TBC Yafanya Kweli!, Yashusha OB Van ya Kufa Mtu!, Ina Kamera 12!. Itarusha HDV Signal Kama DSTV.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,565
Wanabodi,

Heri ya Pasaka,

Mara moja moja huwa ninatembelea Kituo cha TBC kwa shughuli zangu, leo Jumapili ya Pasaka nimepita pale na kuushuhudia bonge la OB Van mpya ya Kufa Mtu ikitua TBC!, kwa maelezo ya juu juu, OB Van hii, ina Kamera 12!, na moja ya camera hizo ni camera ya slow motion. Itarusha HDV Signal Kama DSTV.

Gari hili na vifaa vilivyomo ndani yake, vitaifanya TBC kuwa ndicho kituo cha Televisheni cha kwanza nchini Tanzania, kinachoongoza kwa vifaa bora vya kisasa vinavyotumia teknolojia ya kisasa hali ya juu ya full HD.

Kituo kingine chenye vifaa vya full HD ni Azam TV ila wao OB Van yao ni ya kamera 8!, hivyo hivyo hii OB Van ya TBC ya kamera 12, ndio OB Van funga kazi kwa Tanzania kwa sasa!.

Japo uongozi wote wa juu wa TBC ulikuwepo kushuhudia OB Van hiyo ikishuka, mimi sikuweza kuuliza lolote kuhusu OB Van hii zaidi ya kuikodolea tuu macho, maana sicho kilichonipeleka mahali hapo siku hiyo!.

Haya ndio baadhi ya mambo yake!.
image.tiff



Kwa gari hili, sasa TBC ndio inapaswa Televisheni kiongozi kwa Tanzania kwa kuwa the best TV Station in Tanzania kwa sababu ndio yenye vifaa bora na the best kuliko TV nyingine yoyote nchini Tanzania!, ila kiukweli, kuwa na vifaa bora ni jambo moja, kuwa na watu wenye uwezo wa kuvitumia (technical) hivyo vifaa bora ipasanyo ni jambo jingine!, yaani TBC kuwa na maproducer creative na ma talented presenters wa kutosha wenye uwezo, ari, moyo, na vipaji vya kuvishibisha vifaa hivi pia ni jambo jingine!.

Mabingwa wa utangazaji duniani, the BBC, waliishaligundua hili siku nyingi, hata uwe na vifaa vya kujaa kutoka duniani hadi mbinguni, pekee yako hauwezi!. Wanachofanya BBC, ili kupata the best kutoka kwenye market, wana commissions outside producers na presenters wazuri, kuwaletea a diverse contents kwa sababu wao peke yao, hawawezi!. Vivyo hivyo, TBC lazima uendelee kufungua milango yake kwa outside producers/presenters wenye creativity na vipaji vya hali ya juu kuleta a diverse contents.

TBC wao wenyewe tuu wao kama wao, hawawezi, ndio maana mnawaona kina Joti, wamehama kutoka EATV sasa wako TBC, na wakati wa maonyesho ya Saba Saba na Nane Nane, mnawaona watu kama Pasco Mayalla na PPR akivurumisha vipindi TBC, hivyo TBC iendelee kufungua milango yake na sisi Tanzania tuwe na Soap Opera zetu kama Isidingo kwa kila mwenye uwezo, kipaji alete vipindi TBC na wengine wengi upcomming talents wafuatie.

Paskali.
OB VAN MPYA YA TBC.JPG
596922.jpg
 

Attachments

  • TECHNICAL SPECIFICATION OUTSIDE BROADCASTING VAN.pdf
    108.4 KB · Views: 604
You mean Kodi zetu zinafanya kazi ?

Alafu hawa watu washauri TV inapata ruzuku ili kutengeneza programs zenye manufaa kwa jamii hata kama sio profit oriented sio wenyewe wanajikita kwenye kutafuta profit na kuonyesha chereko chereko na matangazo (nilitegemea hayo mambo yafanywe na private TV) sio TV ya taifa
 
Nakuheshimu sana Pascal Mayalla, ila ukweli lazima usemwe. TBC is no longer a credible News Station. Haina tofauti na gazeti la Uhuru na Mzalendo na it can't have the guts to present itself as a public entity.

Hata wanunue OB Van yenye ubora wa namna gani, hawawezi kupata heshima kama walonayo Sahara Communications na IPP Media.

After all nilishaiblock kwangu na hata nikikuta Star tv, ITV, Ch 10 na nyingine wamejiunga kupitia TBC1 nahama completely. Bora niangalie cartoon network kuliko TBC1
 
Last edited by a moderator:
Nakuheshimu sana Pascal Mayalla, ila ukweli lazima usemwe. TBC is no longer a credible News Station. Haina tofauti na gazeti la Uhuru na Mzalendo na it can't have the guts to present itself as a public entity.

Hata wanunue OB Van yenye ubora wa namna gani, hawawezi kupata heshima kama walonayo Sahara Communications na IPP Media.

After all nilishaiblock kwangu na hata nikikuta Star tv, ITV, Ch 10 na nyingine wamejiunga kupitia TBC1 nahama completely. Bora niangalie cartoon network kuliko TBC1
  • Uko sahihi mkuu, hili lilozungumzia bila shaka pasco analifahamu.
  • Amejaribu kugusia ya nini kifanyike ili TBC iwe bora katika aya za mwishoni
..........ila kiukweli, kuwa na vifaa ni jambo moja, kuwa na watu wenye uwezo wa kuvitumia (technical) ipasanyo ni jambo jingine!, na kuwa na maproducer na presenters wenye uwezo, ari, moyo, na vipaji vya kuvishibisha vifaa hivi pia ni jambo jingine!.

Mabingwa wa utangazaji, BBC, waliishaligundua hili siku nyingi, wanachofanya BBC, ili kupata the best kutoka kwenye market, wana commissions outside producers na presenters wazuri, kuwaletea contents kwa sababu wao peke yao, hawawezi!.Vivyo hivyo, TBC lazima uendelee kufungua milango yake kwa outside producers/presenters kuleta contents
............
 
ninachofahamu Bajeti hii inayoishia, TBC ilitengewa tsh 6 Bilion kwa ajili ya kuiboresha. so nadhani haya ndio hayo maboresho yenyewe
 
Nakuheshimu sana Pascal Mayalla, ila ukweli lazima usemwe. TBC is no longer a credible News Station. Haina tofauti na gazeti la Uhuru na Mzalendo na it can't have the guts to present itself as a public entity.

Hata wanunue OB Van yenye ubora wa namna gani, hawawezi kupata heshima kama walonayo Sahara Communications na IPP Media.

After all nilishaiblock kwangu na hata nikikuta Star tv, ITV, Ch 10 na nyingine wamejiunga kupitia TBC1 nahama completely. Bora niangalie cartoon network kuliko TBC1
Hayo ni mawazo yako yanayotokana na upeo wako
 
Last edited by a moderator:
Wanabodi,

Heri ya Pasaka,

Mara moja moja huwa ninatembelea Kituo cha TBC kwa shughuli zangu, leo Jumapili ya Pasaka nimepita pale na kuushuhudia bonge la OB Van ya Kufa Mtu!, kwa maelezo ya juu juu ina Kamera 12!. Itarusha HDV Signal Kama DSTV.

Gari hili na vifaa vilivyomo ndani yake, vitaifanya TBC kuwa ndicho kituo cha Televisheni nchini Tanzania, kinachoongoza kwa vifaa vya kisasa vinavyotumia teknolojia ya hali ya juu ya HD.

Kituo kingine chenye vifaa vya HD ni Azam TV ila wao OB Van yao ni ya kamera 8!, hivyo hii ya TBC ya kamera 12, ndia funga kazi kwa sasa!.

Japo uongozi wote wa juu wa TBC ulikuwepo kushuhudia OB Van hiyo ikishuka, sikuweza kuuliza lolote kuhusu OB Van hii zaidi ya kuikodolea macho tuu.

Haya nido baadhi ya mambo yake!.



Kwa gari hili, TBC ndio inapaswa kuwa the best TV Station in Tanzania kwa sababu ndio yenye vifaa the best kuliko TV nyingine yoyote nchini!, ila kiukweli, kuwa na vifaa ni jambo moja, kuwa na watu wenye uwezo wa kuvitumia (technical) ipasanyo ni jambo jingine!, na kuwa na maproducer na presenters wenye uwezo, ari, moyo, na vipaji vya kuvishibisha vifaa hivi pia ni jambo jingine!.

Mabingwa wa utangazaji, BBC, waliishaligundua hili siku nyingi, wanachofanya BBC, ili kupata the best kutoka kwenye market, wana commissions outside producers na presenters wazuri, kuwaletea contents kwa sababu wao peke yao, hawawezi!.Vivyo hivyo, TBC lazima uendelee kufungua milango yake kwa outside producers/presenters kuleta contents.
TBC wenyewe tuu wao kama wao, hawawezi, ndio maana mnawaona kina Joti, na wengine wengi wafuatie.

Paskali.
New wine in old skin bottles...................
 
Mabadiliko ya mwanzo lazima yaonekane kwenye kipindi cha habari coz nahisi ndo kinaongoza kuangaliwa na watu wengi,if they are realy serious
 
TBCCM siyo bwana Paskali?
Mkuu Makenzi, hili TBC kuitwa TBCCM, nakiri lipo na linaonekana wazi, ila lazima tukubali tukatae, japo nchi yetu iko kwenye mfumo wa vyama vingi, ile dhana ya party supremacy bado iko kichinichini, hivyo CCM kwa vile ndio chama tawala, CCM bado kinabehave kichama dola!, Tido alipokuwa Mkurugenzi TBC, CCM was not happy jinsi alivyoendesha ule "Mchakato Majimboni" wakamuonya afute agagoma, akiamini TBC ni TV ya umma (Public Television) na sio TV ya CCM au TV ya serikali ya CCM!. Kukaa kwake ulaya muda mrefu kulimpofusha kuhusu power ya CCM!. Alisahau kuwa Mwenyekiti wa CCM ndie The head of the executive!, ndie appointing authority yake and he is the one who pays the piper for TBC to play the tune!. Hivyo kilichompata sote tunakijua!. Unategemea nini kwa atakayevaa viatu vya Tido, afanye makosa yale yale akitegemea matokeo tofauti?!.

The way out kuifuta hii chana kuwa TBC ni TV ya CCM, ni kwa TBC kujikita katika ethics kwa kutoa haki sawa kwa vyama vyote!, ila changamato kubwa katika kulitekeleza hili ni kuwa na able people ambao anaweza kusimama kwenye program na watu kama kina Lipumba, Dr. Slaa, Lissu, Mtikila na wewe mtangazaji ukawa ndio uko on controll, na sio wao, ili kuziepuka zile nonsense kama Bungeni.

Mfano Tundu Lissu na hoja zake za muungano batili, bado naamini ukimpata mtangazaji mzuri, well informed kuhusu haya mambo ya muungano, unaweza kufanya kipindi na Lissu na ukazipangua hoja zake moja baada ya nyingine, na ukweli ukasimama!.

Ila pia kwenye kusimama na ukweli, Uongozi wa TBC na serikali, lazima iwe tayari sio tuu kusifiwa, bali na kuupokea ukweli mchungu, where it goes wrong, ali mradi ukosoaji huo uwe ni constructive criticism based in good faith, kwa nia ya kujenga na sio kubomoa!.

Mfano, kwenye program zangu za Miaka 50 ya Muungano, nimekuwa nikiwauliza viongozi wakuu wa CCM, kuwa kwa nini CCM imeweka msimamo wa serikali mbili kama chama?!, kwa sababu hatutengenezi katiba ya vyama!. To my opinioni hili ni kosa kwa upande wa CCM na hakuna mwenye guts kuwaambia kistaarabu kuwa kwa hili CCM ilikosea!. CCM ilichopaswa kufanya, maadam sera yake ni ya serikali mbili, ilipaswa kuwaendeshea semina ya siri wajumbe wake na kuwapika what they should stand for, hivyo kila mmoja kuzitetea serikali mbili kwa hoja bila kumkashifu Warioba, hivyo hata hoja ya serikali mbili ikipita, itapita kama ndio msimamo wa wajumbe walio wengi, kuliko hali ilivyo sasa ikipita itaonekana imelazimishwa kwa vile ndio hoja ya CCM, chama tawala.chama kubwa!.

TBC inaweza kuendesha vipindi vya kuyazungumza hayo objectively kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na sio maslahi ya vyama, ila mwisho wa siku, hata katiba ya serikali mbili ikipita, waTanzania waelewe imepita kwa sababu serikali mbili ndio maslahi halisi ya taifa, na imepita kwa sababu ya taifa la Tanzania na sio kwa sababu ndio msimamo wa CCM.
Program kama hiyo iendeshwe kwa kushindanisha hoja za utaifa na sio sera za vyama.

Paskali
 
Mimi sijaona wapi ametukanwa huyu waryoba.
Wanasema amechakachua data na kudai watanzania wengi wametaka serikali tatu wakati si ukweli.
 
Nakuheshimu sana Pascal Mayalla, ila ukweli lazima usemwe. TBC is no longer a credible News Station. Haina tofauti na gazeti la Uhuru na Mzalendo na it can't have the guts to present itself as a public entity.

Hata wanunue OB Van yenye ubora wa namna gani, hawawezi kupata heshima kama walonayo Sahara Communications na IPP Media.

After all nilishaiblock kwangu na hata nikikuta Star tv, ITV, Ch 10 na nyingine wamejiunga kupitia TBC1 nahama completely. Bora niangalie cartoon network kuliko TBC1
Mkuu Genekai, nauona msimamo wako kama ni apathy against TBC!, utakuwa bhujitendei haki hata kidogo, mfano ni TBC tuu ndio pekee iliyopewa right a kulitangaza live Bunge Maalum, TV nyingine zote zinajiunga na TBC!, kama unaacha kuangalia Bunge Maalum kwa sababu ya TBC na kuamua bora uangalie Cartoon!, then you have a problem my friend!.

Nakuona unaweza kuwa kama wale wenzangu na mimi, ambao leo wanatangaza "hawamtambui fulani!" kisha kesho unawaona wakinywa chai na juisi nyumbani kwa huyo "fulani wasiyemtambua" kwa vicheko na bashasha.

Kwenye masuala makuu ya Kitaifa, TBC hana mpinzani!, ukimuona mtu anakuambia haangalii kabisa TBC!, then atakuwa ana matatizo!, ila kwenye lile la news, nakubaliana kidogo na wewe, ila tatizo sio credibility but a friendly angle kwa whoever pays the piper!.

Paskali.
 
Back
Top Bottom