Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Status
Not open for further replies.
MMH kazi ipo.

Ok lakini kama waliotajwa wanahisi au kuona kuwa wameonewa na kusingiziwa basi wana nafasi kwenda mahakamani kudai haki yao.

Milango iwazi mahakamani.
 
Huyo slaa angeanza kutaja mafisadi waliyomo ndani ya chama chake! Hii kukimbilia kujitia anajua sana mambo ya CCM ni kutafuta ujiko usio na mshiko!

ccm ni mpinzani kwa cdm hivyo yeye kama anao ushaihidi juu ya mafisadi waliopocdm
basi autoe maake wananchi ndio majaji wetu Bw. Kibunango (Kinango).
jina la Kinango katika vitabu vya kiada alikuwa ni mtu juha asiyetambua anachokiona au nusa n.k
 
Siku zote huwa siwaamini watu wanaopenda umaarufu! M gufuli ni bomu huwa nawashangaa watu wa humu wanaomteteta !
 
Huez kuwa kiongozi CCM bila kuwa kingunge au mfadhili wa ufisadi..hio ndio principle ktk MAFIA system yeyote.
 
Moelex23, asante sana kwa hili, Chadema ina udhaifu mkubwa wa kukosa long time strategiest hivyo kukalia kushindana kulipua mabomu.
Mimi ni miongoni mwa wapenzi wachache wa Chadema (sio mwanachama) ambao sikubaliani na baadhi ya moves za viongozi wa juu wa chama hiki.

Baada ya uchaguzi mkuu, nilisema it was wrong move kwa Dr. Slaa kususia kutangazwa kwa matokeo, nikasisitiza siku ya kutangazwa matokea was the best opportunity ya kueleza kutoridhishwa kwake na kutoyatambua matokeo.

Baada ya kutoyatambua matokeo yale, nilitegemea by now, Chadema wangekuja na altenative matokeo yao kujusfy kile wanachopinga, mpaka leo hakuna.

Sipendi Chadema ibaki kuwa ni chama cha kulalamika na kuendesha maandamano, natamani Chadema wewe chama chenye vision ya kuona political opportunity and seize such opportunities for their advantage.

CCM kujivua gamba is an opportunity huku ni kuvuja kwa pakacha (CCM), ambayo inatakiwa kuwa nafuu kwa mchukuzi (Chadema), badala ya mchukuzi kujituliza na kujiachia tuu mpaka pakacha libaki tupu, yeye ndio wa kwanza kumweleza mwenye pakacha, kuwa pakacha linavuja!, hivyo kumpa nafasi kuziba matundu yote hata yale ambayo yangempa unafuu mchukuzi!.

Kwenye hoja ya ufisadi, tayari CCM wanashikana mashati kutafutana uchawi, Chadema ilitakiwa ikae kimya iangalie tuu hii sinema. Kitendo cha Chadema kupiga kelele mpya, na kuwataja vipenzi vya watu kama kina Magufuli, kutaifanya CCM kuwasamehe hata mafisadi wake kama kina RA, EL na Mzee wa Vijisenti!.

Kwa mfano mtu kama Magufuli, hata ukiutangaza ufisadi wake kwa mabango, vipeperushi na maandamano nchi nzima, halafu uchaguzi ukaitishwa kesho, John Pombe Magufuli akasimama na Dr. Slaa, John Pombe, atamtupa kwa mbali Dr, kwa sababu moja tuu, watu watachagua mtu na sio chama. Pombe ana good track record ya kudeliver, Dr. yeye ndio kwanza anaitafuta hiyo opportunity ya kuwathibitishia Watanzania kuwa ata deliver.

Ndani ya Chadema, nadhani kitu vitu vikipangwa, hakuna wa kushauri otherwise, and this is not good kwa chama makini.

Pasco.

- Great thinking by a great thinker!

William @ NYC, USA.
 
HTML:
Kwanini ya Facebook yabaki Facebook wakati aliyeandika hayo ni the same person,on same subject matter,ila tofauti sasa ni imemhusu mzazi.

