Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Status
Not open for further replies.
Siasa za baba na mwana zinaingamiza Afrika ya magharibi kwa sasa, wananchi wamechoka kuibiwa kwenye mstari wa utukufu. Hawa kina william M , ni kati ya vijana wanaoona kuwa tonge linatoka mdomoni kama watoto wa Gadafi, Mubaraka nk. Mlitutawala mkatusahau na baya zaidi wazazi wenu wamekuwa wakiwahubiria kwamba watanzania ni wajinga hivyo hawataamka.

mmepanga oradha ya kututawala kikoo , sasa tumejua, tumeelewa, mmetumia fedha zetu kujitajirisha kusomeshwa na sasa mnzazitumia kututukana baada ya kuiba. Tunakataa na tunasema hatutaki tunachotaka tulipwe mpaka senti ya mwisho.

Vita hii lazima iwatoa madaraka na hapo sheria itafuata mkondo, mtajua mahakama zipo na nini maana ya haki. hapa uswa mbele ya sheria utajulikana, tunataka taifa ambalo kila mtu ataheshimu sheria na hamtakuwa tena na kiherehere cha kijeli baada ya kuiba.
 
Umeamua kuweka busara zako pembeni.Hivi na usomi wako hujui kwanini Dkt Slaa hakwenda mahakamani?Rejea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria za Uchaguzi kuhusu matokeo ya urais.

Umeng'ang'ania kwanini Chadema hawajaenda mahakamani kuhusu tuhuma kuwa wanapewa fedha kutoka nje.Usijaribu kusaka utetezi kwenye hoja hii kwa vile Chadema WALITANGAZA NIA YA KWENDA MAHAKAMANI.Sasa kama wameshaenda au wataenda mwakani,la muhimu ni kuwa WALITANGAZA HADHARANI.What about Mzee Malecela?Anaona aibu hata kujibu maswali ya waandishi wa habari.Je Chadema nao waliona aibu kujibu maswali ya waandishi wa habari walipotuhumiwa kupewa fedha kutoka nje ya nchi?

Eti maoni ya watu hapa yanaonyesha kuwa Slaa ameharibu?Kaharibu kwa vile kamtaja baba yako?Well,anaweza kuwa ameharibu hadhi ya familia yenu lakini kwa sie wenye nchi,tuliochoka kuibiwa huku wezi wakipeleka watoto wao ng'ambo,na kuwarithisha madaraka serikalini wakijifanya watetezi wa mfumo huo wa kisultani.

Katika kuropoka kwako unaweza kutuonyesha udhaifu wako.Mtikila hakwenda mahakamni kupinga matokeo ya urais.Ungekuwa na uelewa mdogo tu ungetambua kuwa matokeo ya urais yakishatangazwa hayawezi kutenguliwa na mahakama.Na kama baba yako alipoenguliwa mara kadhaa katika jitihada zake za kuutaka urais wa Tanzania kwa tiketI ya CCM hakwenda kulalamika japo kamati ya malalamiko ndani ya chama hicho,how come umtolee mimacho Dkt Slaa?

Na je baba yako aliposhindwa kwenye kura za maoni huko Mtera alikwenda mahakamani?Slaa hakWenda mahakamani kwa vile anafahamu kanuni na sheria zinasemaje.Badala yake amehamasisha mabadiliko ya Katiba kwa ajili ya free and fair elections huko mbeleni.What about Mzee Malecela?

Malecela hawezi kuwa fisadi kwa vile ni mwadilifu sana au kwa vile ni baba yako?Angekuwa mwadilifu angekubali "kuwa JUMANNE" kwa ajili tu ya tamaa za urais?Angekuwa mwadilifu angewatukana Watanzania kwa kuwaambia they could go to hell?Huyu mzee amejiumbua mwenyewe hata kabla ya kutajwa kwenye list ya ufisadi.Miaka nenda miaka rudi ameng'ang'ania madaraka mpaka wapiga kura walipompa za uso....wakamgaragaza,kisa tamaa ya madaraka.Halafu unasema "Malecela hawezi kuwa fisadi".Labda hawezi kuwa fisadi kwenye familia yenu lakini sio kwa taifa letu.

Na utasema kila baya kuhusu Dkt Slaa au Chadema lakini ukweli ndio ushawekwa hadharani kuwa JOHN (a.k.a JUMANNE) CIGWIYEMISI MALECELA NI MIONGONI MWA MAFISADI,period!

- Kwa kweli huu ushahidi unaweza kumfunga Malecela mahakamani kwa wizi wa EPA, mkuu you are a genius!

William @ NYC, USA.
 
- Mkuu unasema kwamba tuna sheria iliyomruhusu Mtikila kwenda mahakamani na kuishinda Serikali? Hivi ni lini umewahi kumsikia Slaa akisema alishinda Urais? niwekee nukuu moja tu kutoka mdomoni mwa Slaa akidai alishinda Urais? Anyways ninakushukuru sana kwa usahidi wako mzito sana unao onyesha Malecela na Mangula kuhusika na wizi wa EPA!

William @ NYC, USA.
Naona kutajwa mzee kume kutachi sana lakini ndiyo siasa ukiamua kuwa mwanasiasa vumilia yote wakati ukiwa unakula kivulini usisahau kuupalilia mti unaokupa kivuli.
 
Moelex23, asante sana kwa hili, Chadema ina udhaifu mkubwa wa kukosa long time strategiest hivyo kukalia kushindana kulipua mabomu.
Mimi ni miongoni mwa wapenzi wachache wa Chadema (sio mwanachama) ambao sikubaliani na baadhi ya moves za viongozi wa juu wa chama hiki.

Baada ya uchaguzi mkuu, nilisema it was wrong move kwa Dr. Slaa kususia kutangazwa kwa matokeo, nikasisitiza siku ya kutangazwa matokea was the best opportunity ya kueleza kutoridhishwa kwake na kutoyatambua matokeo.

Baada ya kutoyatambua matokeo yale, nilitegemea by now, Chadema wangekuja na altenative matokeo yao kujusfy kile wanachopinga, mpaka leo hakuna.

Sipendi Chadema ibaki kuwa ni chama cha kulalamika na kuendesha maandamano, natamani Chadema wewe chama chenye vision ya kuona political opportunity and seize such opportunities for their advantage.

CCM kujivua gamba is an opportunity huku ni kuvuja kwa pakacha (CCM), ambayo inatakiwa kuwa nafuu kwa mchukuzi (Chadema), badala ya mchukuzi kujituliza na kujiachia tuu mpaka pakacha libaki tupu, yeye ndio wa kwanza kumweleza mwenye pakacha, kuwa pakacha linavuja!, hivyo kumpa nafasi kuziba matundu yote hata yale ambayo yangempa unafuu mchukuzi!.

