The Radar Scandal: Investigation & Progress

Tulishasema CCM ni wezi, wnawatumia Whindi. Hamkubali. Sasa kama Mr. Clean ni mchafu hivi, itakuwaje kwa hawa walioingia kwa pesa za Waarabu? Na kama wao ni safi basi wawakamate wezi waliotagulia. JK akiwalinda, anajua anachofanya - kinachotuudhi sisi. Na hatutamwamini.
 
Watanzania wote tunonekana mafara kwa kuwaachia hawa Wahindi kutjirika
kwa migongo y watu ambao wanakufa kwa malaria.

Tunachojua ni kuvaa sare za CCM kujipendekeza kwa rais.

Hivi kwa wanasheria, hakuna sheria TZ ambayo inaweza kuwafanya raia wakawafungulia mashtaka hawa wahujumu uchumi bila kusubiri serikali?
 
Waheshimiwa msikose matangazo ya Alhamisi... !!!! yatawapa kichinachina!! Nitaunguruma kama simba aliyejeruhiwa! Majina yanatajwa na maswali yanaulizwa!
 
na wewe ushaingia katika mambo ya kutaja majina?

haya bwana

TTJ naye alisema anarudi on THURSDAY
 
Mimi nawauliza watanzania wenzangu . Hili swala la rada JK anakuwa upande gani ?Si kweli kwamba alishiriki ununuzi ule akiwa na Lowasa maana wote walikuwa na Mkapa kwenye baraza la mawaziri ?
 
Professor Ibrahim Lipumba, Chairman of the opposition Civic United Front says the deal has been shrouded in secrecy.



Tanzania is a sovereign country and surely should be able to decide what to do with its loans

Rebecca Muna
Debt campaigner

But the Minister for Foreign Affairs and International Relations, Jakaya Kikwete, rejects such arguments.

"People say we do not need this system, what are they waiting for? When two jumbo jets crash over Tanzania, will people accept the need for us to have a radar system? This problem is real not fiction," he says.
Hayaa.........I wish our journalists to remind him squarely...sijui ata respond nini?Naona giza jamani....is there a future for our children..kama nchi yenyewe ndio inaliwa hivi?Sijui mpaka sasa hiv hii radar itakuwa imeingiza USD ngapi...minus hizi safari zetu...
 
Mama Lu, Hii Quote yako nzito! Asichomoke mtu hapa tunataka wote wawepo!Tunapiga kelele RUshwa!,Rushwa!,Rushwa!,Kumbe wenyewe ndio VINARA?
 
Wana Jambo Forum:
Wakati ni huu, kusiwepo kurudi nyuma tena. Acheni mambo ya kujadili kijumla jumla tu sasa, mwenye taarifa na aitoe kiwazi watu wajue. Huyo mtu atakuwa ni shujaa katika vita hii. Hii ni vita, na ni lazima ipigwe dhidi ya rushwa kila upande na kwa kila njia.
Kama ni kutaja majina, tutaje majina watu wajulikane. Enzi za kulalamika ..... 'Ooooh, sijui tufanye nini, ....Oooh sijui nani yule anakula rushwa' huku tukimsema kwa mafumbo bila ya kumbainisha!
Watu tumekuwa waoga mno; kiasi kwamba tunaonekana kama wajinga hivi.
Wabunge hao hao, hata hawaeleweki kabisa kazi zao ni nini hasa. 'Generalities' zinazotolewa na akina Ndesambulo hazitusaidii chochote.... wewe mbunge kama umeona rushwa unazuiwa nini kuishughulikia kikamilifu? Rushwa isiwe ni siasa, hata huko kwenye vyama vya upinzani isiwe tu ni kupigia kelele CCM sasa hivi, huku watu wakijua huko huko kwenye upinzani rushwa zinaendelea. Hii vita ya rushwa isiwe ni ya 'unazi' wa kisiasa.

Ninasubiri taarifa ya Mzee wa Kijiji kwa hamu; ninatumai kuona majina.
 
UKWELI LAZIMA UJULIKANE
Na. M. M. Mwanakijiji

Hatimaye sakata la ununuzi wa rada liko karibu kuwatokea watu puani! Kampuni kubwa zaidi ya uundaji wa silaha na zana za kijeshi ya Uingereza BAE systems imedaiwa imemlipa dalali wa Uingereza malipo ya zaidi ya shiling bilioni 12 kwa kufanikisha kwake kuiwezesha serikali ya Tanzania kununua rada ya kijeshi ijulikanayo kama Plessey Commander Fighter Control System kutoka kwenye kampuni hiyo kwa gharama za shilingi Bilioni 40. Dalali huyo Bw. Sailesh Vithlani amekiri kuwa licha ya kulipwa malipo ya kawaida ya udalali ya shingili milioni mia tano sawa na asilimia moja ya mauzo hayo kitu ambacho kinakubalika katika biashara hiyo, alipokea pia malipo ya shilingi Bilioni 12 kupitia akaunti yake iliyofunguliwa huko Uswisi na alilipwa na kampuni tanzu ya BAE systems ili kuficha uhusiano wa malipo hayo na kampuni hiyo.

Siri hii imefichuliwa baada ya maofisa wa serikali ya Uingereza kwenda Tanzania na kufanya mahojiano na dalali huyo pamoja na mshirika wake wa kibiashara, mfanyabiashara mwingine wa Kitanzania Bw. Tanil Somaiya ambaye pia amekiri malipo hayo.

Bila ya shaka unashangaa kwanini nimesema Bw. Vithlani na dalali wa uingereza wakati vyombo vingine vya habari vinamuita ni Mtanzania? Ukweli wa mambo ni kuwa Vithlani siyo Mtanzania yeye ana passport ya Uingereza na kwa vile Tanzania haina uraia wa nchi mbili, mtu huyo ni raia wa Uingereza! Ukweli wa mambo mfanyabiashara huyo hakuhusika na ununuzi wa rada tu bali pia ununuzi wa ndege ya kisasa ya Gulfstream 550 inayotumiwa na Rais na pia manunuzi ya hivi karibuni ya helikopta na malori ya kijeshi!

Kwa mujibu wa Somaiya aliyezungumza na gazeti la The Guardian lililotoboa habari za uchunguzi huo kampuni ya BAE ilipanga malipo ya aina mbili, moja ni malipo ya asilimia moja ya bei ya mauzo na ya pili ni malipo ya siri ya asilimia 30! Hapa ndipo penye tatizo! Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali malipo ya asilimia moja ya mauzo katika biashara ya silaha ni ya kawaida ila hayo ya 30 yananuka rushwa iliyo dhahiri!!

Penye utata zaidi ni kukataa kwa Bw. Vithlani kukiri kama baada ya kupata malipo hayo huko Uswisi alimlipa mtu yeyote huko nyumbani Tanzania. Bw. Vithlani alikataa kufanya hivyo, na alipoulizwa kama alimlipa mtu yeyote kutoka kwenye akaunti hiyo nje ya nchi Bw. Vithlani alikataa kusema lolote. Kukataa kwa Bw. Vithlani kusema kama kuna mtu alilipwa nje ya nchi (awe ni mtanzania au vinginevyo) kunaishara mbaya kwa uongozi wa Rais Benjamin Mkapa! Hapa ndipo wananchi wa Tanzania hatuna budi kupiga kelele ili ukweli ujulikane!

Jinsi mambo yalivyo, kampuni ya BAE imechunguzwa mara kadhaa kwa tuhuma za kutoa malipo kwa viongozi wa serikali na maafisa mbalimbali wa serikali duniani ili iweze kupata tenda za kuuza silaha au vyombo vya kijeshi. Zaidi ya kuchunguzwa kuhusiana na Tanzania Shirika hilo la BAE linachunguzwa pia kwa tuhuma za kulipa wanasiasa na maofisa wa serikali katika nchi za Chile, Cheki, na Romania na Afrika ya Kusini.

Kampuni hiyo ya BAE inadaiwa pia kuhusika na mipango ya aina hiyo na serikali ya Wasaudi, lakini Wasaudi wakaipiga mkwara serikali ya Tony Blair na uchunguzi dhidi yao ukafutwa.

Licha ya pingamizi toka Benki ya Dunia na vyombo mbalimbali ya kijamii ikiwemo Oxfam, na licha ya maombi ya Bunge la Uingereza kutaka kampuni ya BAE kupunguza bei ya rada hiyo, shirika hili lilishikilia uamuzi wake wa kuiuza kwa bei ya juu rada hiyo kwa Tanzania. Cha kushangaza zaidi ni kuwa serikali ya Tanzania ikiongozwa na Rais Mkapa walitetea kwa nguvu haja ya nchi yetu kuwa na rada hiyo ya kijeshi ambayo kwa kweli haikuhitajia au kuongeza usalama katika sekta ya kiraia. Kampuni ya BAE walipata kibali tarehe 20, 2001 toka Wizara ya Biashara na Viwanda ya Uingereza.

Kwa vile siri hii ndo imeanza kufichuka, tunapenda kwa niaba ya Watanzania wengi kusema yafuatayo.

1. Kwanza serikali ya Tanzania ione aibu kuwa hatimaye chombo cha nje kinaonesha kujali maslahi ya nchi yetu au hali yetu zaidi kuliko viongozi wetu tuliowachagua. Inakuwaje wazungu waoneshe kutujali zaidi yetu na kufunga safari kuhoji watu wetu kuhusu ununuzi wa rada hii. Hili linasikitisha. Inakuwaje tuweze kutumia shilingi bilioni 80 kununua vitu ambavyo kwa kweli si vya lazima na tungeweza kupata mbadala wake au ndio tunajaribu kununua gari la aina ya Maybach wakati gari linapoegeshwa ni kwenye nyumba ya kibanda cha nyasi! Gari linagharimu zaidi kuliko nyumba!!!

2. Serikali ya Rais Kikwete ialike wachunguzi toka nje ili waje kuendesha uchunguzi wa kwanini tulinunua rada hii, ni nani walihusika, na watu hao walinufaika vipi kwa manunuzi ya rada hiyo. Rada tuliyonunua haiangalii nchi nzima isipokuwa theluthi moja tu ya nchi yetu, wakati tungenunua rada ya kiraia kwa bei ya chini tungeweza kufanikisha lengo la usalama wa anga! Ni nani aliyeshawishi serikali kuendelea na manunuzi ya rada hii na mtu huyo alinufaika vipi? Je ni Bw. Vithlani? Kama yeye ni dalali bila ya shaka kuna mtu toka serikalini aliyempa ofa hiyo, ni nani huyo?!

c. Tunaitaka serikali ya Uingereza kufuatilia (monitor) akaunti za Bw. Vilathni na Somaiya ili kujua kama kuna malipo yaliyofanyika kwa mtu yeyote mwingine na hususan afisa au kiongozi wa serikali ya Tanzania. Habari ambazo KLH News imezipata na bado hazijathibitishwa ni kuwa kuna baadhi ya maofisa wa ngazi za juu wa serikali iliyopita na wengine waliopo madarakani hivi sasa ambao mara baada ya ununuzi wa rada hiyo walifunga safari kwenda nje ya nchi ambako walikatiwa gawiwo lao baada ya kufanikisha dili hilo. Inadaiwa watu hao wamefungua na wenyewe akaunti Uswisi na sehemu nyingine offshore ambako mifumo ya kodi ni ya siri. Watu wafuatao tunapenda wajitaje hadharani jinsi walivyoshiriki na kunufaika na mipango hiyo na kama wao, familia au jamaa zao wa karibu hawakupokea malipo yoyote yale toka BAE kupitia dalali huyo. Viongozi niwatajao wawe tayari kuruhusu akaunti zao za nje zichunguzwe na SFO na pesa zozote zilizoingizwa kwenye akaunti hizo zijulikane zimetoka wapi.

