Abdul Nondo
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 515
- 2,875
Tarehe.27/Novemba/2023 niliwasilisha malalamiko yangu kwa Kamishna Sekretariati ya Maadili ya viongozi wa Umma dhidi ya aliyekuwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria na Mbunge wa Babati Mjini Mh.Pauline Gekul juu ya tuhuma za unyanyasaji dhidi ya Hashimu Ally Philimone.
Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Maadili ya viongozi wa Umma Sura.No.398( R.E 2020) kifungu cha 25(1) kinachotoa fursa kwa mtu yeyote kuwasilisha malalamiko yake dhidi ya kiongozi wa Umma juu ya uvunjifu wa sheria ya Maadili ,pia kwa mujibu wa Katiba 1977 ibara ya 26(2) inayotoa agizo la wajibu na haki kwa kila mtu kulinda katiba ya JMT na sheria zingine za nchi.
Nikiamini ya kwamba Mh.Pauline Gekul amevunja sheria ya Maadili ya viongozi wa Umma Sura No.398 (R.E 2020) kifungu cha 6(1)(a) na 6(1)(b)(i) vifungu hivi vinahitaji viongozi wa Umma kutenda majukumu yao ya kiofisi hata majukumu binafsi kwa kuzingatia Maadili,uaminifu,huruma na uadilifu.
Hivyo,niliwasilisha malalamiko yangu kwa Kamishna Sekretariati ya Maadili ili ianze uchunguzi wa tuhuma hizi kwa mujibu wa Katiba ya JMT 1977 ibara ya 132(1) na sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Sura 398 [R.E 2020)] kifungu cha 16(2)(b)(c)(e), 25(2)(b) na 25(4-7). Na ikiwa itathibitika kwamba tuhuma hizi dhidi ya Mh.Pauline Gekul basi Mh.Gekul atakuwa amevunja masharti ya sheria ya Maadili ya viongozi wa Umma kifungu cha 6(1)(a) na 6(1)(b)(i).Na hivyo moja kwa moja Mh.Pauline Gekul atakoma kuwa Mbunge wa JMT ,Katiba ya JMT 1977 ibara ya 71(1)(d) inasema kwamba "Mbunge atakoma kuwa Mbunge ikiwa itathibitishwa kwamba amevunja masharti ya sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma".
Tarehe 6/Januari /2024 ,Ofisi ya Kamishna Sekretariati ya Maadili ya Viongozi wa umma ilinijibu barua yangu na kudai suala hilo lipo Mahakamani tayari kama kesi ya Jinai chini ya Mahakama ya Wilaya Babati . Ofisi ya Kamishna Sekretariati ya Maadili kama haina taarifa ya kwamba sasa hivi hakuna kesi yeyote ya jinai inayoendelea Mahakamani dhidi ya Mh.Gekul kwani kesi iliyofunguliwa na Wakili Peter Madeleka kesi ya Jinai Na.179 ya 2023 tayari iliondolewa na mwendesha mashtshtaka (DPP) tangu tarehe 26 Desemba 2023.
Hivyo wiki inayoanza kesho J.tatu 22/Januari/2024 nitamjibu Kamishna wa Sekretariati ya Maadili kwa barua ya kwamba hakuna kesi ya Jinai inayoendelea Mahakamani, pia masuala ya Maadili ya Viongozi wa umma hayana mahusiano na kesi za jinai . Hivyo hawapaswi kukwepa wajibu wao,wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Katiba ya JMT 1977 ibara ya 132(1) na sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Sura 398 [R.E 2020)] kifungu cha 16(2)(b)(c)(e), 25(2)(b) na 25(4-7).
Ahsante.
Abdul Omary Nondo.
Mwenyekiti wa Ngome ya vijana Taifa -ACT Wazalendo.
Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Maadili ya viongozi wa Umma Sura.No.398( R.E 2020) kifungu cha 25(1) kinachotoa fursa kwa mtu yeyote kuwasilisha malalamiko yake dhidi ya kiongozi wa Umma juu ya uvunjifu wa sheria ya Maadili ,pia kwa mujibu wa Katiba 1977 ibara ya 26(2) inayotoa agizo la wajibu na haki kwa kila mtu kulinda katiba ya JMT na sheria zingine za nchi.
Nikiamini ya kwamba Mh.Pauline Gekul amevunja sheria ya Maadili ya viongozi wa Umma Sura No.398 (R.E 2020) kifungu cha 6(1)(a) na 6(1)(b)(i) vifungu hivi vinahitaji viongozi wa Umma kutenda majukumu yao ya kiofisi hata majukumu binafsi kwa kuzingatia Maadili,uaminifu,huruma na uadilifu.
Hivyo,niliwasilisha malalamiko yangu kwa Kamishna Sekretariati ya Maadili ili ianze uchunguzi wa tuhuma hizi kwa mujibu wa Katiba ya JMT 1977 ibara ya 132(1) na sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Sura 398 [R.E 2020)] kifungu cha 16(2)(b)(c)(e), 25(2)(b) na 25(4-7). Na ikiwa itathibitika kwamba tuhuma hizi dhidi ya Mh.Pauline Gekul basi Mh.Gekul atakuwa amevunja masharti ya sheria ya Maadili ya viongozi wa Umma kifungu cha 6(1)(a) na 6(1)(b)(i).Na hivyo moja kwa moja Mh.Pauline Gekul atakoma kuwa Mbunge wa JMT ,Katiba ya JMT 1977 ibara ya 71(1)(d) inasema kwamba "Mbunge atakoma kuwa Mbunge ikiwa itathibitishwa kwamba amevunja masharti ya sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma".
Tarehe 6/Januari /2024 ,Ofisi ya Kamishna Sekretariati ya Maadili ya Viongozi wa umma ilinijibu barua yangu na kudai suala hilo lipo Mahakamani tayari kama kesi ya Jinai chini ya Mahakama ya Wilaya Babati . Ofisi ya Kamishna Sekretariati ya Maadili kama haina taarifa ya kwamba sasa hivi hakuna kesi yeyote ya jinai inayoendelea Mahakamani dhidi ya Mh.Gekul kwani kesi iliyofunguliwa na Wakili Peter Madeleka kesi ya Jinai Na.179 ya 2023 tayari iliondolewa na mwendesha mashtshtaka (DPP) tangu tarehe 26 Desemba 2023.
Hivyo wiki inayoanza kesho J.tatu 22/Januari/2024 nitamjibu Kamishna wa Sekretariati ya Maadili kwa barua ya kwamba hakuna kesi ya Jinai inayoendelea Mahakamani, pia masuala ya Maadili ya Viongozi wa umma hayana mahusiano na kesi za jinai . Hivyo hawapaswi kukwepa wajibu wao,wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Katiba ya JMT 1977 ibara ya 132(1) na sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Sura 398 [R.E 2020)] kifungu cha 16(2)(b)(c)(e), 25(2)(b) na 25(4-7).
Ahsante.
Abdul Omary Nondo.
Mwenyekiti wa Ngome ya vijana Taifa -ACT Wazalendo.