Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

FMES,

Rushwa haishi, hata tukirogana.

Katika nchi za Afrika Mashariki, ni Tanzania peke yake, yenye mishahara mizuri.

Tunaweza kujifunza mengi kutoka kwa Waganda!(alternatively)

Rushwa inahitajika kupigwa vita. Period.
 
- Mkuu ninakusikia, lakini mifano ipo bongo siku hizi masirika ya wageni huwezi pata mtu wa kula rushwa maana mishahara ni safi hakuna aliye-willing ku-take the risk,

- Ila thanks kwa elimu ya bure kuwa bongo ndio tunaongoza kwa mishahara minono, sikujua hilo lakini nafikiri basi haitoshi bado kukidhi maisha ya wananchi hasa kwa wafanyakazi wa serikali, maana wakianza kugombea safari huwa ni huruma sana mkuu.
 
waasisi walisema ukishaondoa 'mirija', utaondoa rushwa.

mimi naamini rushwa yaweza punguzwa tu, haitaweza fishwa milele. mfano; Iwapo kila mtanzania angekuwa na ufahamu wa haki zake za uraia, na watendaji wa serikali wakazisimamia, rushwa ingepungua.

wananchi wengi wamekata tamaa na kulemazwa na kutaka mambo kwa njia za mkato, hata inafikia mfano; mgombea kutamka wazi wazi eti "mkinichagua nitawaletea maji, barabara nk" na wananchi wanaamini na kuendelea kusubiria ahadi hiyo kila baada ya miaka mitano, ebo!?...

imekuwa kana kwamba kupatiwa maji safi na barabara si haki yetu!
 
- Hela ya mishahara wanayolipwa ni ndogo sana, infact hawako mbali sana na wabunge kwa mishahara, wao hutegemea safari hasa za nje, ndio maana wanakuwa mstari wa mbele kupora haraka haraka wakipewa tu!

Wananchi wanaolipwa vizuri kulingana na hali ya maisha, hawawezi kutaka wala kushirki kwenye rushwa.
Mkuu, Rushwa is such a dynamic issue in its own measures. one can only control it but not stop it completely.
Hata huko Stan.Chart,Aga Khan, you name it kuna hongo za aina yake mkuu!!-najua kuwa unakijua hilo!!
 
Ili kupunguza na hatimae kuondoa kabisa rushwa, ni vema kwa Watanzania wachukie shortcut.. Kama kupata kibali cha ujenzi inachukua miezi mitatu, na kabla ya kupata kibali hicho unatakiwa uwe na nini... ukijua vyote hivyo na kukamilisha taratibu zote bila ya kupenda shortcut sidhani kama utadaiwa rushwa ama kushawishika kutoa rushwa.

Ili kupata driving license unatakiwa ujifunze gari kwa miezi mingapi, unatakiwa upasi majaribio mangapi? Kwa nini usijifunze kwa muda uliopangiwa ili kuepuka kutoa ama kudaiwa rushwa?

Machinga unajua fika kuwa eneo fulani hapana ruhusa ya kufanya biashara ndogondogo, lakini kwa kuwa unapenda njia za mkato unapeleka biashara zako huko kwa kutegemea kutoa rushwa..

Ipo mifano mingi ya kupenda kutofuata taratibu na kupenda kupata kila kitu hapo hapo ambapo inachangia kwa kiasi kikubwa utoaji na upokeaji rushwa.

Kwa serikali ni vema kuweka sheria wazi na taratibu zote katika kupata huduma wazi ili wananchi wawe na ufahamu mpana kuhusu taratibu hizo. Hii kwa kiasi fulani itasaidia kuondokana ama kupunguza rushwa.
 
Leo katika kipindi cha Tuongee Asubuhi cha Star TV Mkuu wa Usalama Barabarani Kamanda Kombe amesikika akisema Askari wake hawapokei rushwa, lakini kwa wale mfano Askari polisi wa usalama barabarani wanaoshinda ubungo tangu saa 3 asubuhi mpaka usiku kuna ubaya gani wakipokea maziwa kutoka kwa Azam. Akasema kuna ubaya gani wa kampuni kama Azam kuwapelekea maziwa?