Kwenye hoja ya ufisadi, tayari CCM wanashikana mashati kutafutana uchawi, Chadema ilitakiwa ikae kimya iangalie tuu hii sinema. Kitendo cha Chadema kupiga kelele mpya, na kuwataja vipenzi vya watu kama kina Magufuli, kutaifanya CCM kuwasamehe hata mafisadi wake kama kina RA, EL na Mzee wa Vijisenti!.

Kwa mfano mtu kama Magufuli, hata ukiutangaza ufisadi wake kwa mabango, vipeperushi na maandamano nchi nzima, halafu uchaguzi ukaitishwa kesho, John Pombe Magufuli akasimama na Dr. Slaa, John Pombe, atamtupa kwa mbali Dr, kwa sababu moja tuu, watu watachagua mtu na sio chama. Pombe ana good track record ya kudeliver, Dr. yeye ndio kwanza anaitafuta hiyo opportunity ya kuwathibitishia Watanzania kuwa ata deliver.

Ndani ya Chadema, nadhani kitu vitu vikipangwa, hakuna wa kushauri otherwise, and this is not good kwa chama makini.

Pasco.


Kaka naungana mkono nawe ktk hili. Ukweli ni kuwa hadi sasa watanzania tumepewa two choices. The proven worst choice which is CCM and clearly Catastrophic choice which is Chadema. We should start to seriously focus on how to come about with the better choice ASAP
 
Kaka naungana mkono nawe ktk hili. Ukweli ni kuwa hadi sasa watanzania tumepewa two choices. The proven worst choice which is CCM and clearly Catastrophic choice which is Chadema. We should start to seriously focus on how to come about with the better choice ASAP
Omari, hakuna perfect political party kama jinsi hakuna absolute freedom kwenye jambo lolote. Hivyo kila chama, kina madhaifu yake. Kwenye mada yangu humu jf ya 'CCM imechokwa Chadema Haijajipanga', niliorodhesha madhaifu ya CCM na ya Chadema. wapenzi wa CCM humu walijikalia kimya, wapenzi wa Chadema na viongozi wao humu wakanishukia kuwa nina chuki binafsi dhidi ya Chadema.

Wenzao CCM hawakujibu kitu lakini madhaifu yale wameanza kuyafanyia kazi kwa kusafisha nyumba yao, wao Chadema kila wakikosolewa, kamwe hawataki kukubali makosa, they play difensive huku manazi wao wakiporomosha kila aina ya matukano humu!.

Hakuna ubishi kuwa listi ya mafisadi na vita ya ufisadi, imewapa Chadema good political mileages, nawashauri wasikalie kushupalia vita ya ufisadi tuu kutwa kucha kwa maandamano na mikutano ya hadhara, its about time, wajenge chama, wajipange strategicaly over and above kubadili mind set ya Watanzania kuwa wao wanaweza, concetration iwe kusonga mbele.

Kwa vile vita ya ufisadi ndio mtaji pekee wa Chadema, sasa CCM inajipanga kuula mtaji huo, na believe me, CCM ikijipanga na kusafisha nyumba yake ikatakata dhidi ya tuhuma zote za ufisadi, 2015 ikasimamisha mgombea makini, Chadema itakosa pa kupumulia, tutarudi kule kule kwenye nchi ya chama kimoja, save CUF kwa Zanzibar!.

Mimi binafsi naikubali sana Chadema na naiwish all the best ili kufikisha idadi ya simple majority ndani ya bunge la 2015, ila kwa mwendo huu wa kuimba wimbo ule ule, wananitia mashaka!.
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, kimetoa ufafanuzi juu ya orodha mpya ya ufisadi na mafisadi nchini, iliyosomwa juzi Mjini Tabora na Katibu Mkuu wa
chama hicho, ikiwa ni mwendelezo wa ile iliyotolewa mwaka 2007, Mwembeyanga, Dar es Salaam.

CHADEMA kimelazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya taarifa ya baadhi ya vyombo vya habari jana kumnukuu Dkt. Slaa akisema kuwa Waziri Mkuu Mstaafu, Bw. Fredrick Sumaye ni mmoja wa watuhumiwa wa ufisadi nchini, kwa mujibu katika orodha hiyo mpya.

Akizungumza jana Dar es Salaam na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Mafunzo na Oganaizesheni, Bw. Kigaila Benson, alisema kuwa wamelazimika kufafanua jambo hilo kwani hawataki kumtuhumu mtu bila kuwa na ushahidi wa tuhuma hizo, kwani kufanya
hivyo haingekuwa sahihi.

"Hili suala tumeamua kulifanyia ufafanuzi kwa sababu hatutaki wala hatuwezi kumtuhumu mtu au watu bila kuwa na ushahidi, kama mnavyojua sisi tunapoamua kusema fulani na fulani ni fisadi huwa tunaweka ushahidi bayana, kwa maana kuutaja ufisadi
waliofanya, si maneno matupu.

"Sasa imeandikwa kuwa katibu mkuu wetu Dkt. Slaa amemtaja Sumaye kuwa ni mmoja wa walioko katika orodha mpya ya mafisadi, hii si kweli, katika orodha hiyo hatukumtaja...hatusemi kuwa Sumaye ni fisadi au si fisadi, tunachosema ni kuwa sisi hatujamtaja katika orodha yetu.

"Kama kuna mtu anao ushahidi juu ya ufisadi wake anaweza kumtaja, hata sisi siku tukipata ushahidi juu ya Sumaye tutamtaja ...asubuhi nimeongea na Dkt. Slaa na Marando
(Mabere) wanasema Sumaye hakutajwa katika orodha, mazingira ambayo Dkt. Slaa alimzungumza Sumaye hayakunukuliwa sahihi," alisema Bw. Benson.

Aliongeza kuwa Dkt. Slaa alitaja jina la Bw. Sumaye alipokuwa akisema kuwa mafisadi na ufisadi ambao ameutaja mara kwa mara haujali dini, uhusiano, kabila, rangi wala umri wa mtu, hivyo akatolea mfano jinsi alivyowahi kumshambulia waziri mkuu huyo
mstaafu ambaye anatoka naye eneo moja huko Arusha, wakati akiwa madarakani kwa kushindwa kudhibiti ufisadi serikalini.

Bw. Benson pia alizungumzia kauli iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri ya Taifa (NEC) ya CCM, Bw. Nape Nnauye kuwa kuna vyama vya upinzani vimetumwa na mafisadi kumchafua Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, huku pia akidai kuwa kuna
wanasiasa wa upinzani wametumwa Tabora kufanya kazi hiyo hiyo.

"Unajua kitu kimoja ambacho mtu mwenye akili hawezi kuwaelewa CCM, hususan wanapoamua kutuhumu, wanaimba sana ngonjera. Unapoamua kusema kuwa kuna mafisadi wanatumia vyama vya upinzani kumchafua rais, ili ueleweke na kuaminika unawataja hao mafisadi
au huyo fisadi na vyama au chama kinachotumika.

"Ndiyo maana sisi tunapenda kuwaonesha njia sahihi ili wajikosoe vizuri, tukitaja mafisadi tunaonesha na ufisadi wao, hatubahatishi, sasa wao wanaimba tu ooh tunawapatia mafisadi siku tisini wajiuzulu lakini hawana ubavu wa kuwasema kwa
majina hao mafisadi ni akina nani na ufisadi wao uko wapi na wanachukua hatua gani za kisheria juu ya ufisadi wao.

"Tena sasa wanataka kuleta utamaduni mbaya sana ambao utatengeneza mwanya kwa watu walioko madarakani kufanya ufisadi maana wanajua wataambiwa wajiuzulu tu, hakutakuwa na hatua za kisheria juu ya yao, tulitegemea kwa chama chenye serikali kama CCM, kuiagiza serikali kuchukua hatua si kulalamika au kuimba ngonjera kama wanavyofanya sasa."

Bw. Benson alisema kuwa si sahihi watu wanaotuhumiwa ufisadi katika chama kinachounda serikali, huku wakiwa na dhamana ya uongozi sehemu zote mbili, kuachia nafasi zao ndani ya chama husika pekee, badala ya kuchunguzwa, kisha kufikishwa
mahakamani kwa ajili ya hatua za kisheria.

"Alitakiwa ataje jina la huyo fisadi au mafisadi na hivyo vyama vya upinzani. Pia fisadi ni mwizi, amefilisi taifa, raslimali za nchi sasa unaposema ajiuzulu nini kinafuata sasa, mwizi anakamatwa, mwizi hasemwi tu, sisi hatuna serikali sasa, lakini
tumewataja, hawa wana serikali mbona hawachukui hatua."

Juzi katika mkutano wake wa ujenzi wa chama hicho mkoani Tabora, Dkt. Slaa akiwa na pamoja makada wengine wa chama hicho, wakiwemo wanasheria Profesa Abdalla Safari na Mabere Marando pamoja na baadhi ya wakurugenzi na maofisa wa chama hicho walitaja
orodha ya watuhumiwa wa ufisadi nchini.

Dkt. Slaa ambaye aliwahi kutoa orodha aliyoita ya aibu ya watuhumiwa 11 wa ufisadi mkubwa unaolifilisi taifa, mwaka 2007, juzi aliongeza majina mengine matatu, ambapo alimtaja Dkt. John Magufuli kuhusiana na uuzaji wa nyumba za serikali, Bw. Phillip Mangula na Dkt. John Malecela kuhusiana na Fedha za EPA, huku
akimtaja Rais Kikwete kwa kushindwa kuwachukulia hatua mafisadi na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, katika uuzaji wa nyumba za serikali bila kufuata utaratibu.
 
Naona serikali yetu ni ina dini, ndiyo maana inasamehe hata wezi wakubwa (sio wadogo) ili mradi wanarudisha walichoiba au wanajiuzulu chamani.

Ndio maana ni ngumu sana kuwaamini wanachosema ,kila kitu wanafanya ili kutupumbaza tu.
 
TBC watarusha live? Si Wanajiendesha kwa kodi zetu bana. La sivyo nao wajumuishwe kwenye orodha ya mafisadi, wanatuibia kodi zetu

Imeipata wapi?jibu ni humo humo ccm!sasa ni staili ya mwaga mboga nitupe ugali.
Kazi ipo tusubiri majina.

Saturday, 16 April 2011
Fidelis Butahe

WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikijivua gamba kwa kuwataka wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajiondoe wenyewe kwenye uongozi wa chama hicho, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbroad Slaa leo anataja orodha mpya ya mafisadi ndani ya chama hicho tawala ili nao waunganishwe katika orodha hiyo.

Mkurugenzi wa Organaizesheni na Mafunzo wa Chadema, Singo Bensoni aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Dk Slaa atataja majina hayo leo mkoani Tabora katika mkutano wa hadhara kama alivyofanya mwaka 2007, katika Viwanja vya Mwembeyanga, Dar es Salaam.

Alisema katika mkutano huo, Dk Slaa akiwa na viongozi wengine wa Chadema, atataja majina hayo ya mafisadi ili kuipa CCM wakati mzuri wa kuwatambua na kuwachukulia hatua kama kweli ina nia njema ya kujivua gamba.

Hii ni changamoto mpya kwa CCM ambayo tayari imenyooshea kidole genge la mafisadi lililoko ndani ya chama hicho na kuwapa siku 90 watuhumiwa hao kujiuzulu ili kukinusuru.

Bensoni aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa orodha hiyo mpya ya mafisadi inayotarajiwa kutajwa leo, ni kubwa kuliko ile ya mwaka 2007.

"Ushahidi tunao ndiyo maana hata tuliowataja mwaka 2007 hadi leo hawajafungua kesi yoyote mahakamani. Wanasema kuwa wamejivua gamba. Gamba la CCM siyo uzee ni ufisadi," alisema Bensoni na kuongeza: "Tutawakumbusha gamba wanalotakiwa kujivua ni lipi ili Watanzania watambue. Dk Slaa ataweka mambo hadharani katika mkutano huo akiwa pamoja Profesa Abdalah Safari na Mabere Malando."

Alisema licha ya CCM kutoa siku 90 kwa watuhumiwa wa ufisadi wanaotajwatajwa, wapo ambao hawajatajwa kati ya waliotakiwa kujiuzulu kwa tuhuma za hizo. "Hapa sasa ndiyo watajua mafisadi ni kina nani. Tunataka kuwakumbusha gamba ni lipi."

Alisema kuwa orodha hiyo ni mpya na ina tofauti na ile ya Mwembeyanga kwa kuwa tangu kipindi hicho mpaka leo kuna matukio mengi ya ufisadi yaliyoendelea nchini. "Ufisadi wa sasa ni mkubwa sana hivyo orodha itakuwa kubwa, ‘Ni ngoma nzito' na tukimaliza kutaja orodha hiyo tutaendelea na mikutano yetu nchi nzima," alisema Bensoni.

Akizungumzia hatua hiyo ya Chadema, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema: "Chadema wamefilisika kisiasa, walidhani wataitisha CCM kwa hoja ya ufisadi lakini sasa CCM ni chama safi. Kwa mabadiliko tuliyoyafanya, Chadema inatakiwa kucheza ngoma yetu (CCM) na siyo sisi (CCM) kucheza ngoma yao."

Nape alitumia fursa hiyo kuipongeza Serikali kwa uamuzi wake wa kukubali kurudisha muswada wa Katiba kwa wananchi na kuwapa fursa zaidi kujadili suala hilo.





