Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Status
Not open for further replies.
mnaojua nisaidieni wengine technology imekaa kulia. nataka kuweka opinion poll nani fisadi zaidi kati ya mbowe na magufuli.

sioni pa kukandamiza kuandika opinion poll

nimeambiwa slaa analipwa milioni 15 kwa mwezi. no wonder anachakachua wake za watu.

Offcourse majibu yatakuwa Magufuli lini mbowe aalitawala hata kijiji au kata akashika fedha ya umma
 
TBC watarusha live? Si Wanajiendesha kwa kodi zetu bana. La sivyo nao wajumuishwe kwenye orodha ya mafisadi, wanatuibia kodi zetu

Ndugu yangu Kieleweke, Ukiwa kama kiongozi wa juu wa Chadema unadhani ni sawa kuwajumuisha watu kwenye listi ya mafisadi mradi tu hawajarusha mkutano wenu wa hadhara live? Hii inajenga sura gani kuhusu suala zima la siasa za ufisadi?

Imeipata wapi?jibu ni humo humo ccm!sasa ni staili ya mwaga mboga nitupe ugali. Kazi ipo tusubiri majina.

Pia inaelekea hii faslsafa ya kubomoa Tanzania ya CCM ili kujenga Tanzania ya Chadema sio falsafa ya wachache tu miongoni mwa uongozi wa juu wa Chadema bali ni falsafa ya chama. Ina maana CCM wakiendelea kufanya siasa hovyo nanyi mtaendelea kufanya siasa hovyo badala ya kujenga siasa mbadala zenye kulenga kujenga Tanzania makini na sio ile iliyo hovyo zaidi

Anasema kuwa ni wakati wa kudai nyumba za serikali kwa nguvu ya umma , kwani kwenda mahakamani sio muafaka kwani hata majaji wenyewe walijiuzia hivyo hawawezi kutoa haki.

Ina maana Dr Slaa haamini katika uongozi wa sheria? Hivi kwa maneno haya bado mtadai kuwa Chadema haifanyi uchochezi wa kuvunja sheria? Hivi kwa siasa hizi ni vipi tutaweza kujenga mfumo wa Haki sawa mbele ya sheria, Uongozi Bora na Demokrasia? Hivi mnaamini kuwa mkivunja misingi hii sasa wakati hamna ulabu wa nguvu za dola mtaweza kuheshimu hiyo misingi mkiwa mnamiliki nguvu hizo? Hivi mnadhani utamaduni unaoshamiri miongoni mwa jamii kutokana na siasa hizi utaweza kuondoka pale mtakapofanikisha lengo lenu kuu ambalo ni kuondoa CCM na kumiliki utawala wa nchi yetu?

[
FONT=Calibri]Zidaiwe kwa nguvu ya umma ndio njia pekee ya kupata nyumba hizo kwani viongozi wengi wanakaa hotelini.[/FONT]

Ni viongozi gani hao wakaao hotelini? Mnaweza kuwataja na kutonyesha ushahidi ama itakuwa uleule ujanjaujanja wa agenda ya kuwa Kikwete alimpora DR Slaa ushindi na hadi leo hakuna chembe ya ushahidi wa wazi uliotolewa zaidi ya hearsay's? Hivi Dr Slaa naye miaka yote hii kukaa hotelini nalo limesababishwa na sera za CCM ama uzembe wa chama chenu? Hivi mkoa tayari pia kuwataka viongozi wenu ambao wanamiliki majengo na majumba lukuki hapa Dar lakini bado wanamiliki numba za Shirika la Nyumba nao warudishe nyumba hizo ili watanzania mnaowapigania kuweza kupunguza janga la makazi hovyohovyo?

Nchi haiwezi kutawalika ni mpaka mafisadi wote wakamatwe kwani haiwezekani kluwa na mafisadi na nchi ikaweza kutawalika.

Je huu sio ushahidi wa nia ya kufanya nchi isitawalike? Nia inayonadiwa na viongozi walio wengi wakiwemo wenye historia ya uhaini?


Kama JK kawapa mafisadi siku 90 ndani ya chama chake nay eye Tunampa JK na eye siku 90 ataje fedha za mabango yake dola 1.5 milioni aseme zilitoka wapi zilizotumwa CANADA kutengeneza 2010 election .na yeye anapaswa kujitoa kama atashindwa kuchukua hatua hizo.

Je na Chadema mtakuwa tayari kusema na kuweka wazi fedha zilizotumika kutengenezea mabango, mavazi, helikopta, usafiri na mengineyo? Je mnaweza kueleza kulikuwa na uwazi gani katika mfumo mzima wa kukusanya, kusimamia na kutumia michango hiyo bila ya kuficha kitu? Hivi Chadema wameshakabidhi kwa ukaguzi wa Mkaguzi Mkuuwa Fedha za Umma ama mkaguzi indipendant ripoti ya matumizi ya fedha za ruzuku za 2007-2008, 2008-2009 na 2009-2010 kama sheria iliyopigiwa debe na mbunge wenu lipopitisha na kuanza kutumika?
 
Offcourse majibu yatakuwa Magufuli lini mbowe aalitawala hata kijiji au kata akashika fedha ya umma

Ina maana ufisadi mnaopigana nao ni ule wa waliotawala? Vipi kuhusu wakwepa kodi, vipi kuhusu wakopaji fedha za umma bila ya kurudisha? Vipi kuhusu wanaotumia fedha za RUZUKU bila ya uwajibikaji? Vipi kuhusu wanaotoa hongo ili kupata tenda ama vibali vya biashara?
 
Udini.
Wakoloni waliwagawa watu kwa njia za makabila ili wawatawale ,wakagawa watu kwa njia za udini mf.waingereza waliingiza dini na kjuweka watu wao serikalini , na waislamu wengi walikosa nafasi ya kusoma ndio maana hawakuingia serikalini mapema .
Waislamu walipigania uhuru ila , kutokana na waingereza kuwabagua , ndio maana waliamua kupinga ukoloni ili waweza kuweka serikali ambayo haiwabagui, anasema ugomvi wa Nyerere na shehe takadir kuhusu waislamu kubaguliwa , na anasema kuwa ndani ya CDM hakuna udini ila ndani ya nchi kuna tatizo la kihistoria la kidini.
Anasema kuwa ni mbinu ya serikali kuwagawa watanzania ili waweze kuwatawala .
Alipojitoa CUF na kujiunga na CDM alifuatwa na mashehe wakimwambia kuwa yeye ameamua kujiunga na wakristo , yeye akajibu kuwa walitaka yeye aende kwenye chama gani? Mbona CCM sio ya waislamu kwani ukiondoka JK wengi waliopo serikalini ni
Anasema yeye hajabatizwa na pia Slaa sio yohana mbatizaji na amewataka waislamu kuungana pamoja ili kupigania haki za waislamu kwani CCM ndio ambao wanawakandamiza waislamu hivyo ni bora wakajiunga na CDM kwa wingi ili waweze kudai haki zao tangu awali na wasisubiri , waingie cdm tangu mwanzo ili wawe sehemu ya kupigania haki zao na njia nzuri ni kuhakikisha nkuwa wanajiunga ili kuingiza hoja zao kabla ya cdm kuingia serikalini na ni lazima waislamu wakitaka madai yao yasikilizwe wanapaswa kuingia sasa na sio wawasusie cdm kwa hoja za udini halafu baadae waje walalamike .
Kuna haja ya kujiunga na cdm sasa.

Ndugu yangu mpaka kieleweke,

Hili gamba la UDINI mnahitaji uthubutu zaidi wa kujirekebisha na kujenga umakini kuliko kutegemea ujanjaujanja wa kumtumia Dr Safari ama kukwepa hoja kwa kutpia mzigo CCM ambao wao wamejenga misingi ya muda mrefu ya kulishughulikia suala hili ambalo lipo na litaendelea kuwepo....By the way Dr Safari ni bomu litakalowalipukia very soon...
 
dah! kwastaili ili Tanzania itafika pale ambapo siku zote imeshindwa kufikia. nikiwa namaanisha pale yalipo maendeleo maendeleo huu ni mzigo hatunabudi kutafuta njia ili kujinasua big up
 
Jiskie aibu japo kidogo.Wangekuwa wamefulia ungepoteza muda wako japo kuwataja?Badala ya kupanua vingine,jaripu kupanua upeo wako na kufikiria mbali zaidi ya hapo ofisini kwako.Mwangalie jirani yako,angalia hali katika kijiji ulichozaliwa,ongea na wazazi wako,fanya tathmini mwenyewe.

Ni rahisi kumlaumu Dkt Slaa au Chadema,kwa vile wapo wanaodhani anafanya anayofanya kwa maslahi yake binafsi na ya kisiasa.Lakini hebu jaribu kumwondoa Dkt Slaa kwenye picha,kisha chambua hali halisi ya nchi yako.Weka hisia pembeni bali zingatia facts katika utafiti wako usio rasmi.

Kama una mapenzi ya kweli na nchi yetu ni dhahiri utabaini kuwa tuna matatizo lukuki,huku kubwa likiwa umasikini wa kupindukia miongoni mwa Watanzania wengi japo watawala wetu wanaishi kifalme.Sidhani kama utapata shida kugundua uwepo wa mgao wa umeme, au bei za vyakula zinazozidi kupanda,au hata namna ya kuweza kumudu maisha yako kwa mshahara unaolipwa.

TAFAKARI

Well written and presented Mkuu.

Respect.
 
Mkuu kwani kuna kitu chepesi ukiwa na fikra gonjwa? Nina uhakika kabisa,hata wengine humu wakijaribu kuniamnisha vinginevyo, CCM wanfahamu kuwa wamefikishwa pabaya kwa move hii. Kelele unazozisikia ni za kila siku. Zimekuwepo tangu enzi hizo. Ni wakati tu ndio huwa unakuja kupambanua mambo na hautazisikia tena. Hapa unasikia sana kelele za aina mbili:

  1. Beneficiaries wa ufisadi kwa namna moja au nyingine,uwe ule wa first eleven au huu wa substitute bench. Humu utaona ndugu wa mafisadi tajwa; waajiriwa wao, au waishio kwenye nyumba zilizokua za serikali kisha wakajigawia kwa mujibu wa taratibu walizojiwekea. Kelele ni nyingi zaidi kutoka kwa wanaohusika na hii substitute list kwa sababu kwa muda mrefu sasa walidhani wameachwa salama,wengi wakiuchuna kimyaa wakiombea mambo yaendelee vile yalivyokuwa.
  2. "Wapinzani" wa namna moja au nyingine wa kila move ambayo CDM inafanya. Kila mmoja ana yake nia, wengine mbaya wengine nzuri. Wengine kwa kujua na kufanya makusudi kwa malengo yao, wengine kwa kutokujua au kutokuelewa siasa zinavyoendeshwa. Mie ningekua CDM, ningechukulia hii kama changamoto tu, na hata kutumia criticism nyingine kujikamilisha na kujithibitisha zaidi. That's politics.
Katika yote, ndani ya siku hizi 90, tutasubiri kuona lolote likitokea kati ya haya:

  • Watu kutishia au kwenda mahakamani kufungua kesi za madai ya kuzushiwa. Dr. Slaa et al watatakiwa kuwasilisha ushahidi ambao wanadai kuwa nao. Hata akina mie tutausikia au kuuona kwa mara ya kwanza.
  • Wachezaji wa first eleven kugoma kuwajibika wakishinikiza hawa sub bench nao kuwajibika. Hapa uma utapata nafasi ya kuona na kuthibitisha kama kujivua gamba ni suala linalomaanishwa kweli au la? Au ni nini maana yake haswa?
  • Wote, first eleven na sub wao wataamua "kuwajibika" (kwa chama walau, japo tunataka wawajibike kwa uma). Hapa uma utapata kujua kama ufisadi chamani upo kwenye ngozi/gamba au damuni. CCM itaweza kusimama baada ya tendo hili? Pia sioni kama hili linawezekana.
Kwa vyoyote itakavyokua katika siku tisini hizi, ndipo tutakua kwenye nafasi nzuri ya kusema kama hii ilikua ni move sahihi au mbaya kwa CDM. In the mean time let's see if it's Nape et al dancing to CDM tunes or the vice versa.
Sikuwahi kudhani kama politics ni mchezo mgumu hivi kwa baadhi ya watu! Wanaopinga hatua ya CDM kutaja mafisadi wapya, kwa kweli hawajui kabisa mchezo wa siasa.

Baada ya muda mrefu wa CCM kudhibitiwa na kuwa hawana ujanja, wamejitutumua na kuja na kauli (sio matendo), ya kujivua gamba. Kwa taarifa yenu hili lilikuwa shuti zuri sana la kuwarudisha CCM kwenye chati. So, CDM kukaa kimya ikiangalia, ingekuwa na grave mistake, kwani CCM wangekuwa wameenda mbali sana. Kwa hiyo CDM wameamua wadeflect move ya CCM.
Effect zake tayari mnaziona. Akina Nape hawana tena focused direction, anapambana na mambo mawili kwa wakati mmoja. Anapambana na mafisadi na anapambana na CDM. Anaenda mikoani sasa hivi, hajui lipi alipe uzito. Anapinga hoja ya mafisadi wapya lakini hana ubavu wa kuwataja kwa majina wale wa zamani. Anapotamka sentensi kuwa 'mafisadi' wajitoe kwenye nafasi zao, lazima ajitahidi kufafanua kuwa mafisadi anamaanisha kuwa wale waliotajwa mwanzoni, sio hawa wa sasa. Kimantiki hii inapunguza uzito wa kauli yake ya kwanza.
Akina nape hawana ushahidi wa ufisadi wa wale wa Mwanzo, lakini Slaa anao. Hii ina maana kuwa Nape hawezi tena kumshupalia Lowassa aondoke NEC kwa sababu ametajwa kwenye ufisadi, na hapo hapo anamwacha malecela, mabye naye ametajwa.

Uwepo wa EL, RA, AC, na wengine ndani ya CCM, ni mtaji mzuri kwa CDM. Kwa hiyo wanachofanya CDM ni kuwapa kazi ngumu CCM kuwaondoa hawa ili CDM wawe na attacking point bana...
 
Superman, vita vya kisiasa, hupiganwa kama vita vingine vyone, the one with the right strategies na right tactics, ndiye siku zote atashinda vita, ndio maana hata Amini, tulifanikiwa kumshinda na kumtimua pamoja na silaha zake za kisasa kabisa ambazo alipowa na Ghadafi.

Chadema ilipiga ule muziki wa Listi ya Mafisadi pale Mwembeyanga, sasa ndio CCM imeingia line, na inacheza to the tune of Chadema. Chadema walitakiwa now just to sit back and watch how CCM dance to the music. Wakati ndio kwanza CCM wanaingia ukumbini kuanza kucheza muziki kwa dakika 90 (90 days) mara wewe wewe Chadema uliowapa wimbo wa kwanza, unaibuka na taarifa vyombo vyote vya habari, kuwa utatoa single nyingine kali zaidi, mara unaingia ukumbi ule ule huki CCM ikijipanga kuucheza ile single ya Mwembeyanga na EPA, wewe unawatupia single nyingine uliodai ni mpya kumbe wimbo ni ule ule, hakuna jipya.

Ufisadi wa EPA ni ule ule, kuongeza majina, belive me, hakuiongezea Chadema milage yotyote kwenye political war tactics zaidi ya kuongezea majuruhi. Hata sisi ambao tunaisuport Chadema kwenye every good move they make, tutafikia wakati tuchatoshwa na single ile ile ya maandamano, mikutano ya hadhara na kupinga ufisadi.

Niliipongeza Chadema, kwa mafanikio kiliyo yapata kwenye uchaguzi plus ongezeko la Ruzuku, nikawaambia kuna sehemu wamechaguliwa, sio kwasababu wagombea wao ni vidume, no, just kwa sababu CCM ilichokwa kwa sura zile zile. Kwa mnaomjua Livingstone Lusinde jinsi alivyo mtema pumba na mdomo mchafu, kuna anayeamini wana CCM wa Mtera, wangemtosaa Mzee Malechela na kumpa Lusinde kwa lipi?. Jibu ni moja tuu, wana CCM wamechoka wanataka sura mpya, na wananchi wameichoka CCM, wanataka mabadiliko.

Ndio maana nikashauri, Chadema wautumie muda huu, kujijenga na sio kupoteza muda kulalamika tuu. Wakati nikitoa ushauri huo ilikuwa ni mwaka jana Novemba baada ya uchaguzi, leo tunaelekea May, ni miezi 6 imekata, sijaona Chadema inafanya nini kujiadress kwenye kujijenga, unless inajifariji na umati wa watu kwenye maandamano na mikutano yake ya hadhara.

Nilitegea single mpya ya ufisadi, itakuwa na majina mapya na ufisadi mpya wa Stumulus Package, kumbe ni majina mapya ya ufisadi ule ule wa EPA, kupitia kampuni ya Kagoda wa mwaka 1994!. Hizi nyimbo zitachusa!.

Nawashauri tena na tena Chadema, nilipoposti posti 'CCM Imechokwa!, Chadema Haijajipanga!, wana CCM hawakujibu kitu, ila wametekeleza kwa vitendo ushauri ule. Chadema na manazi wao, waliishia kunishukia and they did nothing. The clock is ticking 2015 inakuja, tuendelee kuhudhuria maandamano na mikutano ya hadhara ya Chadema, huku CCM ikipiga bao, halafu wakati ukifika kikitokea cha kutokea Chadema wanaishia kulia lia!.

Mkuu Pasco;

Heshima mbele sana Kamanda!

Wakati naheshimu sana maoni yako, bado nina maoni kuwa SIASA is not a Physical law au law yoyote ambayo lazima ifuate pricipal fulani. Hiki ndicho kitua unacho argue na ambacho umekuwa uki argue.

Kukijenga chama kuna strategy zake, na kwa siasa za nchi yetu strategy unayosema ya kufungua matawi nchi nzima nk, japo ni strategy nzuri na ambayo inategemewa inaweza isifanye kazi. Muulize Mpinzani wa Mugabe Zimbambwe; Muulize Raila na mifano mingine lukuki baadhi ya Nchi za Afrika.

Muda unakwenda, society zinabadilika na siasa pia zinabadilika.

Haiitaju PhD kujua kuwa katika uchaguzi wa 2010 CHADEMA wasingeshinda hata kama wangeshinda na hata kama wangekuwa na matawi kila shina. Ni vema ukweli huu ukazingatiwa. the only approach ya jambo hili ni kuwaelemisha watu wajue haki zao na kuwa sensitized, then ndiyo ufungue matawi. bado nina maoni kuwa kwa kuwa CHADEMA wameanza mapema basi wanao muda wa kutosha kukijenga chama chao.

Kumbuka reserach zote za lasy election zinaonyesha kuwa turn uo was only 42%. For sure this to a big % has nothing to do with Matawi ya Chama.

In both cases TIME WILL TELL. Time is of so much importance than what we think.


Respect.

QED.
 
Hebu dadavua kidogo mkuu "uthubutu zaidi" unaweza kuwa kama upi vile? Kwa faida tu ya CDM au jamii au basi walau kwa faida yangu tuu. Inaonekana kama una solution mkuu,usiibanie bana!
Hapo kwenye red mkuu, ni misingi kama ipi hapo tena CCM imejenga?mbona naona ni kama udini ni kama una umri sawa na CCM yenyewe vile? Fafanua pliz kwa faida yangu. Thanks in advance!
Ndugu yangu mpaka kieleweke,

Hili gamba la UDINI mnahitaji uthubutu zaidi wa kujirekebisha na kujenga umakini kuliko kutegemea ujanjaujanja wa kumtumia Dr Safari ama kukwepa hoja kwa kutpia mzigo CCM ambao wao wamejenga misingi ya muda mrefu ya kulishughulikia suala hili ambalo lipo na litaendelea kuwepo....By the way Dr Safari ni bomu litakalowalipukia very soon...
 
Pasco Mkuu,

Umejichanganya sana kwa maneno yako. Kama kweli unaanza kwa kusema kuwa vita ya siasa ni kama vita vingine, basi huko chini umemaliza vibaya sana. Nashindwa kuelewa kama ulipitia JKT na kama ulipitia basi au umesahau au hukupitia mafunzo mazuri ya msituni.

Mrusi VS NATO walikuwa wakishindana kwa kutengeneza silaha. Mrusi akaja na AK-47 na NATO/USA wakaja na Mibunduki yao mikubwaa na risasi za kutisha. Ukipigwa na silaha ya NATO, unakuwa vipandevipande na kufa wakati AK-47 inakupa jelaha kubwa ila kuna uwezekano UKAWA BADO HAI.

Ubaya wa kukufanya uwe bado hai ni kuwa walio wazima itabidi wakubebe. Kama ukifa, wanakuacha na kuendelea mbele. Hivyo basi hakuna mbinu bora vitani kama kutengeneza majeruhi kwa sababu ukiwa na majeruhi wawili, basi askari wanne wanaacha kupigana. Ukiwa na maiti wawili, basi unakuwa na askari wawili zaidi na wenye hasira wakitaka kulipa kisasi kifo cha ndugu zao.

Nafikiri CHADEMA watakuwa wanatengeneza MAJERUHI ndani ya CCM wa kisiasa. CCM itakuwa na maamuzi kadhaa ambayo itabidi iyafanye na nakubaliana kwa upande huo wa shilingi maneno ya Superman:

Code:
CHADEMA wanajua kwa kulitaja hili CCM wana chaguzi 3: 
 
 1. Kufuta mpango wao wa kujivua Gamba na kukaa kimya kama hawajui kitu.
 
 2. Kuwatosa mafisadi wa Phase 1 na Phase 2 kitu ambacho hakiwezekani
 
 3. Kuwasamehe mafisadi wote wa Phase 1 na Phase 2 kama ulivyosema.

Nafikiri kilichowasukuma Chadema kufanya hivi si kuwa CCM walikuwa hawachezi Single yao. Ila tatizo ni kuwa mziki uliokuwa ukipigwa na Chadema ulikuwa Reggae na CCM wakaanza kuucheza kama Vijana wa Atlanta yaani CRANK. Beat hazina tofauti ila kucheza kunatofauti. Chadema watakuwa wameshtukia deal kuwa hawa jamaa wanacheza Staili nyingine kwa wimbo unaotakuwa kuchezwa kwa staili nyingine. Sasa dawa yake ni kuwawekea PURE Reggae ili wasitake tena kubadili uchezaji.

Kitendo cha kufukuza watu watatu ndani ya CCM na kuwaita kuwa ndiyo mafisadi, ni kichekesho na tuuite kwa jina KAFARA. Wakishafanya hivyo, watapiga kelele Tanzania nzima kuwa WAMEJIOSHA tayari sasa mnataka nini? German, yule Mzee Chancellor Helmut Kohl alipokea pesa kutoka kampuni la mafuta la ELF (France) kwa ajili ya chama. Ilipogundulika, alishambuliwa hadi ndani ya chama chake na mmoja ya waliompiga madongo aondoke ni huyu mama Chancellor wa sasa Angela Merkel ambaye walikuwa chama kimoja na ndiyo alimlea ndani ya chama hicho.

Kwenye SIASA nilishasikia maneno haya kuwa "Adui yako ni nyoka, ponda kichwa na tupilia mbali....." Kikwete alifanya hivyo kwa adui zake na wengi wao hadi leo wako HOI kama si Marehemu Ki-Siasa. Sijui Chadema kama pia wanalitumia hilo kuwaponda woote wanaoweza kugombea mwaka 2015 ili kuwamaliza kisiasa mapema kabisa.

Kwa hali ilivyo sasa na Ukorofi wa Lowassa, sidhani kama atataka kuondoka tena na kuwa KAFARA. Sababu ya kutokuondoka kapewa na SLAA. Akigoma kuondoka, Chadema watasema "Magamba ya CCM bado yapo." Kwa sasa ndani ya CCM, wameshapewa mziki mzito sana ambao hadi namhurumia Kikwete.

Huo ufisadi mpya, unasubiri siku yake. Ukiwa unacheza karata, huonyeshi karata zako zote na ukiwa vitani, unatumia kwanza bunduki za kawaida. Mambo yakianza kubadilika, unahamia kwenye bunduki nzito/Kubwa, unakuja mizinga, vifaru, ndege na hadi akina SCUD. Pili kumbuka Slaa hawezi kukurupuka kutumia datas ambazo hana uhakika nazo. Zinaweza kuwa zimepikwa na hata CAG kaingizwa mjini na wewe ukizidandia, unakwenda na maji.

Jibu pekee zuri kwa CCM ni kuondowa watu wengi sana ndani yake jambo ambalo sidhani wako tayari kulifanya. Wakigoma, Chadema ndiyo wanafurahi na kwenda kuwashtaki kwa wananchi. Ngoja tuone/tusubiri kama ambavyo jana Mwenyewe Slaa kaandika kuwa "Mtuachie wenyewe tucheza kama hili jambo hamlifahamu vizuri kwa ndani.........." TIME WILL TELL.




Superman, vita vya kisiasa, hupiganwa kama vita vingine vyone, the one with the right strategies na right tactics, ndiye siku zote atashinda vita, ndio maana hata Amini, tulifanikiwa kumshinda na kumtimua pamoja na silaha zake za kisasa kabisa ambazo alipowa na Ghadafi.

Chadema ilipiga ule muziki wa Listi ya Mafisadi pale Mwembeyanga, sasa ndio CCM imeingia line, na inacheza to the tune of Chadema. Chadema walitakiwa now just to sit back and watch how CCM dance to the music. Wakati ndio kwanza CCM wanaingia ukumbini kuanza kucheza muziki kwa dakika 90 (90 days) mara wewe wewe Chadema uliowapa wimbo wa kwanza, unaibuka na taarifa vyombo vyote vya habari, kuwa utatoa single nyingine kali zaidi, mara unaingia ukumbi ule ule huki CCM ikijipanga kuucheza ile single ya Mwembeyanga na EPA, wewe unawatupia single nyingine uliodai ni mpya kumbe wimbo ni ule ule, hakuna jipya.

Ufisadi wa EPA ni ule ule, kuongeza majina, belive me, hakuiongezea Chadema milage yotyote kwenye political war tactics zaidi ya kuongezea majuruhi. Hata sisi ambao tunaisuport Chadema kwenye every good move they make, tutafikia wakati tuchatoshwa na single ile ile ya maandamano, mikutano ya hadhara na kupinga ufisadi.

Ndio maana nikashauri, Chadema wautumie muda huu, kujijenga na sio kupoteza muda kulalamika tuu. Wakati nikitoa ushauri huo ilikuwa ni mwaka jana Novemba baada ya uchaguzi, leo tunaelekea May, ni miezi 6 imekata, sijaona Chadema inafanya nini kujiadress kwenye kujijenga, unless inajifariji na umati wa watu kwenye maandamano na mikutano yake ya hadhara.

Nilitegea single mpya ya ufisadi, itakuwa na majina mapya na ufisadi mpya wa Stumulus Package, kumbe ni majina mapya ya ufisadi ule ule wa EPA, kupitia kampuni ya Kagoda wa mwaka 1994!. Hizi nyimbo zitachusa!.
 
Aisee! maneno mazito haya Jenifa. Uliombwa au ni mtu wako wa karibu aliombwa nini,maana una hasira si kidogo. Pole sana mama. Nakuonea huruma kwasababu pengine huna evidence,si unajua mambo haya yanafanyika sirini mama, lakini wenzako wana eviedence za nyumba za serikali zilizouzwa kifisadi under Magufuli's watch. Pole tena
...............
 
Pasco Mkuu,

Umejichanganya sana kwa maneno yako. Kama kweli unaanza kwa kusema kuwa vita ya siasa ni kama vita vingine, basi huko chini umemaliza vibaya sana. Nashindwa kuelewa kama ulipitia JKT na kama ulipitia basi au umesahau au hukupitia mafunzo mazuri ya msituni.

Mrusi VS NATO walikuwa wakishindana kwa kutengeneza silaha. Mrusi akaja na AK-47 na NATO/USA wakaja na Mibunduki yao mikubwaa na risasi za kutisha. Ukipigwa na silaha ya NATO, unakuwa vipandevipande na kufa wakati AK-47 inakupa jelaha kubwa ila kuna uwezekano UKAWA BADO HAI.

Ubaya wa kukufanya uwe bado hai ni kuwa walio wazima itabidi wakubebe. Kama ukifa, wanakuacha na kuendelea mbele. Hivyo basi hakuna mbinu bora vitani kama kutengeneza majeruhi kwa sababu ukiwa na majeruhi wawili, basi askari wanne wanaacha kupigana. Ukiwa na maiti wawili, basi unakuwa na askari wawili zaidi na wenye hasira wakitaka kulipa kisasi kifo cha ndugu zao.

Nafikiri CHADEMA watakuwa wanatengeneza MAJERUHI ndani ya CCM wa kisiasa. CCM itakuwa na maamuzi kadhaa ambayo itabidi iyafanye na nakubaliana kwa upande huo wa shilingi maneno ya Superman:

Code:
CHADEMA wanajua kwa kulitaja hili CCM wana chaguzi 3: 

1. Kufuta mpango wao wa kujivua Gamba na kukaa kimya kama hawajui kitu.

2. Kuwatosa mafisadi wa Phase 1 na Phase 2 kitu ambacho hakiwezekani

3. Kuwasamehe mafisadi wote wa Phase 1 na Phase 2 kama ulivyosema.

Nafikiri kilichowasukuma Chadema kufanya hivi si kuwa CCM walikuwa hawachezi Single yao. Ila tatizo ni kuwa mziki uliokuwa ukipigwa na Chadema ulikuwa Reggae na CCM wakaanza kuucheza kama Vijana wa Atlanta yaani CRANK. Beat hazina tofauti ila kucheza kunatofauti. Chadema watakuwa wameshtukia deal kuwa hawa jamaa wanacheza Staili nyingine kwa wimbo unaotakuwa kuchezwa kwa staili nyingine. Sasa dawa yake ni kuwawekea PURE Reggae ili wasitake tena kubadili uchezaji.

Kitendo cha kufukuza watu watatu ndani ya CCM na kuwaita kuwa ndiyo mafisadi, ni kichekesho na tuuite kwa jina KAFARA. Wakishafanya hivyo, watapiga kelele Tanzania nzima kuwa WAMEJIOSHA tayari sasa mnataka nini? German, yule Mzee Chancellor Helmut Kohl alipokea pesa kutoka kampuni la mafuta la ELF (France) kwa ajili ya chama. Ilipogundulika, alishambuliwa hadi ndani ya chama chake na mmoja ya waliompiga madongo aondoke ni huyu mama Chancellor wa sasa Angela Merkel ambaye walikuwa chama kimoja na ndiyo alimlea ndani ya chama hicho.

Kwenye SIASA nilishasikia maneno haya kuwa "Adui yako ni nyoka, ponda kichwa na tupilia mbali....." Kikwete alifanya hivyo kwa adui zake na wengi wao hadi leo wako HOI kama si Marehemu Ki-Siasa. Sijui Chadema kama pia wanalitumia hilo kuwaponda woote wanaoweza kugombea mwaka 2015 ili kuwamaliza kisiasa mapema kabisa.

Kwa hali ilivyo sasa na Ukorofi wa Lowassa, sidhani kama atataka kuondoka tena na kuwa KAFARA. Sababu ya kutokuondoka kapewa na SLAA. Akigoma kuondoka, Chadema watasema "Magamba ya CCM bado yapo." Kwa sasa ndani ya CCM, wameshapewa mziki mzito sana ambao hadi namhurumia Kikwete.

Huo ufisadi mpya, unasubiri siku yake. Ukiwa unacheza karata, huonyeshi karata zako zote na ukiwa vitani, unatumia kwanza bunduki za kawaida. Mambo yakianza kubadilika, unahamia kwenye bunduki nzito/Kubwa, unakuja mizinga, vifaru, ndege na hadi akina SCUD. Pili kumbuka Slaa hawezi kukurupuka kutumia datas ambazo hana uhakika nazo. Zinaweza kuwa zimepikwa na hata CAG kaingizwa mjini na wewe ukizidandia, unakwenda na maji.

Jibu pekee zuri kwa CCM ni kuondowa watu wengi sana ndani yake jambo ambalo sidhani wako tayari kulifanya. Wakigoma, Chadema ndiyo wanafurahi na kwenda kuwashtaki kwa wananchi. Ngoja tuone/tusubiri kama ambavyo jana Mwenyewe Slaa kaandika kuwa "Mtuachie wenyewe tucheza kama hili jambo hamlifahamu vizuri kwa ndani.........." TIME WILL TELL.

Kamanda Sikonge;

Heshima sana Mkuu.

Nimecheka sana ulivyopangilia arguments zako.

Zimetulia na zinajitosheleza. Bravo!

Respect.
 
Hivi Huyu January Makamba ana usafi kiasi gani ina maana kesi yake ya kuiba mitihani iliishia wapi? CCM ina maana watakatifu wake ndo hao hapo kwenye kamati kuu na Secreterieti yake. Hakika kama hawa ndo gamba jipya basi kumbe CCm ime tuthibitishia haina watu. Nawashauri wasitumie nguvu sana jamani kwani KILA CHENYE UHAI IKIWEPO CCM SHARTI KIONJE MAUTI, hAPA ccm INATAKA KUPINGANA NA NATURE TU WAKATI UKWELI NI KWAMBA tayari imezeeka na mauti yanakaribia . Wanapambana na kurudisha umri nyuma ili wasife . Wafanye wafanyalo hawana uwezo wa kujisafisha wakae tu ICU wasubiri Israel mtoa roho
 
Halafu leo vipi leo? Kikaanza kupotea kitufe cha senksi sasa hivi hata cha like hakipo! What's going on?!
Senksi Sikonge
Senks Superman
Like Sikonge
Like Superman!
Kamanda Sikonge;

Heshima sana Mkuu.

Nimecheka sana ulivyopangilia arguments zako.

Zimetulia na zinajitosheleza. Bravo!

Respect.
 
Ina maana ufisadi mnaopigana nao ni ule wa waliotawala? Vipi kuhusu wakwepa kodi, vipi kuhusu wakopaji fedha za umma bila ya kurudisha? Vipi kuhusu wanaotumia fedha za RUZUKU bila ya uwajibikaji? Vipi kuhusu wanaotoa hongo ili kupata tenda ama vibali vya biashara?

Ule wa watawala ndiyo roots hao wengine ni branches maana watawala ndiyo haswa wanapaswa ku institute rule of law kama wako corrupt ina maana wanauza hata haki ya ulinzi wa raia wa mali na nafsi zao. So we want to uproot the roots and branches will die automatically.
 
Ufisadi wa EPA ni ule ule, kuongeza majina, belive me, hakuiongezea Chadema milage yotyote kwenye political war tactics zaidi ya kuongezea majuruhi. Hata sisi ambao tunaisuport Chadema kwenye every good move they make, tutafikia wakati tuchatoshwa na single ile ile ya maandamano, mikutano ya hadhara na kupinga ufisadi.

Nilitegea single mpya ya ufisadi, itakuwa na majina mapya na ufisadi mpya wa Stumulus Package, kumbe ni majina mapya ya ufisadi ule ule wa EPA, kupitia kampuni ya Kagoda wa mwaka 1994!. Hizi nyimbo zitachusa!.
!.

Umenikumbusha 1995 zile single za Chavda na Dhahabu Uwanja wa Ndege zilivyokuwa kwenye chart, bahati mbaya Mwimbaji aliendelea kuzirudiarudia mno mpaka akaichosha hadhira!!
 
Pasco Mkuu,

Umejichanganya sana kwa maneno yako. Kama kweli unaanza kwa kusema kuwa vita ya siasa ni kama vita vingine, basi huko chini umemaliza vibaya sana. Nashindwa kuelewa kama ulipitia JKT na kama ulipitia basi au umesahau au hukupitia mafunzo mazuri ya msituni.

Mrusi VS NATO walikuwa wakishindana kwa kutengeneza silaha. Mrusi akaja na AK-47 na NATO/USA wakaja na Mibunduki yao mikubwaa na risasi za kutisha. Ukipigwa na silaha ya NATO, unakuwa vipandevipande na kufa wakati AK-47 inakupa jelaha kubwa ila kuna uwezekano UKAWA BADO HAI.

Ubaya wa kukufanya uwe bado hai ni kuwa walio wazima itabidi wakubebe. Kama ukifa, wanakuacha na kuendelea mbele. Hivyo basi hakuna mbinu bora vitani kama kutengeneza majeruhi kwa sababu ukiwa na majeruhi wawili, basi askari wanne wanaacha kupigana. Ukiwa na maiti wawili, basi unakuwa na askari wawili zaidi na wenye hasira wakitaka kulipa kisasi kifo cha ndugu zao.

Nafikiri CHADEMA watakuwa wanatengeneza MAJERUHI ndani ya CCM wa kisiasa. CCM itakuwa na maamuzi kadhaa ambayo itabidi iyafanye na nakubaliana kwa upande huo wa shilingi maneno ya Superman:

Code:
CHADEMA wanajua kwa kulitaja hili CCM wana chaguzi 3: 
 
 1. Kufuta mpango wao wa kujivua Gamba na kukaa kimya kama hawajui kitu.
 
 2. Kuwatosa mafisadi wa Phase 1 na Phase 2 kitu ambacho hakiwezekani
 
 3. Kuwasamehe mafisadi wote wa Phase 1 na Phase 2 kama ulivyosema.

Nafikiri kilichowasukuma Chadema kufanya hivi si kuwa CCM walikuwa hawachezi Single yao. Ila tatizo ni kuwa mziki uliokuwa ukipigwa na Chadema ulikuwa Reggae na CCM wakaanza kuucheza kama Vijana wa Atlanta yaani CRANK. Beat hazina tofauti ila kucheza kunatofauti. Chadema watakuwa wameshtukia deal kuwa hawa jamaa wanacheza Staili nyingine kwa wimbo unaotakuwa kuchezwa kwa staili nyingine. Sasa dawa yake ni kuwawekea PURE Reggae ili wasitake tena kubadili uchezaji.

Kitendo cha kufukuza watu watatu ndani ya CCM na kuwaita kuwa ndiyo mafisadi, ni kichekesho na tuuite kwa jina KAFARA. Wakishafanya hivyo, watapiga kelele Tanzania nzima kuwa WAMEJIOSHA tayari sasa mnataka nini? German, yule Mzee Chancellor Helmut Kohl alipokea pesa kutoka kampuni la mafuta la ELF (France) kwa ajili ya chama. Ilipogundulika, alishambuliwa hadi ndani ya chama chake na mmoja ya waliompiga madongo aondoke ni huyu mama Chancellor wa sasa Angela Merkel ambaye walikuwa chama kimoja na ndiyo alimlea ndani ya chama hicho.

Kwenye SIASA nilishasikia maneno haya kuwa "Adui yako ni nyoka, ponda kichwa na tupilia mbali....." Kikwete alifanya hivyo kwa adui zake na wengi wao hadi leo wako HOI kama si Marehemu Ki-Siasa. Sijui Chadema kama pia wanalitumia hilo kuwaponda woote wanaoweza kugombea mwaka 2015 ili kuwamaliza kisiasa mapema kabisa.

Kwa hali ilivyo sasa na Ukorofi wa Lowassa, sidhani kama atataka kuondoka tena na kuwa KAFARA. Sababu ya kutokuondoka kapewa na SLAA. Akigoma kuondoka, Chadema watasema "Magamba ya CCM bado yapo." Kwa sasa ndani ya CCM, wameshapewa mziki mzito sana ambao hadi namhurumia Kikwete.

Huo ufisadi mpya, unasubiri siku yake. Ukiwa unacheza karata, huonyeshi karata zako zote na ukiwa vitani, unatumia kwanza bunduki za kawaida. Mambo yakianza kubadilika, unahamia kwenye bunduki nzito/Kubwa, unakuja mizinga, vifaru, ndege na hadi akina SCUD. Pili kumbuka Slaa hawezi kukurupuka kutumia datas ambazo hana uhakika nazo. Zinaweza kuwa zimepikwa na hata CAG kaingizwa mjini na wewe ukizidandia, unakwenda na maji.

Jibu pekee zuri kwa CCM ni kuondowa watu wengi sana ndani yake jambo ambalo sidhani wako tayari kulifanya. Wakigoma, Chadema ndiyo wanafurahi na kwenda kuwashtaki kwa wananchi. Ngoja tuone/tusubiri kama ambavyo jana Mwenyewe Slaa kaandika kuwa "Mtuachie wenyewe tucheza kama hili jambo hamlifahamu vizuri kwa ndani.........." TIME WILL TELL.

Hapo umenikumbusha story ya jamaa yangu Mkongo hapa zamani tulipokuwa tunafanya PhD alikuwa yuko bussy na biashara na alikuwa hakai sana Europe ili biashara zake zisi kuse connections; sasa nika muuliza wewe uko kwenye academia na unahangaika na biashara badala ya kukazana na publications ili upande haraka baadaye kuwa professor. Akaniambia inaelekea wewe ni mwafrika mwenye mawazo ya kizungu. Mimi ni mwafrika ninaye ishi kwa mbinu za vita maana Afrika bado tuko vitani na hii PhD ni Scud yangu pale silaha ndogo ndogo za kivita zikishindwa kumwondoa adui umaskini. Maana nipo hapa kutengeneza maisha si maisha kunitengeneza. So PhD hainiletei ugali kwenye sahani na bia kwenye glass kwa urahisi na kwa uhakika ila hizi biashara zangu. Ila ikitokea Africa ikawa kama Europe watu wakawa kwenye order basi ndo na mimi naingia kwenye silaha hii ambayo nai hifadhi kwa sasa yaani kuishi kwa ubongo uliokuwa formated ambayo kwa Africa kwa hali ilivyo shagalabagala utaishia kuning'iniza vyeti sebuleni na watoto hawana viatu mguuni. So I guess CHADEMA wanaielewa hasa siasa ya Tanzania na wanatumia silaha ndogo ndogo kwanza ku confuse the camp!
 
Mkuu Pasco;

Hivyo ni vile ambavyo wewe unaona. Ni chaguo lako kuona ni upande upi wa shillingi unataka kuuona.

Najiuliza maswali mengi una maana gani unaposema "na kuwataja vipenzi vya watu kama kina Magufuli, kutaifanya CCM kuwasamehe hata mafisadi wake kama kina RA, EL na Mzee wa Vijisenti!". Elewa kuwa wakati mbaya wa CCM kuwatosa makada hawa ilikuwa ni kabla ya uchaguzi. Hawakufanya hivyo kwa kuwa chama kingesambaratika. Hawakuweza kufanya hivyo kimikakati na ndiyo maana JK aliwakumbatia na kuwasafisha kipindi hicho. Lakini si sasa, ulazima wao wa kuwepo ndani ya chama si muhimu kama kipindi kile.

Elewa mpaka sasa move ya EL na timu yake ya kutaka kumwondoa JK kuwa mwenyekiti wa CCM ndiyo iliyowacost sana. Pia wasiwasi wa JK atakapomaliza ngwe yake Nchi amwachie nani na historia itamuhukumu vipi. Ieleweke BWM hana raha hadi leo kwa kelele anazopigiwa.

Wakati wewe unaona move ya CHADEMA ya kutaja mafisadi zaidi ni wrong upande mwingine wa shillingi unaonyesha kuwa hii ni strategy nzuri. Kwa kuwataja "wasafi wa CCM" kuwa mafisadi: Magufuli; Malecela; Mang'ula; na vigogo wa kudumu CC na NEC ya CCM: Sumaye; Mkapa na JK ina maana wao pia wafukuzwe uanachama. je watafukuzwa? RA na sophia simba alisema ndani ya CC kuwa hakuna ushahidi lakini CC safari hii haikukubali na ikawatosa, so suala la ushahidi si issue kwa sasa ila issue ni ushahidi wa kimazingira na kisiasa.

CHADEMA wanajua kwa kulitaja hili CCM wana chaguzi 3:

1. Kufuta mpango wao wa kujivua Gamba na kukaa kimya kama hawajui kitu.

2. Kuwatosa mafisadi wa Phase 1 na Phase 2 kitu ambacho hakiwezekani

3. Kuwasamehe mafisadi wote wa Phase 1 na Phase 2 kama ulivyosema.

Katika hali yoyote CHADEMA wanao mtaji wa kisiasa wa kuendelea kuwapaka CCM kuwa si lolote si chochote na ni Wasanii katika vita vya Ufisadi. hapo bado kuna mafisadi wa 'stimulus package' hawajatajwa.

Nadhani move ya CHADEMA kisiasa inalipa na again kama walivyo prove kwa Phase 1 list na kuwalazimisha CCM kuchukua hatua, I believe also this one will work.

Respect.

QED.

Hivi ile thanks mod ameipeleka wapi?? Nimeshindwa kukugongea lakini nakuwekea hapa "Thanks Great Thinker"
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom