The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

tatizo siyo Shs. Bilioni moja benki... ni fedha zilikotoka.. and let me put it very plainly:

a. Fedha hizi siyo malimbikizo ya akiba baada ya muda (not accumulation of savings over time) kama watu wanavyotaka tuamini.

b. Fedha hizi ziliingia kwenye akaunti hiyo baada ya 2001 (ununuzi wa rada) na kwa vile fedha zinavyozunguka huacha alama; za Chenge zimeanzia mbali zikiingizwa kidogo kidogo baada ya kumegwa. Yaani alipata fungu, akazimega kidogo kidogo kwa kutumia "njia mbalimbali" halafu kutoka njia hizo akaziassemble kwenye akaunti yake...

c. Zingekuwa ni za Savings SFO wasingehangaika nazo.. remember.. money will always leave tracks!!


Ahsante sana mkuu mzee mwanakijiji,

Labda kwa kuongeza uliyoandika ni kuwa hawa SFO wameangalia bank transactions 12 mil dollars zilizotolewa commission kwa aliefanikisha kununuliwa rada. Then from there kuna transactions nyingine na pengine hiyo ya chenge ni mojawapo.

Hawa ni watu makini na wenye ujuzi hawawezi kuchunguza kitu pasipo na mashaka na uwezekano wa kutendwa kwa jambo lenyewe.
 
Ahsante sana mkuu mzee mwanakijiji,

Labda kwa kuongeza uliyoandika ni kuwa hawa SFO wameangalia bank transactions 12 mil dollars zilizotolewa commission kwa aliefanikisha kununuliwa rada. Then from there kuna transactions nyingine na pengine hiyo ya chenge ni mojawapo.

Hawa ni watu makini na wenye ujuzi hawawezi kuchunguza kitu pasipo na mashaka na uwezekano wa kutendwa kwa jambo lenyewe.

Wanachojaribi sasa ni kutaka watanzania tuamini kuwa ile ni savings, saving isingewaleta watu kutoka UK kuja TZ wakati account inaonyesha pesa ziliingia kidogokidogo, hii pesa iliingia kwa wakati mmoja au ndani ya kipindi kifupi sana na ndo maana wao wanamuita shaidi muhimum kwa kesi yao.
 
Issue ya Chenge iko based kwenye "Relativity Theory" ya Einstein.

Chenge angekuwa na akina Billy Gates akaongea kuhusu vijisenti wangemuelewa bila matatizo. Bahati mbaya kwa asilimia kubwa sana ya Watanzania dola million moja ni hela nyingi sana.

Jaribu kufikiria wale madaktari wa Muhimbili:

Doctors at Muhimbili Hospital went on strike over pay in November demanding that their starting salary should be raised substantially. On November 20th the government complied by raising junior doctors’ salaries by over 60% from Tsh. 226, 000 to Tsh. 420,000 and to Tsh. 1,141,000 from Tsh. 1,030,000 for specialists and consultant doctors. On November 25th the doctors rejected the award.

wafanyakazi wa kima cha chini na machingas hizi ni hela nyingi sana na wanaweza wasikuelewe ukiwaambia hizo hela ndogo. Hii inatokana na Relativity.

09/08/2007
MOSCOW (AFP) - The richest 10 percent of Muscovites are 41 times richer than the poorest 10 percent, a gap that dwarfs the national divide, Russia's state statistics service said Thursday.

"Moscow's richest 10 percent earned 41 times more in 2006 than the poorest 10 percent," state statistics service assistant director Leonid Arshon told AFP.
Nationwide, there was a 15-fold gap in earnings, he said - up from a gap of 10 times in 2001 and 14 times in 2003.

Russian Academy of Sciences economist Ruslan Grinberg warned that in countries where the gap is a factor of 10 or higher, "the conditions are created for social disorder."
"The only place that rule doesn't hold is in America, where the coefficient holds steady at 10-12. But there it is considered normal, since their philosophy differs from ours," he told daily newspaper Izvestia.

The state statistics service puts the official poverty level at 15 percent nationwide, while Kremlin economic advisor Arkady Dvorkovich has said the real level may be over 25 percent.


Insurgent:
Raising the low wages to 150,000/- brings us to 10-fold gap. Safe?

Gap kati ya matajiri na masikini inaongezeka kwa kasi sana na huyu mzee anaelekea kutokuelewa asilimia kubwa ya Watanzania ni masikini. Kuna umuhimu wa Mawaziri kujua reality ya maisha ya watu wa chini.

Bado sielewi pamoja na hela yote hii bado anatafuta nini na Uwazirii? Huyu angeweza kuendeleza jimbo lake SANA kama angeomba kupumzika kama wenzake. Sasa spotlight inammulika...
 
Mtu Ukiwa Na Hela Zako Tatizo Usipokuwa Nazo Tatizo Kweli Waswahili Noma Sasa Wanaandamana Ili Iweje ? Kwa Faida Ya Nani Mkoa Wa Dodoma Upo Nyuma Sana Kimaendeleo Na Kielimu Wafikirie Mambo Hayo Kwanza Kabla Ya Mengine Yote Waache Longo Longo

Shy vitu vingine ni sensitive kwa watazania wewe unaleta utani ndani yake, hivi hiyo 1.2 Billion kama wangepewa Dodoma impact yake ingekuwaje, madarasa mangapi dodoma yangejengwa, wangapi wangepata maji safi, wangapi wangepata umeme be serious sometomes sio kuleta utani wakati wote.
Tunachoangalia ni timing kama zingeingia kidogo kidogo sioni tatizo na hilo, lakini billion moja within a short period, na kama ana hisa somewhere ni hisa nyingi sana alizinunua na nini?
 
Mimi nafikiri hawa jamaa tuwaunganishe na MAGAIDI / TERRORIST ili wanavyohamisha hela zao nje ya nchi waweze kukamatwa au kuchunguzwa kabla ya hizo hela hazijahama. Mabenki ya dunia ya kwanza ukiingiza hela kiwango fulani wanakuripoti serikalini kwao, mbona hawa jamaa hawajaripotiwa wanapohamisha hela zote hizi?

Nafikiri kuwashitaki hawa jamaa ni kutumia sheria za dunia ya kwanza na kujua mafisadi wote wanaoweka hela katika benki zao. Kimsingi, kwa sababu ni public figures, watueleze wamezitoa wapi.
 
Jamani mambo haya mazito, kufungua kesi si mchezo eti,umesahau waziri mkubwa mwenyewe aliongea waziwazi kua wanawaogopa sasa kama serikali inawaogopa weye utaweza? Utaalamu wa kesi hizo anao mchungaji itabidi aombwe ushauri.Kwa mawazo yangu kushitaki haitasaidia kwani unaposhitaki unapaswa kutoa ushahidi,je, ushahidi upo? nadhani la muhimu ni kutumia asasi mbalimbali na vyombo vya habari kuwajulisha wananchi kinachoendelea ili wawe na busara wanapochagua viongozi waache kuchagua watoa pilau.
 
Jamani mawaziri kama subordinates wa fisadi Mkapa waliona Kingunge yuko busy kukusanya utajiri kwa kila hali, na wao wakaingia kazini.

Chenge amponza Mkapa

na Asha Bani
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

TUHUMA za kujilimbikizia mamilioni ya fedha nchi za nje zinazomwandama Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, zimemgusa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, ambaye sasa ametajwa kuwa chanzo cha viongozi kutumia madaraka yao kujilimbikizia mali.

Mkapa, ambaye kwa kipindi kirefu sasa amekuwa akidaiwa kutumia vibaya madaraka ya urais katika kipindi cha miaka kumi alichokuwa rais, anakabiliwa na shinikizo la kutangaza mali alizochuma katika kipindi chake chote cha uongozi.

Shinikizo hilo limetolewa jana na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) wakati akiwahutubia mamia ya wafuasi wa vyama vya upinzani katika mkutano wa hadhara wa kuhitimisha maandamano ya kukishinikiza Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutekeleza makubaliano ya kuanzishwa kwa Serikali ya mseto Zanzibar yaliyofikiwa na vyama hivyo mwishoni mwa mwezi uliopita, uliofanyikia viwanja vya Ilala Garden, Buguruni, Dar es Salaam.

Katika mkutano huo ambao ulihudhuriwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya Tanzania Labour na CHADEMA, Prof. Lipumba alisema viongozi wanaotuhumiwa kwa kashfa mbalimbali za ufujaji wa fedha za umma na kutumia madaraka yao kujilimbikizia mali, walishirikiana kufanya vitendo hivyo na Mkapa.

Alisema kushindwa kwa Mkapa kutangaza mali alizoondoka nazo madarakani ni ushahidi kwamba anahusika pia katika tuhuma zinazowaandama baadhi ya waliokuwa wasaidizi wake wakati akiwa madarakani.

Huku akishangiliwa na umati wa waandamanaji, Prof. Lipumba alimtuhumu moja kwa moja Mkapa kuwa ndiye chanzo cha ufisadi katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupitia akauti ya malipo ya madeni ya nje (EPA) na Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, kwa kile alichodai kuwa, alitumia madaraka yake kuwalinda viongozi waliokuwa wamepewa dhamana ya kusimamia maeneo hayo.

“Mkapa alishindwa kusimamia vizuri rasilimali za wananchi wake katika kipindi chake cha miaka kumi ya urais. Ni katika kipindi hicho alianzisha asasi yake ya ANBEN.

“Tunajua kuwa ANBEN ilianzishwa baada ya kufariki Baba wa Taifa, hizi ni dalili kwamba walikuwa wanamuogopa kwa sababu alikuwa akikemea rushwa na ufisadi waziwazi, hivyo hawakuthubutu kufanya hivyo alipokuwapo,” alisema Prof. Lipumba.

Alisema tuhuma zinazomkabili Waziri Chenge pamoja na viongozi wengine walio ndani na nje ya madaraka, ni lazima zichunguzwe kwa umakini na Tume ya Maadili yenye mamlaka yote kisheria.

“Tunaelewa kwamba hapo awali viongozi walitakiwa kuorodhesha mali zao katika fomu za maadili, sasa tunataka kuziona ili kubaini kila mmoja ana mali kiasi gani,” alisema Lipumba.

Alisema kesho (Jumatatu) atakuwa mmoja wa viongozi wa upinzani wanaokusudia kwenda katika ofisi za Tume ya Maadili ya Viongozi kuomba fomu za viongozi mbalimbali akiwemo Chenge, Mkapa na Dk. Daudi Balali, kuona wana mali kiasi gani.

Kwamba wamekubaliana katika kambi ya upinzani kuchukua hatua hiyo ili kutambua mali zinazomilikiwa na viongozi wastaafu na walioko madarakani wanaotuhumiwa kuwanyonya Watanzania.

