Tanzania unaweza kusema uongo hadharani na usiwajibike popote. Sheria ya kulinda maadili itungwe

Pascal Ndege

JF-Expert Member
Nov 24, 2012
2,977
1,897
Toka sakata la Bandari lianze nimepitia na kusoma sheria nyingi sana. Nikasoma na sheria mbalimbli za nchi nyingine. Nikagundua nchi haina sheria ya Uongo na upotoshaji wa umma.

Kwa nchi ya Tanzania unaweza kwenye vyombo vya habari ukasema uongo tu ambao si wa kichochezi na usiwajibike popote.

Kidogo serikali inajilinda na sheria ya Uchochezi. Kwa Tanzania ni ruksa kundanya Umma bila kuwajibikaji. Mtu anaweza kuhojiwa kuwa na mahusiano na mtu ambae hawajawahi kuonana bila kuwajibika. Akamletea madhara pamoja na msongo wa mawazo bila kuwajibika kwa lolote.

Kiongozi wa Umma anadanganya Umma tu bila wasiwasi wowote bila kujali madhara yake.

Kuna nchi za Ulaya hata ukigundulika una kimada unawajibika kabisa. Uongo kwenye mahusiano utaleta changamoto za kisaikolojia kwa na kupelekea uvunjifu wa sheria pamoja na mauti.

Nawashauri wadau wa sheria waje na hii sheria ili kulinda maadili ya jamii na kuepusha madhara ya kimwili, kiuchumi, kifedha kisiasa, na kijamii.
 
Toka sakata la Bandari lianze nimepitia na kusoma sheria nyingi sana. Nikasoma na sheria mbalimbli za nchi nyingine. Nikagundua nchi haina sheria ya Uongo na upotoshaji wa umma.

Kwa nchi ya Tanzania unaweza kwenye vyombo vya habari ukasema uongo tu ambao si wa kichochezi na usiwajibike popote.

Kidogo serikali inajilinda na sheria ya Uchochezi. Kwa Tanzania ni ruksa kundanya Umma bila kuwajibikaji. Mtu anaweza kuhojiwa kuwa na mahusiano na mtu ambae hawajawahi kuonana bila kuwajibika. Akamletea madhara pamoja na msongo wa mawazo bila kuwajibika kwa lolote.

Kiongozi wa Umma anadanganya Umma tu bila wasiwasi wowote bila kujali madhara yake.

Kuna nchi za Ulaya hata ukigundulika una kimada unawajibika kabisa. Uongo kwenye mahusiano utaleta changamoto za kisaikolojia kwa na kupelekea uvunjifu wa sheria pamoja na mauti.

Nawashauri wadau wa sheria waje na hii sheria ili kulinda maadili ya jamii na kuepusha madhara ya kimwili, kiuchumi, kifedha kisiasa, na kijamii.
Jiwe kavunja katiba urais wake wote mpaka kajifilia mbali zake mwenyewe, hakuna aliyemfanya kitu.

Sheria kutungwa ni vizuri, lakini sheria ambazo hazitekelezeki, kwa sababu za kiutamaduni, hazitatusaidia kitu.

Tunahitaji utamaduni wa kuheshimu sheria, hapo ndipo sheria zitakuwa na maana.

Vinginevyo, tutatunga sheria nzuri sana na zitabaki vitabuni kama hadithi tu.
 
Jiwe kavunja katiba urais wake wote mpaka kajifilia mbali zaje mwenyewe, hakuna aliyemfanya kitu.

Sheria kutungwa ni vizuri, lakini sheria ambazo hazitekelezeki, kwa sababu za kiutamaduni, hazitatusaidia kitu.

Tunahitaji utamaduni wa kuheshimu sheria, hapo ndipo sheria zitakuwa na maana.

