Saharavoice
JF-Expert Member
- Aug 30, 2007
- 4,057
- 2,637
Hivi awamu ya kwanza ilipopambana na rushwa na kufanikiwa kwa kiwango cha juu wafadhili walishirikishwa?
Ndugu zangu kwa bahati mbaya tuliibahatika kuwa na kaka mhalifu,,yeye alikuwa anaitwa EDGAR,natumainibwana CHICO
anawatambua walikuwa wazee wa kazi,,,huyu kaka yetu ametusumbua sana sana ,,na wengine,,walinaki maskini,,katika kesi hii huyu mama yetu lyamuya aliisimamia,,jamani mimi nilisema tunajitahdi kumtoa lakini ikishindikana tumwache aishie uko,,,hakuna ambae hakula hela ya famili kuanzia mfagizi,wale wa mafaili jamanijamani huko ndio akufai,,faili alionekane kesi imesomwa wiki 2 zilizopita,,pesa anpelekewa watu wa usafi,,au police wa kawaida,,tuliangaishwa faili alionekani huku mheshimiwa,na ma pp wake kila hela unayopeleka anchukua kesho yake waambiwa wenzake hawaridhika,,,,hili naongelea labda sababu tulipata kiuwezo cha kutoa hela,,je huyu mlalahoi wa kawaida anapata wapi hela ya kumpa pp+hakim+mtunza mafaili,,,,
Nilikuwa mmoja wa watu wenye fuuraha sana kusikia hii habari,nasikitika kuona kwenye gazeti leo mkuu wa mahakimu anadai hakuna rushwa kabisa,,ndugu hosea uko unapoenda kukagua rushwa unatafuta dhambi za millele,,nenda au tuma watu wako waende pale kisutu,natumaini uutaahamisha ofisi yako pale kwa idadi ya watu utakaopata,,,,naomba waziri husika wa sheria afwatile hili swala ndugu zangu huu ni mwaka wa haki zetu,tutafute hata kwa kukesha
Source link: HabariLeo.Vigogo wagombea mgawo wa rushwa
Frank Leonard, Iringa
HabariLeo; Tuesday,December 18, 2007 @00:02
WAKURUGENZI wa Halmashauri tatu za Mkoa wa Iringa, wahandisi na wenyeviti wa halmashauri hizo, wanadaiwa kugombea mgawo wa rushwa unaotokana na miradi ya barabara, hivyo kusababisha kazi nyingi za miradi hiyo kukwama. Inadaiwa ugomvi huo unatokana na wakati mwingine rushwa inayotolewa kuonekana haitoshi kwa kuzidiana ujanja; ameibainisha Mkuu wa Mkoa huo, Amina Mrisho.
Pamoja na kuzionya halmashauri hizo, Mkuu huyo wa mkoa ameionya Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) mkoani hapa kwa kudaiwa kuchelewesha utoaji wa zabuni kwa misingi hiyo hiyo ya mpaka wapewe rushwa.
Mrisho alitoa onyo hilo wakati akifunga kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Iringa kilichofanyika jana katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa. Bila kuzitaja halmashauri hizo, alisema viongozi hao wala rushwa wanajivunjia heshima pamoja na kupunguza ufanisi wa miradi ya barabara.
Kazi nyingi katika halmashauri hizo zinakwama kwa sababu ya rushwa. Viongozi hao wa halmashauri hizo wanagombana kwa sababu rushwa wanayopewa wakati mwingine inaonekana haitoshi kwa kuzidiana ujanja, alisema Mkuu wa mkoa. Nawataka mjirekebishe mara moja vinginevyo nitawaumbua na kuwachukulia hatua kali za kisheria, aliongeza.
Wakati huo huo, Meneja wa Tanroads Mkoa wa Iringa, Paulo Lyakurwa amewataka wananchi wasaidie kutoa taarifa ya makandarasi wanaokiuka taratibu za ujenzi ili kuongeza ufanisi katika kazi. Pamoja na ombi hilo, amesema wilaya ya Makete na Ludewa zinakabiliwa na tatizo la makandarasi. Wilaya ya Ludewa ina mkandarasi mmoja tu huku ya Makete ikiwa haina mkandarasi hata mmoja, alisema.
Alisema kujitokeza kwa makandarasi hao kutarahisisha utekelezaji wa miradi ya ujenzi hususani katika ngazi ya wilaya ambayo imekuwa ikijengwa na makandarasi kutoka nje ya wilaya hizo. (mwisho) Maalbino kumuona JK kupinga mauaji Na Theopista Nsanzugwanko CHAMA cha Maalbino Tanzania (TAS) kinatarajia kufanya maandamano ya amani kumuona Rais Jakaya Kikwete, kwa ajili kuitaka serikali kuunda tume maalumu ya kushughulikia mauaji ya maalbino nchini.
Maandamano hayo yatakayokwenda sambamba na kongamano kubwa la kujadili suala hilo, yatafanyika Januari mwakani na yatamalizikia Ikulu, Dar es Salaam na kupokelewa na Rais. Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara Habari (MAELEZO), Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa chama hicho, Ernest Kimaya, alisema wamechukua hatua hiyo baada ya kuona hakuna jitihada zozote zinazofanywa na serikali za kukabiliana na vitendo vinavyoendelea vya kuwaua maalbino na kufukua makaburi yao, ambavyo vinatokea katika mikoa ya Kanda ya Ziwa na Arusha.
Alisema pia wako katika maandalizi ya kukutana na mamlaka zinazohusika zinazoshughulikia masuala ya haki za binadamu kama Wizara ya Usalama wa Raia, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ili kuona namna bora ya haraka ya kukomesha mauaji ya dhuluma yanayofanywa dhidi ya watu hao.
Alisema suala la mauaji hayo ni kipaumbele kama yalivyo matukio mengine, kwani muda si mrefu lilikuwapo tukio la utata wa upasuaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ambalo serikali ililazimika kuunda tume ya kuchunguza suala hilo na tukio lililotokea Hospitali ya Maswa ya kufariki mtoto wa miaka saba kwa kukosa Sh 12,000, imeundwa Tume.
Alisema licha ya watu wanne ambao ni albino kutoka mikoa ya Arusha, Mara na Mwanza, kuripotiwa kuuawa kinyama na wazazi wao au majangili wa binadamu na baadhi ya makaburi kufukuliwa, hakuna hatua yo yote iliyochukuliwa zaidi ya kuliwazwa kwa kisingizio wameuawa kwa imani za kishirikina.
Kwetu sisi tunaamini kwamba huu ni uvunjaji mkubwa wa haki za binadamu huku dola ikionyesha udhaifu mkubwa kulinda raia zake na kutufanya tuishi kwenye mazingira ya mashaka huku tukiamini kama si leo, basi kesho arobaini zangu zitafika; hivyo kuamini kwamba dola linatutoa kafara, alidai.
Alisema maamuzi hayo yamekuja baada ya chama hicho kwa kushirikiana na wadau wengine kufanya warsha ya siku mbili Desemba 10 na 11, kwa madhumuni ya kujadili hali ya kuzorota kwa usalama wa maisha ya jamii ya maalbino nchini kutokana na mauaji ya mfululizo yanayofanywa dhidi yao.
Msemaji wa Jeshi la Polisi, Esaka Mugasa, akizungumzia suala hilo, alisema Polisi haiwezi kupuuzia suala lolote linalohusu mauaji, hivyo mauaji ya maalbino yanafahamika katika jeshi hilo na yanaendelea na upelelezi ili kupata ushahidi utakazowawezesha kuwafikisha mahakamani wahusika wa matukio hayo.