Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Sheria zilizopitishwa nyakati za Mzee Vijisenti, zinagusa wanyonge na Tsh elfu tatu hata nauli ya taxi kufika Posta toka pale Kamata haitoshi. Vyombo vinavyohusika vinanyanyasa wananchi mfano halisi ni kwa hili.
 
invisible hujakosea,jamaa wanavitambi kama vipipa.Halafu hawa jamaa wa usalama wa barabarani wamezidi,sometimes mpaka tzs 1000 wanachukua.We barabara ambazo wao wapo umbali si mkubwa utakuta benk zao"wapiga kiwi,washona viatu nk"Acha tu watiwe adabu
 
Ile kauli ya ku-deal na rushwa uchwara ndio naithibitisha hapa nadhani hata huyo hakimu atakayemhukumu huyo askari kwa rushwa hiyo pamoja na huyo mpelelezi kweli kama watarudi majumbani mwao wakajisifu kuwa wamefanya kazi sio siri nitakuwa na mashaka sana utendaji wao...Jamani hii nchi ina wala rushwa wakubwa wanaotisha na ambao wangeweza kuwa-keep busy hao wapelelezi na mahakimu mpaka waombe likizo.

Lakini watu wanawakimbia wala rushwa wanakamata mtu eti kapoke 3,000 kabisa na imekuwa news kwenye gazeti acheni utani na kazi nyie watu. Hivi kwenye 1,200,000,000,000 za Chenge kuna 3,000 ngapi kwani wasimuweke chini ya ulinzi chenge na hizo 3,000 nyingi kabisa??, what about, Mkapa, Mgonja, Mramba, Karamagi, Msabaha, EL na wengine wengi tu wameiba 3,000 ngapi??? Let's be serious you people...
 
hahahaa hapo pccb ndio wanapowaweza sana sana watendaji wadogo...ma king fish haaaa wanawaundia tume......pccb iwe wazi kwamba uwezo wao mwisho ni.....maafisa wilayani..tuu si zaidi.....jamani wana JF pccb wilayani wanaogopewa mnoooo......lakini si kwa mafisadi...
 
Posted Date::6/16/2008
Serikali yakiri kukithiri kwa rushwa katika safu zake
Na Kizitto Noya
Mwananchi

KATIBU Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo amesema kuwa rushwa, urasimu na ucheleweshwaji wa huduma kwa wananchi bado ni tatizo linaloikabili serikali kupitia taasisi zake.

Akizindua wiki ya Utumishi wa Umma jijini Dar es Salaam jana, Luhanjo alikemea vitendo hivyo na kuwataka watumishi wa taasisi za umma kubadili fikra na kuanza kuwahudumia wananchi kama wafalme.

Alisema mwananchi ni mfalme kwa kuwa ndiye anayewaajiri watumishi wa umma kupitia kodi yake hivyo watumishi wana wajibu wa kumpa huduma bila vikwazo wala ukiritimba.

''Malalamiko mengi ya wananchi yanaonyesha kwamba matatizo ya rushwa, urasimu na ucheleweshaji wa huduma na kutokuwa wasikivu katika kuwahudumia wananchi bado yapo na kwamba watumishi wa umma wanatakiwa kubadilika kifikra,'' alisema Luhanjo.

Alisema taasisi za umma ikiwamo Wizara, idara zinazojitegemea, wakala wa serikali, mikoa na wilaya zinatakiwa kutekeleza mikataba ya Huduma kwa Wateja na kuelimisha watumishi wake kuwa wasikivu wanapowahudumia wananchi.

''Watumishi wanatakiwa kuwaheshimu wananchi na wawatendee haki. Ni lazima kila mtumishi wa umma arudishe fadhila kwa wananchi wanaotulipia mishahara kupitia kodi zao, kwa kutoa huduma bora na wananchi ataridhika na fedha yake,'' alisema

Alisema kwa upande wake serikali imeanzisha kamati maalum za maadili katika kila wizara na mkoa nchini, kwa lengo la kufuatilia utendaji kazi wa taasisi za umma na kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma zinazostahili.

Katika kuendelea utamaduni huo, Luhanjo amezitaka taasisi zinazoshiriki maonyesho ya wiki ya utumishi wa umma, kukusanya maoni ya wateja na kuyapeleka kwake kabla ya mwisho wa mwezi wa Septemba, ili yafanyiwe kazi.

Alitoa wito kwa wananchi kutembelea maonyesho hayo na kutoa kero zao ili kuwapa fursa watumishi wa taasisi husika kuzifanyia kazi.
 
Uzuri wa siasa ndio huo,unabwabwaja basi siku imeingia unasubiri mafao.wakuu wengi wameshakiri hali hiyo mara kibao,hamna kitu.Maneno hayo yametuchosha tunataka vitendo,WaTZ wamechoka jamani na taralila zenu.
 
Posted Date::6/16/2008
Serikali yakiri kukithiri kwa rushwa katika safu zake
Na Kizitto Noya
Mwananchi

KATIBU Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo amesema kuwa rushwa, urasimu na ucheleweshwaji wa huduma kwa wananchi bado ni tatizo linaloikabili serikali kupitia taasisi zake.


Alisema mwananchi ni mfalme kwa kuwa ndiye anayewaajiri watumishi wa umma kupitia kodi yake hivyo watumishi wana wajibu wa kumpa huduma bila vikwazo wala ukiritimba.
''Malalamiko mengi ya wananchi yanaonyesha kwamba matatizo ya rushwa, urasimu na ucheleweshaji wa huduma na kutokuwa wasikivu katika kuwahudumia wananchi bado yapo na kwamba watumishi wa umma wanatakiwa kubadilika kifikra,'' alisema Luhanjo.

Rhetorics at its its best!!
Tangia lini mwananchi - nchi hii akawa mfalme??????
A lot needs to be done to reverse the trend maana viongozi ndio wafalme hata kama wameajiriwa na wananchi/walipa kodi
 
Mkuu wa Kituo Polisi mbaroni kwa rushwa

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Singida, inawashikilia watu wawili akiwamo Mkuu wa Kituo cha Polisi Ikungi kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh 30,000.

Wanaoshikiliwa na Takukuru ni Mkuu wa Kituo hicho, Sajini Bernard Mkinga na Mgambo Mwandamizi wa Kituo hicho, Venance Amasi. Kituo cha Ikungi kipo Wilaya ya Singida Vijijini.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Takukuru mkoani Singida, Daniel Pundu, tukio hilo lilitokea Agosti 15, mwaka huu majira ya jioni katika kituo cha magari cha Ikungi.
Kukamatwa kwa watuhumiwa hao kulitokana na mtego uliowekwa na maofisa wa Takukuru baada ya kubaini kuwapo kwa dalili za rushwa ili kupindisha sheria dhidi ya kesi moja iliyokuwapo kituoni hapo.

Alisema kesi hiyo ilikuwa ikumhusu mkazi mmoja wa Kijiji cha Kipumbuiko aitwaye, Damas Msuta, ambaye alifunguliwa shitaka la kuchoma moto nyumba ya Nicolus Nyasi.

Pundu alisema baada ya mshitakiwa kufunguliwa kesi juu ya tuhuma hizo, watuhumiwa walianza kumshawishi atoe rushwa ya Sh 50,000 ili shitaka lifutwe. Alisema baadaye Damas alimpa Mkuu huyo wa Kituo Sh 20,000 malipo ya awali ambazo wakati akipokea watu waliona tukio hilo.

Alisema wakati Mkuu huyo wa Kituo akipewa Sh 20,000, siku hiyo pia mgambo naye alipewa Sh 10,000 ambazo inadaiwa zinatokana na kazi yake nzuri ya kumuunganisha Damas na Mkuu wa Kituo.

Pundu alisema askari huyo alitumia mbinu ya kumtuma mgambo wao, Venance akampokelee fedha hizo Sh 30,000 na ambaye muda mfupi baada ya kupokea na kuziingiza kwenye mfuko wake wa suruali, maofisa wa Takukuru walimkamata na katika purukushani hizo, alizitupa chini hizo fedha.

Hata hivyo, alisema Takukuru inao ushahidi kuwa Sajini Mkinga ndiye mwomba rushwa hiyo ya Sh 30,000 na ndio maana wameunganishwa pamoja katika shitaka hilo. Alisema watuhumiwa watapandishwa kizimbani wakati wowote wiki hii ili kujibu shitaka linalowakabili.
 
....hakuna cha dagaa wala papa hapo kama wamekula rushwa kamata na sheria ifanye kazi yake,na hawa dagaa wapenda rushwa ndio wasumbufu sana na wanafanya hata maendeleo yarudi nyuma kwa vitabia kama hivi....utakuta mbeba faili anataka rushwa la sivyo analificha na kila kitu kinakwama then unamwita kidagaa kumbe kakwamisha kila kitu.
 
Nguvu inayotumika katika rushwa hizi ndogo, basi itumike vile vile kwa rushwa kubwa.
 
Mkuu wa Kituo Polisi mbaroni kwa rushwa
Hudson Kazonta, Singida
Daily News; Tuesday,September 02, 2008 @20:12

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Singida, inawashikilia watu wawili akiwamo Mkuu wa Kituo cha Polisi Ikungi kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh 30,000.

Wanaoshikiliwa na Takukuru ni Mkuu wa Kituo hicho, Sajini Bernard Mkinga na Mgambo Mwandamizi wa Kituo hicho, Venance Amasi. Kituo cha Ikungi kipo Wilaya ya Singida Vijijini.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Takukuru mkoani Singida, Daniel Pundu, tukio hilo lilitokea Agosti 15, mwaka huu majira ya jioni katika kituo cha magari cha Ikungi.
Kukamatwa kwa watuhumiwa hao kulitokana na mtego uliowekwa na maofisa wa Takukuru baada ya kubaini kuwapo kwa dalili za rushwa ili kupindisha sheria dhidi ya kesi moja iliyokuwapo kituoni hapo.

Alisema kesi hiyo ilikuwa ikumhusu mkazi mmoja wa Kijiji cha Kipumbuiko aitwaye, Damas Msuta, ambaye alifunguliwa shitaka la kuchoma moto nyumba ya Nicolus Nyasi.

Pundu alisema baada ya mshitakiwa kufunguliwa kesi juu ya tuhuma hizo, watuhumiwa walianza kumshawishi atoe rushwa ya Sh 50,000 ili shitaka lifutwe. Alisema baadaye Damas alimpa Mkuu huyo wa Kituo Sh 20,000 malipo ya awali ambazo wakati akipokea watu waliona tukio hilo.

Alisema wakati Mkuu huyo wa Kituo akipewa Sh 20,000, siku hiyo pia mgambo naye alipewa Sh 10,000 ambazo inadaiwa zinatokana na kazi yake nzuri ya kumuunganisha Damas na Mkuu wa Kituo.

Pundu alisema askari huyo alitumia mbinu ya kumtuma mgambo wao, Venance akampokelee fedha hizo Sh 30,000 na ambaye muda mfupi baada ya kupokea na kuziingiza kwenye mfuko wake wa suruali, maofisa wa Takukuru walimkamata na katika purukushani hizo, alizitupa chini hizo fedha.

Hata hivyo, alisema Takukuru inao ushahidi kuwa Sajini Mkinga ndiye mwomba rushwa hiyo ya Sh 30,000 na ndio maana wameunganishwa pamoja katika shitaka hilo. Alisema watuhumiwa watapandishwa kizimbani wakati wowote wiki hii ili kujibu shitaka linalowak
 
Nilishasema hatuna polisi tuna majambazi hayo sasa!!!!!
 
Ukiongelea uchumi wa nchi, Maendeleo, Umaskini, Rushwa, Ufisadi ktk nchi hauwezi tenganisha na CCM

CCM = Maendeleo tuliyo nayo
CCM = Umaskini tulionao
CCM = Elimu duni tuliyo nayo
CCM = Ufisadi unatutafuna
CCM = Rushwa /Takrima inayotafuna nchi

Kwa mtizamo wa haraka, ufisadi ulianzia kwenye SU, PSRC, Procumrement na sasa wamehamia kwenye hazina yetu BOT

JE CCM YAWEZA KUJITENGA NA HAYA NAOMBA MWONGOZO WANA JF
 
Bill

hakuna namna CCM itajitenga na uozo wa nchi. Sababu kubwa ni kuwa ili CCM idumu inalazimika kukumbatia rushwa na ufisadi. Na popote kwenye rushwa na ufisadi lazima umasikini uwakumbe walalahoi.
Kwa hiyo hesabu hii ni rahisi sana: Ni kama 2 + 2 = 4
 
CCM haiwezi kukwepa lawama kwamba matatizo haya ya kutisha ambayo nchi yetu inapitia kwa sasa ni matunda yake.Ni akili za kifisadi tu ndizo zinazoweza kukataa ukweli huo.
 
Takukuru iieleze jamii namna inavyoshughulikia rushwa kubwa
Gloria Tesha
Daily News; Thursday,September 25, 2008 @20:00

HIVI karibuni, Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hosea alizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam na kusema kuwa kazi ya kupambana na rushwa ni ngumu na inahitaji uangalifu mkubwa.

Pia alisema hakuna faida ya kuwa fisadi wakati unamchunguza fisadi kutokana na tuhuma mbalimbali alizozipata kupitia vyombo vya habari, kwamba yeye ni fisadi.

Maneno hayo aliyasema baada ya kuulizwa maswali na waandishi hao wakitaka kujua kazi alizozifanya katika kipindi cha miaka miwili cha ukurugenzi katika chombo hicho na namna anavyoshughulikia kesi kubwa za rushwa.

Aidha, wakati akitoa ufafanuzi wa maswali hayo pamoja na mengine mengi, Hosea alisema jamii inashindwa kuelewa kuwa sheria haibagui rushwa ndogo na kubwa, bali rushwa ni rushwa mbele ya sheria isipokuwa tofauti inakuwapo katika namna uchunguzi unavyofanyika na hatua zinavyochukuliwa.

Namna mkurugenzi huyo alivyofafanua kuhusu uchunguzi wa kesi kubwa za rushwa unavyofanyika, ikiwa ni pamoja na muda wa kukamilika, ni dhahiri kwamba mafanikio ya kushughulikia kesi kubwa tano kati ya 10 zilizopangwa kuchunguzwa na Takukuru kwa mwaka ni ya kujivunia.

Nikinukuu maneno ya Dk. Hosea, kesi hizo ambazo hakuwa tayari kuzitaja, zipo kwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DPP) na mbili kati yake zimerudishwa Takukuru kwa ajili ya marekebisho madogo, kesi hizo zinahusu rushwa katika mikataba ya madini, kutumia mamlaka vibaya na kushindwa kusimamia sheria.

Pamoja na mafanikio hayo yaliyoelezwa na Dk. Hosea bado elimu na uwazi zaidi kuhusu namna kesi hizo zinavyoshughulikiwa unahitajika kwa jamii.

Ule ufafanuzi kwa wanahabari wale kuwa kesi za rushwa kubwa zinaitwa kubwa kutokana na kuvuka mipaka ya nchi, suala husika kupigiwa kelele sana katika jamii pamoja na kumhusu mtu maarufu na endapo imehusisha kiwango kikubwa cha fedha na inaangaliwa namna ilivyoathiri uchumi wa nchi, hautoshi, kwa suala hilo kueleweka kwa jamii.

Nadhani somo alilolitoa Hosea linahitajika kwa jamii nzima, siyo wakati wa kusubiri kuandikwa katika vyombo vya habari ndiyo kutoa ufafanuzi wa namna kesi hizo zinavyoshughulikiwa, ni wazi kama utaratibu wa kuwaelimisha watu namna wanavyoshughulikia kesi hizo wangeutoa mapema, jamii isingekuwa na sababu ya kudhani mafisadi hawashughulikiwi.

Muda wa kutafuta vielelezo na kujiridhisha kwamba kuna kesi ya kupeleka mahakamani ni wazi unahitajika, lakini pia ikumbukwe kuwa jamii inapaswa kuelewa hatua zinazochukuliwa ili kuepuka kudhaniwa visivyo, mambo haya yaende pamoja.

Sipingani na alichosema mkurugenzi wa Takukuru, kwamba upo ugumu wa kushughulikia masuala ya rushwa hata kufikia wanaoshughulika kudhaniwa kuwa nao ni mafisadi, kwa kuwa mafanikio hayaonekani mapema.

Malalamiko ya wengi ni kwamba Sheria ya Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007 katika vifungu vyake bado inabana, lakini kama akina Zephania Musendo walidaiwa kubainika, vipi hayo mapapa?

Ni wakati sasa umefika kwa Takukuru pamoja na kauli nzuri kwamba kuna faida gani ya kuwa fisadi wakati unachunguza mafisadi, wakimaanisha kwamba wao siyo mafisadi, ionekane kwa vitendo. Watanzania wanatamani kuona na kusikia wanaoliingizia taifa hili hasara wanafikishwa mahakamani na wanashughulikiwa ipasavyo. Kila la heri Takukuru.
 
Huyu Fisadi Edward Hosea kazi imeshamshinda, hatuhitaji maelezo yoyote toka kwake bali kumfukuza kazi kwa manufaa ya umma. Kuna ushahidi wa kutosha kwamba pamoja na ufisadi mzito unaendelea ndani ya serikali na chama cha mafisadi mpaka hii leo hajamkamata yoyote au hata kumfungulia mashtaka kwa visingizio mbali mbali ambavyo havina kichwa wala miguu. Kama mtakumbuka kamati ya richmond ilipendekeza huyu fisadi afukuzwe kazi siku nyingi. Cha kushangaza msanii Kikwete pamoja na kuunda tume ya richmond ambayo ilitumia mabilioni ya shilingi katika uchunguzi wake mapendekezo mengi ya kamati hiyo bado hayajafanyiwa kazi.
 
Kila kukicha Tanzania imekuwa ikirudi kinyumenyume matokeo sasa imekuwa ni nchi inayotia aibu mbele ya macho ya watu wa duniani na pia wa mbinguni imekuwa ni desturi ya kila mtawala anayeomba kuitawala nchi hii kuwahadaa wananchi ktk kipindi cha uchaguzi na baada ya wananchi kupumbazika na kumchagua huwageuka na kufanya mambo yasiwapendeza wananchi na Mungu pia, Tatizo kubwa linalowakumba watawala ni tamaa, baada ya kuingia madarakani hubadilika kabisa,na kinachowabadilisha tabia kutoka utu waliokuwa nao na kugeuka wanyama ni RUSHWA. Hiki ni kitu kibaya sana huwa wanasahau kuwa Mungu ndiye apangaye mambo yote ya humu duniani na ndiye msimamizi, huchukua rushwa kwa siri wakifikiri wamewaibia wananchi kumbe Mungu anawaona, matokeo yake hujikuta wamepoteza heshima ndani ya jamii pasipo kuelewa ni kwanini hata kabla ya mwisho wa utawala wao.na mwisho wa utawala wao huishia kuishi maisha ya wasi wasi yasiyo na chembe ya furaha wao, na familia zao na hii imetokea na hii kila mmoja ameishuhudia Kuna mifano mingi ila hii hapa ni michache Nani angejua leo hii mtu mkubwa kama BWM angeishi maisha ya wasi wasi na yasiyo na amani namna hii maana yeye kila kukicha anajificha,je?maisha ya EL kwa sasa yana tofauti gani na ya mmachinga anayetembeza vitu barabarani akihofia kukumbana na askari wa jiji? vipi kuhusu Karamagi,Chenge na wengine wengi ambao kwa sasa hawawezi kujitokeza hadharani kama raia wema. Wote wanaojificha pengine hakuna mtu mwenye shida nao ila tu kwa kuwa roho zao zinawasuta basi wanajikuta mafichoni bila kutafutwa.na hii ndiyo kazi ya Mungu maana imeandikwa lililofungwa duniani na mbinguni pia limefungwa na pia likishafungwa mbinguni na duniani pia.Hayo yote yanasababishwa na kitu kimoja tu TAMAA YA RUSHWA. Sasa basi nijuavyo mimi kuna magonjwa mengi ya hatari yasiyotibika na RUSHWA ni mojawapo ya ugonjwa mmbaya sana usiotibika lakini pia unaambukiza kirahisi sana. DAWA ya huu ugonjwa ni kumpata kiongozi atakayeweza kuutokomeza huu ugonjwa mbaya unaoteketeza jamii yetu kila uchao.Na anachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kila aliyeambukizwa huu ugonjwa ni lazima AUWAWE, RUSHWA ni sawa na KICHAA CHA MBWA KTK TANZANIA na dawa yake ni kuua mbwa wote wenye kichaa hiki maana ukiwaacha wataambukiza wengine kila siku na tutazidi kudidimia.
 
maneno haya yamekuwa ya maana sana lakini wameyatupa pembeni na kuyasigina.

Rushwa ni adui wa haki sinta toa rushwa wala kupoke rushwa.
both ways kwako mwanchi na kwa mtaawala.

Cheo ni dhamana sintu tumia cheo changu kwa faida yangu wala ya mtu yeyote.
Wametumia vyeo kujineemesha na kuneemesha wawakezaji na wachukua tenda.

Bidadamu wote ni sawa.
Tanzania binadamu sio sawa waheshimiwa hawapajui muhimbili ndio maana hawa jali. Wakipelekwa keko wanatoka haraka, rufaa zao ni fast truck.

Nitatumia elimu yangu kwa manufaa ya umma.
Elimu hutumika kuibia na kulaghai wananchi.

Damu ya weusi Afrika ya kusini iliwapa uhuru wa kiuchumi na kifikra, damu ya mtanzania italeta usawa mbele ya sheria.
 
Back
Top Bottom