Tanzia

jamani
Pole sana mtu mmoja pamoja na mkeo...
Lakini inatia moyo sana kuona kiwango ulichonacho cha imani.
Mungu atawapa faraja yake ya kweli.

Pumzika kwa Amani Jr.
 
pole sana Mtu mmoja nimekosa neno la kusema ,nyinyi mlimpenda lakini mwenyezi mungu kampenda zaidi,mungu awapeni nguvu na ujasiri,
 
pole sana muombe mungu akupiganie pole sana kwa lililokutokea ninaiman mungu yu pamoja nawe pole sana
 
Ndugu zangu,

january mwaka huu nilikuja hapa na habari za furaha kuu za kupata mtoto wa kiume (angalia link hiyo hapo chini)

https://www.jamiiforums.com/mahusia...a-kiume-mama-na-mtoto-wanaendelea-vizuri.html



leo hii nina huzuni kuu pia, Mwenyezi Mungu muweza wa yote kamuita mtoto huyo kurejea kwake na kutuacha na majonzi makubwa nisiyoweza kuyaeleza vyema. machozi mengi sana yamenitoka, ila sina la kufanya zaidi.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe

RIP mwanangu mpendwa
pole sana ndg yetu.
 
Mzazi pole! KAZI YA MUNGU HAIJADILIWI na KAMWE MUNGU HAMUONEI kiumbe mtoto hajaonewa wala wewe hujaonewa! Kwa namna alivyokupa kwanza ndivyo atakupa kingine.
 
Pole sana Mtu Mmoja, wewe na familia yako yote.Inasikitisha ila angalau mlipata kuwa nae kwa muda kidogo.

Naomba Mungu awajalie faraja na nguvu za kukabiliana na kipindi hiki kigumu.

RIP little angle!!
 
POLENI SANA - Mama mtoto, wewe pamoja na wanafamilia wote.
Imani yenu kubwa kwa Uwezo wa Mungu itawajazeni subira.
 
Pole sana Mkuu, inauma sana lakini atuna jinsi, ametutangulia nasi tuko njiani. Poleni familia nzima.
 
Pole sana mkuu. Kazi ya Mungu haina makosa. Mungu Azidi kuwapa faraja yake ya kweli katika kipindi hiki. Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa, Jina la Bwana Lihimidiwe! Mungu Amlaze mpendwa mtoto mahali pema!
 
Pole sn Mkuu,mungu na akutie nguvu wakati huu!kwan naye ana mipango yake kwa kila jambo!jina lake libarikiwe.
 
hard to swallow, very hard...but it is a really..have strength bro...just remember the mother needs you now. poleni sana.
 
Back
Top Bottom