“Dalili za Chenge na Mkapa kulindana zilianza siku nyingi kwani Mkapa alipotakiwa kutaja mali zake, Chenge alidai haruhusiwi wakati huo. Baadaye tunasikia baadhi ya viongozi walianzisha benki wakiwa madarakani, lakini kwa unyonge wa Watanzania hatukugundua,” alisema Lipumba.

Alidai kushangazwa na hatua ya Mkapa kushindwa kutangaza mali zake wakati akiondoka madarakani, lakini alipokuwa akiingia Ikulu alitaja mali alizokuwa nazo kuwa ni pamoja na nyumba mbili, moja ikiwa Masasi mkoani Mtwara na Dar es Salaam, pamoja na shamba lenye mikorosho 100.

Kauli hii ya Prof. Lipumba imekuja baada ya Chenge kudaiwa kujilimbikizia kiasi cha zaidi ya sh bilioni moja katika benki moja iliyoko katika visiwa vya Jersey, nchini Uingereza.

Prof. Lipumba pia alitumia sehemu ya muda wa hotuba yake kumshangaa Rais Kikwete kwa kukataa kumaliza mtafaruku wa kisiasa Zanzibar, wakati aliweza kufanya hivyo nchini Kenya baada ya kushiriki kuwapatanisha Rais Mwai Kibaki na Waziri Mkuu Raila Odinga.

Alisema kuwa Rais Kikwete ni sawa na msanii, kwa vile ni mtu anayependa starehe za kutembea katika nchi za watu na kujizolea sifa zisizo na kichwa wala miguu, huku kwake kukiwa na matatizo ambayo hayahitaji hata nguvu kutatua, lakini anafanya mzaha na kuwadharau Watanzania wanaodai haki.

Alisema anachokitaka Kikwete sasa ni ule usemi wa vijana wa ‘jino kwa jino’ na ndicho kinachofuata, kwa kuwa ameshindwa kulinda demokrasia ya Watanzania na kuwachezea.

“Nafahamu Tanzania ni nchi ya demokrasia, lakini viongozi wake hawapendi demokrasia, wanajilimbikizia mali na kushindwa kuwahudumia Watanzania walio wengi, ambao ni maskini na ndio wapiga kura wao.

“Kwa kushindwa kumaliza suala hili na kulifanya liwe la mzunguko, mimi namwita Kikwete kama msanii,” alisema Prof. Lipumba.

Naye Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad, aliwaambia waandamanaji hao kuwa Katibu wa CCM, Yusuph Makamba, hana kitu cha maana anachokifanya katika chama hicho, kwa sababu anashindwa hata kuaminiwa na wenzake waliomtuma kukaa katika meza ya muafaka, kwa kudharau maamuzi aliyoshiriki kuyakifikia katika meza hiyo.

“Na rais akumbuke kuwa haiwezekani kukaa meza moja na Makamba, kwa kuwa Makamba ni kama mtu asiye aminika katika chama chake, yuko hapo kwa ajili ya kula na kuchuma fedha za walalahoi,” alisema Maalim Seif.

Alieleza kushangazwa kwake na kauli ya Rais kikwete ya kutaka kuwepo kura ya maoni ya kuamua uanzishwaji wa serikali ya mseto wakati mambo yalishamalizika na kubaki utiaji saini kwa makubaliano yaliyofikiwa.

“CUF haiwezi kupoteza muda na kuzungumzia suala kama hilo ambalo Rais Kikwete analifanya kama ni la usanii na mzaha,” alisisitiza Maalim Seif.

Mwenyekiti wa TLP Augustine Mrema kwa upande wake alisema Rais Kikwete ana sura tatu zisizofanana.

Naye alimlaumu kwa kushindwa kumaliza mgogoro wa Zanzibar na kufanikiwa kutatua ule wa Kenya.

Mkurugenzi wa Vijana Taifa wa CHADEMA, John Mnyika, ambaye alimwakilisha Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, alisema suala la kutaka kuundwa kwa serikali ya mseto Zanzibar ni suala la wote bila kujali itikadi.

“Watanzania si wajinga, ila CCM inajifanya kama imeweka ganzi katika mishipa ya fahamu na kufumbia macho matakwa ya wananchi, lakini hiyo ganzi itakwisha siku moja,” alisema Mnyika.

Katika maandamano hayo, waandamanaji walibeba mabango yaliyokuwa na ujumbe wa aina mbalimbali, kumtaka Rais Kikwete kukubaliana na majadiliano yaliyofikiwa baina ya CUF na CCM.



Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 5 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)
Kisukuma hela alizonazo Chenge ni mashitabalwa yaani uncountables, tusende ni lugha ya dharau sana kwamba nothing nothing.Halafu nyie wadanganyika wenzangu Sielewi kwa nini hamkumbuki mwanzilishi wa yote haya. Huyu aliwaita mafisadi wenzake huko Zanzibar wakasema azimio la Arusha linatunyima usingizi hatuwezi hata kutajirika yahe futilia mbali hilo azimio kuanzia sasa kila kitu ruksa! Sasa waliotumia vizuri hiyo ruksa mnawalaumu kwa nini? Mbaya ni nani ndugu yako aliyeacha mlango wazi baada ya kupanga na ma******* au ******* aliyefunguliwa na ndugu yako akatwaa bila mlio wa bunduki?

Kwa nini hamkumbuki Mrema alipolalamika nji hii nimekamata sahabu sa vigogo airport? Zilikuwa kilo ngapi? Ni za thamani ya visenti trillion ngapi? Kama Mwinyi alidiriki kukubali hata kuitwa shemeji na watoto wa shule kwenye uporaji alikuwa kinara kiasi gani? Kwa nini mnahangaikia matawi badala ya kuchimba mzizi? Sasa hivi Hussein Mwinyi anaandaliwa kuwa raisi wa Zanzibar ili akafiche siri huu ufisadi hamuuoni?

na Ntemi, Mwanza, TZ, - 20.04.08 @ 14:05 | #7529

Ukweli Tanzania ilishaanza kuharibika enzi za Mwinyi ingawa watu hawataki kuliona hilo.

na *****, Tz, - 20.04.08 @ 14:14 | #7531

Sijui ni nani atakuwa safi Tanzania! Ifikie mahali tuachane na itikadi za Vyama! Nilipokuwa China Juzi watu mafisadi walikuwa wakinyongwa hadi Wakuu wa haki za Binadamu walipiga makelele. Nilimwona Rais wangu Kikwete alikuwapo nchini humo na anajua Mafisadi walikuwa wakinyongwa wakati yeye alikuwa akifanya ziara nchini humo! Kwa bahati nilitembelea sehemu alipokuwapo Rais wangu huyo! Pembeni yake, katika mkutano mmojawapo alikaa CHENGE, mwanasiasa ***** na mwenye dharau anayeita mapesa vijisenti kwanini tusianze naye wakati Rais alikuwa akiona wenzake?

na LCD, Taipei Taiwan, - 20.04.08 @ 14:16 | #7532

Rais kikwete ameshapoteza mwelekeo na sasa hana la maana analofanya zaidi ya usanii.Sasa watz tuamke tudai haki zetu kwa umoja,tuhakikishe mkapa na mafisadi wenzake wanarudisha mali zote walizopora ili zihudumie wananchi wote wa tanzania.

na RUME, DSM, - 20.04.08 @ 14:19 | #7533

Kazi ya kupapambana na mafisadi tuianze sasa. List inazidi kuongezeka ilikuwa JK eleven sasa ni zaidi, tuwang'oe wote kwa nguvu ya umma.

Na huu ni wakati wa kum confront JK na maswali kutoka kwa waandishi wa habari-ambao ni mdomo wa wananchi: Aulizwe na waandishi wa habari kwa nini anakumbatia mafisadi? Kwa nini rafiki zake wa karibu ni mafisadi?. Of course waandishi wamuulize siku ya Jumanne, kwa sababu JK leo na kesho anaomboleza kifo cha Ditopile Mzuzuri ambaye amefia Hotel ya Hilux Morogoro leo asubuhi. Ikumbukwe alimuua dereva wa daladala kwa risasi barabarani

na Kawamala, Ubelgiji, - 20.04.08 @ 14:52 | #7538
 
Je, safari za Kikwete nchi za nje ni kukimbia hali halisi iliyopo nchini kama kuongezeka kwa gharama za maisha, kutochukua hatua zozote dhidi ya mafisadi, kuonekana hana uwezo wa kuiongoza Tanzania n.k.?

Chenge kamtia aibu Rais Jakaya Kikwete

Christopher Nyenyembe
Tanzania Daima

AMA kweli Waswahili walikwisha kusema sikio la kufa halisikii dawa, ndivyo hali inavyojidhihirisha kwa baadhi ya viongozi wa serikali wanaoendelea kusakamwa na jinamizi la ufisadi, licha ya wengine kujiuzulu.

Tuhuma dhidi ya vitendo vya ufisadi kwa viongozi waandamizi wa serikali inawezekana ikawa ndiyo chimbuko la tabia ya watawala hao kuoneana aibu, kulindana na kutosikia kilio cha wananchi.

Sikutegemea katika mlolongo wote wa ubishi na kukana, mtu anaumbuliwa na vyombo vya nje.

Sijui Rais Kikwete analipokeaje hili la Chenge, maana si siku nyingi viongozi wa upinzani na wananchi kadhaa walipaza sauti wakisema, Andrew Chenge, hafai kuwa waziri katika baraza jipya.

Chenge alizivunja hoja za watu hao alipokejeli kuwa rais ndiye anapaswa kueleza kwa nini alimchagua kwa mara nyingine.

Kiburi na kujiamini inawezekana ndiko kuliko mshawishi Rais Kikwete akubaliane na ushujaa wa Chenge wa kuukana ufisadi kwa macho makavu na bila aibu akijiaminisha kuwa hao wanaomuandama wanamuonea gere.

Lakini pamoja na mazingira hayo, hali inaonyesha kuwa Rais Kikwete alikuwa hafahamu mchakato mzima wa kumchunguza waziri wake.

Rais kupitia vyombo vya dola, Polisi na Usalama wa Taifa bila kuiweka mbali, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), havikuwa na jukumu lolote la kumjulisha kuwa hali si nzuri kwa mmoja wa mawaziri wake anayetuhumiwa kwa ufisadi.

Uwepo wa shaka na mazingira ya rais aliyechaguliwa kwa kura na Watanzania wengi waliomwamini kuwa anafaa kuwaongoza, kuwatii na kuwasikiliza, umefika wakati ambao sura ya huruma na upole haipaswi kuonekana katika suala la Chenge.

Inawezekana nchi zilizoendelea zinazionea huruma zaidi nchi maskini lakini kwa umaskini wetu mkubwa sisi wenyewe hatuoneani huruma. Hali hiyo ndiyo iliyojenga tabaka katika jamii ya sasa la walionacho na wasiokuwa nacho.