MAFISADI WAPYA HADI SASA NI ;
  1. John Kato mwajiriwa Caspian (KAGODA).
  2. Bharati Goda ni mwajiriwa caspian (KAGODA).
  3. John Samweli Malecela –EPA
  4. Philip Mangula – EPA
  5. John Magufuli – nyumba za Serikali.
SAMAHANI SIJAWEZA KUIHARIRI ILA HAYO NDIO YANAENDELEA .NTAWAJUZA ZAIDI.
PROF.SAFARI.
Anasema kuwa ni wakati wa kudai nyumba za serikali kwa nguvu ya umma , kwani kwenda mahakamani sio muafaka kwani hata majaji wenyewe walijiuzia hivyo hawawezi kutoa haki.
Zidaiwe kwa nguvu ya umma ndio njia pekee ya kupata nyumba hizo kwani viongozi wengi wanakaa hotelini.

Udini.
Wakoloni waliwagawa watu kwa njia za makabila ili wawatawale ,wakagawa watu kwa njia za udini mf.waingereza waliingiza dini na kjuweka watu wao serikalini , na waislamu wengi walikosa nafasi ya kusoma ndio maana hawakuingia serikalini mapema .
Waislamu walipigania uhuru ila , kutokana na waingereza kuwabagua , ndio maana waliamua kupinga ukoloni ili waweza kuweka serikali ambayo haiwabagui, anasema ugomvi wa Nyerere na shehe takadir kuhusu waislamu kubaguliwa , na anasema kuwa ndani ya CDM hakuna udini ila ndani ya nchi kuna tatizo la kihistoria la kidini.
Anasema kuwa ni mbinu ya serikali kuwagawa watanzania ili waweze kuwatawala .
Alipojitoa CUF na kujiunga na CDM alifuatwa na mashehe wakimwambia kuwa yeye ameamua kujiunga na wakristo , yeye akajibu kuwa walitaka yeye aende kwenye chama gani? Mbona CCM sio ya waislamu kwani ukiondoka JK wengi waliopo serikalini ni
Anasema yeye hajabatizwa na pia Slaa sio yohana mbatizaji na amewataka waislamu kuungana pamoja ili kupigania haki za waislamu kwani CCM ndio ambao wanawakandamiza waislamu hivyo ni bora wakajiunga na CDM kwa wingi ili waweze kudai haki zao tangu awali na wasisubiri , waingie cdm tangu mwanzo ili wawe sehemu ya kupigania haki zao na njia nzuri ni kuhakikisha nkuwa wanajiunga ili kuingiza hoja zao kabla ya cdm kuingia serikalini na ni lazima waislamu wakitaka madai yao yasikilizwe wanapaswa kuingia sasa na sio wawasusie cdm kwa hoja za udini halafu baadae waje walalamike .
Kuna haja ya kujiunga na cdm sasa.

MARANDO.
Ameanza kwa kusema Slaa alishinda ila kura zilichakachuliwa na hivyo ndio maana Slaa ameamua kuingia kazini rasmi kujenga chama ili kiwe imara na kuweza kujiandaa na uchaguzi ujao .
Anasedma yeye ataongelea mambo matatu.(KATIBA , EPA , NA MAGAMBA YA CCM).
KATIBA .
Hii ilikuwa hoja ya CDM kwani iliyopo inawafanya mafisadi watamalaki, katiba ni maji, ni unga ni kila kitu ambacho kipo , ukishaweka katiba mengine yote yanawezekana .
Anasema JK alishauriwa na watu kuhusu katiba , ila aliweza kjuipata muswada wa sheria kutokana na taaluma yake ya kishushu aliupata mapema na kuisambaza a kwani jk hakuwa tayari kupata katiba .
Amewataka watanzania kuwa macho kwani nia ya ccm ni kuendelea na katiba iliyopo na sio kweli kjuwa wanataka katiba mpya.
Tofauti ya CCM na CDM kwenye katiba ni kuwa CCM wanataka iliyopo iwekwe viraka , na CDM wanataka mpya .
Cdm wanataka mambo yafuatayo kwenhye katiba mpya.
1. Kupunguza madaraka ya rais haswa ktk kuteua watu mbalimbali.
2. Viongozi wa wilaya wapigiwe kura na sio kuteuliwa na rais…..
3. Madini yalindwe na katiba
4.Power of recall kwa wabunge na madiwani
Kuhusu EPA na magamba ya CCM.
Ccm ndio gamba la watanzania na tunapaswa kuliondoa hilo gamba ccm na sio wao waondoane wenyewe
Ccm ndio gamba lenyewe na linapaswa kuondolewa moja kwa moja
Lissu amewafundishwa wabunge sheria .
Epa ni ya jk kwani ndio ilimuingiza madarakani.
Kikwete amesamehe wezi wa EPA wakati wezi wanapaswa kupelekwa jela .
Slaa alipotaja mafisadi ccm walisema ni uongo kuwa hakuna mafisadi , jk juzi kakiri kuwa kuna mafisadi wengi ndani ya chama na walitaja listi yao ya mafisadi , lowass,change na rostam.
Jk sio jasiri na hana ubavu wa kuweza kupambana na mafisadi wa ndani ya chama chake kwani hawezi kuchukua hatua .
Jk alishindwa hata kujua mafisadi dowans.
Kagoda .
Kuna visamaki vidogo vimeshitakiwa ila kagoda hawajapelekwa mahakamani ,rais alisema hawajui wahusika wa Kagoda ,
Kemhondo willium ni jina la bandia – John Kato mwajiriwa Caspian
Francis wilium jina bandia –Bharati goda na ni mwajiriwa caspian
Aliweka majeshi yake kwa siku tatu na majina halisi ni haya;
Na jk kama hawajui aende ofisini kwake atampa mpaka picha
Kama jk anataka atume watu ofisini kwake ili waende kuchukua picha .
Anasema yuko tayari kama jk akimtaka kujitolea apewe jalada la kagoda na atawafikisha mahakamani na wataishia keko.
Wengine kagoda ni malecela na Mangula .
Cdm tulimuita safari ili aje aweze kutueleza ni jinsi gani tunaweza kiutatua matatizo ya waislamu na pindi tukiingia madarakani tutakuwa tayari kuzitekelezaz kwani ccm kwa miaka 60 wameshindwa kutatua matataizo hayo.


DR.SLAA.
Ameanza kwa kuwataka maasikari kuacha siasa na haswa jana walipoamua kuzuia maandamano kwa madai kuwa hali ya nchi ni tete , amewataka polisi kuacha kufanya siasa.hiyo hali wameipima hospitali gani mpaka kujua hali ni tete , na pia pesa zimeibiwa ndani ya jeshi la polisi na hata mdhibiti mkuu amesema uozo wa polisi.
Sababu ya pili waliyotoa polisi kuwa hoja yetu ya maandamano imefutwa na serikali ,hiyo sio kazi ya polisi kusema kuwa maandamano yamevunjwa .
Polisi kuweni na uchungu na nchi hii kwani mama, baba , watoto wenu wanaumia sana kutokana na ufisadi wan chi hii, pia usalama wa taifa wanapaswa sasa kuamka na kulinda masilahi ya taifa na sio kulinda masilahi ya viongozi kama wanavyofanya sasa.
Nchi haiwezi kutawalika ni mpaka mafisadi wote wakamatwe kwani haiwezekani kluwa na mafisadi na nchi ikaweza kutawalika.
Wananchi wa tabora kwa ujumla wenu mmefanywa kuwa wateja wa CCM kwani hii ni ngome yao ya kuvuna kura wakati hakuna hata barabara kwenye mkutano wenu.
Hawezi kujibu vyama wanaozunguka kuisema CDM ila hoja yake ni maisha ya watanzania tuu na sio vinginevyo kwani maisha ni magumu kwa kila mwananchi bila kiujali vyama vyao.
Maeneo waliyoikataa ccm kuna lami ila huku ambako kuna ccm hakuna barabara , za kwenda Urambo,Bukene, Nzega … huku mmetelekezwa .
Rais anaahidi kujenga viwanja vya ndege wakati cha Tabora hakitumiki sasa hivyo vipya anaweza?
Kwa taarifa yenu mimi ni mwana Tabora kwani nilikulia na kusoma Itaga , wakati huo kulikuwa na viwanda vya nyuzi, maziwa n.k. na kwelina sababu nzito ya kuikataa CCM.
Makisio ya kodi ya tabora mwaka huu ni kulipa serikali kuu 9.9 bilioni.ila hakuna barabara je?kodi zenu zinapelekwa wapi?
Anazungumzia juu ya nyumba za serikali na sasa muda umeisha wa kuendelea kuvumilia kuhusu nyumba za serikali lazima sasa zirejeshwe mara moja .
Mkapa anahusika na uuzwaji wa nyumba za Serikali.
Wale wanaosema kuwa slaa anamchukia jk kwa sababu ya dini . kwani alimshughulikia sumaye .
Mkapa na Magufuli kwenye kuuza nyumba za serikali na wao ni mafisadi .
Ndege za jk za kampeni zilitoka kwa watu walioiba EPA na ndio maana ameshindwa kuchukua hatua kwani anashirikiana nao .
Kama JK kawapa mafisadi siku 90 ndani ya chama chake nay eye Tunampa JK na eye siku 90 ataje fedha za mabango yake dola 1.5 milioni aseme zilitoka wapi zilizotumwa CANADA kutengeneza 2010 election .na yeye anapaswa kujitoa kama atashindwa kuchukua hatua hizo.
Hiyo ina maana gani kwa kiswahili? (hapo kwenye red)
 
Omari, hakuna perfect political party kama jinsi hakuna absolute freedom kwenye jambo lolote. Hivyo kila chama, kina madhaifu yake. Kwenye mada yangu humu jf ya 'CCM imechokwa Chadema Haijajipanga', niliorodhesha madhaifu ya CCM na ya Chadema. wapenzi wa CCM humu walijikalia kimya, wapenzi wa Chadema na viongozi wao humu wakanishukia kuwa nina chuki binafsi dhidi ya Chadema.

Wenzao CCM hawakujibu kitu lakini madhaifu yale wameanza kuyafanyia kazi kwa kusafisha nyumba yao, wao Chadema kila wakikosolewa, kamwe hawataki kukubali makosa, they play difensive huku manazi wao wakiporomosha kila aina ya matukano humu!.

Hakuna ubishi kuwa listi ya mafisadi na vita ya ufisadi, imewapa Chadema good political mileages, nawashauri wasikalie kushupalia vita ya ufisadi tuu kutwa kucha kwa maandamano na mikutano ya hadhara, its about time, wajenge chama, wajipange strategicaly over and above kubadili mind set ya Watanzania kuwa wao wanaweza, concetration iwe kusonga mbele.

Kwa vile vita ya ufisadi ndio mtaji pekee wa Chadema, sasa CCM inajipanga kuula mtaji huo, na believe me, CCM ikijipanga na kusafisha nyumba yake ikatakata dhidi ya tuhuma zote za ufisadi, 2015 ikasimamisha mgombea makini, Chadema itakosa pa kupumulia, tutarudi kule kule kwenye nchi ya chama kimoja, save CUF kwa Zanzibar!.

Mimi binafsi naikubali sana Chadema na naiwish all the best ili kufikisha idadi ya simple majority ndani ya bunge la 2015, ila kwa mwendo huu wa kuimba wimbo ule ule, wananitia mashaka!.

Heshima zikufikie mkuu Pasco,
Najua swala hili la CCM kumtoa Makamba na kumwingiza Makamba linaonekana kwa wana CCM na wapenzi kwamba ni jambo jema. Ila ukweli ni kwamba hakuna kitu kimetokea mpaka sasa zaidi ya kupwaya kimamlaka, dira, mfumo na mshiko wa kuwa na uthubutu wa kuwaletea wananchi maisha bora.

CDM imekuwa mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi kuzitambua kerao zao, hasa maisha magumu, ukosefu wa elimu bora, ukosefu wa miundo mbinu thabiti na huduma zote muhimu za jamii. na imekuwa ikiwakumbusha wananchi matokeo ya umasikini huu ni kushindwa kwa uongozi wa CCM kwa miaka 50. Wapo wananchi wengi wanaoipenda CDM kwa sera za ukombozi.

Ili kuweza kuendesha nchi lazima ujue ni matatizo gani yaliyopo na jinsi ya kuyatatatua kwa resources zilizopo.
Hatuwezi kutumia rasilimali zetu wakati tukivuna baadhi wanakuala, ufisadi utaendelea kupigiwa kelele siku zote kwani huo upo sehemu nyingi na ndio bomba kubwa linalokula uchumi wa nchi.

CCM kubadili sura hukuwezi kurudisha mapenzi kwa Mtanzania ambaye hana ajira, anakosa dawa hospitali, hana maji wala barabara. Ananguzo ya umeme isiyotoa nishati. Akiingia mahakamni hana haki mpaka atoe kitu. Mtoto wake anakwenda shule yenye mwalimu mmoja.
Anachopata nia ahadi ndani ya VX kila baada ya miaka mitano na kunedelea kuisikia jina la Mwinyi, Mkapa, Makamba, Kikwete , karume. Malecela nk kila mwaka hadi mwaka kwani linabadilika la kwanza tu , na hakuna mtanzania mwenye nafasi ya sawa ya kufika huko walipo.

Pasco,
CDM imejipanga kisera na kimkamkati, kuwataja mafisadi ni sawa na kujiweka wazi kuwa mbadhirifu na mwizi hakubaliki kwenye nyumba hii, hata CDM ikiingia ikulu haitavumilia kiongozi wake mchafu.

CCM inatakiwa ibadilike kimfumo, itoa mzizi wa kulindana na kuacha kuwa tumbili kuficha kichwa na kuacha mwili mzima wazi. Kelele za jukwaani wanazopiga CCM wenye dola haziwezi kuwaletea mabadiliko.
Sidhani kama mwenye akili timamu atanunua kufanya suluhu ya kijuha na mafisadi bila kuwachukulia hatua, kama CCM wamekubali kuwa kweli wao ndio mafisadi, na wameona hawawezi kukaa na watu wenye tuhuma za kuibia taifa masikini, kwa nini wasimruhusu DPP awafungulie mashitaka ya makosa waliohusika nayo, wasiwatoa kwenye nyadhifa za serikali? wawaachia wapepelezi na CAG kufanya kazi yake na kila mtu kwa wajibika kisheria?

Ni wangapi wapo serikalini leo wanatuibia na kulitia taifa hasara? Je ni kweli ni lazima tuwe gizani kupoteza uzalishaji eti hatuna uwezo wa kuwa na nishati ya uhakika? Huu wote ni ufisadi.

Kamanda Ngoma ya Rushwa, ufisadi, madaraka mabovu na utawala wa urithi umewatoa viongozi na vyama vingi vikongwe madarakani kama Mexco, Misri, Tunisia, Kenya, Zambia, nk Si dhani kama Tanzania chini ya CCM itaweza kuendelea kuhadaa kizazi cha sasa chenye kiu ya kweli ya Maisha bora bila usawa wa mafanikio.

Leo Tanzania tunazaidi ya vyuo vikuu 25 amabavyo kila mwaka vinaongeza wahitimu mtaani bila mategemeo yeyote ya maisha bora. Graduates hawa ndio wamejaa vijiweni wakiona hali halisi ya maisha mabovu, na kila aliyedarasani sasa hivi hana uhakika wa nini kitatokea baada ya kumaliza. Sasa unasema kweli ngonjera za January na Nape zinawaletea ajira na maisha bora?

CCM wanatakiwa kujua wajibu wa chama tawala sio kujifanya na wao wanataka kuwa wakati ni watawala. Akili za yeyote mwenye kadi ya ccm huwa kama zinakutu, ya kufikiri, kuona, na kutenda.

Tanzania inahitaji watawala wanaojua shida zao na utatuzi, usanii wa CCM umefika kikomo na hawana jipya zaidi ya kuendekeza siasa za kiimla badala ya kuwajibika.
 
CHADEMA sasa imeanza kutumika kuwasafisha Rostam Aziz, Edward Lowassa na Andrew Chenge wasifukuzwe kwenye nafasi zao za uongozi ndani ya CCM.

Kutumika kwa CHADEMA ni sehemu ya mkakati wa Rostam, Lowassa na wenzake kuzuia wasifukuzwe kuwa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) na nafasi zao nyingine za uongozi.

Mkakati huo unahusu kuitumia CHADEMA na viongozi wa vyama vingine vya upinzani, kama CUF, NCCR Mageuzi, UDP, TLP na DP ya Christopher Mtikila, kutoa tuhuma za kupikwa kwa viongozi wengi zaidi ndani ya CCM ili ionekane kuwa viongozi wote wa CCM wana tuhuma za ufisadi na si Lowassa, Rostam na Chenge tu.

Tuhuma hizo za kutengenezwa sasa zimeanza kusambazwa na kina Rostam dhidi ya Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Jakaya Kikwete, na viongozi wengine waandamizi wa chama ambao wanaheshimika katika jamii, akiwemo John Magufuli, Samuel Malecela, Frederick Sumaye, Samuel Sitta, Bernard Membe na wengine.

Rostam na Lowassa wanaitumia CHADEMA ili kuzuia kufukuzwa kwenye CCM kupitia LIST OF SHAME mpya ya chama hicho cha upinzani ambayo imewataja kina Magufuli na Malecela. Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilibrod Slaa, ameingizwa mkenge
na viongozi wenzake ndani ya chama hicho kuitoa LIST OF SHAME mpya bila kujua kuwa mpango huo umepikwa na kina Rostam.
Rostam na Lowassa kwa kutumia viongozi wa CHADEMA ambao wako nao karibu wamemuingiza mkenge Dk. Slaa aitoe List of Shame mpya ili kuleta mvurugano ndani ya CCM.

Siyo "coincidence" hata kidogo kuwa CHADEMA waliibuka na LIST OF SHAME yenye majina mapya siku chache tu baada ya CCM kuwataka kina Rostam, Lowassa na Chenge wajiuzulu.

Inaeleweka wazi kuwa Rostam na Lowassa wako karibu sana na baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA (siyo Dk. SLAA) na wamekuwa na mawasiliano ya mara kwa mara nao.

"Wanachotaka kufanya kina Rostam, Lowassa na Chenge ni kuibua tuhuma mpya za uongo dhidi ya Kikwete, Magufuli, Malecela, Sitta, Mwakyembe, Sumaye na viongozi wengine wa CCM ili wapate kujitetea kwenye vikao vya NEC vijavyo kuwa mbona kuna viongozi wengi za CCM wenye tuhuma lakini wanatakiwa wajiuzulu wao tu," alisema mpambe mmoja wa Lowassa.

Pia, Rostam na Lowassa wamekuwa wakitumia baadhi ya magazeti, likiwemo Tanzania Daima linalomilikiwa na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, katika mkakati huo wa kuibua tuhuma za kupikwa za ufisadi dhidi ya viongozi wengi zaidi ndani ya CCM ili wajinurusu kufukuzwa.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wiki hii CHADEMA ililazimika kukanusha habari za Tanzania Daima, gazeti la mwenyekiti wa chama hicho, zilizodai kuwa Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, ametajwa kwenye List of Shame mpya ya CHADEMA.

Lowassa amemuajiri mhariri mkuu wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda, kwenye jarida lake la UMOJA na amekuwa akimtumia Kibanda mara kwa mara kutoa habari na makala za kumsafisha Lowassa, Rostam na Chenge kwenye Tanzania Daima.

Inafahamika wazi kuwa Kibanda ana urafiki wa karibu sana na Lowassa na Rostam na amekuwa akitumiwa mara kadhaa kuwachafua maadui zao, ikiwemo Samuel Sitta, Bernard Membe, Harisson Mwakyembe, na wengine.

Mafisadi wamekuwa wakipenda kulitumia sana Tanzania Daima mara nyingi kujaribu kujisafisha kwa kuwa linaheshimika kwenye jamii kwa kuonekana kuwa gazeti "huru" kuliko magazeti ya RAI na Mtanzania yanayomilikwa na Rostam.

Kwa kufuata maelekezo ya Lowassa, Tanzania Daima juzi iliandika habari ya uongo kwa makusudi kuwa CHADEMA imemtaja Sumaye kwenye List of Shame mpya.

Bado ni kitendawili kikubwa kwa nini Mbowe anamruhusu mhariri wake mkuu, Kibanda, kuwa mwajiriwa wa Lowassa na hivyo kuwa na mgongano wa kimaslahi na kimaadili (conflict of interest/ethical dilemma) katika kazi zake Tanzania Daima.
 
Hakuna aliye msafi NDANI ya CCM - But - RA, EL na AC ni wachafu sana - hawasafishiki!!!
 
andikeni maneno mengi kama biblia lakini jibuni swali langu

kati ya mbowe na magufuli nani fisadi.

mbona ndesamburo kanunua majumba mpaka ulaya na halipi kodi hilo hamlioni.

Enyi vipofu wa kanda ya kaskazini, mmejawa na tama ya madaraka hata hamuoni matatizo yenu.

malecela fisadi sawa lete ushahidi nyie mnaleta ngonjera.

hii mmefulia kweli hamtaonja ikulu waroho nyie
 
CDM tulimuita Safari ili aje aweze kutueleza ni jinsi gani tunaweza kiutatua matatizo ya waislamu na pindi tukiingia madarakani tutakuwa tayari kuzitekeleza kwani CCM kwa miaka 60 wameshindwa kutatua matataizo hayo.

My Take: Wakati CCM inategemea mabadiliko ya sura za uongozi kujiondoa gamba la UFISADI, Chadema wanamtegemea Dr Safari kuwakwepesha na gamba la UDINI.

Sijui wenzangu mnapata ujumbe gani kutoka kwa kauli kama hii. Na pia nawashauri Chadema kufanya vetting ya ripoti ama matamko yanayotolewa na viongozi wenu wa juu kama Mpaka Kieleweke ambaye kila mara huishia kuwaingiza matatani. Ofcourse kama mnalenga watanzania makini katika ajenda zenu ambao husoma zaidi ya maandishi.
 
CHADEMA sasa imeanza kutumika kuwasafisha Rostam Aziz, Edward Lowassa na Andrew Chenge wasifukuzwe kwenye nafasi zao za uongozi ndani ya CCM. Kutumika kwa CHADEMA ni sehemu ya mkakati wa Rostam, Lowassa na wenzake kuzuia wasifukuzwe kuwa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) na nafasi zao nyingine za uongozi. blah blah blah................................
Duh, Mkuu Fareed naona namba ya mliokubali kutumiwa kama kitambaa cha kupangusia mafua ya CCM inazidi kuongezeka. Mnachosahau ni kuwa hayo si mafua ya kawaida na mtatumiwa sana lakini CCM haiponi, imebanwa kisawasawa. Chadema inajua kuwa kumuua nyoka yabidi apondwe kichwa hata akijivua magamba hadi damu kuchuruzika. Eti leo Chadema waungane na Lowassa kumchafua Kikwete, loo hawa jamaa ujue hawakukutana barabarani hebo. Kikwete anamhitaji Lowassa kuliko hata Lowassa anavyomhitaji Kikwete na kama unabisha vuta subira. Kikwete bila Rostamu na Lowassa ni kama gari lisilo na engine !
 
andikeni maneno mengi kama biblia lakini jibuni swali langu

kati ya mbowe na magufuli nani fisadi.
Nani akujibu wakati jibu unalo?Unaelekea unamfahamu Magufuli kwa undani zaidi ya sie unaotuuliza.Why not ask hime mnapokuwa faragha?
mbona ndesamburo kanunua majumba mpaka ulaya na halipi kodi hilo hamlioni.
Ulaya ni kubwa bimdogo.Did you mean Poland au United Kingdom?Na huko Ulaya ni mashabiki wa Chadema mpaka wamwachie Ndesamburo asilipe kodi?
Enyi vipofu wa kanda ya kaskazini, mmejawa na tama ya madaraka hata hamuoni matatizo yenu.
Mwanadada,usirushe mawe ilhali wewe ni mkazi wa nyumba ya vioo.
malecela fisadi sawa lete ushahidi nyie mnaleta ngonjera.
Umelewa njaa au kuna shughuli umefanya usiku kucha imekuchanganya akili.Kwa hiyo ushahidi wa ufisadi unahitajika kwa Malecela na mwenza wako Magufuli pekee lakini kwa Mbowe hakuhitajiki ushahidi?
hii mmefulia kweli hamtaonja ikulu waroho nyie
BoRa uroho wENYE minajili ya kuikomboa nchi yetu kuliko ukahaba wa kifikra.Unaweza kukesha hapa kujipendekeza kwa Magufuli kwa matarajio ya kuwa another nyumba ndogo lakini kama huwajui mafisadi vizuri muulize Tido Mhando....used and abused is name of their game
 
- Kwa kweli huu ushahidi unaweza kumfunga Malecela mahakamani kwa wizi wa EPA, mkuu you are a genius!

William @ NYC, USA.

Kumbe ndio maana mnaogopa kwenda mahakamani?Mnaogopa jela.Hatuhitaji kumfunga fisadi huyo.Wana CCM wenzake walishamwadhibu kwa kumbwaga kwenye kura za maoni.Inclusion yake kwenye listi hii mpya ya mafisadi ni mwendelezo tu wa payback kwa matusi yake kwa Watanzania kuwa they could go to hell.Apelekwe jela ili atubebeshe mzigo mwingine wa kumtunza huko jela?Na presha ikimpanda huko jela si itakuwa mzigo mwingine kwa taxpayers?No,atajifunga mwenyewe kisaikolojia.Mshahara wa dhambi ni mauti.Kila fisadi aliyefisadi wanyonge wa Tanzania hii ataonjeshwa joto ya jiwe hapa hapa duniani,hayo mengine tunamwachia Muumba.

Mzee wako ni mtu anayependa sana madaraka,ndio maana licha ya kushauriwa apumzike na kuziacha damu changa kwenye uongozi akang'ang'ania na matokeo yake akapigwa chini.Na hiyo ni baada ya majaribio yake mfululizo kutaka urais through CCM lakini kila mara akapigwa chini.Huyu ni mtu mchafu aliyewahi kukemewa na Baba wa Taifa,na laana ya Nyerere itamwandama mpaka anamfuata mbele ya haki.

Sasa kwa wapenda hadhi na madaraka,adhabu pekee kwao si jela tu.Angalia mwanae unavyohangaika kutetea hadhi.Unadhani kama iko hivyo kwa mwana,je kwa baba mwenyewe ikoje?
 
Mlalahoi;1873359]
W. J. Malecela;1873084

Mzee wako ni mtu anayependa sana madaraka,ndio maana licha ya kushauriwa apumzike na kuziacha damu changa kwenye uongozi akang'ang'ania na matokeo yake akapigwa chini.

Hivi Dr Slaa ana umri gani vile?
 
Jamani,

Mlitegemea mtoto wa Tingatinga Malecela huyu aliyeko majuu akubali kwamba baba yake ni fisadi?? Inawezekana kabisa hajui baba yake alipataje pesa ya kumsomesha mpaka hapo alipo, au anajua wazi the whole deal kama alivyosema yeye kwamba TANU na baadaye CCM walikuwa wanakopa kupitai EPA.

So, William as from today uelewe kwamba huo ndo ufisadi unaosemwa, inawezekana mzee hakuchukua hata senti moja, lakini yuko kwenye group la watu waliopitisha sera hiyo. Kwa kujua au kutojua, hiyo siyo excuse.
 
CHADEMA sasa imeanza kutumika kuwasafisha Rostam Aziz, Edward Lowassa na Andrew Chenge wasifukuzwe kwenye nafasi zao za uongozi ndani ya CCM.

Kutumika kwa CHADEMA ni sehemu ya mkakati wa Rostam, Lowassa na wenzake kuzuia wasifukuzwe kuwa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) na nafasi zao nyingine za uongozi.

Mkakati huo unahusu kuitumia CHADEMA na viongozi wa vyama vingine vya upinzani, kama CUF, NCCR Mageuzi, UDP, TLP na DP ya Christopher Mtikila, kutoa tuhuma za kupikwa kwa viongozi wengi zaidi ndani ya CCM ili ionekane kuwa viongozi wote wa CCM wana tuhuma za ufisadi na si Lowassa, Rostam na Chenge tu.

Tuhuma hizo za kutengenezwa sasa zimeanza kusambazwa na kina Rostam dhidi ya Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Jakaya Kikwete, na viongozi wengine waandamizi wa chama ambao wanaheshimika katika jamii, akiwemo John Magufuli, Samuel Malecela, Frederick Sumaye, Samuel Sitta, Bernard Membe na wengine.

Rostam na Lowassa wanaitumia CHADEMA ili kuzuia kufukuzwa kwenye CCM kupitia LIST OF SHAME mpya ya chama hicho cha upinzani ambayo imewataja kina Magufuli na Malecela. Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilibrod Slaa, ameingizwa mkenge
na viongozi wenzake ndani ya chama hicho kuitoa LIST OF SHAME mpya bila kujua kuwa mpango huo umepikwa na kina Rostam.
Rostam na Lowassa kwa kutumia viongozi wa CHADEMA ambao wako nao karibu wamemuingiza mkenge Dk. Slaa aitoe List of Shame mpya ili kuleta mvurugano ndani ya CCM.

Siyo "coincidence" hata kidogo kuwa CHADEMA waliibuka na LIST OF SHAME yenye majina mapya siku chache tu baada ya CCM kuwataka kina Rostam, Lowassa na Chenge wajiuzulu.

Inaeleweka wazi kuwa Rostam na Lowassa wako karibu sana na baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA (siyo Dk. SLAA) na wamekuwa na mawasiliano ya mara kwa mara nao.

"Wanachotaka kufanya kina Rostam, Lowassa na Chenge ni kuibua tuhuma mpya za uongo dhidi ya Kikwete, Magufuli, Malecela, Sitta, Mwakyembe, Sumaye na viongozi wengine wa CCM ili wapate kujitetea kwenye vikao vya NEC vijavyo kuwa mbona kuna viongozi wengi za CCM wenye tuhuma lakini wanatakiwa wajiuzulu wao tu," alisema mpambe mmoja wa Lowassa.

Pia, Rostam na Lowassa wamekuwa wakitumia baadhi ya magazeti, likiwemo Tanzania Daima linalomilikiwa na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, katika mkakati huo wa kuibua tuhuma za kupikwa za ufisadi dhidi ya viongozi wengi zaidi ndani ya CCM ili wajinurusu kufukuzwa.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wiki hii CHADEMA ililazimika kukanusha habari za Tanzania Daima, gazeti la mwenyekiti wa chama hicho, zilizodai kuwa Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, ametajwa kwenye List of Shame mpya ya CHADEMA.

Lowassa amemuajiri mhariri mkuu wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda, kwenye jarida lake la UMOJA na amekuwa akimtumia Kibanda mara kwa mara kutoa habari na makala za kumsafisha Lowassa, Rostam na Chenge kwenye Tanzania Daima.

Inafahamika wazi kuwa Kibanda ana urafiki wa karibu sana na Lowassa na Rostam na amekuwa akitumiwa mara kadhaa kuwachafua maadui zao, ikiwemo Samuel Sitta, Bernard Membe, Harisson Mwakyembe, na wengine.

Mafisadi wamekuwa wakipenda kulitumia sana Tanzania Daima mara nyingi kujaribu kujisafisha kwa kuwa linaheshimika kwenye jamii kwa kuonekana kuwa gazeti "huru" kuliko magazeti ya RAI na Mtanzania yanayomilikwa na Rostam.

Kwa kufuata maelekezo ya Lowassa, Tanzania Daima juzi iliandika habari ya uongo kwa makusudi kuwa CHADEMA imemtaja Sumaye kwenye List of Shame mpya.

Bado ni kitendawili kikubwa kwa nini Mbowe anamruhusu mhariri wake mkuu, Kibanda, kuwa mwajiriwa wa Lowassa na hivyo kuwa na mgongano wa kimaslahi na kimaadili (conflict of interest/ethical dilemma) katika kazi zake Tanzania Daima.

Kama kweli Lowassa anamchafua Kiwete ili kujinusuru, kwanini Kikwete asitoe maagizo kwa DPP kuwa watu wote weny tuhuma wafikishwe mahakamani? Hapo ndio mizizi yote ya Fitina ingekatwa. MAFISADI PAPA KIKWETE. LOWASSA, ROSTAM NA CHENGE WOTE NI KITU KIMOJA
 
Nani akujibu wakati jibu unalo?Unaelekea unamfahamu Magufuli kwa undani zaidi ya sie unaotuuliza.Why not ask hime mnapokuwa faragha?

Ulaya ni kubwa bimdogo.Did you mean Poland au United Kingdom?Na huko Ulaya ni mashabiki wa Chadema mpaka wamwachie Ndesamburo asilipe kodi?

Mwanadada,usirushe mawe ilhali wewe ni mkazi wa nyumba ya vioo.

Umelewa njaa au kuna shughuli umefanya usiku kucha imekuchanganya akili.Kwa hiyo ushahidi wa ufisadi unahitajika kwa Malecela na mwenza wako Magufuli pekee lakini kwa Mbowe hakuhitajiki ushahidi?

BoRa uroho wENYE minajili ya kuikomboa nchi yetu kuliko ukahaba wa kifikra.Unaweza kukesha hapa kujipendekeza kwa Magufuli kwa matarajio ya kuwa another nyumba ndogo lakini kama huwajui mafisadi vizuri muulize Tido Mhando....used and abused is name of their game

wewe sio mlalahoi ni mtetea mafisadi wa chadema kisa ukaskazini unawasumbua.

nimeuliza magufuli na mbowe nani fisadi.

legeeni wote hamna la maana mnatetea matumbo na uroho wenu. mafisi nyie mnavizia mkono uanguke.

ndesamburo na mbowe ni mafisadi wakubwa.

mmefulia kuwaambia magufuli malecela mangula mafisadi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom