Kauli za wananchi kuhusu rushwa ndani ya CCM
Wasemavyo Wasomaji
Kutoka Tanzania Daima
Gazeti hili sasa linachapisha maoni yenu yatakayotumwa kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS), kujadili mjadala utakaokuwa unaanzishwa na gazeti hili.
Mimi ni mwanaCCM hai. Nasikitishwa na matendo ya wanaCCM wachache wanaokiaibisha na kukipaka matope chama. Namuomba Mwenyekiti Rais Jakaya Kikwete awachukulie hatua kali wale watakaothibitika kutumia rushwa katika chaguzi mbalimbali (yaani chaguzi za chama na zile za kiserikali kama ubunge). Kinyume na kuchukua hatua, Mwenyekiti Rais Kikwete atakiweka chama na yeye mwenyewe katika mazingira magumu katika uchaguzi mkuu wa 2010 (0754 695 662)
Kwa kitendo cha CCM, tena chama tawala na viongozi wake waliochaguliwa na wananchi kukamatwa kwa rushwa na TAKUKURU ni aibu kubwa sana kwa Serikali ya Kikwete, tutaonana katika uchaguzi wa mwaka 2010 S. Mtunu, Kilombero, Mkamba, Kidatu (0786 011 060)
Rushwa ndani ya CCM haijaanza leo, wameshazoea, si unajua ukiwasha moto ndani ya shimo halafu ukafunika nini kitatokea? Tufumbuke macho. Tujiulize, kama angekuwa Zitto Kabwe amekamatwa anatoa rushwa unadhani wangemfanya nini, kama si kumfunga gerezani miaka hata kumi? Lakini ya kwao watafichiana, yatapoa. Binafsi najua wa kumpa kura mwaka 2010, lakini si mla rushwa Mercy, Kawe, Dar es Salaam (0714 833 583)
Yanayotokea CCM yanadhihirisha wazi sampuli ya viongozi wa kitaifa tulionao, ingawa hawataki kukubali ukweli huu. Ikumbukwe kuwa wengi wao walipata madaraka kwa takrima! Ila za mwizi ni arobaini. Tunazidi kuwatambua - Godwin, Tegeta, Dar es Salaam (0787 232 942)
Kwa maoni yangu, ili rushwa iishe, TAKUKURU ibinafsishwe, kwa sasa haiwezi kufanya kazi vizuri, serikali na TAKUKURU viwe vitu viwili tofauti, vinginevyo rushwa ndani ya CCM haitakaa iishe - Edwin Tillya, Babati, Manyara (0717 766 608)
Waliotuhumiwa kuhusika na rushwa waadhibiwe, vinginevyo hata anayefuatilia TAKUKURU wananchi nao wataona wamepewa rushwa wazibe mdomo Johnson Materu, Arusha (0754 217 318)
Iliyobaki Watanzania tusiwe wajinga, kwani hata Mungu ameamua kutuonyesha madhambi ya chama tawala, kwamba CCM hali si shwari na wala hawatujali sisi, je, iweje sisi tuwajali wao? Hebu tuamke (0754 856 672)
Kama kweli CCM imedhamiria kwa dhati kuondoa rushwa ionyeshe mfano kwa watu ambao tayari wameshabainika, isiishie tu kwa madiwani wanyonge waliouza viwanja wakawatimua. Mfano katika uchaguzi uliofanyika Kiteto, mgombea mmoja anadaiwa kununua mchele kama chakula kwa wajumbe na mgombea huyo alipita kwenye nafasi aliyowania. Kwa hali hiyo, uongozi wa kuchaguliwa ndani ya chama utabaki kwa wenye fedha tu. Kama dhamira ya kuondoa rushwa ni kweli, basi serikali iiondoe TAKUKURU Ikulu, iwajibike kwa Bunge, japokuwa Bunge lenyewe ni walewale wanaoonekana kuikumbatia mikataba feki (0786 029 170)
Rushwa imezidi sana kwenye chama tawala kuanzia ngazi ya ubalozi wa nyumba kumi ni rushwa hadi wabunge wao, rushwa inatoa harufu mbaya CCM. Jamani, tuwabwageni kwenye uchaguzi ujao Veneranda, Mwanza (0717 494 943)
Rafu za CCM zimepita ukomo. Katika kiwango cha rushwa kilichopo CCM, sioni uwezekano wa Watanzania kubadili serikali yao kwa kura za kawaida, lazima tuungane kuonyesha haturidhiki. Yanayoendelea kwenye serikali hii ya CCM mengine ni aibu hata kuyazungumzia hadharani (0787 442 559)