Uzoefu mwepesi tu unastahili kukuonyesha kuwa jitihada za mafisadi kujisafisha au kusafishwa so far hazijaweza kufanikiwa.Unaweza kuweka kambi hapa kumtetea mzazi (who wouldnt anyway) lakini court of public opinion haihitaji hizo documentary evidence.Watanzania si wajinga wa kuaminishwa kitu kisichopo,na wana uwezo wa kuchambua pumba na mchele.Kwahiyo,laiti tuhuma za ufisadi dhidi ya Mzee Malecela ni uzushi mtupu basi same court of public opinion itamtakasa.[/QUOTE]

[SIZE=3][COLOR=blue]- Slaa hajaenda mahakamani kuhusu kuibiwa kura za urais alioushinda, Chadema haijaenda mahakamani kuhusu kupokea hela za nje kuleta vurugu, mkuu wewe na Slaa ndio waamuzi wa mwisho kuhusu public opinion soma vizuri mawazo ya watu hapa utaona kwamba kwenye haya majina mapya Slaa ameharibu so is Chadema, ndio maana kuna siku nilisema hivi kuna wananchi wengi Tanzania hawajui kwamba Slaa ni kiongozi wa Chadema, kwa sababu it is always about him na kuwepo kwenye media kila siku, ameibiwa kura za uchaguzi hajaenda mahakamani mpaka leo, Mtikila kesi ya mgombea binafsi ameenda kwenye sheria na kuishinda serikali, now you wonder nani mwenye nafuu!

- Mangula na Malecela hawawezi kuwa mafisadi for that Slaa ametuhadaa na binafsi nimekosa heshima tena na huyu kiongozi wenu mlipua mabomu, niliongea na mtu mmoja aliyewahi kugombea ubunge na Slaa, akaniambia ni tabia yake kukuzushia maneno mengi sana ya uongo, anasema hata yeye mpaka leo hana hamu naye, Slaa arudi chini kukijenga chama badala ya kulilia media headlines kila siku hazikijengi chama huko vijijini ambako kuna majimbo Chadema haikuweka wagombea kabisa kwa kutokuwa na presence, ni ushauri wa bure tu![/COLOR][/SIZE]
[SIZE=4][COLOR=red]
William @ NYC, USA.   [/COLOR][/SIZE]
 
chadema wamefulia

weka magufuli na upande mwingine mbowe. waulize wananchi nani fisadi. jibu kwa asilimia zaidi ya 90 litakuwa mbowe.

kuwataja magufuli na malecela kumemwokoa lowassa kuchukuliwa hatua na ccm.

Jenifa, Nadhani unahitaji kuwa muungwana na kujadili hoja badala ya kujaribu tu kujibu kishabiki!!!

Labda aliyelala anaona kuwa Magufuli si fisadi. Kwa uchache tu, mikataba ambayo Magufuli aliyavunjwa alipokuwa waziri wa Ujenzi awamu ya mkapa zimeigharimu nchi zaidi mabilioni kama damages kwa contractors.

Uuzaji wa nyumba za serikali amefanya yeye, wakijua kuwa wao ndiyo wanastahili kuishi Masaki na Oyserbay and uzunguni kwa baadhi ya miji. Waliamimi kuwa wao ndo wataendelea kuwa viongozi na wengine wakija basi watajijua. Hata hivyo hii ilikuwa move pia ya kifisadi kwani baada ya kumaliza kuuza serikali imekuwa ikijenga nyumba sub standards kwa mabilioni ya fedha.

Ukija kwenye samaki wa Magufuli, hili pia sio kitu ya kusema kuwa watu hawajui kilichotendeka! Fedha nyingi alizolipwa mhifadhi ni fedheha hasa kwa maamuzi yaliyofanywa na mtu anayeonekana kuwa ni safi. Haingii akilini kuwa yeye Magufuli hakuwa na kiasi chake katika hilo au hata kama hana kwa maamuzi hayo tu ya kuingiza nchi hasara kwa kutotumia hazina ya watu anaofanya kazi nao ili kutotuingiza katika unnecessary cost.

Siyo hayo tu, angalia nyumba alizoamuru zijengwe Chalinze ili ajustify nyumba kama hizo kule kwao CHATO. Sasa hivi hizi ni white elephants!! Je huu nao tuiteje? siyo ufisadi? Ufisadi sio lazima uwe milionea lakini unapofanya maamuzi ambayo yanaigharimu nchi na wananchi wake, huo ni ufisadi kwanza mkubwa sana. Kama fedha hizo zingejenga ward za akina mama kujifungulia tungeweza kunusuru maisha ya akina mama na watoto wengi katika nchi hii. Tungepunguza matatizo kama ya mwananyamala ya kuzika watoto kama mbwa katika shimo moja.

Lazima tujifunze kuangalia mambo kwa undani zaidi kabla ya kukurupuka. Kama ni utendaji Lowassa ni zaidi lakini ni fisadi. Hivyo Magufuli yawezekana watu wanamwona mtendaji lakini mimi namwona kuwa ni mtu wa media zaidi lakini hata kama anatenda kazi kwa kiasi fulani, haimwondolei doa la ufisadi!!!!
 
Dr Slaa amefanya vizuri kutaja haya mafisadi kwa sasa kwani CCM walitaka kutuzuga kuwa tatizo ni EL,AC,RA tu na hamna wengine
Kifupi ni kwamba Dr AMEZIDISHA UGUMU WA CCM kuwazuga wanainchi kujivua gama.
Hongera Dr na kwa sasa EL,RA,AC komaeni ccm haiwezi kuwatumia halafu leo muitwe gamba bora izame ccm nzima.
 
- Slaa hajaenda mahakamani kuhusu kuibiwa kura za urais alioushinda, Chadema haijaenda mahakamani kuhusu kupokea hela za nje kuleta vurugu, mkuu wewe na Slaa ndio waamuzi wa mwisho kuhusu public opinion soma vizuri mawazo ya watu hapa utaona kwamba kwenye haya majina mapya Slaa ameharibu so is Chadema, ndio maana kuna siku nilisema hivi kuna wananchi wengi Tanzania hawajui kwamba Slaa ni kiongozi wa Chadema, kwa sababu it is always about him na kuwepo kwenye media kila siku, ameibiwa kura za uchaguzi hajaenda mahakamani mpaka leo, Mtikila kesi ya mgombea binafsi ameenda kwenye sheria na kuishinda serikali, now you wonder nani mwenye nafuu!

- Mangula na Malecela hawawezi kuwa mafisadi for that Slaa ametuhadaa na binafsi nimekosa heshima tena na huyu kiongozi wenu mlipua mabomu, niliongea na mtu mmoja aliyewahi kugombea ubunge na Slaa, akaniambia ni tabia yake kukuzushia maneno mengi sana ya uongo, anasema hata yeye mpaka leo hana hamu naye, Slaa arudi chini kukijenga chama badala ya kulilia media headlines kila siku hazikijengi chama huko vijijini ambako kuna majimbo Chadema haikuweka wagombea kabisa kwa kutokuwa na presence, ni ushauri wa bure tu!

William @ NYC, USA.
William, Katiba ya Tanzania na sheria ya uchaguzi haitoi sehemu yoyote ya kushitaki kwa wizi wa kura za urais kama tume ikishamtangaza mgombea mmoja kuwa mshindi. That is end of it. Na ndiyo maana Watanzania tunataka Katiba mpya.
Lakini kumbuka kuwa wa kwanza kumwambia Malecela ni fisadi ni Sophia Simba wakati huo akiwa waziri. Hapo hujasema chochote, kama ufisadi wa Mzee Malecela ulionekana mpaka na walio ndani ya CCM na wakathubut kusema, basi nadhani kwetu sisi wananchi wa kawaida, tunadhani kuna makubwa zaidi na mengi kwa Mzee Malecele. Kama watu wana data zaidi za ufisadi wa huyu Mzee Malecele watujuze labda ni zaidi tu ya kusema ni fisadi.
Pia kumbuka kuwa kama mtu ameshiriki katika maamuzi ambayo yamepelekea fedha za nchi kutumika isivyo kwa manufaa ya kikundi fulani haijalishi kama yeye kama mtu amechukua kiasi gani au hajachukua lakini ni fisadi. Ukiangalia Mangula na Deep Green,Kagoda, nk. nadhani anafahamu zaidi kwani alikuwa katibu mkuu wa CCM wakati huo na kama alibariki zitokee maana yake yeye ni part of it, hawezi kukwepa lawama!!!
 
Wait a minute!
Tabora ni nyumbani kwa Lipumba
Lipumba ni Mkiti wa Kafu
Kafu ni Mke wa ccm
JK ni Mkiti wa ccm

Kwa nini Chadema wanakwenda nyumbani kwa mke wa mtu kwenda kumwambia kuhusu mume wake alivyo fisadi? Je mume atakubali hili litokee? Basi tusubiri kuona polisi na TBC watakavyo handle hili

Kwa kawaida mke ni mali ya mume.lakini kuna mambo huwa wanahitilafiana.Hivyo si dhambi kuwafikia pengine family members wanaweza kuangalia njia sahihi ya kufuata kama wazazi hawabadiliki.
 
Mkuu Pasco;

Hivyo ni vile ambavyo wewe unaona. Ni chaguo lako kuona ni upande upi wa shillingi unataka kuuona.

Najiuliza maswali mengi una maana gani unaposema "na kuwataja vipenzi vya watu kama kina Magufuli, kutaifanya CCM kuwasamehe hata mafisadi wake kama kina RA, EL na Mzee wa Vijisenti!". Elewa kuwa wakati mbaya wa CCM kuwatosa makada hawa ilikuwa ni kabla ya uchaguzi. Hawakufanya hivyo kwa kuwa chama kingesambaratika. Hawakuweza kufanya hivyo kimikakati na ndiyo maana JK aliwakumbatia na kuwasafisha kipindi hicho. Lakini si sasa, ulazima wao wa kuwepo ndani ya chama si muhimu kama kipindi kile.

Elewa mpaka sasa move ya EL na timu yake ya kutaka kumwondoa JK kuwa mwenyekiti wa CCM ndiyo iliyowacost sana. Pia wasiwasi wa JK atakapomaliza ngwe yake Nchi amwachie nani na historia itamuhukumu vipi. Ieleweke BWM hana raha hadi leo kwa kelele anazopigiwa.

Wakati wewe unaona move ya CHADEMA ya kutaja mafisadi zaidi ni wrong upande mwingine wa shillingi unaonyesha kuwa hii ni strategy nzuri. Kwa kuwataja "wasafi wa CCM" kuwa mafisadi: Magufuli; Malecela; Mang'ula; na vigogo wa kudumu CC na NEC ya CCM: Sumaye; Mkapa na JK ina maana wao pia wafukuzwe uanachama. je watafukuzwa? RA na sophia simba alisema ndani ya CC kuwa hakuna ushahidi lakini CC safari hii haikukubali na ikawatosa, so suala la ushahidi si issue kwa sasa ila issue ni ushahidi wa kimazingira na kisiasa.

CHADEMA wanajua kwa kulitaja hili CCM wana chaguzi 3:

1. Kufuta mpango wao wa kujivua Gamba na kukaa kimya kama hawajui kitu.

2. Kuwatosa mafisadi wa Phase 1 na Phase 2 kitu ambacho hakiwezekani

3. Kuwasamehe mafisadi wote wa Phase 1 na Phase 2 kama ulivyosema.

Katika hali yoyote CHADEMA wanao mtaji wa kisiasa wa kuendelea kuwapaka CCM kuwa si lolote si chochote na ni Wasanii katika vita vya Ufisadi. hapo bado kuna mafisadi wa 'stimulus package' hawajatajwa.

Nadhani move ya CHADEMA kisiasa inalipa na again kama walivyo prove kwa Phase 1 list na kuwalazimisha CCM kuchukua hatua, I believe also this one will work.

Respect.

QED.
Superman, vita vya kisiasa, hupiganwa kama vita vingine vyone, the one with the right strategies na right tactics, ndiye siku zote atashinda vita, ndio maana hata Amini, tulifanikiwa kumshinda na kumtimua pamoja na silaha zake za kisasa kabisa ambazo alipowa na Ghadafi.

Chadema ilipiga ule muziki wa Listi ya Mafisadi pale Mwembeyanga, sasa ndio CCM imeingia line, na inacheza to the tune of Chadema. Chadema walitakiwa now just to sit back and watch how CCM dance to the music. Wakati ndio kwanza CCM wanaingia ukumbini kuanza kucheza muziki kwa dakika 90 (90 days) mara wewe wewe Chadema uliowapa wimbo wa kwanza, unaibuka na taarifa vyombo vyote vya habari, kuwa utatoa single nyingine kali zaidi, mara unaingia ukumbi ule ule huki CCM ikijipanga kuucheza ile single ya Mwembeyanga na EPA, wewe unawatupia single nyingine uliodai ni mpya kumbe wimbo ni ule ule, hakuna jipya.