Tabaka hilo limewafanya viongozi waandamizi wa serikali kuwa juu kabisa kwa kila kitu huku kundi kubwa la wananchi wakiendelea kuwa maskini na wanaoishi maisha ya dhiki, maisha magumu na taabu zisizokwisha.

Ufisadi unaowaandama baadhi ya watendaji wa juu wa serikali unazidi kuwakatisha tamaa wananchi, hawaoni mbele huku kundi la watu wachache likiendelea kunufaika na jasho la wanyonge na kuwaondolea matumaini ya maisha bora.

Gazeti la The Guardian la Uingereza si tu kwamba limeifahamisha dunia nzima jinsi nchi maskini zinavyotafunwa na viongozi wake wenye tamaa, na mioyo ya inda, kama ilivyo kwa Chenge ambaye ana nguvu za kusimama hadharani na kuzikana tuhumu hizo ambazo kwa mbeleko ya serikali zimeichafua Tanzania.

Ni aibu na kuna maswali mengi; inakuwaje mtoto wa mkulima na mfugaji kama Chenge kwa dhamana kubwa aliyopewa na serikali aamue kutunza kiasi kikubwa cha fedha kwenye benki za nje, hivi ameshindwaje kuzitunza kwenye Benki ya makabwela (NMB).

Hivi hakuweza kujua kuwa kukua kwa utandawazi kumeifanya dunia kuwa kama kiberiti, kila jambo lipo wazi, bora angeziingiza fedha hizo kwenye mfuko wa Rais wa kuwasaidia wajasiriamali wakopeshwe kwa masharti nafuu.

Bilioni moja zilizowekwa na kulala kwenye benki moja katika visiwa vya Jersey, Uingereza kwa namna yoyote ile zisingeweza kuwanufaisha Watanzania na ndivyo inavyodhihirisha aina ya viongozi tunaowachagua kwa sura ya pesa.

Kama tunawachagua viongozi kwa pesa zao, kwa wapiga kura kununuliwa, leo hii wananchi wanawezaje kuwakana viongozi waliowaweka madarakani kwa kipande cha kitenge, fulana, kofia na lita moja ya pombe ya aina ya komoni, wakaonekana wabaya kwao?

Hata wanaolalamikia ufisadi ni kundi ndogo tu la wananchi wasomi na waelewa, lakini naamini kabisa idadi kubwa ya watanzania kutokana na uelewa mdogo hawajui fisadi ni dudu la aina gani na pengine wanaulinganisha ufisadi sawa na dalali wa kuuza mitumba kwenye minada na magulio.

Nasema hivi kwa kuwa nataka kuzigusa nyoyo za Watanzania wengi wanaozichukulia tuhuma nzito za ufisadi na rushwa kama sehemu ya uonevu, chuki na itikadi za kisiasa na wanasahau kuwa dhambi ya uhujumu uchumi ndipo ilipowafikisha hapo walipo.

Leo hii, Waziri Chenge amezama kwenye lindi la tuhuma hizo ambazo nadhani katika historia ya nchi maskini kama Tanzania haijawahi kutajwa kiongozi yoyote katika serikali kuwa na kiasi kikubwa cha fedha kama hizo nje ya nchi.

Kutokana na uzoefu na hulka ya mwanasiasa huyo mbali ya kushika nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali, ana kila sababu ya kusimamia utetezi wake na kuukana kwa nguvu zote ufisadi unaomwandama ili aweze kujikosha.

Naamini kabisa, ana kila sababu ya kunena ukweli na kukana ubaya unaotajwa juu yake kwa kuwa maadili mema aliyopewa tangu alipobatizwa ni kukana dhambi, kumkana shetani na hila zake zote.

Sifikirii leo hii ndugu yetu huyo ageuke na kuwa mfuasi wa shetani, kwa kuwa viongozi wengi wa madhehebu ya dini muda mwingi wamepiga kelele wakikemea ufisadi ambao umeliweka taifa kwenye alama nyekundu ya kiuchumi kiasi kwamba tumegeuka kuwa ombaomba.

Ufisadi uliokithiri ndio unaomfanya Rais Kikwete asitulie ndani ya nchi yake na amekuwa akitumia muda mwingi kupita huku na kule ili kuomba misaada katika nchi zilizoendelea, hali hii inatutia aibu lakini hakuna jibu jepesi.

Tanzania imekosa nini kwa Mungu imejaliwa kila kitu lakini inatawaliwa na viongozi wenye uchu na tamaa ya kujilimbikizia mali kupita kiasi.

Kama Rais anafanya kazi ya kuzuru nchi mbalimbali tajiri duniani, iweje awe na shingo ngumu ya kushindwa kuwachukulia hatua viongozi aliowateua, wanaotuhumiwa kwa rushwa na wanaoweka utetezi wa kiini macho mbele yake, hiyo inatia shaka.

Naamini, hata kwa kauli ipi iliyo nzito na nyepesi, Chenge hawezi kukiri kile anachoamini kuwa kitamuondosha katika ujasiri wake wa kukiri ukweli au uongo na kuufanya uongo uwe ukweli huku moyoni akiwa amejifunga kwa dhambi zisizoungamika kwa wanadamu wenzake.