1.Rais Benjamin William Mkapa ambaye chini ya uongozi wake rada hii ilinunuliwa.
2.Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa wakati huo na Rais wa sasa Bw. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alitetea ununuzi wa rada hiyo. Na hata jana ametetea.
3.Mwanasheria Mkuu wa Wakati huo Bw. Andrew John Chenge ambaye ni Waziri wa Miundo Mbinu wa sasa ambaye ofisi yake ilisimamia mkataba kati ya serikali na Bw. Saileth Vithlani
4.Prof. Mark Mwandosya aliyekuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi ambaye sasa ni Waziri wa Mazingira.
5.Maafisa (wanasheria na washauri) wa Wizara husika ambao walihusika na mikataba hiyo.
6.Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa wakati huo kwani rada hiyo ni ya matumizi ya kijeshi zaidi kuliko ya kiraia.
7.Maafisa na Wanasheria waliohusika katika majadiliano hayo. Na hasa kama ni maofisa hao hao walioshiriki katima manunuzi ya Ndege ya Rais, Helikopta za Bell na Malori ya kijeshi.

d. Siku hiyo kilipopatikana kibali cha kununua rada hiyo (yaani Disemba 20, 2001), Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Tanzania alidai kuwa upatikanaji wa rada hiyo utachangia katika ukusanyaji wa kodi kwa ndege zinazoruka katika anga la Tanzania na pia na utasaidia katika mapato ya utalii. Waziri huyo wa wakati huyo Bw. Jakaya Kikwete ambaye leo ndiye ni Rais atuambie je tumefanikiwa katika mambo hayo mawili? Yeye akiwa Waziri wa Mambo ya Nje alihusika vipi katika upatikanaji wa rada hiyo, alinufaika kwa namna yoyote ile binafsi?

e. Waziri wa Miundo Mbinu Bw. Andrew Chenge alikataa kuwa Tanzania inachunguzwa kuhusika na rushwa akidai kuwa taratibu zote za ununuzi wa rada hiyo zilifuatwa. Alidai kuwa maneno hayo ni "maneno ya wazungu". Ukweli wa mambo ni kuwa wakati rada hiyo inanunuliwa yeye alikuwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, tungependa tuelezwe yeye Bw. Chenge anawajua vipi kina Vithlani na Somaiya, na mkataba wa serikali kununua rada hiyo ulikuwa unawalipa watu hao kiasi gani? Pia atuambie maofisa walioshiriki katika majadiliano na madalali hao walilipwa kiasi gani? na Je kiongozi yeyote wa serikali akiwemo yeye mwenyewe walilipwa na madalali hao mara baada ya rada kununuliwa? Je ushahidi ukiletwa na kuoneshwa kuwa Bw. Chenge, Maafisa wa serikali na familia zao za karibu zilifungua akaunti nje zenye kiasi kikubwa cha fedha wako tayari kutueleza fedha hizo zimetoka wapi?

f. Uchunguzi wowote utakaofanywa matokeo yake yatangazwe hadharani, tumechoka na ripoti za ki spika!
 
Now I know that the less you know the safer you are:
Tangu nimeanza kusoma na kusikia mambo haya ya kihuni yanayofanywa na hawa viongozi wetu walafi naona umri wangu unapungua; hasa ninapoona kabisa kuwa tunaishia kupiga debe na wenyewe hawajali.
Hii imekuwa kesi ya -nani amfunge paka kengele shingoni-
Kweli Hosea na PCB yake anaweza kum-summon Mkapa au JK na kum-interrogate kuhusu hii issue?
MJJ umetaja majina ya watu ambao wako madarakani, mbaya zaidi mkuu wa nyumba JK nae yumo; who is going to question who?
Hapa naona tuombe Mungu atende miujiza; the country is sooooo corrupt, its stinking! No wonder they dared not to question the Richmonduli deal despite our efforts to point out the facts in detail- wanajuana hawa wezi wakubwa hawaogopi hata Mungu! Ona sasa wanavyoumbuliwa na watu wa nje.
I wonder how JK felt when he was in UK at a time when this saga was hot in the media..au ndo wameshakuwa sugu mpaka hawajali

On the other hand, this is the time when I expect the opposition to come up strong and call for action; where are you Mbowe? umeingia mitini? Did I not tell you that you will not dare come up openely in this forum and kata issues like the other wazees are doing?
And, Ndesamburo had the guts to resign cos of corruption; now its the time that he and the other opposition leaders should come up with a strong statement on these corruption scandals-otherwise we are in for more and more of them- are we really going to wait for outsiders to do it for us,
Au ndo imekuwa 'nani amfunge paka kengele shingoni'?
 
Mzee Mwanakijiji: Great contribution. Actually, those are some of the issues people wanted to raise at the meeting with Kikwete. Lakini ndio hivyo tena, akaingia mitini.
 
Naam mkuu ameondoka, things are slightly back to normal na tunaweza kuchagia



Kipi kilikuwa bora:
Kujibu maswali mawili matatu ya wabongo na hivyo kuharibu miadi uliokwishaipanga well in advance ambayo imepelekea kupatikana kwa msaada wa Paundi milioni 105?

Nadhani watu waliowengi suala hili la RADAR hawajalielewa vizuri, Rais amekwishasema kwamba hilo suala ni mfano wa mtu aliekwenda ukweni kutaka mke, akapewa kwa mahari ya kiasi kadhaa,sasa kwa vile mke wako unae huko ukweni watu wanadai mahari wakidhulumiana hiyo haikuhusu mwenye mke!

RADAR tulikuwa tunaihitaji, hakuna wa kutukorofisha katika ulinzi wa nchi yetu, tumeinunua toka katika kampuni ya serikali ya Uingereza, haiyumkini kwamba kampuni hii ya serikali inayotusaidia ituzime! Halafu SFO wamesema wanataka kuhoji watu kadhaa pale Tanzania.

Wameruhusiwa in our spirit of good governance, hakuna mtanzania hata mmoja seuze wa serikalini anaehojiwa wanaohojiwa ni wafanyabiashara tena wa kiingereza waliopo DAR, serikali inahusika vipi, wao wamekwishapata RADAR na matunda yake yanaonekana, kuna baadhi ya mashirika ya ndege yaligoma kutua DAR kwa vile tulikuwa hatuna vifaa vya kisasa vya kuguide ndege zao, RADAR hii ni moja ya vifaa hivyo, Qatar wameshaanza kuonesha mfano na mazungumzo na kampuni nyingine yanaendelea.

Tuwe na objective criticism baada ya kutafiti vizuri...Anyway to be fair to all tuuachie uchunguzi ukamilike ndio tujadili negatively vinginevyo ni contempt of investigation.
 
Kwa hiyo unachosema ndugu yangu tafitithenjadili ni kuwa kama Rais asingekuja Uingereza tusingepata huo msaada? Je, huko nyuma ambapo Tanzania imepokea misaada lukuki ikiwemo kufutiwa madeni na kuingizwa katika mpango wa HIPC ni kweli kwamba marais waliopita ilipita wazunguke dunia nzima kwa ajili hiyo? Nafikiri hili la kuhusisha misaada ya wazungu na mafanikio ya safari za Rais lipo misplaced.

Uingereza kama wangeamua kutunyima misaada wangefanya hivyo bila kujali Rais Kikwete kaenda kushuhudia Tottenam wakicheza au la!

Bado hujajibu swali la "kwa ubalozi uliona fahari kugawia watu wavae uniform za CCM katika mkutano wa watanzania na Rais wao? Huoni basi ingekuwa ni busara ubalozi kugawiwa watu wavae nguo zenye bendera ya Taifa na kupeperusha vibendera vya Taifa badala ya CCM? Ina maana kwenu nyie ubalozi CCM ni muhimu kuliko utanzania na utaifa wetu?
 
Ni muhimu pia utueleza ilikuwaje Rais akose dakika 30 za kujibu maswali ya watanzania lakini akapata muda wa kuongea na wana CCM?
 
Mwanasiada this tafiti ni mnafiki sana .Tunajua alipokuwa NY ubalozini kabla ya UK .Huyu jamaa ndiyo maana tuna waalani watu wa aina yake kwamba mnapashwa kusimamia Usalama wa Nchi na si CCM na matumbo yenu. Huyu jamaa na Radhia they did al they could ku score points kwa JK kwa kukwepesha mkutano na maswali maana walijua Muungwana uwezo wake ni limited kukata issues. Tunapewa misaada huku na nyumbani wazungu wanavuna sana kuanzia mbuga zetu hadi madini . Misaada si bure hii .
 
Naam mkuu ameondoka, things are slightly back to normal na tunaweza kuchagia



Kipi kilikuwa bora:
Kujibu maswali mawili matatu ya wabongo na hivyo kuharibu miadi uliokwishaipanga well in advance ambayo imepelekea kupatikana kwa msaada wa Paundi milioni 105?

TTJ, msaada huu ni pole baada ya kula 40 milioni zetu?

Nadhani watu waliowengi suala hili la RADAR hawajalielewa vizuri, Rais amekwishasema kwamba hilo suala ni mfano wa mtu aliekwenda ukweni kutaka mke, akapewa kwa mahari ya kiasi kadhaa,sasa kwa vile mke wako unae huko ukweni watu wanadai mahari wakidhulumiana hiyo haikuhusu mwenye mke!

Tatizo hapa ni kuwa wewe ukidhani umempata mke uliyemhitaji kumbe sivyo, mshenga amekuingiza mjini kwa kudai mahari ya juu zaidi wakati sehemu ya mahari hiyo imeenda mfukoni mwake. Na hiyo mahari uliyotoa umekopa toka huko huko kwa wakwe!

RADAR tulikuwa tunaihitaji, hakuna wa kutukorofisha katika ulinzi wa nchi yetu, tumeinunua toka katika kampuni ya serikali ya Uingereza, haiyumkini kwamba kampuni hii ya serikali inayotusaidia ituzime! Halafu SFO wamesema wanataka kuhoji watu kadhaa pale Tanzania.

TTJ, je kuna rada yoyote ya matumizi ya kiraia ambayo ina gharama ndogo lakini inatupatia ulinzi wa hali ya juu wa anga letu? Je rada hiyo inalinda sehemu ngapi ya Tanzania nzima kiasi cha kusema kwa kujiamini kuwa "hakuna wa kutukorofisha katika ulinzi wa nchi yetu". Hivi kabla ya kuwa na rada hiyo tulkuwa tunatishiwa na nchi gani katika anga letu?

Wameruhusiwa in our spirit of good governance, hakuna mtanzania hata mmoja seuze wa serikalini anaehojiwa wanaohojiwa ni wafanyabiashara tena wa kiingereza waliopo DAR, serikali inahusika vipi, wao wamekwishapata RADAR na matunda yake yanaonekana, kuna baadhi ya mashirika ya ndege yaligoma kutua DAR kwa vile tulikuwa hatuna vifaa vya kisasa vya kuguide ndege zao, RADAR hii ni moja ya vifaa hivyo, Qatar wameshaanza kuonesha mfano na mazungumzo na kampuni nyingine yanaendelea.

Una uhakika kuwa hakuna Mtanzania "hata mmoja seuze wa serikalini" anayehojiwa? Unafikiri kuna ulazima wa kuhoji Watanzania hao kuhusu sakata hili zima?

Tuwe na objective criticism baada ya kutafiti vizuri...Anyway to be fair to all tuuachie uchunguzi ukamilike ndio tujadili negatively vinginevyo ni contempt of investigation.

Huo ni uchunguzi wao, na huo mchakato wao, sisi tunazungumza mambo yanayohusu watu wetu!!
 
Ukisoma majibu ya Tafiti na kama kweli ni ofisa wa ubalozi wetu London, sishangai serikali inawatumia middlemen kwenye deals mbalimbali wakati mambo hayo yalitakiwa yafanywe na maofisa wa ubalozi.

Kuna mambo ambayo binadamu mwenye akili hawezi kuyatetea unless he/she thick and stupid.

Anasifia kupew pounds milioni 105 wakati mabilioni yanaibiwa na watu hao hao? Huu ni ujinga uliojaa kifani.

Endeleeni na ujinga huo na una mwisho wake.
 
Mimi nilisha jua kwamnba Mzee tafiti akili zake hazina akili tangia aliposema uongo juu ya Konsulate ya Holland akaja akazimwa na Muhaya mwenzake Mugishwagwe . Tokea hapo nilijua huyu anaganga njaa na mtetea uozo wenyewe muone sasa . Tunajisifia kwa kupewa misaada badala ya sisi wenyewe kujiendesha maana uwezo tunao ubaya ni akina tafiti ku sapoti 30% za akija JK na kulamba viatu vyao kwa jina la mkate wangu mimi tafiti wengine wajijue .
 
Back
Top Bottom