Taratibu za kufuata ili kumiliki Silaha ya Moto Tanzania

Vibali havitolewi hadi 2025 hivyo vumilieni.
Hakuna shortcut mtaliwa hela na hao wanaojiita usalama wa wilaya......
Utapita huko utakwama kwa Mkuu wa Mkoa

Sio kweli! Siku hizi watu hawamalizi hata mwaka wanapata’ wapo ninaowafahamu
 
Kaka utaratibu ni kununua kwanza then unaomba kibali cha kumiliki silaha. Mimi nipo kwenye hatua hizo lakini ni ngumu sana siku hizi na kuna urasimu sana. Nimenunua silaha toka July pale Tanganyika Rifle, nikajaziwa fomu pale nikaenda kwa kamati ya ulinzi na usalama ngazi ya mtaa na kata walinitembelea nyumbani kukagua na kurithika kisha walisaini na kuniidhinishia. Mwezi huohuo nikawakilisha kwenye kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya. Nilifika polisi Wilaya nikajaza fomu , nikaenda polisi makao makuu nikachukuliwa alama za vidole na kurudisha fomu wilayani, zikaenda kwa afisa usalama wa wilaya kazipitia kwa sasa zipo chini ya mkuu wa wilaya fulani alkini amezikalia hadi leo. Anapaswa apange tarehe ya mimi kuitwa kuhojiwa laini hadi leo hajafanya hivyo ni miezi mitano sasa. Ikitoka hapo inabidi iende mkoani napo nadhani itakaa mwaka mzima. Ingawa nafahamu umuhimu wa vetting kuhakikisha kuwa anayemiliki silaha anastahili bila kuiweka silaha kwenye mikono isiyostahili ila muda inayochukua kulifanya hilo inasikitisha sana ni muda mrefu sana. Mimi nimetumia tshs 6,500,000 kununua silaha tu, pesa zimelala pale Tanganyika Rifles sijapata kibali na wala sitegemei kupata chini ya mwaka mmoja bila sababu za msingi. There is something wrong somewhere!!!!
Duuu kumbe hivi vidude vina gharama hivi? Kuna jamaa alinambia pistol ni kuanzia laki 5 hadi nane inapatikana kumbe haikuwa sahihi?
 
Hatua ya kwanza ni kwenda kununua silaha yenyewe,maduka kwa Dar ni Tanganyika Arms karibu na Stesheni na Duka la Jeshi Ngome,ukishalipia unaiacha palepale dukani lakini unapewa forms za kuanza kuzijaza na risiti ya silaha yako,ukitoka pale unaenda Police HQ kitengo cha IB,pale watakuchukua finger prints nia ni kuona kama ulishawahi kuwa na record za uhalifu,baada ya siku 3 ndio watakupa clearance certificate (hii ni barua ambayo inaku-clear kwamba hawajakukuta na criminal record yoyote).Gharama ya kulipia hapo Polisi ili kupata hiyo Clearance Report ilikuwa ni tsh 2000 mwaka 2015,sijui sasa ni tsh ngapi.
 
ukipata hiyo Clearance Report ya Polisi ndio unaanza mchakato wa kupeleka form zako Serikali ya Mtaa,huko Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mtaa itakuhoji na kukujazia sehemu wanayotakiwa kujaza wakiambatanisha na muhtasari wa kikao cha Kamati yao,kikubwa huko andaa pesa ya chai ya kuwapa
 
ukitoka hapo unaipeleka kwa OCD wa eneo lako nae anaijaza,chai iwe mbele kama tai,akiijaza OCS unaiacha hapo,wao wataipeleka Idara ya Usalama wa Taifa ya Wilaya nao wataijaza lakini watakuita kwa mahojiano kidogo,kisha wataijaza na kuirudisha Polisi then Polisi wataipeleka kwa Mkuu wa Wilaya uliopo,huko itakaa mpaka kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya kitakapoitishwa ndio mtaitwa waombaji wote siku hiyo kwa kuhojiwa,mimi yangu ilikuwa ni Kinondoni na tulihojiwa na Bwana mdogo Ally Happi akiwa DC pale
 
kwa kifupi mlolongo ni huo,ikitoka Wilaya inapelekwa mkoani mpaka hatua ya mwisho unapopewa kibali,ni mlolongo ulionichukua mwaka mmoja na miezi 10 mpaka nakuja kukamilisha,sijui kwa sasa kama kuna unafuu,haya kazi ni kwako
 
Kuinunua ndugu yangu ni kama vile kununua suruali dukani ila kuichukua ni nafuu kupata visa ya USA kuliko kupata kibali cha kuimiliki, cyo kwa zama hizi kama haukupata silaha kwenye utawala wa jk basi sahau kimiliki iyo kitu, kuna jamaa zangu wana kwenda mwaka wa3 hkna cha kibali wala nini, wamebakiza kuzitembelea silaha zao pale Tanganyika Arms na kuonyeshana2 kama watoto wadogo yangu hii!
 
Kaka utaratibu ni kununua kwanza then unaomba kibali cha kumiliki silaha. Mimi nipo kwenye hatua hizo lakini ni ngumu sana siku hizi na kuna urasimu sana. Nimenunua silaha toka July pale Tanganyika Rifle, nikajaziwa fomu pale nikaenda kwa kamati ya ulinzi na usalama ngazi ya mtaa na kata walinitembelea nyumbani kukagua na kurithika kisha walisaini na kuniidhinishia. Mwezi huohuo nikawakilisha kwenye kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya. Nilifika polisi Wilaya nikajaza fomu , nikaenda polisi makao makuu nikachukuliwa alama za vidole na kurudisha fomu wilayani, zikaenda kwa afisa usalama wa wilaya kazipitia kwa sasa zipo chini ya mkuu wa wilaya fulani alkini amezikalia hadi leo. Anapaswa apange tarehe ya mimi kuitwa kuhojiwa laini hadi leo hajafanya hivyo ni miezi mitano sasa. Ikitoka hapo inabidi iende mkoani napo nadhani itakaa mwaka mzima. Ingawa nafahamu umuhimu wa vetting kuhakikisha kuwa anayemiliki silaha anastahili bila kuiweka silaha kwenye mikono isiyostahili ila muda inayochukua kulifanya hilo inasikitisha sana ni muda mrefu sana. Mimi nimetumia tshs 6,500,000 kununua silaha tu, pesa zimelala pale Tanganyika Rifles sijapata kibali na wala sitegemei kupata chini ya mwaka mmoja bila sababu za msingi. There is something wrong somewhere!!!!


Huo ndo utaratibu lakini ukiufuata utasubiri sana. Kuna watu nawafahamu wamepata silaha hata miezi 2 haifiki. Weka pesa mezani kila kitu kinapelekwa fasta na utaratibu hauvunjwi.
 
Dunia hii ya sasa kutaka kumiliki bunduki kwa kigezo cha kujilinda dhidi ya wezi na wanyang'anyi ni udhaifu tu,
labda kama ni kwa sababu zingine za show off na kutisha raia mtaani.

Waharifu wakiamua kufanya yao wanafanya tu hata kama unamiliki mitungi ya nyuklia au makombora ya masafa marefu.
.
.
Hizo pesa na nguvu inayotumika kufuatilia umiliki ni vema zitumike kujiongezea kipato zaidi.
 
Back
Top Bottom