Muuza viatu
JF-Expert Member
- May 14, 2020
- 3,840
- 7,916
Na azam xtra pamoja na zbc2 kwa pamoja wanaonyeshaga mechi za mwisho wa ligiJe azam anae rusha live 3 kwa wakati mmoja? Sport1HD mpira kutoka mbeya sport2HD mpira kutoka Tanga na UTv live kutoka chamwino
No, ob van yenyewe inakuwa imefungiwa link, hivyo vituo ambavyo havina link, wanafunga link kwenye hiyo sehemu au kwenye gari yoyote.Inamaana ITV wanaporushaga laiv huwa wanaazima hizo OB Van
It's true, bei ya OB sio mchezo!. Kwa Tanzania wenye OB mpya ni TBC na Azam only. Star TV na Clouds wao wana used. Wengine wote hawana.hongera sana tbc.hayo ma ov van bei yake kwanza lazima ukae.
Wewe ni kada mtafuta teuzi tu ndugu yangu sjui kwa nini uko hvo. Hyo tabia ya uchawa achana nayo ili uwe flexible. Sasa wakirusha hzo live mbili itasaidia nn kama content znalengo la kuisifia ccm tuu. Acha hyo tabia, alafu usiwe kma mshamba technology imesha advance wanachokifanya hao TBC hakina maajabu. Ingekuwa ndo kitu kpya kufanyika hapa ulimwenguni ndo tungeelewa na kuwasifia licha ya maudhui ya hovyohovyoWanabodi
Kwanza wale wenye access, Watch, TBC 1 na TBC 2...shuhudia...!.
Kwa watu wasiojua what it takes kurusha matangazo ya TV live mubashara kutoka sehemu mbili tofauti kwa wakati mmoja, mnaweza msielewe, hapa ninashangaa nini!.
Kiukweli kituo cha Television ya Taifa, TBC, kimetisha!. Kitendo cha kurusha matangazo ya moja kwa moja, Live Mubashara kutoka maeneo mawili tofauti kwa wakati mmoja, sio jambo dogo!. Hongera sana Dr. Ayub Rioba na timu yako.
Live moja ni kutokea jijini ya Dodoma kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Posta Duniani, live hiyo iko live on TBC1. Wakati huo huo, yaani at the same time, kuna Live ya pili ikitokea Arusha, kwenye uzinduzi wa maonyesho ya Utalii ya Africa Mashariki ambayo iko TBC2- maarufu Safari Channel.
Matangazo ya moja kwa moja ya Redio au TV yanaitwa OB, au Outside Broadcasting.
Ili kituo cha TV kiweze kurusha live, lazima uwe na dude kama hili.
View attachment 1969159TBC Yafanya Kweli!, Yashusha OB Van ya Kufa Mtu!, Ina Kamera 12!. Itarusha HDV Signal Kama DSTV.
Wanabodi, Heri ya Pasaka, Mara moja moja huwa ninatembelea Kituo cha TBC kwa shughuli zangu, leo Jumapili ya Pasaka nimepita pale na kuushuhudia bonge la OB Van mpya ya Kufa Mtu ikitua TBC!, kwa maelezo ya juu juu, OB Van hii, ina Kamera 12!, na moja ya camera hizo ni camera ya slow motion...www.jamiiforums.com
Hilo dubwana, lione tuu kwa nje kama lori tuu, humo ndani shughuli yake sio mchezo!.
View attachment 1969177
Hii inamaanisha sasa TBC inayo hii midude zaidi ya moja.
Leo ndio mara yangu ya kwanza kushuhudia live mbili concurrently zikirushwa na kituo kimoja cha TV. Kwa nchini Tanzania, ukiondoa live za DSTV, na zile za Azam, TBC ndio imefungua pazia la live mbili kwa wakati mmoja. Huu ni uthibitisho TBC ndio TV kiongozi nchini Tanzania.
Hongera sana TBC.
TBC Baba Lao.
Paskali
Hivi azam ,,,dstv ni cable tv ?Kila nchi rights zinatolewa kwa TV za Taifa tuu. Hivyo kwa Tanzania ni TBC, ila cable kama DSTV pia wanaweza kununua rights kutoka Fifa, hii maana yake na Azam wanaweza!.
Ndio maajabu ya mayala hayoHivi azam ,,,dstv ni cable tv ?
Hahahaha mbona daraja la kigamboni mlisema ni kazi ya Kayafa mpaka mkawarubuni wakina Harmonize watoe nyimbo kusifiaHamna hata aibu, hizo chuki zenu zitawamaliza, ndege nazo mnasema mama wakati zimeandikwa Hapa kazi tu, hizi mitambo na uboreshwaji wa TBC alifanya JPM lakini leo watu wanasema tofauti...hehe
Kuna copyright issues wakiziweka zile Cha kufanya warekodi zetu wenyeweWashauri safari channel watafte ama kutengeneza documentary mpya, kila siku ni kisiwa cha Rubondo tuuu.
Waambie warekodi zile zinaonyeshwa NG Wild halafu watafsiri ama waingize sauti kwa juu kuliko kila siku ni makala zile zile.
Ama hata waweke za sauti ya kizungu hakuna shida.
Mimi ni mpenzi wa makala za wanyama nimeona nitoe maoni yangu.
tunatizama sana shanel yetu.hasa has atafakuri baada ya habari.ila siku za hivi karibun aliyekuwa anasoma tafakuri baada ya habari sijui yupo wap.kuna saut ila sio ya yule wa mwanzo.Bado unaangalia TBC!?
Hicho kituo kiboreshwe, hasa kisiwe na mrengo wa wazi wa kisiasa! Kinakwaza sana
DSTV sio TV ya FTA, DSTV ni Cable TV kama ilivyo Azam TV ni Cable TV. Hapa Bongo Tanzania, tuna FTA TV na pia tuna Cable. TBC ni FTA, jee umeisha wahi kuona live mbili za kituo kimoja kingine chochote cha FTA, mimi ndio nimeona leo.
P
Aliyekuwa anasoma Tafakuri mwanzo ni Shabani Kissu, sasa amekuwa Mkurugenzi wa Channel Ten, msomaji wa sasa ni Sued Mwinyi.tunatizama sana shanel yetu.hasa has atafakuri baada ya habari.ila siku za hivi karibun aliyekuwa anasoma tafakuri baada ya habari sijui yupo wap.kuna saut ila sio ya yule wa mwanzo.
Kwenye hili nipo nyuma yako mkuuNje ya mada. Nachukua nafasi hii kuipongeza Twiga star Kwa kutwaa ubingwa wa COSAFA.
Nalog off