The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Tafiti then Jadili,

Mshikaji umenisikisha sana kwa mchango wako na pengine haitakuwa vizuri kukulaumu kwa sababu umesimama upande wako -CCM.

Kibaya ni kwamba hoja nzima umeifanya kuwa rahisi na jambo la utani vile kwani huyu mke tuliyempata na uzuri wake wote - Mume ni MMOJA. kwa hiyo mwenye furaha na mke huyu ni mume (CCM) sio watoto (wananchi), wakwe (Uingereza) na ndugu na jamaa wote wa pande mbili. Yet, kwa ujeuri wenu JK kweli anasimama na kutuambia kuwa CCM ndiye mume kwa hiyo anaweza kuamua anachotaka hata kama mke huyu hatufai!..

Inasikitisha zaidi kuona kuwa wewe umefurahia sana kupewa mikopo zaidi ambayo interest yake huifahamu hata kidogo zaidi ya kutazama figures tulizopata.
Jadili, ni 12/m zimeyeyuka toka ktk mali ya wanao ambayo walirithishwa na kibaya zaidi huyu baba Mkapa alifuja mali ya wanawe kwa kuongeza mke!..
Brother, jaribu kulitazama swala zima kwa faida ya watoto na sio CCM kwa sababu tu wewe ni mpambe unayebebwa kila jioni kwenda kutumia club!..
Chakula chetu usiku na mchana ni mzungu (Ugali) miaka nenda rudi kiafya maisha yetu dhaifu kisha unafikiri kweli hata hiyo mikopo ikijenga shule watoto wataweza kusoma wakiwa hawapati huduma bora!
Think, about it my brother!

Mwanasiasa,
Nakubaliana sana na signature yako bob - "It is not part of CCM political culture to listen to voices other than its own"
 
Hivi kuna haja gani ya kutumia Middlemen na serikali ina wafanyakazi wengi tu kwenye Balozi zetu!Hivi hamuoni kuna kila harufu ya Rushwa ktk suala zima la ununuzi wa Radar?Mimi nawashangaa sana hawa akina TTJ ambao kwa nguvu zote wanashabikia UOZO wa hawa waungwana wanaopitisha mambo ambayo si matakwa ya wengi!.Leo hii tuna vijana kibao ambao wamefaulu mitihani yao,lakini wanashindwa kuendelea na Elimu yao kwa sababu tu hatuna shule (madarasa).Hizi milioni za dola zinazonunua radar zingeelekezwa kwenye sekta ya Elimu au Afya ingekuwa kwa faida ya Umma zaidi kuliko kununua radar ambayo haina faida kwa wengi!.
Nashangaa hapa TTJ anaposema kuwa watakaohojiwa nyumbani ni wale akina Sailesh Vithlan na Somaiya tu,hao ni kweli kwamba wamehusika,lakini naamini kabisa kwamba wakisema ukweli wapi zimekwenda hizo $12m,Tutakuwa wadogo mno kwenye Forum hii,ni aibu tupu! kwani kuna viongozi wengi wamepata mgao wao!.
Kwa mawazo yangu nafikiri yeyote anayeshiriki/pokea/shabikia rushwa nae anapaswa kuadhibiwa kama mla Rushwa,kama ni hivyo wale wote waliotajwa kwenye Ripoti ya Prof.Baregu wanapaswa kuwajibika na kashfa yote ya BAE..Enough is Enough Jamani,kikwapi kitambaa jeusi tuwaning'inize watu! TJJ angalia kwa sababu kushabikia Rushwa pia ni kosa.
 
We Tafiti,
Usituletee mifano isiyo na akili ambayo kiongozi wako aliitumia kwa kuwa ni mzinzi. Watanzania walimkataa huyo unayemwita mke,lakini Chama cha majambazi kwa kuhitaji pesa za kampeni ,matumbo yao na kununulia vidonge vya kuongezea muda, wakalazimisha.Wahajali kwa kuwa wanajua soon they will be dying.Unajua wazi kuwa Radar hiyo haikununuliwa ku-serve interest za watanzania ila ku-serve mtandao wa Majambazi.Tatizo lako njaa, na ujinga ndo viinakusumbua.Hatupendi wajinga wanaotaka kupotosha ukweli.Issue serious kama hizi usituletee jokes.Watu wanakufaa mahospitalini kwa kukosa huduma shauri ya issue hizi.Lack of integrityand priotization.
 
Huyu TTJ itabidi akasomee namna ya kutetea wakubwa zake. Haishangazi serikali yetu inafanya maamuzi inayoyafanya, kama watu wenyewe ndio hawa! Yaani haoni tatizo katika manunuzi ya radar mpaka dakakika, na yeye anaishi UK na anaona jinsi hili swala linavyoimbisha serikali ya Tony Blair. Kwa nini usikae kimya tu ndugu yangu katika jambo hili. Huo mfano wa mke wa boss wako unafaa katika mikutano ya CCM tu na wala sio katika forum hii.
 
Uozo unaoendekezwa katika nafasi za kibalozi ndio unachangia matatizo ambayo tutaendelea kuwa nayo. Alikuwa busy wakati rais yupo hapa sasa ameondoka ndio muda mwingi atautumia kuweka propaganda hapa kutetea ujinga badala ya kurekebisha makosa waliyofanya.

Hivi anafikiri sisi watanzania kutokuweza kumhoji rais tumesahau? Pamoja na yeye kuwa hapa hajajifunza mbinu muhimu za kuweza kumsaidia mbongo kuondokana na umasikini, wala hana aibu. Umepewa cheo hiki ili ujifunze wenzetu wanafanya nini ili kujiendeleza na kutumia fulsa hii kuwasaidia wabongo lakini inaonekana unaendeleza ubaguzi wa kichama, yaani sisi wengine ambao hatuna chama basi sio watanzania?

Hata hiyo ya tarehe 17/02/2007 kama mambo yenyewe haya unafikiri watanzania watakuja kwa tabia hii? Nilishangaa sana pale mkutanoni eti watu walidiriki hata kusema JK ana mvuto? Huu haukuwa mvuto tulitaka kum-engage rais katika masuala muhimu ya kulisaidia taifa, sisi ndio tunafahamu matatizo kuliko wale wanaokaa ubalozini - nani anawafahamu waingereza zaidi kati ya TTJ na wale ambao wanafanyakazi nao? nafikiri TTJ na kundi lako mna kazi kubwa lakini wote tulio hapa hatukufika hapa kwa pesa ya walipa kodi inabidi mjiulize?
 
Mzee Mwanakijiji

Bravo kwa mahojiano uliyoweka, tunasubiri ya mwandishi wa The Guardian TUTAFIKA TU.
 
Kwa taarifa tu TTJ kumpongeza JK naelewa ni sababu wote wana akili za kizinzi na wizi pia . Huyu jamaa kule US aliondoka na skalndali la kuwalala wake za marfiki zake na uongo yaani umbeya . Hata leo ukija dar ukauliza juu ya jamaa watakwambi ni mkabila , mroho , mzinzi na mpenzi wa madaraka . Muulezeni kwa nini analala kila siku kwa madai ya kuumwa mgongo na kapata nguvu baada ya kusikia mkubwa wake anakuja UK ? Sisi tunamjua ni mtu wa hovyo na lazima atetee ujinga . Anaseka JK anapenswa zaidi sisi tuna angalia kupendwa ama kushabikiwa ? Nchi inakufa analewa mawazi ya kijinga . Hawa ndiyo wanao tumiwa kuja na maneno ya kijinga nyakati za kampeni kule TZ na wajinga wenzao wanaishia ushabiki baadaye wanakufa yeye anarudi UK kula pesa za wavuja jasho .

Muulizeni kaacha uzinzi lini hadi asiweze kushabikia mzinzi mwenziwe .
 
Nyie wanasiasa mnatuchanganya tu wengine. Kichwa cha habari kinasema ndege ya rais ndani mnaongelea radar system hivi wengine tuelewe mnaongelea nini. Nimefuatilia hizo post nimeshindwa kujua hizo hela zilizotolewa ni mkopo au msaada? Na hizo 12bil ni rushwa au commission? Kuna wengine wanasema hizo 12bil zingeingizwa kwenye afya au elimu hebu tuelewesheni wengine. HOW? Mnataka kusema hizo 12bil badala ya hao vigogo ambao hamwataji kuchukua hizo hela wangeziingiza kwenye afya au elimu. Nitakuwa na matatizo makubwa kama hizi hela zilikuwa mikopo kama ni misaada basi nitawachia ninyi wanasiasa mpambane. Naomba mtu mmoja alieleweshe vizuri na mimi niweze kutoa mawazo yangu.
Huyo TTJ nadhani anaongea vitu ambavyo hata yeye mwenyewe haviamini.
 