Ufisadi wa EPA ni ule ule, kuongeza majina, belive me, hakuiongezea Chadema milage yotyote kwenye political war tactics zaidi ya kuongezea majuruhi. Hata sisi ambao tunaisuport Chadema kwenye every good move they make, tutafikia wakati tuchatoshwa na single ile ile ya maandamano, mikutano ya hadhara na kupinga ufisadi.

Niliipongeza Chadema, kwa mafanikio kiliyo yapata kwenye uchaguzi plus ongezeko la Ruzuku, nikawaambia kuna sehemu wamechaguliwa, sio kwasababu wagombea wao ni vidume, no, just kwa sababu CCM ilichokwa kwa sura zile zile. Kwa mnaomjua Livingstone Lusinde jinsi alivyo mtema pumba na mdomo mchafu, kuna anayeamini wana CCM wa Mtera, wangemtosaa Mzee Malechela na kumpa Lusinde kwa lipi?. Jibu ni moja tuu, wana CCM wamechoka wanataka sura mpya, na wananchi wameichoka CCM, wanataka mabadiliko.

Ndio maana nikashauri, Chadema wautumie muda huu, kujijenga na sio kupoteza muda kulalamika tuu. Wakati nikitoa ushauri huo ilikuwa ni mwaka jana Novemba baada ya uchaguzi, leo tunaelekea May, ni miezi 6 imekata, sijaona Chadema inafanya nini kujiadress kwenye kujijenga, unless inajifariji na umati wa watu kwenye maandamano na mikutano yake ya hadhara.

Nilitegea single mpya ya ufisadi, itakuwa na majina mapya na ufisadi mpya wa Stumulus Package, kumbe ni majina mapya ya ufisadi ule ule wa EPA, kupitia kampuni ya Kagoda wa mwaka 1994!. Hizi nyimbo zitachusa!.

Nawashauri tena na tena Chadema, nilipoposti posti 'CCM Imechokwa!, Chadema Haijajipanga!, wana CCM hawakujibu kitu, ila wametekeleza kwa vitendo ushauri ule. Chadema na manazi wao, waliishia kunishukia and they did nothing. The clock is ticking 2015 inakuja, tuendelee kuhudhuria maandamano na mikutano ya hadhara ya Chadema, huku CCM ikipiga bao, halafu wakati ukifika kikitokea cha kutokea Chadema wanaishia kulia lia!.
 
pasco

unajisumbua bure baba.

swali dogo tu tuweke mbowe upande mmoja na mwingine magufuli. watu tupige kura nani fisadi zaidi.

kuna mtu anaweza feli swali hilo.

mbowe ni fisadi tena awafanyia mbaya wale wabunge wanawake chadema. anawafanya changudoa yake.

magufuli oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee. chadema walegeeeeee tu.
 
Saafi saana!!!!
Single(Orodha Fisadi I) + Double (Orodha Fisadi 2) + KATIBA BOMU!! =Vua GAMBA!!! REMIX itakuwa nn?? Yeketeyekete ya ccm bana! pracatah!!hiyo.

ukisataajabu ya mussa......................!!!
 
Sikuwahi kudhani kama politics ni mchezo mgumu hivi kwa baadhi ya watu! Wanaopinga hatua ya CDM kutaja mafisadi wapya, kwa kweli hawajui kabisa mchezo wa siasa.

Baada ya muda mrefu wa CCM kudhibitiwa na kuwa hawana ujanja, wamejitutumua na kuja na kauli (sio matendo), ya kujivua gamba. Kwa taarifa yenu hili lilikuwa shuti zuri sana la kuwarudisha CCM kwenye chati. So, CDM kukaa kimya ikiangalia, ingekuwa na grave mistake, kwani CCM wangekuwa wameenda mbali sana. Kwa hiyo CDM wameamua wadeflect move ya CCM.
Effect zake tayari mnaziona. Akina Nape hawana tena focused direction, anapambana na mambo mawili kwa wakati mmoja. Anapambana na mafisadi na anapambana na CDM. Anaenda mikoani sasa hivi, hajui lipi alipe uzito. Anapinga hoja ya mafisadi wapya lakini hana ubavu wa kuwataja kwa majina wale wa zamani. Anapotamka sentensi kuwa 'mafisadi' wajitoe kwenye nafasi zao, lazima ajitahidi kufafanua kuwa mafisadi anamaanisha kuwa wale waliotajwa mwanzoni, sio hawa wa sasa. Kimantiki hii inapunguza uzito wa kauli yake ya kwanza.
Akina nape hawana ushahidi wa ufisadi wa wale wa Mwanzo, lakini Slaa anao. Hii ina maana kuwa Nape hawezi tena kumshupalia Lowassa aondoke NEC kwa sababu ametajwa kwenye ufisadi, na hapo hapo anamwacha malecela, mabye naye ametajwa.

Uwepo wa EL, RA, AC, na wengine ndani ya CCM, ni mtaji mzuri kwa CDM. Kwa hiyo wanachofanya CDM ni kuwapa kazi ngumu CCM kuwaondoa hawa ili CDM wawe na attacking point bana...
 
TUJIKUMBUSHE ORODHA YA 2007
1. Dr. Daudi T.S. Balali
2. Andrew J. Chenge
3. Basil Pesambili Mramba
4. Gray S. Mgonja
5. Patrick P.R Rutabanzibwa
6. Nazir Karamagi
7. Nimrod Mkono
8. Rostam Aziz
9. Edward Lowassa
10. Benjamin W. Mkapa
11. Jakaya Mrisho Kikwete

Hah hah hah, hawa ndiyo mafisadi wa orodha ya kwanza, ama kweli bongo ni mbongo. Halafu wako kimya na wengine bado makatibu wakuu wa wizara.
 
- Slaa hajaenda mahakamani kuhusu kuibiwa kura za urais alioushinda, Chadema haijaenda mahakamani kuhusu kupokea hela za nje kuleta vurugu, mkuu wewe na Slaa ndio waamuzi wa mwisho kuhusu public opinion soma vizuri mawazo ya watu hapa utaona kwamba kwenye haya majina mapya Slaa ameharibu so is Chadema, ndio maana kuna siku nilisema hivi kuna wananchi wengi Tanzania hawajui kwamba Slaa ni kiongozi wa Chadema, kwa sababu it is always about him na kuwepo kwenye media kila siku, ameibiwa kura za uchaguzi hajaenda mahakamani mpaka leo, Mtikila kesi ya mgombea binafsi ameenda kwenye sheria na kuishinda serikali, now you wonder nani mwenye nafuu!

- Mangula na Malecela hawawezi kuwa mafisadi for that Slaa ametuhadaa na binafsi nimekosa heshima tena na huyu kiongozi wenu mlipua mabomu, niliongea na mtu mmoja aliyewahi kugombea ubunge na Slaa, akaniambia ni tabia yake kukuzushia maneno mengi sana ya uongo, anasema hata yeye mpaka leo hana hamu naye, Slaa arudi chini kukijenga chama badala ya kulilia media headlines kila siku hazikijengi chama huko vijijini ambako kuna majimbo Chadema haikuweka wagombea kabisa kwa kutokuwa na presence, ni ushauri wa bure tu!


William @ NYC, USA.

Ana hasira ya Watanzania kumpa kura Kikwete alifikiri akipayuka basi atapata kura. Watanzania tuna akili akija mgombea mwingine mzuri wenye akili timamu, tutampa kura na atakuwa raisi lakini kama mgombea 2015 wa chadema atakuwa Slaa Watanzania wengi hatutampa tena kura zetu.
 
mnaojua nisaidieni wengine technology imekaa kulia. nataka kuweka opinion poll nani fisadi zaidi kati ya mbowe na magufuli.

sioni pa kukandamiza kuandika opinion poll
 
Chadema wamefanya vizuri kuongeza tune ya bass kwenye single yao ya kwanza bila kuwatifulia CCM walikuwa wamepiga bao la kisigino sasa hivi umeona wameshaingiza mambo mawili matatu makubwa, List ya vigogo iliyotajwa na Dr Slaa Tabora ni danganya toto ,Mafisadi wanaotakiwa kujitoa CCM wanamtumia Dr Slaa,Mafisadi wanataka kummaliza Nape, na Mafisadi wanatumia vyombo vya habari viongozi wa dini tayari hiyo ni vita badala ya kutekeleza CCM inayotaka kutekeleza sasa wako kwenye defensive side wanamtetea mwenyekiti wao na familia yake lakini walipokuwa wnafamilia Baba ,Mwana Na Mke wakifanya kampeni kwa fedha za umma hawakuwaheabia kama mafisadi,huu muziki umefikia sauti ya juu sasa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom