecceded in being a party against, but we have to invest more into being a party for.

Ila ukisikiliza kwa makini utabaini nyuma ya kuwa 'dhidi ya' kuna kuwa kwa 'ajili ya'. Nichukulie mfano- Zitto alikuwa dhidi ya Karamagi kusaini mkataba wa Buzwagi bila kuzingatia maslahi ya taifa na kufanya hivyo kabla ya mabadiliko ya msingi ya kisheria na mazingira ya kuingia mikataba kufanyika.

Lakini kwa kufanya hivyo, Zitto amesimama pia kuwasilisha na kuwakilisha sera ya CHADEMA ya kutaka rasilimali za Tanzania zitumike kwa manufaa ya watanzania. Hatimaye serikali imeunda kamati ya kupitia sheria na mikataba(pamoja na mapungufu yake tuliyoyajadili) lakini kwa kiasi imetekeleza ilani ya CHADEMA (japo si kwa ukamilifu wake) maana sisi ndio tulisema tutapitia upya mikataba ya yenye utata ikiwemo katika madini.

Dr Slaa alipotaja orodha ya mafisadi alikuwa 'dhidi ya' lakini kwa kufanya hivyo ameweka bayana sera ya CHADEMA ya kuwa mfumo mpya wa utawala wenye serikali adilifu inayopambana na rushwa bila kutazama 'sura ya mtu'; hapa amebeba vizuri rangi nyeupe ya bendera ya CHADEMA inayowakilisha ukweli, uwazi na uadilifu.

Jambo moja nakubaliana nawe- bado hatujaweza kuhusisha vizuri kupanda kwa gharama za maisha, ukosefu wa huduma za msingi za kijamii na huu ufisadi na matumizi mabaya ya rasilimali za Taifa ili watanzania wajue vizuri zaidi kwanini taifa letu liko lilivyo, na ni kwa vipi kwa sera yetu maisha yao yatakuwa bora zaidi.

Hii ni changamoto kwa kila kiongozi anavyopanda jukwaani.

Lakini kuna changamoto pia; kwa nyinyi ambao mnapata zaidi kusikia kutoka kwenye vyombo vya habari mnapata habari ambazo zimechujwa sana. Nikupe mfano- pale Jagwani, Zitto alizungumza uhusiaono baina ya madini na maisha ya watu- lakini kwa waandishi habari ilikuwa tu ni kusaini mkataba hotelini London ama nyumba ya Rais kuingiliwa, hayo mengine yote hawakuyaona kuwa ni habari.

Dr Slaa pale mwembeyanga alihusisha ufisadi na kukosekana na huduma muhimu za kijamii, lakini hili la huduma halikuwa sehemu ya habari. Nimefurahishwa na habari ya jana ya Tanzania Daima ya "Balali akamatwe" ilichanganya masuala mbalimbali kwa wakati mmoja. Iliweka bayana wakati mjamzito anajifungulia ofisi ya WEO kwa kukosa 20,000( infact ilikuwa ni elfu 20 za mchango wa MMES kwa hiyo ni kama aliwekwa rumande wakati anajifungua) huku Balali anatuhuma za mabilioni anaachwa mpaka sasa. Wakati watuhumiwa wadogo wanauguzwa wakiwa na pingu hospitali, watuhumiwa wakubwa wako huru. Uandishi wa namna hii unasaidia sana kufikisha ujumbe kwa undani wake.

Hili la kusaidia miradi ya kuthibiti umaskikini: Linahitaji mjadala zaidi, tujiulize- duniani kote, kazi ya vyama vya siasa ni nini? Imani yangu ni kuwa tumeweza kufanya vizuri katika miradi mbalimbali katika halmashauri ambazo tumeongoza Kigoma Ujiji, Hai na Karatu; na tuendelea katika halmashauri ambazo tumeanza kuongoza baada ya 2005, sasa tunaoongoza pia Halmashauri mpya moja ya Tarime.

Sidhani kama upinzani unatakiwa kugawa fedha za miradi ya kuondoa umasikin- kufanya hivyo, kuna vikwazo vifuatavyo: Mosi, tutakuwa tunatoa takrima ya maendeleo kwa wananchi toka mifukoni mwa chama ambayo kimsingi ni rushwa, Pili, tutatoa fursa kwa mafisadi nao kuanza kutoa michango hiyo kupitia vyama vyao- sasa mwenye kisu kikali ndio atakula nyama. Tatu, tutakuwa tumetoka katika malengo ya msingi ya chama cha siasa.

Kwa maoni yangu, chama cha siasa ni muunganiko wa watu wenye mawazo yanayoshabihiana kwa lengo la kuchukua dola ili kutekeleza mawazo hayo, na kabla ya kuchukua dola kuiwajibisha dola iliyoko madarakani kwa misingi ya mawazo hayo! Kwa hiyo bidhaa za vyama vya siasa ni 'uongozi', 'sera' na 'oganizesheni'. Kwa hiyo, tunaondoa umasikini kwa kutoa viongozi bora, sera bora na oganizesheni bora.

Kwa sasa pamoja na kuwa upinzani tumewatoa wakina Dr Slaa, Zitto nk ambao wanaiwajibisha serikali kwa sera zinazopinga ufisadi na kutetetea rasilimali za taifa, kwa kweli matokeo ya harakati zao ni fedha zetu za kodi kutumika vizuri zaidi katika miradi ya kuondoa umaskini. Naamini kabisa, serikali ya sasa(pamoja na ufisadi unaoendelea) kwa staili hii ya Orodha ya mafisadi kila mmoja yuko tumbo joto- hivyo, sidhani kama watakuwa na ari, nguvu na kasi mpya ya kufuja fedha za miradi ya kuondoa umaskini kama ilivyokuwa wakati wa Mkapa- sasa kama hali ikiwa nzuri kiasi nani atanufaika kama sio mwananchi? Nani amesababisha manufaa hayo kama si upinzani?

Na ikifika 2009 na 2010 changamoto kwetu ni kuwafanya watu waelewe kwamba wakituchagua sisi tutaingia wenyewe kutekeleza sera hizo vizuri zaidi tofauti na CCM inayofanya mambo machache tena baada ya shinikizo.

Umewahi kusoma mchango wangu kuhusu "Huduma za Kijamii zinazotolewa na Vyama vya Upinzani?", soma utapata mtizamo wangu kuhusu "Nini mchango wa upinzani katika kuleta maendeleo"

Kuhusu Muungano- sera za vyama karibu vyote vikubwa vya upinzani nchini vinataka Serikali tatu.....

JJ
 
Kila linalohitajika kufanywa na vyama vya upinzani ili kuleta mabadiliko katika mstakabali wa nchi yetu limekwishazungumziwa katika michango iliyomo humu.

How I wish these people (wapinzani)would heed the call and 'fanya' kweli!

Rev. kudosfor this topic.
Kitila Mkumbo - tunatarajia kuyaona hayo ya Mwenyekiti akitoa msimamo na mwelekeo wa chama katika vikao vizito, sio kukalia ulalamishi tuuuu, kuhusu mambo ambayo yanafanywa na CCM. It is high time they set their own agenda; isiwe mambo ya ku-react tu kila mara.

Vyama haviweki wala havijadili 'malengo' wanayotarajia kuyafikia; na wala hakuna 'evaluation and assessment' ya malengo hayo.
Wekeni na jadilini malengo mnayotaka kuyafikia, malengo mnayoweza kuyapima utekelezaji wake katika muda mliouweka wa kuyafikia hayo malengo. Kama hamkuyafikia, changanueni sababu zilizowazuia kuyafikia na kufanya marekebisho.

Tulishasema humu, vyama vya upinzani kila mara wanasubiri uchaguzi ndipo waonekane wanafanya kazi. Mtindo huu hausaidii kabisa. Nendeni vijijini; viongozi wenu huko vijijini wapeni agenda ya mambo mnayotaka yatimizwe na kuwafikia wananchi, bila ya kusubiri uchaguzi utakapokuwa karibu, au HELIKOPTA itakapokuwa tayari kufika hko (what a joke?)

Hii 'myth' ya viongozi wazuri walipo CCM, lakini wasiotaka waonekane is driving me crazzy - They need to come out and be counted, vinginevyo hawana uzuri wowote hawa.


Kalamu:

Katika vikao vyetu huwa tunajadili mwelekeo wa CHAMA na mwelekeo wa TAIFA; tunajadili hali ya chama na hali ya Taifa. Kwa waandishi, habari kubwa zaidi ni hali taifa-ama kauli za viongozi kuhusu masuala ya kitaifa.

Huwa tunajadili malengo ya kila mwaka kutokana na malengo mama ya miaka mitano. Hapa tulipo tunajua kabisa ni majimbo mangapi tutajikita zaidi na namna gani. Mambo mengine hayapigiwi baragumu kwa kuwa ni mikakati ya ndani. Tunakawaida pia ya kupima na kutoa ripoti- ingawa 'outcome and impact assessement' hatujafanya, lakini evaluation za kawaida za kujua output zinafanyika.

Mapambano ya kisiasa na kama mapambano ya kivita; unaweza kuwa na vikosi vya aridhini na vya angani. Viongozi wa kitaifa hawawezi kwenda kila kijiji hapa Tanzania- nchi hii ina zaidi ya vijiji elfu 10; kata pekee ni zaidi ya elfu mbili.

Viongozi wa kitaifa wakilenga kufika kila kijiji hii nchi tutaimaliza Mtu Issa akirudi! Njia pekee ni viongozi wa kitaifa kulenga maeneo ya vijijini mahususi ambayo ukiwasha moto unasambaa kwa kasi zaidi, ndio maana ya Ziara za viongozi wa kitaifa. Ukiona CCM wanaweweseka kulalamika kwamba CHADEMA inafanya vibaya kuwaapiza wananchi vijijini kuichukia serikali yao(Soma chama chao) ujue moto unasambaa.

Kwa hiyo ziara hizo ni muhimu. Vikosi vya pili vya mapambano ni Makada wa chama; sasa ukifuatilia jinsi tunavyotekeleza Mpango wa CHADEMA ni Msingi utaona kwamba ni kama jeshi la aridhini la makada ambalo linakwenda kuweka kambi wilaya mojawapo na kujenga oganizesheni ya chama pamoja na kusambaza sera za msingi za chama kijiji mpaka kijiji.

Changamoto ni rasilimali, mpaka sasa tumefikia wilaya chache kwa mfumo huu. Tunachohitaji ni watu kuunga mkono hii michakato! Lakini pia ni wajibu wa wananchi kuamka huko walipo- si kusubiri tu upinzani uje kuwaamsha, wananchi wanapaswa kumka na kuwa wapinzani na kuviita vyama. Uzoefu wa maeneo kama Mpanda Kati unaonyesha kwamba kuna wakati wananchi wanaweza wakaamka wenyewe na kukiita chama mbadala kiwafuate walipo!

Je, kama kila mmoja hapa akiamua tu kukipeleka chama mbadala kijijini kwake- hata kama kwa remote control, vijiji vingapi vya Tanzania yetu vitakuwa chini ya uongozi mbadala? Nasema kwa remote control kwa kuwa unaweza kuwa mbali lakini una ndugu, jamaa na marafiki ulipotoka- unaweza kuwashawishi na kuwaunga mkono. Ama kama huna kabisa, unaweza kuchagua eneo- tukiwasiliana tunaweza kujua jinsi ya kushirikiana kupitia waliopo wengine.

Lazima tukabali gharama ya kuwa wakala wa mabadiliko tunayotaka kuyaona- gharama yaweza kuwa muda, rasilimali- lazima tukabali kuwa matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno.

JJ
 
Hii ni sauti ya kukata tamaa na siyo sauti ya mapinduzi!si kubaliani nayo hata kidogo.Jamani tunaweza kabisa kufanya mabadiliko 2010.It is possible!.Kumbuka wewe unaangalia tu list ya wapinzani kwa sasa ila napenda kukuambia kuwa kuna watu wazuri tu wapo hata ndani ya CCM ambao wanaweza kujoin upinzani na kuleta mapinduzi makubwa sana mwaka 2010.Tatizo ninaloliona hapa ni jinsi watu wanavyoangalia tu list ya wapinzani wa sasa kama akina Maalimu,Tambwe,Mrema na wengineo na kukata tamaa nao.Napenda kukuhakikishia kuwa we can still get good people within CCM na kwingineko.Na hapo ndipo utakapoona kama 1995 kwa Mrema.

Sasa nini cha kufanya sasa hivi:
1) Ni lazima tuanze mara moja kuwaelimisha wananchi kwa sasa.
Na elimu yenyewe ilenge kwenye mapinduzi ya kuwakomboa wananchi.Ni lazima tuwafikie wapiga kura sasa hivi bila ya kusubiri eti mwaka au miezi kadhaa ndiyo tuanze.Halafu tuwaeleze kuwa Tanzania yenye neema inawezekana kabisa bila ya kusubiri ahadi za za uongo za CCM.Tutumie kila liwezekanalo kufikisha ujumbe huu.Kwa kupitia magazeti,radio binafsi,internet blogs,midahalo,fulana zenye kubeba ujumbe wa mapinduzi,kuongeza mikutano ya hadhara hasa vijijini na kadhalika!

2) Kufunua uozo ndani ya CCM.Wananchi siyo wajinga kama baadhi yetu wanavyofikiri.Zipo sehemu nyingi tu za Tanzania ambazo wananchi wake wameshaamka na huwezi kuenda na kuwapa ahadi za kusubiri ati 2010 mambo yatakuwa safi kama JK alivyosema huku wao wakifa sasa hivi.
Kwa hivyo tufanye kila namna kufichua uozo wote na vilevile kutoa solutions ya nini kingefanyika kama mbadala na siyo kulalamika tu kama alivyosema mchangiaji mmoja hapo juu.

3) Ni lazima wapinzani waweke mazingira mazuri ya kukaribisha damu mpya na fresh kwenye vyama vyao na kwamba wafanye kazi kama timu.
Mimi naamini kabisa kuwa kuna viongozi wazuri tu wapo CCM na kwamba wamechoshwa na mwenendo mzima wa chama chao hivyo wanaweza kabisa kujoin kambi ya upinzani na kuleta vuguvugu kubwa la mageuzi.

4) Kuanzisha vitu kama fundrise ya kusaidia vyama vyao financially bila kusubiri ruzuku.Kwa nini hata siku moja sijasikia chama kama Chadema au muunganiko wa vyama vinafanya fundrise yao pale hotel ya kilimanjaro(Kempinski) ili kufadhili shughuli zao ndani ya vyama?..hivyo ndiyo vyama vya nje vinavyopata fedha za kuendesha shughuli zao....

-wembe

Wembe

Nakubaliana na maudhui ya hoja zako zote nne, ingawa sikubaliani nazo neno kwa neno.

Ili chama kikue na kuendelea kinahitaji mambo manne makubwa- yanayofuatana kwa misingi ya umuhimu wake; wanachama bora(ikiwemo viongozi wa zuri); ajenda zenye kukubalika(ikiwemo sera bora); oganizesheni(muundo mzuri wa chama na mtandao uliojengeka) na rasilimali(ikiwemo fedha). Masuala haya yanakua na kupanuka kama mzunguko, ya yanategemeana kwa kiasi.

Kuhusu kuchanganisha- wapinzani wanafanya hivyo kwa kiasi(ni wazi, hakuna aliyekwenda Kempinsinki- labda gharama!). Na ukweli ni kuwa watu wengi wenye kuweza kuwa na fedha za kuingia mahali kama Kempiski kwenda kuchangia ni ama ni mafisadi ama kama ni waadilifu basi ni waoga wakujitokeza hadharani na kuhesabiwa. Hivyo, tukisubiria halfa kubwa za namna hiyo tutalala mlango wazi. Nchi za wenzetu watu hawaona shida kujitokeza na kuchangia upinzani, lakini demokrasia ya nchi yetu bado haijafika hali hiyo, lakini taratibu tutafika kadiri watu wanavyoona umuhimu wa upinzani na kuondoa hofu dhidi ya chama dola!