Dua
Maelezo ya Mwanakijiji hayajajibu maswali yangu. Kwa maelezo ya wanabodi wengi inaonekana kama hizo 12bil inabidi tuzilipe toka mifukoni mwetu ndiyo maana nataka kujua hizo hela zote ni mkopo au msaada. Nilivyoelewa mimi hiyo 12bil siyo rebate ambayo ilitakiwa irudi serikalini baada ya kununua hiyo rada. Hiyo ni commisssion aka rushwa kama mlivyoibatiza. Hizi hela za ununuzi zilitolewa na serikali ya uingereza sasa nataka kujua ni kwa makubaliano gani, again kama ni mkopo hapo lazima tushikane mashati na hapo inabidi tuwarudishie ka rada kao kama kweli hatuihitaji na kuwaambia we are not going to pay. Whats a big deal? Hapo sasa watapambana na hao waliwapa 12bil. Hayo majina yaliyoandikwa ni watu ambao kama kuna mgao basi wao ndiyo watu wakwanza kuchukua lakini bado ninajiuliza kwa nini hizo hela achukue Mkapa siyo Tony ambaye ndiye aliyeidhinisha kutowelewa kwa hizo hela licha ya kupingwa. Kuna maswali mengi ya kujiuliza ila at the end of the day itabaki siasa hii kampuni itakuwa cleared na itaendelea na biashara yao ya silaha na huku nyumbani kila mtu atakuwa cleared. Nadhani issue ya Mahalu is the same type of situation kulikuwa na two payments na ikaja kuwa clear why na kama mtu ameiba hakuna ushahidi na kesi hakuna.
 
Sam,

nadhani wewe ndio umechanganya vitu hapa.
Taarifa iliyotolewa na Mwakijiji inasema hivi:-
1. tanzania ilinunua rada kwa bei ya shilingi billioni 40.
2. Kisha huyo dalali alipewa millioni 500 kama commission ya udalali wake toka hao BAE. Hii sio rushwa inafahamika kanlakini nayo pia ikibidi kui-question -it's well and good.
3. Baada ya yote haya Huyu dalali alipewa fedha zaidi billioni 12 kwenye account yake ya Uswiss toka kampuni hiyo ya BAE.
Sasa kwa wale wanaofahamu deal za Kibongo hii rada bei yake ilikuwa chini kabisa ya billioni 40 na wahusika walipokwenda waliambiwa mathlan bei yake ni billioni 26. Sasa mhusika yaani mhindi akawafuata wale wanaotakiwa kupitisha hii kitu (viongozi). Wao wakamwabia safi sana ila kinachotakiwa ni huyu dalali kuwasiliana na hao BAE ili wabadilishe bei yake kimakaratasi ionekane billioni 40. Wao BAE watapewa chao yaani 26/b, na za wafanyakazi wa deal la BAE Uingereza chao ni billioni 1.5, wahusika wa Bongo (viongozi) watakatiwa billioni 12. Huyu mdosi akadai chake ni millioni 500.. hapo hesabu nzima ni 40/b.
Tunachohoji wananchi ni kuwa tumeibiwa, hatufahamu ni kiasi gani hasa lakini kile kinachofahamika hadi sasa ni hizo billioni 12 zilizokwenda ktk account ya huyu dalali nje ya bei halali ya rada. Tunafahamu kabisa kuwa hizo billioni 12 zimeingia ktk mifuko ya baadhi viongozi nchini na walimtumia huyu dalali kukosha mikono na majina yao kutumika moja kwa moja. Deal lilipoitikia inasemekana walikwenda Uswiss kuhakikisha mabadilishano yanafanyika na wote hawa walifungua account zao huko ama nchi zenye sheria rahisi isiyouliza kiini cha upatikanaji wa fedha hizo.
Sam huo ni mfano mdogo wa mgao kila Mtanzania anafahamu kuwa huchezwa! Sii jambo geni isipokuwa kama alivyosema Kenyatta.. Ukitaka kuiba iba lakini usije kamatwa!
Na kibaya zaidi ni huyu huyu dalali aliyehusika tena na ununuzi wa ndege ya rais ambayo pia hatufahamu deal lilikwenda vipi... mikono ni ile ile!...
 
Hiyo ya ndege ya rais imeongezwa kwa sababu aliyekuwa middleman is the same person ( Mr Vithlani's)

Bei ya rada ilikuwa 40 billion na ya ndege ya rais 40 billion kwa wakati tofauti tofauti. Commission ya rada ilikuwa 12 billion Tsh. alilipwa huyo mhindi kwenye Swiss account ambayo ni sawa na 30% sio ile ya kawaida ya 1%.

Hiyo ya kuingizwa hizo pesa kwenye afya ni kwamba TZ walikuwa hawahitaji hiyo rada ya 40million ambayo ni ya kijeshi. The civilian radar was far more cheaper kwa hiyo pesa zingine zingetumika kwa mambo mengine. (this argument is not part of commission.)

pesa sio msaada wabongo mtalipa.

BAE system ni kampuni ya Uk but private walikuwa na mikataba tofauti na TZ na middleman ambaye anashughulikia vilevile magari yaliyouzwa kwa jeshi la TZ. Tembelea hapa kwa mwanakijiji usikilize taarifa aliyoongelea kuhusu rada http://mwanakijiji.podomatic.com/

Hizo pesa Blair hawezi kuchukua kwa sababu hapa mambo magumu ni huko nyumbani ambako kamisheni ilikuwa kubwa mno ie 30%. Where is our priority?

Na huyo middleman anakubali kwamba pesa alilipa kwa watu wengine huku majuu ambao hakuwataja. ( theory ni hao wenye majina yaliyotajwa na MKJJ.)

Nenda kwenye link hii ya BBC: http://news.bbc.co.uk/1/hi/world/africa/6266535.stm

Ukifika hapo fuatilia links za BAE system Probe; Background and analysis utapata picha zaidi.

Ununuzi huu ulipigiwa kelele kwenye House of Commons (Bunge) kwa nini wafute madeni wakati tunanunua rada ambayo siyo necessary kwa wakati ule, lakini kwa sababu watu walikuwa wanategemea hiyo commission ya 30% ndio ikabidi inunuliwe tu.
 
Dua,
Samahani kidogo.. nadhani sasa hata mimi unaniweka nje hapa unaposema:-
Bei ya rada ilikuwa 40 billion na ya ndege ya rais 40 billion kwa wakati tofauti tofauti. Commission ya rada ilikuwa 12 billion Tsh. alilipwa huyo mhindi kwenye Swiss account ambayo ni sawa na 30% sio ile ya kawaida ya 1%.

Ukisema commission ilikuwa asilimia 30 hapa mshikaji tunajifunga wenyewe! kwa sababu kama ukisoma taarifa vizuri inasema kuwa huyu Vithlan alisema kuwa LICHA ya kulipwa malipo ya kawaida ya udalali wake (Commission) ya shilingi millioni 500. Alipokea pia shilingi billioni 12 ktk account yake Uswiss. Kwa hiyo 12/b sio commission, yeye Vithlan kasema alipokea 1% ya Udalali - billioni 12 ni kuficha uhusiano wa malipo.
 
Nilisubiri kwa hamu sana hiii issue na man=jina ya Mwanakijiji lakini sioni kitu

Kama mwandishi nilitegemea SMOKING GUN lakini hakuna kitu hapa

Majina ni yale yale BM,JK,CHENGE Aand so on

nilifikiri tutaletewa majina ya hao maofisa walionegotiate hiii issue na waliofungua akaunti na ishu nzima kwa ujumla

Jmani ndio kwanza nimeingia lakini nitarudi punde baada ya kupata rizki kuiweka my two cents kuhusu hii issue
 
hiyo 12bil kama tumeibiwa nataka kujua HOW? Utaibiwa vipi hela siyo yako, hiyo hela ya Uingereza na sisi tumeibiwa vipi. Kitu pekee ambacho kinaweza kufanya hiyo hela ikawa yetu ni kama huo ulikuwa ni mkopo na tunatakiwa kuilipa na kama ni mkopo tuelezeni huo mkopo ulikuwa na mkataba gani. Nimetokea kuwachukia sana wanasiasa kwa maana vichwani mwao ni zero. Hao hao waingereza wametuongezea hela kwenye bajeti zaidi ya hiyo 40bil kwa nini tusitoe hizo hela na kuwalipa sasa na kukwepa interest tutakuwa tumewalipa kwa hela yao wenyewe badala ya kukaa kupigishana hapa kelele kwa hela ambayo siyo yetu. Ingekuwa hela ya kahawa si tungechinjana wenyewe kwa wenyewe. Hivi leo hii wao waingereza wakisema kati ya watu walaiochukua hela mmoja wapo ni Mkapa sisi watanzania tutafanya nini? Mtamuondoa madarakani? NO. Mtamshtaki? Kila mtu atawashangaa kwa kumshataki mtu kwa hela ambayo siyo yenu. Hii issue nzima ikija kuibuka ni Tony ndiye yuko mashakani.
Nadhani tubadilishe jinsi ya kuchangia kwenye hii mada labda nimpe shule kidogo TTJ, kama anatetea hii issue atupe data ni kivipi tunafaidika na hii rada. Kabla ya rada tulikuwa tunapata hasara gani na baada ya rada tunapata faida gani.
Ukienda kuomba hela lazima uwe na sababu kama ingewezekana kuomba hizo hela kwa ajiri ya afya au elimu kwa nini wasingefanya hivyo? Au tulivyoomba hela za afya na elimu je tumenyimwa au tumepewa nyingi zaidi ya hizo za rada.
Hii issue ya 12bil ni debatable. Kwa kuwa walikubali kuwa wamechukua sasa ilikuwa ni rushwa au commission? Je viongozi wa serikali wanaruhusiwa kuchukua commission aka rushwa kutokana na miradi ya serikali? Na sheria zetu zinasemaje kuhusu hili jambo. DrWho mwanasheria wetu unasemaje kuhusu hili. Kama ikitokea kulikuwa na rushwa kwenye issue nzima tunaweza kukataa kuilipa let just close our eyes JK hayumo kama yumo we have to pay.
Wenye data tupeni, ni kiasi gani tunatakiwa kulipa kutokana na dili nzima.
 
Mkandara

Fraud Office inquiry into BAE Tanzania deal


· Commission of 29% may have been paid, police say
· Blair forced African arms deal past Clare Short

David Leigh
Monday November 13, 2006
The Guardian


BAE Systems is being investigated for suspected corruption over an arms deal with the heavily indebted African country of Tanzania, in which commissions of more than 29% may have been paid, Westminster sources confirmed last night.
Of all the company's international deals being investigated by the Serious Fraud Office (SFO), the Tanzanian deal is the most politically sensitive, although it was relatively small in cash terms. The £28m military air traffic control sale was pushed through the cabinet in 2001 by Tony Blair against the heated opposition of then-development minister Clare Short, who subsequently alleged corruption. Both the prime minister and BAE reassured critics at the time that the sale was above board.

Tanzania, one of the poorest countries in Africa, had no need for an expensive military system to handle its civilian air traffic, and was at the time asking for its debts to be cancelled.
Ms Short has confirmed that she was approached by the SFO some weeks ago, who told her it was investigating. It was reported last night that SFO investigators had also approached the Liberal-Democrat MP Norman Lamb, who has compiled a dossier on the affair.

Westminster sources say that the SFO and the Ministry of Defence police, who are conducting a joint investigation into BAE's deals around the world, believe that millions of pounds were paid into Swiss banks to cement the sale. One said: "I was told the SFO would not be surprised if commissions exceeded 29%". In previous cases, the SFO has identified agents close to the party in power in countries that have bought BAE weapons.

Ms Short's disenchantment with the government's invasion of Iraq led her to resign from the cabinet. Most recently, she has resigned the Labour whip, and is expected to leave parliament at the next election.

Last month, the SFO signalled the widening of its investigations to Africa when it raided the Windsor premises in Berkshire of John Bredenkamp, a Zimbabwe-based tycoon who acted as a agent for BAE in the sale by the Labour government of Hawk and Gripen warplanes worth £1.6bn to the ANC government in South Africa. He is also believed to have acted as a BAE agent in other African countries. The SFO investigations started three years ago following disclosures in the Guardian of corruption allegations against BAE, and began by inquiring into alleged "slush fund" payments to Saudi Arabia. Inquiries moved to Chile, Romania, South Africa and now Tanzania.

Last night the SFO said "We are looking at suspected corrupt acts ... For operational reasons we cannot assist in providing confidential information."

BAE declined to comment, other than to say: "We fully believe BAE Systems has done nothing wrong."





Special report
The arms trade

Useful links
Campaign Against Arms Trade
Control Arms campaign site
Stockholm International Peace Research Institute
Federation of American Scientists
Carnegie Endowment for International Peace
saferworld.org.uk
Wisconsin Project
Foreign Policy magazine


Hiyo ndio story ilitoka wakati ule lakini, anavyosema huyu sasa ndio unavyosema mimi niliweka estimate as 30%. SASA NDIO UKWELI WA HUYO MIDDLEMAN
The link is here: http://www.guardian.co.uk/armstrade/...946486,00.html
 
Sam

Ina maana viongozi watumie nafasi zao kujitajirisha kwa rushwa n.k.?

Sasa Kama Richmondulian anatoa 60 million kwenye mchango ni sawa tu eh?

Kwa nini basi UK na nchi nyingine wasiwape hizo pesa bila kuihusisha serikali kama wanahitaji kufanya hivyo?
 
Sam,
Sasa mwenzangu hata sikuelewi kabisa?... Kutaibiwa vipi? kwani hiyo rada imepatikana bure? hela sii yetu kivipi maanake hata ukiwa mkopo bado mwenye deni ni sisi Tanzania. Kisha kama umesikia hotuba ya JK kasema tumetoa mahali kumchukua mke.. sasa hapa unauliza mahali gani? na tumeibiwa vipi wakati bei zimetolewa wazi.
What's UP?
 
Sam,
Sasa mwenzangu hata sikuelewi kabisa?... Kutaibiwa vipi? kwani hiyo rada imepatikana bure? hela sii yetu kivipi maanake hata ukiwa mkopo bado mwenye deni ni sisi Tanzania. Kisha kama umesikia hotuba ya JK kasema tumetoa mahali kumchukua mke.. sasa hapa unauliza mahali gani? na tumeibiwa vipi wakati bei zimetolewa wazi.
What's UP?
Mkandara
Sikutaka kuendelea kuchangia hii hoja ila naona unaandika mambo ambayo sikusema. Nimesea kitu pekee ambacho kinaweza kufanya hiyo hela kuwa yetu ni kama hiyo hela imetolewa kwa mkopo sasa sijui wewe unaongea nini. Nadhani mfano wa mahali ni mzuri. Mahali inaweza kuwa hela uliyoitoa mfukoni mwako, au washkaji wamekuchangia au umekopa. Ninapouliza tumeibiwa kivipi siyo kwamba nataka kubishana ila nataka kueleweshwa. IPTL ni rahisi kusema tumeibiwa kwa maana tunalipia umeme ambao hatutumii. Watu wanavyochangia hii mada utadhani hela imetoka hazina kama hela ya Richmond. Unajua kuna kitu nashindwa kuelewa kama ni mkopo wenye riba ni kivipi serikali ya uingereza inavalia njuga kitu ambacho watapata faida? Hizi ni siasa tu za kampeni za uchaguzi kule UK. Ni lini uingereza imekuwa na uchungu na umaskini wetu? Na hii itawanyima watu kura.
 
@Mwanakijiji

nimefurahi kuona kuwa umetimiza ahadi yako ya kuwa utarudi humu siku ya AL-HAMIS kuja kuweka mambo sawa na nafurahi kwa hili lakini pia ningependa kusema kuwa pamoja na kukubaliana nawe lakini nadhani kuba baadhi ya hoja ambazo itabidi nikujibu
HOJA NUMBER1

Hii nakubaliana nayo na sishangai kuwa haya yanatokea kwani kuna mambo mengi tuu ambayo wanasiasa na maofisa wa serikali walifanya maamuzi bila kufikiria maslahi ya Taifa au wananchi hivyo uko right katika hili...lakini sio sababu ya kurudia kosa

HOJA NUMBER 2

Serikali ya jamhuri ya Muungano ya Tanzania kuita wachunguzi toka nje kitakuwa ni cha kushangaza kwani tunavyo vyombo vya kufanya kazi hiyo na kama vikipewa nafasi na uhuru huo vitafanya kazi yake sasa kuwaita Scotland Yard kuchunguza rushwa kwetu n aibu na inaonyesha jinsi gani ambavyo hatujiamini na hiii pia itazua kitu kinaitwa CONFLICT OF INTEREST baina ya yetu na Serikali ya UK.

Walio husika ni wahindi wenye uraia wa Uingereza na hakuna sheria inayowakataza kufungua off shore acounts be it in Swiss au Dominica republic hivyo itakuwa tunatafuta mchawi na kuwalaumu hao wahindi bure wakati wao wamekuja kutafuta dili na wakalipata sasahizi hoja zingine zinakuwa tu kuwa wanaojiita watoto wa mjini walikuwa wapi mpaka wakapigwa bao na wadosi?

Umezungumzia kuwa wahusika walikuwa akina nani ambao walishawishi serikali kununua hiyo RADA na walinufaika vipi? of course washawishi wanatoka sehemu mbali mbali Wizara ya ULINZI,wizara ya MIPANGO, wizara ya MAWASIALIANO, wizara ya FEDHA, IDARA YA ANGA a hawa matokeo yake wanapleka proposals zao kwa hao waheshimiwa then hapo ndipo wataamua kama pesa zipo basi wago ahead sasa kama unataka kujua hii inafanyika vipi then kuna umuhimu ukaelewa kwa nini wengine tunapigania TRANSARENCY KATIKA TENDA kwani bila hivyo ni ngumu hata kujua kuwa akina nani walikuwa shortlisted na kama BAE SYSTEMS walipewa je walipewa baada ya kuwashinda akina nani katika bidding? Je bwana MKJJ hili ulilinvestigate? na kama ungejaribu kulivutia muda then ungejua kwa nini waliamua kununua rada ambayo haitoshi thuluthi moja ya nchi kama ulivyosema na maybe ungeelewa kuwa cost ya kuimaintain hiyo RADA katika hiyo AFTER SALES SERVICE cost angezichukua nani na kwa estimates zipi?


HOJA C


Bwana MKJJ umtoa hoja kuwa serikali ya UK imonitor akaunti za Bwana Vilathni na Somaiya ili kujua kama kuna malipo yaliyofanyika kwa mtu yeyote mwingine na hususan afisa au kiongozi wa serikali ya Tanzania.

Sasa kwanza lazima uelewe jinsi gani mambo haya yalivyo kuwa complicated na hii inachangiwa zaidi ya mfumo wa banking huku UK na Europe kwa ujumla na hata kama kutakuwa na payments zimeonekana zilifanyika kisheria hao wahindi hawawezi kueleza mengi kwani kwanza hao Barclays bank wanaendeshwa na pesa nyingi za HARAM toka katika rogue states kama MYAMAR au BURMA,IRAN,ZIMBABWE na zinginezo na kwa taarifa tu ni kuwa hili hata ahao ma financial regulators hapa UK (FSA) hawezi kuligusa kwani punde wakiaanza tu basi ujue kuwa unaweza kuangusha serikali nzima ya UK ambayo of course imejaa wala rushwa kuanzia house of Lords mpaka huko Whitehall na kama huamini basi tazama kesi ya CASH FOR PEERAGE

pilikuna ma lawyer wako stand bay kuwalinda hawa jamaa ambao kusema ukweli ni kuwa hakuna kitu kitakachopatikana kwani pesa zitakuwa zimeshaingizwa either kwenye TRUST au STOCK MARKET AU KWENYE HEDGE FUNDS ambayo imewatajirisha jamaa wengi huko THE CITY na ndio maana WEALTH MANAGEMENT corporations kama GOLDMAN SACHS,MERRYLL LYNCH,CREDIT SUISSE FIRST BOSTON,BARCLAYS GLOBAL INVESTORS,LEGG MASON, JP MORGAN ASSET MANAGEMENT na kadhalika ...hao ni wajanja wa kuzificha pesa na ndio wanao lipia campaigns za akina BLAIR na LABOUR.....hivyo hiyo haiwezi peke yake kujenga hoja za kuwa akaunti ichunguzwe kaama wakithubutu kuanza hiyo witch hunt basi waingereza yatawakuta yaliyowakuta waamerika baada ya kuanza kunusa akaunti za WASAUDI matokeo yake waarabu waliamua kufanya Capital flight from USA to UK and CHINA na si kwamba wazungu wahawalijui hilo..wanalijua sana na ndio hiyo hiyo pesa ambazo zinaendesha uchumi wa nchi hizi

Vile vile usisahau kuwa serikali ya Tanzania hawawezi kuinchunguza BAE SYSTEM kwani kazi hiyo wanaifanya FSO ambao kama wakiwa na la zaidi then wanaweza kuwa SUMMON watuhumiwa kujibu mashitaka. Hilo la kutaka kuchunguza akaunti za watu mjomba nalo litakuwa ngumu kwani huku ulaya kuna suala zima la CONFIDENTIALITY na BANKING CODE na hii ndio mpaka leo waNIGERIA wameshindwa kupata pesa zote alizoziiba SANI ABACHA na waSWISI waliamua kuwapa hao WANIGERIA DOLA BILIONI MOJA kati ya dola zaidi ya bilioni 4 aliziiiba

Kwa hiyo ndugu yangu hiyo ni uphill task na itacheleweshwa na LAWYERS ambao wao they make a living out of kuchelesha mambo kama haya na sasa hebu niambie utaanza wapi na utamalizia wapi?Mfano mdogo ni kuwa Kampuni kubwa za law firm kama SKADDEN,ARPS,SLATEMEAGHER& LOM LLP & ASSOCIATES au CLIFFORD CHANCE unafikiri kinachowaaweka mjini ni kucheza na sheria na wanaweza kuzungusha hao mpaka kiama na ndio hao washaui wa hao ma middle men ambao unataka wahojiwe kwa hiyo huo ni mwamba

umewataja OBVIOUS viongozi lakini vile vile naweza kukujibu maswali yako kama ifuatavyo:


1.Rais Benjamin William Mkapa ambaye chini ya uongozi wake rada hii ilinunuliwa.

Lakini huoni kama kumshitaki Mkapa kama ni kutafuta scapegoat? kwani ukimpandisha BM kizimbani it means that TONI BLAIR also has to be there with BM but like the other loans for honours(or CHASH FOR PEERAGES) 'scandal', one major fly in the ointment; Blair was/is a lawyer. It's unlikely he'll ever be caught bang to rights on this kind of thing. And even so, he has a rather more serious crime to answer for, which is also unlikely ever to come to charges. it's not his sticky paws that are the issue, it's his paw print. Is he really directly culpable in this case, as he was a lawyer I'd be surprised if he didn't leave himself wiggle room which is opposite to our dear Mheshimiwa BENJAMIN WILLIAM MKPA who is a JOURNALIST by profession unless sijui kitokee nini but its a win win situation for BLAIR but not for MKAPA




2.Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa wakati huo na Rais wa sasa Bw. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alitetea ununuzi wa rada hiyo. Na hata jana ametetea.


Hoja hii inajibiwa kuwa JK naye kwa taarfa yako alikuwa anafuata tu instructions toka kwa wakubwa zake akama ambavyo CLARE SHORT baadae ilibdi akubali matokeo na majibu ya JK juzi ni sawa kwa sababu hao jamaa wa FSO washampa njia nzuri ya kutokea kwa kusema kuwa uchunguzi bado unaendelea na kwa kweli angeropoka basi kama kuna kesi ya kujibu BAE SYSTEMS wangedai kuwa JK karopoka hivyo hawawezi kupata FAIR TRIAL...and this includes HAO WAHINDI akina SOMAIYA


3.Mwanasheria Mkuu wa Wakati huo Bw. Andrew John Chenge ambaye ni Waziri wa Miundo Mbinu wa sasa ambaye ofisi yake ilisimamia mkataba kati ya serikali na Bw. Saileth Vithlani


Hoja hii haikataliwi lakini ukumbuke kuwa naye anapelekewa recomendation toka wizara ya FEDHA na MIPANGO ambao kuishi kwao kunatokana na WORLD BANK..NA KAMA KWELI BWANA MWANA KIJIJI UNGETAKA KUJUA ZAIDI BASI NADHANI investigation yako ingelenga huko WORLD BANK ..ambao wanaofisi DAR na hapo WASHINGTON...lakini hili nalo waandishi wetu huko Dar wangemuuliza huyo rais wa WORLD BANK bwana Paul Wolfowitz ...amabye anahamu sana wanafunzi tanzania wawe na first class eductaion




and maybe we should have gone back to SQUARE 1

And the OBVIOUS QUESTIONS you should have asked is WHERE DID WE GET THE MONEY TO BUY THIS EQUIPMENT?



ASSUMPTIONS:


Now who are the donors/contributors of the aid money? Is it govts in the west or is it charitable organisations? If the latter there some political bargain/wrangling could result in Blair escaping personally unscathed. If the latter, they are duty-bound and presumably required by their own charter/constitution to persue the money or in other words kuchelewesha haki na hapo tena Ma-lawyer wataingia kuanza kuidadua constitution ambayo nadhani unaelewa kuwa iko pungufu

Now kwa upande wa BAE SYSTEMS...I see that it's small fry for them so it won't be the end of the world for them if they had to cough up the dough. But then they are duty-bound to their shareholders that they contest any claims of that nature.....UPO HAPO MWANA KIJIJI?

fURTHERMORE, The World Bank is involved, apparently. Isn't Wolfowitz very convenient its president these days? Now that's an old friend of Bush/Blair....




4.Prof. Mark Mwandosya aliyekuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi ambaye sasa ni Waziri wa Mazingira.

Huyu labda hii kwake isngekuwa na nguvu zaidi kwani naye anapata directions toka juu..unless unataka kumuuliza kuhusu hiyo project yake ya uwanja mpya wa ndege


5.Maafisa (wanasheria na washauri) wa Wizara husika ambao walihusika na mikataba hiyo.


SASA HAPA MWANAKIJIJI UMENENA lakini kama na yeye alikuwa anapewa DIRECTIVES ?

6.Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa wakati huo kwani rada hiyo ni ya matumizi ya kijeshi zaidi kuliko ya kiraia.

Kuna umuhimu walipa kodi wakajua KODI zao hawa wanajeshi wanazituia vipi na PROCUREMENTS ZA JESHINI ZINAENDAJE ....

7.Maafisa na Wanasheria waliohusika katika majadiliano hayo. Na hasa kama ni maofisa hao hao walioshiriki katima manunuzi ya Ndege ya Rais, Helikopta za Bell na Malori ya kijeshi.

hOJA HII inaendana zaidi na majibu yaliopo hapo juu


HOJA D

JK nilimshajibia na yeye alikuwa anasema hayo aliyo ambiwa na wakubwa zake yaani MKAPA ambaye alikuwa hawezi kupindua kwa BLAIR so its kesi ya kujaza maji kwenye gunia ....labda ungeuliza ule mkataba tuliosaini na waamerika kutumia anga ya Tanzania small print zake zinasemaje na so far umemnufaisha nani?

HOJA E

hii nilishakujibu kutumia mfano wa NIGERIA wanaohaha kuhusu pesa zilizoibiwa na ABACHA USWISI na nadhani unajua kuwa ISSUE ILIOPO hapa ni nani atapata WIGGLE ROOM...nadhani unajua kuwa post ENRON & KEN LAY maybe we as Tanzanians we can be a bit optimistic of a successful trial of corporate frauds..only in the west.... Incidentally, Ken Lay's death has now resulted in his conviction being set aside:

http://tinyurl.com/y9tpb5

Blair and Mkapa can always escape with a heart attack
 
Back
Top Bottom