Lakini pamoja na mtazamo wa yote hayo, mwenye dhamana ya kuwadhihirishia Watanzania kuwa Serikali ya Awamu ya Nne haipendi rushwa na ufisadi ni Rais Kikwete.


cnyenyembe@yahoo.com
0754 301864
0787 862586
 
""AMA KWELI CHUMA HUNOLEWA KWA CHUMA"" walioyatenda wanamtandao 2005 sasa ndio wakati wao pia kuyarudi yaana namaanisha ""WHAT GOES AROUND COMES BACK..........""mtamalizia
 
""AMA KWELI CHUMA HUNOLEWA KWA CHUMA"" walioyatenda wanamtandao 2005 sasa ndio wakati wao pia kuyarudi yaana namaanisha ""WHAT GOES AROUND COMES BACK..........""mtamalizia

Hakuna mshipa wa noma ndani ya CCM , kama mambo ya EPA na danadanam hadi sasa watu wanashikilia ofisi na wezi wanaombwa kurudisha pesa basi hakuna la kutegemea toka kwa Rais kwenda kwa mshikaji wake wa karibu mzee wa Vijisenti .
 
naamini neno "aibu" limefutika kwenye msamiati
wa mafisadi
 
Sisi watanzania kusema kweli kama ni usingizi..majority wetu tunauchapa kisawasawa!Inashangaza sana kuona kwamba mtu kama Mh Rais ameshindwa kujiweka upande wa wananchi na kuwateteta kama katiba inavyomtaka!Ni jambo la busara sana kwa viongozi kuhakikisha kwamba bado wako intouch na wananchi na sio kuwa out of touch!Kwamba mh rais anashindwa kuwa na empathy na kujiweka kwenye nafasi ya mtanzania wa kawaida!Nashangazwa saana na utofauti ambao wameuonyesha..mpaka inafikia mahali tunajiuliza"HIVI KWELI VIONGOZI WETU NI WATANZANIA HALISI?"Ni maswali ambayo huwa nashindwa kuacha kujiuliza kadri ninavyozidi kupata muda wa kufuatilia mwenendo wa siasa zetu nchini!Inanishangaza sana pale ninapoona kuwa either kwa makusudi ama kwa ulazima Mh Rais ameshindwa kuyatumia madaraka makubwa aliyonayo katika mpampano huu dhidi ya mafisadi!Mimi ni mmojawapo wa watu ambao nilikuwa nikimuona Kikwete kama "mtu wa watu"Raisi wa wanyonge na masikini..ambao ndio waliompeleka ikulu!Kwamba walipewa pilau,malapa,na kanga..hiyo sijui kama ilikuwa ndio the only reason walimpigia kura!Kikwete alikuwa kipenzi cha watu na ndio maana mwalimu ilibidi azungunke nchi nzima kumnadi Mkapa..wote tunakumbuka hayo!Lakini kitendo cha mheshmiwa raisi kuwageuka wanyonge na masikini na kujikita kwenye siasa za mafisadi waliyoiuza nchi yetu kwa bei ya jumla huku wakigawana mifupa na mabaki.. na kuzidi kuwakumbatia wale wanaokiri kuwa "BILIONI NI VIJISENTI"..Kama yale yaliyotokea huko Ufaransa wakati wa French revolution pale malkia alipowaambia wakina mama waliokuwa hawana hata mkate wa kuwalisha watoto wao..kwa maana kuwa njaa ilikuwa kubwa..malkia aliwajibu kina mama hao walioandamana hapo ikulu kuwa"KWANINI MSILE KEKI?"Wakina mama hao walishangazwa kwani malkia alikuwa out of touch!Yeye akila keki badala ya mkate huku watoto na kina mama hao wakililia walau mkate kwa watoto wao!Mapinduzi ya ufaransa ndio hapo yalipoanza!Chenge kutuambia watanzania kuwa bilioni anazoshutumiwa kuzipata isivyo halali ni visenti inaonyesha jinsi ASIVYOJALI KABISA!Hana hata chembe ya huruma wala ubinadamu!Inasikitisha ndugu wana jf kwani wote tunatembea mitaani na vivjijini na kujionea jinsi umasikini ulivyokithiri!Mimi nionavyo..nchi yetu inayapitia mambo ambayo wenzetu pia waliyapitia miaka mingi iliyopita...ni wazi kuwa pengo kati ya masikini na matajiri litapelekea mgawanyiko mkubwa!Nimegundua kuwa CCM wanapenda upinzani uwepo!Kwasababu distraction itakuwepo!Wakiitwa mafisadi na wao wanaeneza propaganda na kuwaingiza wapinzani kwenye listi ya ufisadi lii kuwaneutralize na kuwa confuse wananchi wa kawaida ambao wao wanafikiria watapata wapi mlo!CCM inabidi wawe accountable this time na wafanye mabadiliko ambayo yatainufaisha nchi hata kama upinzani wataonekana kuwa wana nia nzuri..hiyo haijalishi!Nia ambayo wameanza kuionyesha mahsusi kuanzia pale "mwemne yanga"Nawaeleza viongozi wetu Tanzania kuwa UANAUME WA KWELI NA UONGOZI BORA NI KUCHUKUA MAAMUZI MAGUMU KWA NIABA YA WANANCHI!Mh rais hata kama Ufisadi utakuwa umekupitia kwa ukaribu..kuchukua uamuzi wa kuushughulikia kwa nia njema..na kuwawajibisha wote..na kuwaomba wananchi msamaha na kulimaliza hili suala kihistoria na kuwa kiongozi atakaye kuwa kwenye upande wa wazalendo kwenye historia ya nchi yetu!Mh Rais kwa waelewa wa mambo ni wazi tunajua yuko kwenye wakati mgumu..wakati ambao ndio kipimo kikuu cha uongozi!Hata kama ikifikia kuunda timu mpya ya wasaidizi!watu wapya,uongozi mpya..ndio walichokuwa wakililia wananchi mara baada ya wewe kuupata uraisi..lakini bado inaonyesha kwamba unakumbatia upande wa ule msemo wa mkaa hauwezi kuwaka peke yake!Mh Rais pangua mikaa yote weka mipya..washa moto!utawaka tu!tunajua inachukua muda ila eventually utawaka!utakuwa moto mpya..utakaopelekea hari mpya!UWAJIBIKAJI NI LAZIMA!Mh rais wanaokushauri wanakosea..ama umeamua mwenyewe kukosea!?Zamani mwalimu aliweza kuidhibiti Tanzania kwani alikuwa akiwanyima haki nyingi tu za kimsingi..kama vile kukutana..enzi hizo kila mtu spy!na hamruhusiwa watu kufanya mkusanyiko wa aina yeyote..sasa dunia ya sasa ni tofauti..watu hawana hata haja ya kukusanyika physically..jf ni mfano..tunakusanyika na kutoa maoni yetu..kuna bubu humu ndani kuna mwiba,wanavijiji,mapadre,masheik,viongozi wazalendo,wanasiasa wa tofauti kama makada na kina John Mnyika..na pia wewe mheshmiwa rais sometimes i am sure unakong'otea jf hapa na pale..na kwa hivyo basi tunakuwa tumeshakutana bila hata kibali..huku usalama wa taifa ukitumbua macho tu bila kuwa na uwezo wa kufanya lolote!wa kupingana na dunia mpya bila kutumia ugaidi!Maisha ya watu tu ndio hala hala yasiwekwe hatarini hata siku moja!Badala yake Mh raisi ujue kuwa sote tuna nia nzuri na nchi yetu..ila labda kimaamuzi flani flani tunatofautiana!Naamni deep inside your heart there is still something..something that you yourself needs to revive it..and then umshinde shetani na uwakomboe wananchi kutoka kwenye makucha ya ufisadi!Kwenye hili ..yes time is a factor lakini nachelea kusema kuwa history inweza isije kuwa upande wako kama usipoitumia nafasi hii muhimu na hadimu kihistoria kama "lulu"Uongozi ni mgumu mh rais..sijui kama ugumu unaouchukulia wewe ni wa u "busy" wa kishughuli ama ni wa maamuzi!mimi nauzungumzia wa kimaamuzi kwani unaweza ukawa rais na ukafanya maamuzi ambayo yatawanufaisha wananchi hata kama utapata wakati wa kuwa "broken hearted" kwa kuwasukumia pembeni marafiki wapenzi wa siku nyingi..uliokuwa ukifanya nao kazi siku nyingi tu! na wasaidizi mafisadi..na kujikita kwenye timu mpya..yenye maono mapya na mapenzi dhabiti na yakweli kwa nchi yetu!Na sio wanaokula na kufakamia bila huruma na hapo hapo bila kujali na kuwatukana wanyonge!kuwaambia ndio nimeiba hivyo visenti lakini Mh rais hawezi kunifukuza kazi!Chenge alikuwa mwamuzi wa mwisho kwenye kila mkataba na keshawatega viongozi na hawawezi kumminya!Wao walikuwa wana imani nae kwani yeye kama mwanasheria mkuu..alikuwa na uwezo wa kuhakikisha hata kama kuna ufisadi..sheria za nchi zitakuwa zimefuatwa na mafisadi watakuwa wamelindwa na sheria hizo!Issue ilivyokaa kwa maoni yangu ni kwamba ikiwa kuna siku upinzani utachukua nchi..then kuna hatari kubwa ya viongozi kufikishwa mahakamani!Kwa ajili hiyo mh rais akaamua kuendelea kumkumbatia!Lakini sidhani kwamba Chenge kuwa mwanasheria mkuu kunamfanya kuwa na uwezo wa kuziba mianya yote!Hatoweza kwani maslahi ya wananchi hayajawahi kupewa kipaumbele!Dola ndio inayowalinda viongozi wetu!Where are we going?Nina imani kuwa kabla hata ya sheria ama uchunguzi wowote ule..mazingira ya matukio yenyewe yana nguvu za hoja za kutosha kumfanya mh rais awasimamishe kazi viongozi wote..kutangaza hali ya hatari na kuutokomeza ufisadi!
 
Inategemea yeye ni msafi kiasi gani. Kwani yeye hakuwa kwenye serikali wakati haya madudu yanafanyika. Lazima tufikirie mbali kuna sababu zinazompa kigugumizi.
 
Inategemea yeye ni msafi kiasi gani. Kwani yeye hakuwa kwenye serikali wakati haya madudu yanafanyika. Lazima tufikirie mbali kuna sababu zinazompa kigugumizi.
Na ndio maana nikasema kuwa Mh rais yuko kwenye wakati mgumu kwasababu ili kuumaliza ufisadi..ni lazima awaombe watanzania msamaha na atumie madaraka aliyonayo kikatiba hivi sasa kwa kuwa upande wa wananchi na kuwawajibisha mafisadi wote!Mifano halisi ipo kwenye vitabu vitakatifu kwa mambo ambayo yaliwakumba viongozi wa enzi hizo ambao walikuwa ni wafalme!Kuna waliokuwa wakikabiliwa na wakati mgumu lakini hawakuthubutu kuwatosa wananchi!Walikubali kujishusha na kuvaa magunia kwa masikitiko huku wakilia kisiri siri kwa uchungu wa maamuzi hayo!Hii issue ya ufisadi ndio jinsi ilivyokaa!Asipofanya something this time then ajue kuwa atakuwa ameifumbia macho opportunity kubwa ya kuweka historia madhubuti na kuinusuru nchi yetu na machafuko mabaya ambayo ni wazi yatatokea kwani katiba itakuja kubadilishwa one time na hapo viongozi wa nyuma wataletwa mbele ya sheria..na kwasababu watakuwa wamejijengea ngome..mpambano utakuwa mkubwa na hala hala.Mungu atuepushe na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe!Mh rais ajue kuwa yuko kwenye wakati ambao naweza kusema ni "Defining moment" in our country's history!
 
Na ndio maana nikasema kuwa Mh rais yuko kwenye wakati mgumu kwasababu ili kuumaliza ufisadi..ni lazima awaombe watanzania msamaha na atumie madaraka aliyonayo kikatiba hivi sasa kwa kuwa upande wa wananchi na kuwawajibisha mafisadi wote!Mifano halisi ipo kwenye vitabu vitakatifu kwa mambo ambayo yaliwakumba viongozi wa enzi hizo ambao walikuwa ni wafalme!Kuna waliokuwa wakikabiliwa na wakati mgumu lakini hawakuthubutu kuwatosa wananchi!Walikubali kujishusha na kuvaa magunia kwa masikitiko huku wakilia kisiri siri kwa uchungu wa maamuzi hayo!Hii issue ya ufisadi ndio jinsi ilivyokaa!Asipofanya something this time then ajue kuwa atakuwa ameifumbia macho opportunity kubwa ya kuweka historia madhubuti na kuinusuru nchi yetu na machafuko mabaya ambayo ni wazi yatatokea kwani katiba itakuja kubadilishwa one time na hapo viongozi wa nyuma wataletwa mbele ya sheria..na kwasababu watakuwa wamejijengea ngome..mpambano utakuwa mkubwa na hala hala.Mungu atuepushe na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe!Mh rais ajue kuwa yuko kwenye wakati ambao naweza kusema ni "Defining moment" in our country's history!

Pamoja na kuomba msamaha kama na yeye ana hako kaugonjwa ( kuna kila dalili) je ataweza kukaacha. Je kama ana yeye ana akaunti kibao nje ataweza kuwarudishia wananchi hela zao? Kuomba msamaha ni jambo moja kujirudi ni lingine. Sie yetu macho.
 
Mimi naamini kabisa kama Mh.Kikwete ni msafi tena msafi wa uhakika.kama kuna wachafu basi hao walidandia basi la Mh.Kikwete na kutaka kumsaidia wakiweka matumaini kuwa atawapatia lifti ,mara nyingi wanaosaidia kusukuma gari nao hutaka msaada wa kufikishwa wendapo.
Kwa ufupi Mh.Kikwete hakuwa mwizi wa fadhila aliwapa msaada na kuwafikisha waendapo ,kama walikula dawa ili wapate nguvu za kumsaidia hilo litakuwa tatizo lao ,Mh.Kikwete hakutaka kujua jamaa walipata wapi nguvu za kulisukuma gurudumu lake la kupanda kilima cha Uraisi kwa kishindo ,yeye aliona tu kuwa gari limeshika kasi na kuondoka hivyo aliowapakia aliwasaidia kwa kuwalipa shukurani.Sasa kusema Kikwete alishinda kwa sababu wasukumaji wake walikula vidonge vya kuongezea nguvu ili waweze kulisukuma gurudumu na wao wapatiwe lifti ,hilo litawagusa hao waliotumia vidonge si kwa msukumwaji.Kawafikisha safari yao ,sasa kama waliiba fedha za kupata nguvu au hapo walipofikishwa ndipo walipokusudia kuiba ,that will be another case ,fagio la chuma likipitishwa inavyotakiwa Mh.Kikwete asiukumbuke ule wema aliotendewa kwani alikwisha walipa wema ,atimize majukumu ya Uraisi na kuangalia mbele awache sheria ichukue mkondo wake huku yeye akiwa msimamizi na kuwaeleza wasaidizi waliomsaidia kusukuma gurudumu kuwa kama angelijua ni majambazi asingeliwafikisha safari yao.
 
jmushi,
pamoja na maelezo yako mazuri.....kumbuka pia kuwa kwenye keyboard yako kuna keys zifuatazo

1.Enter - hii itakusaidia kutengeneza paragraph
2.Space bar -

hii itasaidia maandishi yako kusomeka vizuri.......ni maoni tu
 
jmushi,
pamoja na maelezo yako mazuri.....kumbuka pia kuwa kwenye keyboard yako kuna keys zifuatazo

1.Enter - hii itakusaidia kutengeneza paragraph
2.Space bar -

hii itasaidia maandishi yako kusomeka vizuri.......ni maoni tu

mkuu unaua...

ungemtumia pm
 
jmushi,
pamoja na maelezo yako mazuri.....kumbuka pia kuwa kwenye keyboard yako kuna keys zifuatazo

1.Enter - hii itakusaidia kutengeneza paragraph
2.Space bar -

hii itasaidia maandishi yako kusomeka vizuri.......ni maoni tu
Nimekwisha ifanyia marekebisho!Ila pia nina imani hata wakati wa kuongea kwenyewe tunakubali "ulimi hauna mfupa"..sembuse kutype?Hata hivyo nashukuru na nitajitahidi ku"edit" before posting kwani hata Mwanakijiji alishawahi kunipa ushauri huo!
 
Back
Top Bottom