Lakini wakati tukisubiria wakati huo, ziko njia nyingine mbadala. We can do some ordinary things extra ordinarly well. Vijana wa CHADEMA tumeamua kuanza; tulishafanya tukio la kuwakutanisha vijana wenzetu kuchangia kidogo. Haba na haba hujaza kibaba kwa kweli. Tuna ndoto ya kuongeza wakina Zitto wengi zaidi bungeni 2010; lakini kikwazo kikubwa cha wagombea vijana ni rasilimali.


Lakini hebu tutafakari. Nitoe hapo mfano tu, unajua kwamba vijana 4,000 kila mmoja akichangia walau elfu 10 tu kwa mwenzi(ambayo ni kama dola 100 kwa mwaka) ifikapo 2010 tutakuwa na bilioni moja za kuwawezesha vijana kuchukua majimbo? Unajua kwamba jimbo moja- kama hutoi rushwa linahitaji kati ya milioni 10 na 20 kushinda? Kwa kiasi hicho unadhani vijana tukiamua kuchukua hii nchi tunashindwa? Mimi naamini, tunaweza. Bila kuwategemea mafisadi kutuchangia mabilioni, tunaweza kwa umoja wetu, fedha zetu za kiadilifu tukiamua kujikamua kidogo tu kwa ajili ya mabadiliko. Tunaweza kabisa, tukiamini- Maneno matupu hayavunji mfupa! Tunaweza kabisa! Tunaweza kupunguza hodhi ya chama kimoja bungeni. Tunaweza, ni kiasi cha kuchukua hatua.

Nimetoa mfano tu- kama unaamini ni mfano ambao unaweza kuwekwa kwenye matendo tuwasiliane tafadhali kupitia mnyika@yahoo.com au 0754694553 tubadilishane mawazo zaidi kuhusu FOCUS 2010

JJ
 
Kweli Mimi nimechoka yaani sasa tunalaani kweli hii serikali lakina utashangaa 2010, inaibuka na kura nyingi hivi bongo kuna nini pale !!!!
 
Niko tayari:

Lakini ni 2015 nitakuwa 48 years old. Kwa 2010 watanzania wengi bado wamelala hawajawa tayari kujikomboa! Kizazi cha akina mtikila , John Cheyo (na muungano wao kiboyo) kitakuwa kimekuwa kibogoyo. Shule za kata zitakuwa zimetoa wanafunzi wengi katani kwa hiyo kuelewa somo itakuwa kazi rahisi! Zitawarudi tu!
kabisa!

CV

(1)Married.
(2)shule ipo ya kutosha kabisa siyi ndogo! Lakini cha maana ni busara na uzalendo zaidi( hii sifa ya uzalendo ninayo nitafanya makubwa katika miaka mitano tu( yaani katika nchi yetu huduma za maji na umeme ni kama luxuary au kutafuta dhahabu!).
(3)Wawekezaji ni lazima iwe win win siyo hii danganya toto ya kikwete! ikiwezekana watakimbia hakutakuwa na lele mama katika kututea haki yetu na kuendeleza au kuijenga nchi yetu.
(4) Ubia na mtu hautakuwepo! Bali nitashirikia na vyama vyote vya upinzani( Mseto?).
(5) Kikwete alisema hana ubia na mtu lakini inaoeneakana ana ubia mkuwa na mawaziri wake!
(6) Niko katika chama kikubwa lakini any time nitaamua nini cha kufanya.

Nitawashirikisha wenye mawazo mazuri hata humu JF lakini ni kazi kuwajua kama haoa aliowasema FMES.

wapinzania hawa Chadema Cuf TLP, ukiwaona hawajawa na nia ya kuungana ila wamekaa kiujanja ujanja tu( hii ni kweli tupu)! Kuwasoma watanzania wakoje! Ndiyo maana ninasema bado 2010 JK atapeta tena kwa kura nyingi kama huo muungano wao hautageuka sasa na kuweka mizingi ya wazi ya kutaka kuwakomboa watanzania!

(7) Ila tu ninajua ni vigumu kiongozi mwenye nia halisi ya kuwakomboa watanzania kupata nafasi! Mafisadi wamejiandaa vya kutosha.
 
Back
Top Bottom