Rushwa ndani ya CCM si jambo jipya, inaonekana ndivyo walivyozoea na kuzoeshwa kupata na kutoa uongozi, kwani nani kasahau habari za takrima? Ndiyo maana matajiri na wahuni wa kisiasa wote wanakimbilia huko, kwani ni rahisi kununua uongozi ukiwa huko. Hili jinamizi linaloonekana kukitafuna chama ni kama danganya toto tu kwa jamii. TAKUKURU kama kweli iko huru, kwanini isubiri agizo la Mkubwa ndipo ifanye kazi? Bado tunadanganywa tuone eti sasa kazi imeanza, hakuna kitu hapo, wanaibiana, kwanini tusiamini tukiambiwa wanawaibia wananchi kura zao kwenye uchaguzi mkuu? Mkwanzania (0754 422 518)
Ama kweli mwisho wa mfanyabiashara ni hasara. Wanajua tujue wakati mwingine Mungu naye ana makusudi yake. Ipo siku Mungu atatusaidia, amina (0754 327 103)
Rushwa imekithiri CCM, cha kufanya ni kuwanyima kura mwaka 2010 ili tuwashikishe adabu (0717 494 943)
Kusema kweli rushwa ndani ya CCM ni sawa na donda ndugu kwa sababu wala rushwa wanafahamika, lakini wanashindwa kunyooshewa kidole kwa sababu ya kulinda maslahi, lakini wakipatikana watu kama Zitto, naamini tutapiga hatua Gazza Muzungu, Dar (0756 396 991)
Nafikiri kuhusu suala la rushwa ndani ya CCM, Mungu sasa ameamua kuwaumbua, umefika wakati sasa kazi iwe kwetu kuamua kukizika chama hiki, maana wanayotufanyia sasa yametufika shingoni Abbas Ahmed, Dar es Salaam (0755 826 210)
CCM kimekuwa chama cha wanaotaka kufanya biashara bila usumbufu, ndiyo maana wanatoa rushwa na mara kadhaa tumesikia ukitaka mambo yako yakuendee sawa, uingie CCM! John Kalalu (0763 484 900)
Rushwa ndani ya CCM. Kama CCM wao kwa wao wanaibiana na kutumia rushwa namna hii! Vipi inapokuwa CCM na upinzani, si ndiyo balaa kabisa? Hii imetudhihirishia Watanzania kuwa kumbe ushindi wa CCM wa kishindo siku zote huwa unatokana na mchezo mchafu. Serikali ya CCM haiwezi kuipiga vita rushwa - (0713 502 497)
Rushwa CCM inatupa ukweli juu ya uozo uliomo ndani ya chama hicho na jinsi viongozi walivyo, kwa ujumla tujifunze kuwa chama kimeoza Mwasanga David, Mbeya (0713 650 765)
Jasiri haachi asili, CCM imezoea kushinda kwa rushwa, Mungu amewafichua kutokana na dua za wapinzani Saktay, Karatu (0754 958 254)
Kwa kushikwa wabunge wa CCM na TAKUKURU, hata kama hawajathibitika, ukweli ni kwamba, mambo si shwari Magagula S. Magagula, Korogwe, Tanga (0786 107 240)
Rushwa na CCM ni sawa na Kulwa na Dotto, kwani viongozi wote wa CCM hupatikana kwa njia ya rushwa hivyo hakuna wa kukemea ndani ya chama M.G.G, Musoma (0784 794512)
Rushwa ndani ya CCM ni kielelezo tosha kinachothibitisha kwamba chaguzi zote kuu pamoja na ndogo zilizopita ziliambatana na rushwa. Hii ni aibu kwa chama kikongwe. Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kwamba, mficha maradhi, kifo kitamuumbua, hayo ndiyo yanayoitokea CCM kwa sasa (0784 688 333)
Rushwa ni suala baya kila pahala, hivyo chama kinachoongoza kuwa na kashfa ya rushwa ni dhuluma ya haki ya wananchi, hivyo bora watoa rushwa ndani ya CCM wafutwe uanachama, na wakabidhiwe kwenye chombo husika kwa hatua zaidi. Wananchi tujue viongozi wanaotoa rushwa ili kupata viongozi, lazima nao watatoa huduma kwa kuomba rushwa ili kufidia fedha zao walizohonga. Kamwe tusilee maovu ya rushwa kwenye CCM Gumbo Zacharia, Mahenge (0787 531 615 )
Ndugu mhariri, binafsi sishangai, yaani inaonekana kama vile rushwa imekuwa kama ibada CCM kuanzia balozi hadi ngazi za juu, ni aibu kubwa sana kwa chama kikongwe, kama CCM kufikia hatua kama wewe ni kandambili ndani ya CCM hupati nafasi ya uongozi. Wananchi kama hao wanatafuta uongozi kwa malengo yao wenyewe dawa yao ni 2010 tu, hakuna kulala Hassan Kibari, Musoma (0787 763 559)
Mwenye macho haambiwi tazama. Watanganyika tunashuhudia live uozo wa rushwa ndani ya chama tawala. Mambo yaliyotokea bungeni na yanayoendelea katika chaguzi za CCM yanatosha kutuamsha Watanganyika. Mungu katufichulia uozo unaotendeka, saa ya kujikomboa ni sasa - Sallu Chamungwana (0755 538 720)
Tusitegemee rushwa kwisha au kupungua CCM kwa sababu imeshaota mizizi mikubwa na kusababisha nyufa tangu pale walipoamua kuwakumbatia mabepari, sisi walalahoi tuombeleze A. Said (0754 378 226)
Naunga mkono kwamba, suala la rushwa limekithiri ndani ya CCM. Chama tunakipenda, lakini tunawaachia wenye pesa, haki haipo kwa wanyonge Wanyonge, Sikonge, Tabora (0787 971 789)
Rushwa CCM haiwezi kutoweka kwa sababu TAKUKURU ni kama jibwa lisilo na meno mbele ya vigogo. (0717 090 892)
Sahani chafu haiwezi kuwekewa chakula safi, rushwa ndani ya CCM inaanzia mbali, kuanzia kwenye mtandao hadi ufamilia kwenye chama Daudi Samson, SUA, Morogoro (0756 683 553)
Ni rushwa tu iliyokithiri katika serikali yetu na Zitto kawaumbua na ndiyo sababu wamemtimua bungeni. Na wote waliochangia hoja ya Zitto kusimamishwa shughuli za Bunge ndio wale wale wala rushwa Salum, Tabora (0754 408 502)
Rushwa kwisha ni ndoto za alinacha, labda tuungane kukisakama chama tawala katika uchaguzi mkuu ujao. Angalia kilichotokea Arusha, wabunge wanaotuhumiwa kwa rushwa wamefikishwa mahakamani na kuachiwa kwa dhamana, ingekuwa sisi walalahoi si tungefia mahabusu? - Andrew William, Sumbawanga (0754 069 205)
Kwisha kwa rushwa ndani ya CCM sijui! Kwa sababu ndani ya chama hakuna anayekemea rushwa kwa dhati na isitoshe, matajiri wanapewa nafasi kubwa kama ilivyo kwa watoto wa wakubwa. Nani amfunge paka kengele? Kea Baba, Kasumulo, Kyela (0754 244 547)
Kama wao CCM wanaonyeshana ujuzi wa kuibiana kura na kutoa rushwa, wananchi hatuwezi kuwa na imani na serikali ya chama tawala Kocha (0784 480 025)
CCM na rushwa, rushwa na CCM. Hivi viwili haviwezi kutenganishwa, hata Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kwamba CCM imeoza na inanuka rushwa, ni kama pete na chanda. Wabunge wa CCM huko Arusha wamekamatwa kwa tuhuma za rushwa, pesa hizi za kununua kura zinatoka wapi au wenzetu wana mashamba ya fedha? - Issa Mtuli, Dar (0714 515 747)
Ukiwauliza CCM watakuambia hakuna rushwa, ukimuuliza mtu kama Mudhihir atakuambia chama ni safi kabisa. Waingereza hunena, time will tell. Watanzania tuamke jamani (0786677046)
Mungu hamfichi mnafiki. Rushwa inayorindima katika chaguzi za CCM ni kivuli cha yaliyotokea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Hata zile tambo za ushindi wa tsunami bila shaka ulikuwa na mkono wa rushwa. Rushwa ndani ya Tanzania haiwezi kuondoka kwa sababu ndiyo inayoonekana kuwa staili ya viongozi wetu. Dawa pekee ni Watanzania kuzinduka na kuwakataa matapeli wa kisiasa Douglas Sallu (0755 538 720)
Wakubwa wengi ndani ya chama tawala, wana harufu ya rushwa, lakini hawayaoni haya, wanayaona ya Zitto Kabwe tu (0713 481 383)
Rushwa ilionekana kama sehemu ya imani ya chama, lakini sasa ndiyo wanaanza kujisafisha. Ile dini yao ya takrima waliyotumaliza nayo mwaka 2005 sasa wameanza kuisahau na Mungu atawalaani kwa kuwaumbua kama hali inavyoanza kuonekana sasa Kimaro Raphael (0754 449 256)
Mimi naona sasa chama hiki kinastahili kikae pembeni ili kijipange upya, kimechoka hiki Tamtam, Tarime (0784 500 974)
CCM ninayoifahamu si hii inayonuka rushwa. Haikuwa ya kiukoo, familia au hata ya kirafiki. Ni dhambi ya mauti kwa CCM kufanya uchaguzi wowote bila rushwa. Ogopa watu wa chama hicho kinachotawala nchini wanapojaribu kutumia kila njia kupata uongozi. Tusidanganyane, hakuna mtu ndani ya CCM anayeweza kukemea rushwa, kwani wengi wamepita katika tanuru hilo. Kama Mwalimu Nyerere akifufuka, atawatawanya karibu wote CCM (0784 329 918)
Kutokana na wingi wa ujumbe wa wasomaji, tumeshindwa kuuchapa wote, hivyo utaendelea katika toleo lijalo Mhariri