Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,580
- 23,915
Malecela aisafisha CCM dhidi ya tuhuma za ufisadi
2009-01-12 10:34:05
Na Pendo Fundisha, Mbeya
Wakati Chama Cha Mapinduzi kinatuhumiwa kuhusika katika matukio ya ufisadi, Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chama hicho Tanzania Bara, John Samwel Malecela, amekitetea chama chake dhidi ya tuhuma hizo.
Chama hicho kinaelekezwa tuhuma kwamba kilihusika katika uchotaji wa fedha kutoka Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kupitia Kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, ambayo wamiliki wake hadi sasa hawajulikani.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa juzi jioni katika Hoteli ya Ifese Community Centre baada ya kuwasili kwa ajili ya kuiongezea nguvu timu ya kampeni za CCM za ubunge wa Mbeya Vijijini, Malecela alivitaka vyama vya upinzani kutokukihusisha CCM na tuhuma za ufisadi na rushwa, akisema kuwa hayo ni mapungufu na dosari za mtu mmoja mmoja na hazihusiani na Chama hicho. Hata hivyo,hakufafanua kauli yake.
Alisema katiba ya chama hicho inapiga vita mambo maovu na kwamba watu wote wanaojihusisha na vitendo viovu wachukuliwe hatua za kisheria kwa mujibu wa taratibu na sheria zilizopo.
Alisema kila palipo na viongozi lazima kuna dosari zinazoweza kujitokeza na kwamba dosari za mtu binafsi zisihusishwe na CCM, ambayo ipo mstari wa mbele kutekeleza ilani yake ya uchaguzi iliyolenga kuleta maendeleo kwa wananchi.
Aidha, Malecela alisema kuwa hata vyama vya upinzani ambavyo vimekuwa mstari wa mbele kukituhumu CCM, navyo vimekuwa vikikabiliwa na migogoro ambapo baadhi ya viongozi wake wamekuwa wakituhumiana kutumia vibaya fedha za vyama vyao.
Makamu Mwenyekiti huyo mstaafu amekuwa kada mwandamizi wa kwanza kukitetea chama chake dhidi ya tuhuma za ufisadi katika kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge wa Mbeya Vijijini.
Wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo Januari 4, Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Ali Hassan Mwinyi alikwepa kuzungumzia tuhuma za ufisadi dhidi ya CCM.
Hata viongozi wote waliohutubia, wakiwemo Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Pius Msekwa; Katibu Mkuu, Yusuf Makamba; Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na mgombea wa CCM, Mchungaji Jackson Mwanjale, hakuna aliyezungumzia chochote kuhusu ufisadi, ambao hivi sasa ndiyo ajenda kubwa nchini.
Kauli za kuitetea CCM dhidi ya ufisadi hususan tuhuma za uhusiano wa CCM na Kagoda katika uchotaji wa fedha za EPA, zimekuwa zikitolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Kapteni John Chiligati.
Malecela alisema amekwenda Mbeya Vijijini kwa ajili ya kusaidia kampeni za kumnadi Mchungaji Mwanjale, lakini akaongeza kuwa wenye jukumu la kufanya kampeni ni kamati ya siasa ya Wilaya ya Mbeya.
Kweli za mwizi ni arobaini !
2009-01-12 10:34:05
Na Pendo Fundisha, Mbeya
Wakati Chama Cha Mapinduzi kinatuhumiwa kuhusika katika matukio ya ufisadi, Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chama hicho Tanzania Bara, John Samwel Malecela, amekitetea chama chake dhidi ya tuhuma hizo.
Chama hicho kinaelekezwa tuhuma kwamba kilihusika katika uchotaji wa fedha kutoka Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kupitia Kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, ambayo wamiliki wake hadi sasa hawajulikani.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa juzi jioni katika Hoteli ya Ifese Community Centre baada ya kuwasili kwa ajili ya kuiongezea nguvu timu ya kampeni za CCM za ubunge wa Mbeya Vijijini, Malecela alivitaka vyama vya upinzani kutokukihusisha CCM na tuhuma za ufisadi na rushwa, akisema kuwa hayo ni mapungufu na dosari za mtu mmoja mmoja na hazihusiani na Chama hicho. Hata hivyo,hakufafanua kauli yake.
Alisema katiba ya chama hicho inapiga vita mambo maovu na kwamba watu wote wanaojihusisha na vitendo viovu wachukuliwe hatua za kisheria kwa mujibu wa taratibu na sheria zilizopo.
Alisema kila palipo na viongozi lazima kuna dosari zinazoweza kujitokeza na kwamba dosari za mtu binafsi zisihusishwe na CCM, ambayo ipo mstari wa mbele kutekeleza ilani yake ya uchaguzi iliyolenga kuleta maendeleo kwa wananchi.
Aidha, Malecela alisema kuwa hata vyama vya upinzani ambavyo vimekuwa mstari wa mbele kukituhumu CCM, navyo vimekuwa vikikabiliwa na migogoro ambapo baadhi ya viongozi wake wamekuwa wakituhumiana kutumia vibaya fedha za vyama vyao.
Makamu Mwenyekiti huyo mstaafu amekuwa kada mwandamizi wa kwanza kukitetea chama chake dhidi ya tuhuma za ufisadi katika kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge wa Mbeya Vijijini.
Wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo Januari 4, Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Ali Hassan Mwinyi alikwepa kuzungumzia tuhuma za ufisadi dhidi ya CCM.
Hata viongozi wote waliohutubia, wakiwemo Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Pius Msekwa; Katibu Mkuu, Yusuf Makamba; Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na mgombea wa CCM, Mchungaji Jackson Mwanjale, hakuna aliyezungumzia chochote kuhusu ufisadi, ambao hivi sasa ndiyo ajenda kubwa nchini.
Kauli za kuitetea CCM dhidi ya ufisadi hususan tuhuma za uhusiano wa CCM na Kagoda katika uchotaji wa fedha za EPA, zimekuwa zikitolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Kapteni John Chiligati.
Malecela alisema amekwenda Mbeya Vijijini kwa ajili ya kusaidia kampeni za kumnadi Mchungaji Mwanjale, lakini akaongeza kuwa wenye jukumu la kufanya kampeni ni kamati ya siasa ya Wilaya ya Mbeya.
Kweli za mwizi ni arobaini !