Lakini hapo hapo akasema jeshi la Polisi linawaadabisha trafiki wala rushwa. Hivi hii maana yake nini, upande mwingine anapinga rushwa na mkono mwingine anahalalisha, au ndiyo Bongo style katika vita dhidi ya ufisadi.

Ila huyu Mzee simjui vema mwema profile yake naomba, maana anaonekana hastahili kuwapo alipo.
 
Hili ni tatizo la KITAIFA; watu wasiostahili kuwapo katika nafasi fulani ndiyo unawakuta.

Katika maeneo mengi ya serikali kutoa huduma kujuwana ndiko kunatawala katika kupeana nafasi no transparency in allocating\recruiting staff in most of governments departments\institutions.

Kubwa bado tunafanya kazi kwa mazoea na ubabaishaji, siyo kwamba nchi hii haina watu qualified and competative, ila there is no proper set mechanism ya allocation of our human resources.

kwa hilo wachache wanatumia mwanya huo kujifanyia watakavyo, na kwa vile pia hakuna watch-dog setup; then ni midudu juu ya midudu.

yule jamaa wa traffic anastahili kuongoza kituo kidogo cha police kama kule CHARAMBE na si zaidi ya hapo.

bado kwa mwendo huu tuna safari ndefu SAAAAAAAAAAAAAAAAAANA!!
 
Jana usiku ITV ilirusa kipindi maalumu cha Mheshimiwa Lembeni Mbunge wa Kahama akikabidhi hundi ya sh. 100,000,000.00 ambayo ilitolewa na Mwenkikiti wa Makampuni ya IPP Bwana Reginald Mengi kwa VIKOBA Kahama. Sina shida na uchangiaji wa Bwana Mengi, bali ni staili iliyotumika katika kuikabidhi hundi hiyo kwa walengwa. Kipindi hicho kilionyeshwa Mh. Lembeni akianza kwa maelezo sifa, vijembe, sifa na shukrani kwa makundi na watu tofauti ambao aliwahusisha na VIKOBA. Moja wapo ya maneno aliyoyasema ni kwamba hataacha kusaidia VIKOBA hata kama atakuwa siyo Mbunge wa Kahama.

Baada ya Mh. Lembeni kumaliza ya kwake, alifuatiwa na Nape Mnauye ambaye ni Mjumbe wa NEC na kwenye tukio hilo alikuwa mgeni rasmi. Na hapa ndipo mimi nilipoanza kukwazika. Miongozi mwa maneno ya Bwana Nape ambayo aliyasema na mimi kunikwaza hi haya; Katika NEC moja wapo ya mambo ambayo tumekubaliana ni kwamba Mbunge anayetekeleza ilani ya CCM kwa vitendo, anatufaa kwa uchaguzi wa mwaka 2010, na Mh. Lembeli kwa tukio hili anatekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM, hivyo anatufaa kwa uchaguzi wa 2010. Sawa wadau haya mazingira siyo ya kutoa rushwa? Mh. Lembeli amekabidhi hundi ya sh 100,000,000.00 kwa VIKOBA, halafu inafuatiwa na yeye kufagiliwa kuwa anafaa kuwa Mbunge tena wa Kahama, mnaonaje hapo?

Lakini jingine ninalojiuliza Bwana Mengi atatoa sh. 100,000,000.00 kwa wabunge wangapi katika kutekeleza ilani ya uchaguzi wa CCM?

Naliweka jamvi wazi kwa mjadala
 
siyo rushwa....unadhani wangetumia neno gani zaidi zuri la kumshukuru kama kawasaidia katika shida na uhitaji wao? walimchagua kuwasaidia na kafanya hivyo....sioni shida wakimwambia unawafaa na watamchagua tena
 
Hiyo wala rushwa kabisa, alikuwa anatekeleza wajibu wake kama mwakilishi wa wananchi. Wanaotoa rushwa huwaoni????? Mara, ooo wanaenda gawa mipira, mara khanga, mara tshirt, yaani token things halafu wanajifagilia kwa kwenda mbele. Lembeni endelea wala usivunjike moyo. Tunaonamba matajiri wengine wasiokumbatia ufisadi wawapige tafu Selelei, Mwakyembe, Ane Kilango, Ole Sendeka, Manyanya etc!!!!
 
Hivi vitu vinafanyika dunia nzima, wala si rushwa.

Tena bora ata kama angefanya kisiri siri ungeweza kuhoji, vitu vimefanyika publicly? Where is the beef?
 
Mkuu Kichankuli!

Ati rushwa? Hapana bana! Kila Mbunge anawajibaka kusaidia wale waliomchangua kwa njia yoyote hile halali inayowezekana - na hii ni halali - Unatafuta watu wenye uwezo wa kipesa (kama RM au hata RA) unawapa propozo ya jinsi unavyotaka kuwasaidia wapiga-kura wako na ni jinsi gani ungependa wao wajisaidia kutokana na msaada unaoweza kupata and then unawa-mobilize kuwa na vikundi vinavyokopesheka (VIKOBA in this case).

Baada ya hapo unatafuta watu wanaojua kuandaa matamasha (Prime Time), wanakuwekea mambo sawa kwa ajili ya ku-launch hiyo project. Bila shaka lazima kuwa na watu waalikwa rasmi (Nape in this case) au ukiweza hata "the komedi orijino" kwa ajili ya kuweka "chachandu" na shamra shamra. Na kwa kuwa Mh ni Mbunge (aka mwanasiasa) lazima ufanye "proper timing" - si unafahama uchaguzi unakarabia? Halafu na "life span" ya ubunge ni miaka mitano? na "memory" ya mtanzania ni wa kawaida ni mwaka mmoja? Kwa hiyo lazima utoe msaada kwa wapiga kura wako mwaka mmoja kabla ya uchaguzi!

have a nice weekend.

I hope Mkuu Kichankuli sio mmoja wao wa watakao chukua form za kuwania ubunge Jimbo la analoliongoza Lembeni!!!
 
Fedha ya maendeleo siyo rushwa, tatizo ni Mengi ni mfanya biashara, hawezi kutoa sadaka/zawadi. 'I fier the Greeks, especially when they bring gifts'. Mzee Mengi sio mjinga, anaona mbali sana, there is a way, hiyo milioni 100 itarudi. Ila pia nahisi Mzee wetu huyu, ana agenda fulani, bado sijaweza kuconect the dots.

Hii style ya Mzee Mengi kuwakumbatia wabunge fulani fulani siyo bure, liko jambo. Only time will tell.
 
Mkuu Kichankuli!


have a nice weekend.

I hope Mkuu Kichankuli sio mmoja wao wa watakao chukua form za kuwania ubunge Jimbo la analoliongoza Lembeni!!!


Ndo niko nabangaiza masponsa kama kina Mengi ili nione uwezekano wa kutia timu (JK)
 
Kwani wanawake hawajui kula? Labda waje malaika ndio rushwa itaachwa kuliwa nchi hii.😛ainkiller:
 
Jee kama tunataka kupambana na rushwa tunawachague wakuu wa nchi kuwa wanawake. Kwani wanawake wanahistoria ndogo ya ufisadi nchini
nafasi nyeti za kupambana na wahalifu pamoja na rushwa tuwape wanawake walete mageuzi
Si kweli,Mula rushwa au mutoa rushwa ni tabia ya mtu mwenyewe haijalishi jinsia, umri, rangi, kabila wala chama, hivyo basi kusema wanawake wataleta mageuzi kiongozi itategemea na tabia ya mwanamke mwenyewe or personality. hata wengine wanatoa rushwa ya ngono mbona usemi?
 
zakia megji sio mwanamke?si mnakumbukaalichofanya wizara ya maliasiri na fedha,vitalu vyote na magogo aliuza....pale fedha ndo balaa EPA,
 
Sijajua kama huyu maralia sugu alikuwa anamahanisha nini kwa hili manake katika hizi nafasi wanawake wanafanya nini?

Hii hoja umeshaifanyia utafiti wa kutosha wakati uzoefu unaonyesha hawa wakikaa pamoja kila wakati wanagombana
 
Inawezekana wanawake wakawa na unafuu kidogo ila sikubalianai kabisa na dhana ya kuwa wao siyo mafisadi. Mifano iliyoachwa na akina Mongela na Tibaijuka huko kwenye ofisi za kimataifa ni kipimo tosha kuwa gender siyo factor sana katika mambo hayo. Utakumbuka kuwa hata ANBEN ilitokana na shinikizo la mwanamke.
 
Back
Top Bottom