KakindoMaster
JF-Expert Member
- Dec 5, 2006
- 1,356
- 91
Huyu hawezi kujihudhuru hata siku moja, ana kiburi sana huyu Fisadi na sababu kubwa ya kiburi chake ni kutokana kuwa wakati akiwa mwanasheria mkuu alihusika moja kwa moja katika dili nyingi za wakuu Mafisadi, hivyo wanamuogopa sana hata kumwambia kitu, wakijua wakisema lolote anaweza kuleta noma muda wowote
Hawa jamaa si unajua wamefanya hii nchi kama ka mradi kao, na sisi tunaangalia na kusema eti ngoja 2010, mimi sijapata picha hapa solution ni hipi iliyobaki, kwa sababu kwa nchi kama zetu kura imeonekana sio solution, ukifuatilia yaliyotokea yenya baada ya Chama tawala kushindwa na sasa Zimbabwe, utaona kuwa kura za wanyonge hazisemi lolote kwa sasa
Hawa jamaa hawajiudhuru na kuiba watatuibia na kura wataiba watashinda na nguvu ya hoja imeshindwa na sheria inawabana maskini tu na kuwaacha matajiri, sasa hapa hakuna njia zaidi ya solution ya mwisho kabisa jamani
Mkuu huyu jamaa tukimkamata vizuri anaweza kutwambia kama hata na sisi tumeisha uzwa.
Kiburi alichonacho kinatisha sana maana nilimuona siku Lowassa anatimuliwa Ukuu akidai hiyo haikubaliki. Sijui kwa nini hawezi kwenda naye. Inabidi akimaliza wiki kabla hajajiuzulu tuanze kuandamana.
Otherwise hawezi kutuweka kwenye vyombo vya habari mbali mbali ni fedheha kwa watanzania maana sasa hivi dunia nzima inaweza kuelewa kuwa watanzania siyo waaminifu.
Halafu vile vile yule Mzee aliyechagua kukaa kimya inabidi naye atoke aongee chenge kama wmwanasheria hawezi kulala mitini na kitita hicho chote bila mkuu wa kaya kuwa na hata fununu.
Hivi hakuona mwenzake Tony juzi alivyowekwa kitimoto kwenye vyombo vya habari kuhusu rada?
Inabidi tufuatilie akisafiri kwenda nje waandishi wa habari wa nje wamuhoji maana historia inaonyesha yeye hupenda kuhojiwa na wazungu.