Vinginevyo, tutatunga sheria nzuri sana na zitabaki vitabuni kama hadithi tu.
Sheria ya Uongo si kwa Serikali tu hata mtu kadanganya Umma akidhibika hata alipe faini tu
 
Unakuta mtu huyo huyo leo anasema hili kesho ikibainika amedanganya anasema tena uongo kwakubadiri maneno yake mwenyewe na bado mtu huyo kama kiongozi haoni Kama kudanganya nikukosa staha,,
 
Huo ni uongo mkubwa umeandika, kusema Uongo ni sehemu kubwa ya Siasa za Western, George Bush na Colin Powell walidanganya kwa makusudi kabisa kuhalalisha uvamizi dhidi ya Irak tena UN na hakuna consequences zozote zile zaidi ya kifo cha muongo Colin Powell kama kifo ni adhabu sijui kwani wote tutakufa pia hivyo hakuna kilichompata.

Wanasiasa wote Duniani ni waongo vinginevyo wasingedumu …
 
Sheria ya Uongo si kwa Serikali tu hata mtu kadanganya Umma akidhibika hata alipe faini tu
Nakwambia hivii, hiyo sheria ni jambo zuri iwepo.

Lakini, kama watu wenyewe hawana utamaduni wa kuheshimu sheria na kufuatilia wavunja sheria, hiyo sheria itakuwa haina maana.

Tuondoke kwa serikali na viongozi, naona hapo nakuchanganya.

Tuje kwa wananchi.

Ikiwa kuna sheria kwamba ukitupa takataka barabarani unapigwa faini kali, halafu hakuna jinsi ya kui enforce hiyo sheria, hakuna camera za kurekodi watu (state surveillance, I know), hakuna askari wa jiji wanaofuatilia, na wakiona mtu katupa uchafu barabarani wanaona hilo ni sehemu ya kawaida tu ya maisha, sheria hiyo itakuwa kama mapambo tu kwenye vitabu.

Sheria inapata nguvu kama watu watakuwa na utamaduni wa kuheshimu sheria.

Kama watu hawana huo utamaduni, hata ukiwa na sheria nzuri vipi, itakuwa ni bure tu.

Tatizo letu kubwa si sheria, tuna sheria kali sana, even draconian, kuhusu kutangaza takwimu, kama ukali wa sheria ungekuwa ni suluhisho, hizi zinatakiwa kuondoa tatizo.

Lakini tatizo haliishi, kwa sababu ya utamaduni mbovu, si kwa sababu ya sheria mbovu.

Pia,

Huwezi kutunga sheria kuzuia uongo. Kuna ujanja mwingi sana unatumika kudanganya hata kwenye wanazuoni wa kisayansi.

Na kwenye siasa kuna kitu kinaitwa "pilitical speech", kimsingi wanasiasa wanaruhusiwa kutia chumvi habari fulani kisanii ili kujenga hoja zao za kisiasa. Hutakiwi kubana sana hii politicalnspeech, ni sehemu ya free speech na open society.

Kinachotakiwa ni kuongeza elimu kwa watu wasiweze kudanganywa kirahisi, wawe na ujasiri wa kuhoji na kuwaaibisha wasema uongo. Tusiwe na simile kwa waongo.

Leo hii Waziri Mkuu aliye madarakani anaendelea baada ya kudanganya taifa kwamba rais alikuwa mzima anachapa kazi, wakati rais alikuwa anajifia zake.

Huyu mtu muongo kabisa karuhusiwa vipi kuendelea kuwa Waziri Mkuu?
 
Nakwambia hivii, hiyo sheria ni jambo zuri iwepo.

Lakini, kama watu wenyewe hawana utamaduni wa kuheshimu sheria na kufuatilia wavunja sheria, hiyo sheria itakuwa haina maana.

Tuondoke kwa serikali na viongozi, naona hapo nakuchanganya.

Tuje kwa wananchi.

Ikiwa kuna sheria kwamba ukitupa takataka barabarani unapigwa faini kali, halafu hakuna jinsi ya kui enforce hiyo sheria, hakuna camera za kurekodi watu (state surveillance, I know), hakuna askari wa jiji wanaofuatilia, na wakiona mtu katupa uchafu barabarani wanaona hilo ni sehemu ya kawaida tu ya maisha, sheria hiyo itakuwa kama mapambo tu kwenye vitabu.

Sheria inapata nguvu kama watu watakuwa na utamaduni wa kuheshimu sheria.

Kama watu hawana huo utamaduni, hata ukiwa na sheria nzuri vipi, itakuwa ni bure tu.

Tatizo letu kubwa si sheria, tuna sheria kali sana, even draconian, kuhusu kutangaza takwimu, kama ukali wa sheria ungekuwa ni suluhisho, hizi zinatakiwa kuondoa tatizo.

Lakini tatizo haliishi, kwa sababu ya utamaduni mbovu, si kwa sababu ya sheria mbovu.

Pia,

Huwezi kutunga sheria kuzuia uongo. Kuna ujanja mwingi sana unatumika kudanganya hata kwenye wanazuoni wa kisayansi.

Na kwenye siasa kuna kitu kinaitwa "pilitical speech", kimsingi wanasiasa wanaruhusiwa kutia chumvi habari fulani kisanii ili kujenga hoja zao za kisiasa. Hutakiwi kubana sana hii politicalnspeech, ni sehemu ya free speech na open society.

Kinachotakiwa ni kuongeza elimu kwa watu wasiweze kudanganywa kirahisi, wawe na ujasiri wa kuhoji na kuwaaibisha wasema uongo. Tusiwe na simile kwa waongo.

Leo hii Waziri Mkuu aliye madarakani anaendelea baada ya kudanganya taifa kwamba rais alikuwa mzima anachapa kazi, wakati rais alikuwa anajifia zake.

Huyu mtu muongo kabisa karuhusiwa vipi kuendelea kuwa Waziri Mkuu?
Sheria ya Uongo ikiwepo itaanza huku chini kabisa na kupanda kidogo kidogo. Ukidanganya wananchi wana kushitaki unalipa faini
 
Huo ni uongo mkubwa umeandika, kusema Uongo ni sehemu kubwa ya Siasa za Western, George Bush na Colin Powell walidanganya kwa makusudi kabisa kuhalalisha uvamizi dhidi ya Irak tena UN na hakuna consequences zozote zile zaidi ya kifo cha muongo Colin Powell kama kifo ni adhabu sijui kwani wote tutakufa pia hivyo hakuna kilichompata.

Wanasiasa wote Duniani ni waongo vinginevyo wasingedumu …
Western democracies zinaruhusu kitu kinachoitwa "political speech", kimsingi ni ruhusa kwa wanasiasa kutia chumvi habari fulani ili kujenga hoja zao za siasa.

Hii haihesabiwi kuwa uongo, inahesabiwa kuwa ni sshemu ya free speech.

Na wananchi wanategemewa wawe wameelimika vya kutosha kuchekecha habari kujua mchele upi na makapi yapi.

Lakini, walichofanya kina Bush na Colin Powell ni beyond "political speech", wanaweza ku argue kwamba walighafilika, kwamba walifikiri walikuwa right, lakini, hata hapo kuna maneno aliyasema Colin Powell yalikuwa beyond being that simple.

Kitu kimoja tukiweke maanani, just because Marekani wana matatizo ya wanasiasa kuwa waongo pia (Donald Trump ni mfano mzuri) hili halimaanishi sisi nasi tuache jitihada za kuwawajibisha wanasiasa waongo, na waongo kiujumla katika jamii.

Si lazima turidhike na kinachofanyika Marekani, kuna mambo hata sisi Tanzania tukijipanga tunaweza kuwafunza Wamarekani.
 
Sheria ya Uongo ikiwepo itaanza huku chini kabisa na kupanda kidogo kidogo. Ukidanganya wananchi wana kushitaki unalipa faini
Hujaelewa somo zima.

Sheria ikiwepo lakini hakuna anayeijali, ukisema uongo watu hawajali, wanaona kawaida tu, nani atakushitaki?

Unajua yule Majaliwa angekuwa kwenye nchi yenye watu wanaojali ukweli angeshitakiwa kwa kudanganya taifa kwamba rais ni mzima anachapa kazi?

Lakini Watanzania hatuna utamaduni huo, tumeona ile kauli ni sawa tu. Tumemuachia muongo anaongoza serikalini.

Matokeo yake hizo bajeti zenu zote zimejaa uongo na data za uchumi karibu zote famba.
 
Western democracies zinaruhusu kitu kinachoitwa "political speech", kimsingi ni ruhusa kwa wanasiasa kutia chumvi habari fulani ili kujenga hoja zao za siasa.

Hii haihesabiwi kuwa uongo, inahesabiwa kuwa ni sshemu ya free speech.

Na wananchi wanategemewa wawe wameelimika vya kutosha kuchekecha habari kujua mchele upi na makapi yapi.

Lakini, walichofanya kina Bush na Colin Powell ni beyond "political speech", wanaweza ku argue kwamba walighafilika, kwamba walifikiri walikuwa right, lakini, hata hapo kuna maneno aliyasema Colin Powell yalikuwa beyond being that simple.

Kitu kimoja tukiweke maanani, just because Marekani wana matatizo ya wanasiasa kuwa waongo pia (Donald Trump ni mfano mzuri) hili halimaanishi sisi nasi tuache jitihada za kuwawajibisha wanasiasa waongo, na waongo kiujumla katika jamii.

Si lazima turidhike na kinachofanyika Marekani, kuna mambo hata sisi Tanzania tukijipanga tunaweza kuwafunza Wamarekani.

Sent from my SM-S908U1 using JamiiForums mobile app
Uongo ni ambao ushahidi upo. Umesema huna nyumba ila hii Hati yako ya nyumba. Unalipa faini
 
Hujaelewa somo zima.

Sheria ikiwepo lakini hakuna anayeijali, ukisema uongo watu hawajali, wanaona kawaida tu, nani atakushitaki?

Unajua yule Majaliwa angekuwa kwenye nchi yenye watu wanaojali ukweli angeshitakiwa kwa kudanganya taifa kwamba rais ni mzima anachapa kazi?
Hata kama Majaliwa alidanganya hakuna sheria yoyote inamshitaki
 
Hata kama Majaliwa alidanganya hakuna sheria yoyote inamshitaki
Wanasheria wetu tu wamelala, kwa sababu hatuna utamaduni wa kuheshimu sheria.

Nina hakika kuna sheria za kuruhusu kum sue Majaliwa kwa uongo ule.

Na hata kama sheria hizo hazipo, katika jamii inayoheshinu ukweli, kuanzisha kesi kungeweza kumshitaki kwenye court of public opinion kwa namna ambayo ingemuaibisha na kufanya sheria hizo zitungwe na hata yeye ajiuzulu.

Unaweka umuhimu mkubwa sana kwenye sheria, hilo ni jambo zuri.

Mimi nakuambia hivi, sheria ni kama gari. Kuwa na gari ni kitu muhimu ili uweze kusafiri kwa urahisi.

Lakini, kuwa na gari tu haitoshi.

Gari linahitaji mafuta ili liende.

Kama sheria ni gari, mafuta yanayofanya gari hilo liende ni utamaduni wa watu, utamaduni wa kuheshimu sheria, utamaduni wa kushitaki pale inapotakiwa kufanya hivyo.

Unaweza kupiga kelele kubwa tuwe na gari, unaweza kupata hilo gari.

Lakini, kama huna mafuta ya kuweka kwenye hilo gari, gari lako litapaki tu nyumbani kama mapambo.

Unaweza kutaka ziwepo sheria kali sana dhidi ya uongo, lakini, kama huna utamaduni wa kuheshimu sheria, sheria hizo zitakuwa mapambo tu.

Magufuli alipiga marufuku mikutano ya kisiasa, jambo (mikutano ya kisiasa) ambalo linaruhusiwa si na sheria tu, hili jambo lipo katika katiba kabisa.

Na hakuna aliyemfanya kitu.

Sasa hapo tatizo likikuwa nini?

Tatizo lilikuwa hatuna sheria nzuri za kuruhusu mikutano ya kisiasa? Hapana, hiki jambo lipo kikatiba.

Tatizo lilikuwa utamaduni.

Watanzania waliambiwa hakuna mikutano ya kisiasa, kinyume na sheria, kinyume na katiba, rais alivunja katiba.

Lakini hakukuwa na utamaduni wa kuheshimu sheria uliomuwajibisha.

Utamaduni wa watu ni muhimu kuliko sheria.

Unapotaka sheria kali, usisahau hilo.
 
Sheria zipo ila sasa hazizingazitiwi kiuhalisia wenyewe, maana Kuna kusema uongo ili kumlinda kiongozi flan Kwa hoja flani na Kwa lengo flani
Exactly.

Tuna sheria nyingine nibkali kwa kiasi ambacho inazifanya ziwe mbaya, ziwe repressive, ziwe draconian.

Sheria ya makosa ya mtandao, sheria ya takwimu, ni baadhi yabsheria hizi.

Tunataka sheria kali, wakati mara nyingine hizi sheria tunazo, tena mpaka zinaathiri free speech.

Lakini je, tuna utamaduni wa kuhwshimu sheria?

Halafu, hatuwezi kupiga vita uongo kwa sheria.

Tunatakiwa kuingeza elimu jwa watu wajue kuchambua uongo na ukweli.

Bila kuongeza elimu na kubadili utamaduni wa watu kuwafanya wawe na ownership ya nchi yao, tutatunga sheria kali ambazo hata wananchi hawatazijua na kimsingi zitakuwa kama hazipo.

Na kibaya zaidi, hizo sheria kali zitatumiwa na watawala kuwabana wananchi na kuendeleza uongo wa watawala.
 
Exactly.

Tuna sheria nyingine nibkali kwa kiasi ambacho inazifanya ziwe mbaya, ziwe repressive, ziwe draconian.

Sheria ya makosa ya mtandao, sheria ya takwimu, ni baadhi yabsheria hizi.

Tunataka sheria kali, wakati mara nyingine hizi sheria tunazo, tena mpaka zinaathiri free speech.

Lakini je, tuna utamaduni wa kuhwshimu sheria?

Halafu, hatuwezi kupiga vita uongo kwa sheria.

Tunatakiwa kuingeza elimu jwa watu wajue kuchambua uongo na ukweli.

Bila kuongeza elimu na kubadili utamaduni wa watu kuwafanya wawe na ownership ya nchi yao, tutatunga sheria kali ambazo hata wananchi hawatazijua na kimsingi zitakuwa kama hazipo.

Na kibaya zaidi, hizo sheria kali zitatumiwa na watawala kuwabana wananchi na kuendeleza uongo wa watawala.






Sent from my SM-S908U1 using JamiiForums mobile app
nikweli Kikubwa watu wapewe elimu ya kujua kuchambua ukweli na uongo maana asilimia kubwa ya watu tuna utamaduni WA kuwa sisi hatufatilii mambo, alichokisema kiongozi pengne kuhusu jambo flan katika serikali yetu mtu hawezi kufatilia je ni kweli alichokisema kiongozi ni Cha kweli ama uongo

Kingne upotoshaji Kwa njia ya media baadhi ya waandish WA habali pia wamekuwa ni chanzo cha habali za uongo, unakuta kiongozi ameongea kitu Cha ukwel lakin baadhi ya waandish wanaongea kinyume kabisa na ambavyo ilivyo,,

Mm naona Sheria kama hazipo zitungwe za kusema uongo, na kama zipo basi tupew elimu namna ya kuzifahamu na namna ya kuelimisha vizazi vijavyo
 
Hakuna sheria ya Uongo kabisa. Huwezi kumshitaki kwa uongo
Sidhani kama unakielewa unachoambiwa na sababu huenda ikawa ni udhaifu wako tu kifikra. Sheria kuu ni katiba na kama ndani ya taifa wapo viongozi wanaoweza kuvunja Katiba na wakaendelea na nyadhifa zao, hiyo sheria ya uongo ni kwa manufaa yapi?

Wapo wananchi waliotetea uvunjaji wa Katiba kwa dai kwamba kama hiyo katiba inakuwa kikwazo cha maendeleo ni ruhusa kuivunja. Tukawakumbusha kuwa Katiba yenyewe inatoa fursa ya kufanyiwa marekebisho kama ni kweli ni kikwazo lakini hawakuelewa.

Kama Katiba haiheshimiwi na viongozi walioapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea, sheria haina maana. Kwa ujinga baadhi ya Watanzania wenzetu wataendelea kumuona kiongozi wetu Mkuu kama mungu-mtu na hivyo kumpa sifa za Kimungu asizostahili.
 
Back
Top Bottom