Nilimuombea Mama huyu apate mtoto wa kiume - amepata!

Nilimuombea Mama huyu apate mtoto wa kiume - amepata!

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,759
Reaction score
7,573
Wakuu, sikilizeni habari hii ya ajabu! Ni habari ya mama mmoja ambaye kila alipopata ujauzito, alizaa mtoto wa kike. Mara ya kwanza, mara ya pili, mara ya tatu - wote wa kike. Alifurahi kuwapata hao, na aliwalea kwa upendo. Hata hivyo moyoni alitamani apate na wa kiume.

Kwa imani, nilianza kumuombea. Yesu aliye hai alisikia maombi, mama huyo akapata ujauzito na kujifungua mtoto wa kiume! Sasa amejaa furaha na shangwe kuu.

Je, na wewe una hitaji hilo? Unahitaji mtoto wa kiume au wa kike na hujapata? Yesu hana upendeleo, anaweza kukutendea muujiza huo hata kama madaktari wamekuambia "haiwezekani." Kinachotakiwa tu ni wewe uombe kwa imani, bila mashaka, wala kusikiliza sauti zinazokukatisha tamaa.

Katika Yn 14:13-14 Yesu ameahidi akisema "nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya."

Tena anasema katika Yohana 16:24
"Hata sasa hamjaomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu."

Biblia ni kitabu cha kweli, na ahadi za Mungu zilizoandikwa katika kitabu hiki ni za kuaminika. Haleluya!!
 
Amepata tu, ila siyo kwa maombi yako, Siwa ma mtu anae beti akiweka Over au under, lazima upande mmja ushinde.
Binadamu tu pande mbili Me na Ke hivyo imeangukia ulikochagua.
Maombi kama hayo hata mimi naweza.
 
Kesho nenda Muhimbili mwaisela pale kuna watu wanataabika sana hebu waombee wapone watoke ile wodi iwe nyeupe kesho bila mgonjwa hata mmoja.
 
"Ni Wakati Sasa Wa Kujenga Hema,Mama Mchungaji La Setfree Assembly's Of GOD Tanzania(S.A.G.T)...Naamini Naweza Kuhudumu Kama Katibu Wa Kanisa..Roho Mtakatifu Akikuwia Vivyo...
 
Wakuu, sikilizeni habari hii ya ajabu! Ni habari ya mama mmoja ambaye kila alipopata ujauzito, alizaa mtoto wa kike. Mara ya kwanza, mara ya pili, mara ya tatu - wote wa kike. Alifurahi kuwapata hao, na aliwalea kwa upendo. Hata hivyo moyoni alitamani apate na wa kiume.

Kwa imani, nilianza kumuombea. Yesu aliye hai alisikia maombi, mama huyo akapata ujauzito na kujifungua mtoto wa kiume! Sasa amejaa furaha na shangwe kuu.

Je, na wewe una hitaji hilo? Unahitaji mtoto wa kiume au wa kike na hujapata? Yesu hana upendeleo, anaweza kukutendea muujiza huo hata kama madaktari wamekuambia "haiwezekani." Kinachotakiwa tu ni wewe uombe kwa imani, bila mashaka, wala kusikiliza sauti zinazokukatisha tamaa.

Katika Yn 14:13-14 Yesu ameahidi akisema "nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya."

Tena anasema katika Yohana 16:24
"Hata sasa hamjaomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu."

Biblia ni kitabu cha kweli, na ahadi za Mungu zilizoandikwa katika kitabu hiki ni za kuaminika. Haleluya!!
wadau wamesema ukaombee wagonjwa mahospitalini kama unaupako sana kenge wewe
 
Amepata tu, ila siyo kwa maombi yako, Siwa ma mtu anae beti akiweka Over au under, lazima upande mmja ushinde.
Binadamu tu pande mbili Me na Ke hivyo imeangukia ulikochagua.
Maombi kama hayo hata mimi naweza.
Wewe ni mgeni dunia hii? Hujui kwamba kuna waliojaribu kupata ama mtoto wa kiume au wa kike, wakashindwa, wakakata tamaa na kufunga uzazi? Mnakosa baraka kwa sababu ya kutoamini kwenu.
 
Acha UTAPELI wewe, jinsia kitu chenye 50% kutokea siyo kitu cha kufanyia maombi....
Kama una nguvu za hayo maombi yako twende tukasidie watu wanatafuta FIGO na MAINI.....
 
wadau wamesema ukaombee wagonjwa mahospitalini kama unaupako sana kenge wewe
Hasira za nini sasa. Unakasirika kusikia mwenzako amepata hitaji lake?
Mhubiri 7:9
Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
 
Nyie ndo wale mnasema mmeonyeshwa na Mungu kuwa jambo kubwa litatokea halafu mnafanya maombi na hilo jambo halotokei tena,,.,,,,, 😄 😄 😄 MATAPELI WAKUBWA...
 
Hasira za nini sasa. Unakasirika kusikia mwenzako amepata hitaji lake?
Mhubiri 7:9
Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
sawa nimekuelewa.

wadau wamesema uende mahospitalini ukaombee wagonjwa wapone tujuekua unaupako kweli.acha janjajanja
 
wadau wamesema ukaombee wagonjwa mahospitalini kama unaupako sana kenge wewe
Hivi wewe unafikiri watu wote hospitalini wana imani au wanamwamini Yesu? Miujiza haifanyiki kiholela. Ni mpaka ukubali kwamba Yesu anaweza kutenda miujiza. Hata Yesu alipokuwa duniani, kuna mahali alienda lakini hakutenda miujiza kwa sababu ya kutokuamini kwao.
Marko 6:5
Wala hakuweza kufanya mwujiza wowote huko, isipokuwa aliweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache, akawaponya. Akastaajabu kwa sababu ya kutoamini kwao.
 
Wewe ni mgeni dunia hii? Hujui kwamba kuna waliojaribu kupata ama mtoto wa kiume au wa kike, wakashindwa, wakakata tamaa na kufunga uzazi? Mnakosa baraka kwa sababu ya kutoamini kwenu.
Wewe ndiye mgeni, sasa maana mpaka leo, hujui tupo tusiamini unachoamini, na tunafanikiwa.
 
sawa nimekuelewa.

wadau wamesema uende mahospitalini ukaombee wagonjwa wapone tujuekua unaupako kweli.acha janjajanja
Kama unashindwa kuamini kwamba huyo mama amepata muujiza baada ya kuombewa, hata wakipona wagonjwa elfu utapinga tu. Wewe sio wa kwanza kupinga.
 
Back
Top Bottom