The Radar Scandal: Investigation & Progress

Kwa kifupi hafai, uwezo wake ni finyu kama JK mwenyewe. Kweli hatuna serikali.
 
Hakuna kiongozi anaetoa matamko ya ajabu ajabu kama Mtoto wa Mkulima. Na toka siku ya kwanza niligundua Pinda ni kituko.

Lakini hapa natafuta lakini sioni alipotumia maneno hayo ya 'waache wamalizane.'

Inawezekana ndio tafsiri yake lakini kuna mtu ana nukuu sahihi ya alichosema, zaidi ya taarifa ya Jarida la Tanzania Daima?

Ahsante.
 
Personally sina tatizo na Pinda ila anaonekana kuwa tayari kutetea status quo kwa hiyo amenitisha sana. Hata hivyo nitamualika kwenye babikiu akija kiwanja!

..hana kubwa la kufanya asije enda kinyume na waliomzunguka!

..he has to play it safe,not much choice,i suppose!
 

Mimi hawa waandishi wa habari wananitia kizunguzungu. Ni wapi aliposema Pinda kuwa tuwaache JK na Chenge wamalizane? Nilichokielewa mimi na elimu yangu duni ni kuwa Pinda amesema tumuache Rais alimalize suala hili maana yeye ndiye aliyemteua Chenge. Kumalizana ninavyoelewa mimi ni kuwa hawa wawaili tuwaachie wadundane mpaka hapo wote wawili watakaposhindwa kuendelea! Kitu ambacho sidhani Pinda anaweza kukisema.
 
Chenge anaweza kuwa mmoja wa majambazi wasomi wa kitanzania.

Ana mwanasheria wa kumlinda kutoka Cleveland, Ohio.

Aulizwe anamlipaje?

boat.gif
Bandari ya Elizabeth Marina, Jersey.

Andrew Chenge hatimae amejiuzuru na sasa hivi anapanga mikakati ya kuhakikisha anapona kufikishwa mahakamani na asizijibu tuhuma mbalimbali ambazo anakabaliwa nazo ikiwemo ya kuhifadhi fwedha za mlungula za rada, katika kisiwa cha Jersey ambacho kwa namna moja ama ingine hakiwajibiki sana na sheria yoyoye ile kutaka kuibana endapo kuna matatizo kama ya Chenge.

Lakini nimefanza utafiti kidogo kujua zaidi kuhusu kisiwa hiki maarufu kwa watu wote wenye makusudio ya kuficha na kuhifadhi mali za wizi ama wa aina ya Chenge au watu engine.

Jersey ni moja ya visiwa vinavoizunguka nchi ya Uingereza pamoja na vingine vya Isle of Man ambavyo vinaitwa kwa jina la pamoja la Channel Island.

Visiwa hivi viko mbali ya pwani za kusini mwa Uingereza na kaskazini mwa Ufaransa na ni visiwa maarufu kwa watalii ambao hupenda kwenda huko ama kununua nyumba za mapumziko au meli ndogo zenye mazingira ya kuishi kama nyumba.

Lakini cha msingi kisiwa cha Jersey hakipo katika umoja wa Ulaya wala si sehemu ya Uingereza kwa kusingatia masuala ya kuwa chini ya Malkia au sheria za Uingereza.

Lakini kabla ya kuelezea kuhusu uhuni uliofanzwa na bwana Chenge na genge lake, ni vizuri nikagusia kidogo kuhusu mambo matatu kuhusu Jersey ambayo yanahusu fwedha au uchumi , ulipaji kodi na uhusiano na nchi zingine.

Uchumi wa Jersey umelowea katika shughuli za kibenki na huduma zake na asilimia sitini ya uchumi wa kisiwa hiki inapatikana katika shughuli hizi.

Lakini katika sheria za Uingereza kama benki yoyote ile ina tawi katika kisiwa cha Jersey, basi mamlaka ya Ushuru ya Uingereza inaweza kudai taarifa ya akaunti ya mteja yoyote yule ambae anasadikiwa kufanza shughuli za uhalifu.

Ila kwa kesi ya Chenge bado haifahamiki kama ana akaunti katika benki yoyote ilio katika Jumuiya ya Ulaya ambapo wachunguzi wa kiingreza wanaweza kutafuta kwa kumuuliza bwana Chenge ambae wanasema ni "valuable witness" katika uchunguzi wao.

Suala la ulipaji kodi ni jambo lingine ambalo linaitisha vimulimuli ukizingatia kwamba bwana Chenge ameamua kuwekeza pesa yake kisiwani Jersey huku akipata faida na riba ambapo kwa upande wa Tanzania angelazimika kulipa kodo kutokana na kufanza hivo.

Na sula lingine ni uhusiano wa kisiwa hiki na nchi zingine.Kisiwa hiki kinajetegema chenyewe kama nchi kamili, tofauti na Uingereza. pia kisiwa hiki hakiwezi kushughulikia mambo yoyote yale yenye utata kama yanaingiliana na Uingereza na kwa kesi ya Chenge mambo yanaweza kuchukua miaka kuyatatua.

Jambo la msingi kuelewa hapa ni kwamba Andrew Chenge alikuwa anafahamu hii ni softicated, well documented case ambayo ilibidi amuajiri mwanasheria kutoka Cleveland Ohio,bwana J Lewis Madorsky.

Mambo haya ni magumu na natabiri kuwepo kwa utata katika kuyatatua katika siku zijazo.
 
Ni kweli unavyosema lakini kumbuka kwamba olusegun obasanjo ambae alikuwa raisi wa nigeria aliweza kurudisha ktk serikali ya nigeria vijisenti ambavyo mtoto wa dictator sani abacha alikua amezificha jersey island, kwahiyo nakubali ugumu upo lakini hii case ya nigeria inatupa matumaini.

halafu kitu kingine ni kwamba jersey island bado hawajapitisha sheria ya anti-corruption crime, ila mwaka 2006/07 wameizungumzia lakini bado haijawa sheria, kwahiyo richard mi naona serikali yetu ijaribu tu kuwauliza wanaigeria walifanyaje mpaka wakafanikiwa kurudisha vijisenti vyao.
 
Fundi Mchundo, heshima mbele.

Kungekuwa kuna watu wengi kama wewe, wanaochunguza na kusoma vitu mara mbili mbili, Bongo tungekuwa mbali sana.

Huwa naimba, Tanzania hakuna Media.
 
Mimi hawa waandishi wa habari wananitia kizunguzungu. Ni wapi aliposema Pinda kuwa tuwaache JK na Chenge wamalizane? Nilichokielewa mimi na elimu yangu duni ni kuwa Pinda amesema tumuache Rais alimalize suala hili maana yeye ndiye aliyemteua Chenge. Kumalizana ninavyoelewa mimi ni kuwa hawa wawaili tuwaachie wadundane mpaka hapo wote wawili watakaposhindwa kuendelea! Kitu ambacho sidhani Pinda anaweza kukisema.
Aliposema waachwe wamalizane nadhani ni tahadhari kwa wananchi kuwa masuala ya kitaifa hayawahusu!Ila mh rais na fisadi's!
 

Mimi hawa waandishi wa habari wananitia kizunguzungu. Ni wapi aliposema Pinda kuwa tuwaache JK na Chenge wamalizane? Nilichokielewa mimi na elimu yangu duni ni kuwa Pinda amesema tumuache Rais alimalize suala hili maana yeye ndiye aliyemteua Chenge. Kumalizana ninavyoelewa mimi ni kuwa hawa wawaili tuwaachie wadundane mpaka hapo wote wawili watakaposhindwa kuendelea! Kitu ambacho sidhani Pinda anaweza kukisema.

Kwa maneno ya mitaani, 'kumalizana' pia ina maana mnakutana mahali na kuelewana, kwa mfano unapokuwa unatoa teni parsenti unamwambia mtu, "hebu nifanyie hiyo kazi alafu baadaye tutamalizana." Nadhani inategemea maenno ya Pinda yalisemwa katika mazingira gani. Tusiwe wepesi wa kulaumu media.
 
Fundi Mchundo, heshima mbele.

Kungekuwa kuna watu wengi kama wewe, wanaochunguza na kusoma vitu mara mbili mbili, Bongo tungekuwa mbali sana.

Huwa naimba, Tanzania hakuna Media.
Ni kweli..ndiyo iliyombeba mkuu na sasa tunaona madhara yake!
 
Kwa maneno ya mitaani, 'kumalizana' pia ina maana mnakutana mahali na kuelewana, kwa mfano unapokuwa unatoa teni parsenti unamwambia mtu, "hebu nifanyie hiyo kazi alafu baadaye tutamalizana." Nadhani inategemea maenno ya Pinda yalisemwa katika mazingira gani. Tusiwe wepesi wa kulaumu media.

Kweli Susuviri,

huyu Pinda anajichanganya na maneno yake mwenyewe na wala asije hapa kulaumu media kwa kuandika kile alichosema. Kila kitu watu wake wanasema kuwa media zimekosea - unakumbuka ile story ya majeshi ya Tanzania Comoro?
 
Pinda kachemsha na kauli aliyoitoa bado ni mbovu na yenye madharau kwa wananchi wa kawaida.........unaweza kuona they all think the same.............ni sawa tu na kauli ya Andrew Vijisenti! Haoini kuwa ni muhimu kwa wananchi kushirikishwa kwenye madai muhimu na ya msingi yanaohusiana na ujambazi wa mali na fedha za umma na uhujumu uchumi unaopelekea mateso, vifo, magonjwa na umasikini wa kupindukia!

SASA WANANCHI AMBAO WALIKEMEWA NA KUTISHWA ILI TU WASIULIZE KUHUSU HIVYO VIJISENTI VYAO VILIVYOIBIWA....BADO MH WAZIRI MKUU HATAKI TUJUE HATMA YA VIJISENTI HIVYO KWASABABU KWA MAONI YAO....VIJISENTI HIVYO SIYO KIWANGO CHA WANANCHI! VIWANGO VYA WANANCHI NI VYA CHINI NA WAO WASUBIRI KANDAMBILI, KANGA NA PILAU ILI KUWA KWENYE KIWANGO WANACHOTAKA CHENGE, RAIS NA PINDA......KUWA WANANCHI HAWANA HAJA YA KUJUA ISSUE YA VIJISENTI HIVYO......BALI CHENGE, LOWASSA, PINDA, KARAMAGI, MSABAHA, WEMA, BALALI,MKAPA, MKONO, MRAMBA NA WENGINEO WA MATAWI NA VIWANGO VYA JUU AMBAO LIST OF SHAME ILIWABAINISHA!
 
Nimefanya Google serach ya Law firm nikakuta ina Mtanzania anafanya kazi hapo.Inawezekana ni moja ya sababu Chenge alichagua kampuni hii. Details zake ni:

Evarist H. Mbuya
Firm: J. Lewis Madorsky Co. L.P.A.
Address: 3934 Washington Blvd
Cleveland, OH 44118-3135
Map & Directions
Phone: (216) 371-7600
Fax: (216) 371-7601
 
Back
Top Bottom