- Slaa hajaenda mahakamani kuhusu kuibiwa kura za urais alioushinda, Chadema haijaenda mahakamani kuhusu kupokea hela za nje kuleta vurugu, mkuu wewe na Slaa ndio waamuzi wa mwisho kuhusu public opinion soma vizuri mawazo ya watu hapa utaona kwamba kwenye haya majina mapya Slaa ameharibu so is Chadema, ndio maana kuna siku nilisema hivi kuna wananchi wengi Tanzania hawajui kwamba Slaa ni kiongozi wa Chadema, kwa sababu it is always about him na kuwepo kwenye media kila siku, ameibiwa kura za uchaguzi hajaenda mahakamani mpaka leo, Mtikila kesi ya mgombea binafsi ameenda kwenye sheria na kuishinda serikali, now you wonder nani mwenye nafuu!
- Mangula na Malecela hawawezi kuwa mafisadi for that Slaa ametuhadaa na binafsi nimekosa heshima tena na huyu kiongozi wenu mlipua mabomu, niliongea na mtu mmoja aliyewahi kugombea ubunge na Slaa, akaniambia ni tabia yake kukuzushia maneno mengi sana ya uongo, anasema hata yeye mpaka leo hana hamu naye, Slaa arudi chini kukijenga chama badala ya kulilia media headlines kila siku hazikijengi chama huko vijijini ambako kuna majimbo Chadema haikuweka wagombea kabisa kwa kutokuwa na presence, ni ushauri wa bure tu!
William @ NYC, USA.
Umeamua kuweka busara zako pembeni.Hivi na usomi wako hujui kwanini Dkt Slaa hakwenda mahakamani?Rejea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria za Uchaguzi kuhusu matokeo ya urais.
Umeng'ang'ania kwanini Chadema hawajaenda mahakamani kuhusu tuhuma kuwa wanapewa fedha kutoka nje.Usijaribu kusaka utetezi kwenye hoja hii kwa vile Chadema WALITANGAZA NIA YA KWENDA MAHAKAMANI.Sasa kama wameshaenda au wataenda mwakani,la muhimu ni kuwa WALITANGAZA HADHARANI.What about Mzee Malecela?Anaona aibu hata kujibu maswali ya waandishi wa habari.Je Chadema nao waliona aibu kujibu maswali ya waandishi wa habari walipotuhumiwa kupewa fedha kutoka nje ya nchi?
Eti maoni ya watu hapa yanaonyesha kuwa Slaa ameharibu?Kaharibu kwa vile kamtaja baba yako?Well,anaweza kuwa ameharibu hadhi ya familia yenu lakini kwa sie wenye nchi,tuliochoka kuibiwa huku wezi wakipeleka watoto wao ng'ambo,na kuwarithisha madaraka serikalini wakijifanya watetezi wa mfumo huo wa kisultani.
Katika kuropoka kwako unaweza kutuonyesha udhaifu wako.Mtikila hakwenda mahakamni kupinga matokeo ya urais.Ungekuwa na uelewa mdogo tu ungetambua kuwa matokeo ya urais yakishatangazwa hayawezi kutenguliwa na mahakama.Na kama baba yako alipoenguliwa mara kadhaa katika jitihada zake za kuutaka urais wa Tanzania kwa tiketI ya CCM hakwenda kulalamika japo kamati ya malalamiko ndani ya chama hicho,how come umtolee mimacho Dkt Slaa?
Na je baba yako aliposhindwa kwenye kura za maoni huko Mtera alikwenda mahakamani?Slaa hakWenda mahakamani kwa vile anafahamu kanuni na sheria zinasemaje.Badala yake amehamasisha mabadiliko ya Katiba kwa ajili ya free and fair elections huko mbeleni.What about Mzee Malecela?
Malecela hawezi kuwa fisadi kwa vile ni mwadilifu sana au kwa vile ni baba yako?Angekuwa mwadilifu angekubali "kuwa
JUMANNE" kwa ajili tu ya tamaa za urais?Angekuwa mwadilifu angewatukana Watanzania kwa kuwaambia
they could go to hell?Huyu mzee amejiumbua mwenyewe hata kabla ya kutajwa kwenye list ya ufisadi.Miaka nenda miaka rudi ameng'ang'ania madaraka mpaka wapiga kura walipompa za uso....wakamgaragaza,kisa tamaa ya madaraka.Halafu unasema "Malecela hawezi kuwa fisadi".Labda hawezi kuwa fisadi kwenye familia yenu lakini sio kwa taifa letu.
Na utasema kila baya kuhusu Dkt Slaa au Chadema lakini ukweli ndio ushawekwa hadharani kuwa
JOHN (a.k.a JUMANNE) CIGWIYEMISI MALECELA NI MIONGONI MWA MAFISADI,period!