Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Status
Not open for further replies.
Sasa asingesema ungejuaje kuwa kuna ufisadi huo?Usahalifu au uwezo mdogo wa kufikiri?Kwani EPA ilianzeje?Hayo magamba ya CCM nayo yalianzaje?

Ni vigumu kwa kichwa cha elimu ya watu wazima kuelewa anachoongea genious kama Dkt Slaa

Udini tu unawasumbua!Mbona ufisadi wa MOU ya mwaka 1992 ya makanisa na serikali mbona hausemi! au kwa kuwa wanapewa wakristo wenzake! Serikali haina dini iweje iwe inawapa wakristo tu na wengine hawapati!
 
Hivi karibuni ccm wamejivua gamba na wametangaza rasmi vita zidi ya mafisadi ndani ya chama chao kitu ambacho kinachonifanya nione mtaji wa rafiki yetu slaa ccm wameuchukua

suala la ccm kutangaza vita zidi ya mafisadi litawafanya wanachama wao wengi ambao walikuwa wamepoteza imani na chama chao kurudi kundini
pia kuwachukua hata wale waliokuwa njiani kuelekea ktk peoples power nao kugeuza njia...
Vilevile kurudisha baadhi ya majimbo yao kama iringa mjini na mengineyo mengi sana
hivo namshauri slaa kubadilisha muelekeo badala ya kuendelea kuongeza idadi ya mafisadi ktk listi yake
hili litampotezea muda na halina tija.......mi nazani kama baba mwenyewe kaamua kusema mtoto wangu mwizi sizani kama wewe jirani utakuwa ni shujaa zaidi kumwambia mtoto wa jirani yako mwizi............nazani kwa ushauri huu wenye akili kama slaa mwenyewe atakuwa amenielewa
 
Kwani wewe mkataa uko upande gani? Kama uko upande wa kupambana na ufisadi, nadhani una haja ya kuleta mbinu badala ya ku personalize vita dhidi ya ufisadi kwa Dr. Slaa
 
AMA KWELI KISA CHA MMBWA SHIBE NA YULE MWENYE NJAA KUCHEZA PAMOJA HULETA GUMZO YA AJABU!!!

Kwa watoto wa mafisadi kama wewe ambao midomo yenu inang'ara siagi aina ya Butter kutwa kucha bila kujua kitu tofauti kati ya jua wala mvua, usiku wala mchana, njaa mwanamalegezo wala umasikini wa kupindukia kooote nchini, aaaahhhh kweli nakuunga mkono kwamba vita dhidi ya UFISADI wala hauna maana tena!!!

Na kwa mtindo huo sisi sote kama taifa tutakusubiri wewe mpaka uje ukatupe ubunifu mwingine na vita gani tukaupiganie.

Karibu sana.
 
.......mi nazani kama baba mwenyewe kaamua kusema mtoto wangu mwizi sizani kama wewe jirani utakuwa ni shujaa zaidi kumwambia mtoto wa jirani yako mwizi....
Hasemi mtoto wa jirani ni mwizi anasema JIRANI NI MWIZI... Ni shujaa kuliko ushujaa wenyewe!...
 
chadema wamefulia

weka magufuli na upande mwingine mbowe. waulize wananchi nani fisadi. jibu kwa asilimia zaidi ya 90 litakuwa mbowe.

kuwataja magufuli na malecela kumemwokoa lowassa kuchukuliwa hatua na ccm.

Kwa kweli Slaa anatia huruma, nilimsikiliza jana alivyokuwa anahaha na Kigwangalla (MB) tu nikasema sasa huyu Mkuu akianza kunishughulikia mimi, nani atamshughulikia Rais wa CCM, nikajiuliza au mimi MB wa CCM ni sawa na mgombea URAIS wa CDM aliyegaragazwa? Kwa kweli Slaa hana jipya yule Mzee, labda ma-think tank wa CDM (kama hata mpo!) mtafute agenda nyingine, na siyo ufisadi, kwa ajili ya kuibeba CDM la sivyo itapotea kabla ya 2015. yaani ameishiwa sera na hoja. Kwa mtindo huu basi kasi ya kuporomoka kwa CDM, na Slaa itakuwa kubwa mno. Slaa - hadi kufikia 2015 atakuwa amepoteza prospects za kuingia Ikulu kwa kiasi kikubwa mno!
 
......
suala la ccm kutangaza vita zidi ya mafisadi litawafanya wanachama wao wengi ambao walikuwa wamepoteza imani na chama chao kurudi kundini
pia kuwachukua hata wale waliokuwa njiani kuelekea ktk peoples power nao kugeuza njia...
Ili ndoto yako itimie na Slaa aache kutaja mafisadi, Mwenyekiti wenu mwenyewe asimame hadharan ajitaje kuwa na yeye ni JIZI namba 1, aliiba kura, aliiba pesa BOT anaendelea kuiba raslimali. Akijitaja tu, Slaa hutamsikia tena. Kamshauri mwenyekiti wako afanye hivyo haraka ili aondokane na hii kero
 
Kwa kweli Slaa anatia huruma, nilimsikiliza jana alivyokuwa anahaha na Kigwangalla (MB) tu nikasema sasa huyu Mkuu akianza kunishughulikia mimi, nani atamshughulikia Rais wa CCM, nikajiuliza au mimi MB wa CCM ni sawa na mgombea URAIS wa CDM aliyegaragazwa? Kwa kweli Slaa hana jipya yule Mzee, labda ma-think tank wa CDM (kama hata mpo!) mtafute agenda nyingine, na siyo ufisadi, kwa ajili ya kuibeba CDM la sivyo itapotea kabla ya 2015. yaani ameishiwa sera na hoja. Kwa mtindo huu basi kasi ya kuporomoka kwa CDM, na Slaa itakuwa kubwa mno. Slaa - hadi kufikia 2015 atakuwa amepoteza prospects za kuingia Ikulu kwa kiasi kikubwa mno!

Ninapata shida kuamini kwamba ni kweli huyu ndiye Dr Hkigwangalla, kama Dr ambaye kweli amesoma anandika hivi mvurugano kimawazo kweli haya ni matokeo ya kubeba majina ya walala hoi. najua ilikuwa ni systemic problem wakati ule kurudia shule lazima upewe jina la mtu aliyehama shule au hayupo.

Ila ukweli ni kwamba ubaya ni ubaya tu. Ni vyema ukajitetea kwani unatakiwa kukumbuka Dr. Slaa anarekodi nzuri ya kutokukurupuka, ndio maana nanyi leo mnawaita kina RA mafisadi baada ya kwata ya miaka minne.

Mh Dr wa CCM ambaye unaweza kuwa hata huo U-DR ni wakifisadi kwani kama jina ulifisadi maana yake na chochote ulichopata kwa jina hilo ni ufisadi. Kama kweli hilo jina halikuwa lako darasa la kwanza mpaka la saba na mwenye jina anadai ulimwibia nafasi huo ni ufisadi wa maisha. ninauhakika kama uliiba jina kote ulipopita ulidesa, ulinunua mitihani au ulitumia ufisadi kuendeleza kuwa juu, na ubunge unaweza kuwa ulinunua kama kawa ya CCM.

Mnatia kinyaa na CV za kuchonga ndio maana mnalindana kwa kuogopa kuumbuana.
Mwisho wa kuwashangilia umefika sasa ni mchele hadharani.
 
Kwa kweli Slaa anatia huruma, nilimsikiliza jana alivyokuwa anahaha na Kigwangalla (MB) tu nikasema sasa huyu Mkuu akianza kunishughulikia mimi, nani atamshughulikia Rais wa CCM, nikajiuliza au mimi MB wa CCM ni sawa na mgombea URAIS wa CDM aliyegaragazwa? Kwa kweli Slaa hana jipya yule Mzee, labda ma-think tank wa CDM (kama hata mpo!) mtafute agenda nyingine, na siyo ufisadi, kwa ajili ya kuibeba CDM la sivyo itapotea kabla ya 2015. yaani ameishiwa sera na hoja. Kwa mtindo huu basi kasi ya kuporomoka kwa CDM, na Slaa itakuwa kubwa mno. Slaa - hadi kufikia 2015 atakuwa amepoteza prospects za kuingia Ikulu kwa kiasi kikubwa mno!

- Sema wewe muhogo! ha! ha! ha! Hivi kuiba mke wa mtu sio ufisadi? Ha! ha! ha! ha! ha!

William @ NYC, USA.
 
- Sema wewe muhogo! ha! ha! ha! Hivi kuiba mke wa mtu sio ufisadi? Ha! ha! ha! ha! ha!

William @ NYC, USA.

Anne Kilango Malecela, mzaliwa wa same kakulia kihurio, mkazi wa mamba bwambo, mhhh, unataka kuleta hadithi za ndoa? mtaziweza

Uchafu huu wa kuchukua wake na kuzaa na wake za watu umo CCM.
Fedha za ufisadi zipo CCM kuna mlolongo mrefu wa ufisadi wa ngono kuliko kwenye taasisi yeyote Tanzania tena wanao ongoza ni wale waliozaa na watoto wa primary, na kubaka vitoto vidogo.

Fisadi ni fisadi tu, Malecela katuibia nchi that will stick na historia itaamua. Najua uchungu wa fedha za kifahari kujulikana ulikuwa wizi tena uliyemwibia ndiye ulikuwa unamtambia unauma sana. Tuombeni msamaha, acheni masihara tunauchungu.
 
Kwa kweli Slaa anatia huruma, nilimsikiliza jana alivyokuwa anahaha na Kigwangalla (MB) tu nikasema sasa huyu Mkuu akianza kunishughulikia mimi, nani atamshughulikia Rais wa CCM, nikajiuliza au mimi MB wa CCM ni sawa na mgombea URAIS wa CDM aliyegaragazwa? Kwa kweli Slaa hana jipya yule Mzee, labda ma-think tank wa CDM (kama hata mpo!) mtafute agenda nyingine, na siyo ufisadi, kwa ajili ya kuibeba CDM la sivyo itapotea kabla ya 2015. yaani ameishiwa sera na hoja. Kwa mtindo huu basi kasi ya kuporomoka kwa CDM, na Slaa itakuwa kubwa mno. Slaa - hadi kufikia 2015 atakuwa amepoteza prospects za kuingia Ikulu kwa kiasi kikubwa mno!

Sasa Mheshimiwa Kigwangala,tutegemee nini kutoka kwako zaidi ya shutuma na kebehi kwa Dkt Slaa na Chadema?Kutarajia umpongeze Slaa au Chadema ni sawa na kutarajia mwana JF mwenzetu aliye-"like" post yako W.J.Malecela awapongeze Chadema kwa kumtaja mzazi wake,John Malecela,kuwa ni miongoni mwa mafisadi.

Kwani Slaa alipoibua ishu za EPA alionekana ana jipya?Hivi sio Slaa huyu huyu aliyetishiwa kupelekwa polisi akathibitishe tuhuma hizo,lakini baadaye ikathibitika kuwa alichosema ni kweli?

Hivi sio Slaa huyu huyu aliyetaja List of Shame pale Mwembeyanga,watajwa wakatishia kumburuza mahakamani (hadi dakika hii hakuna hata mmoja aliyediriki kufanya hivyo),CCM ikatumia kila nguvu na raslimali ilizonazo kukebehi na kupinga tuhuma hizo,lakini hatimaye-na kwa vile njia ya mwongo ni fupi-mmelazimika kulamba matapishi yenu na kukiri kuwa ufisadi upo,na salama yenu ni kuuvua.

Sasa unaleta siasa za kudai oooh Dkt Slaa ameishiwa,ohh hatofika 2015!!Be careful what you wish for.Ripoti zinaeleza kuwa Chadema wameweka kambi kwenye jimbo lako,na mtu anayedai umempora jina lake amekuwa karibu na viongozi wa chama hicho.

Mnaweza kumkebehi kadri mtakavyo,mnaweza kumchukia kadri muwezavyo,lakini deep in your hearts you certainly know kwamba Dkt Slaa sio mwanasiasa wa kuchukuliwa lightly,hususan anapotoa public announcements.

Na kwa upeo wenu finyu mnawekeza nguvu nyingi kwa kuamini Slaa na Chadema ndio tatizo badala ya kuangalia jamii inayowazunguka,watu mnaowaongoza na kisha mngetambua umaarufu na kukubalika kwa Slaa/Chadema kunatoka wapi.

Halafu bado mnatuzuga mmejivua magamba ilhali fikra zenu bado ni zile zile za kifisadi.Mko uchi lakini mnataka umma uamini kuwa mmevaa suti,mnateleza lakini mnataka umma uwaone mmesimama.At the moment kuna mkanganyiko kuhusu the so-called magamba.How come Lowassa,Rostam na Chenge wawe wasafi Oktoba 2010 lakini leo wawe mafisadi?And how come you kept on refuting Chadema's claims that CCM was every fisadi's choice of a refuge,only for you to concede publicly that ufisadi was indeed a problem within the party,and some people were to go!

Walalahoi mnaowapuuza-ambao ni majority-ndio mtaji mkubwa wa Chadema.Hizo public announcements kuhusu mafisadi ni mazungumzo ya kawaida kati ya Chama hicho na wazalendo wenzake (walalahoi),ya kujulishana namna nchi inavyozidi kutafunwa,na nini kifanyike huko mbeleni.

Siku zenu zinahesabika
 
- Sema wewe muhogo! ha! ha! ha! Hivi kuiba mke wa mtu sio ufisadi? Ha! ha! ha! ha! ha!

William @ NYC, USA.

Usirushe mawe ilhali umekaa kwenye nyumba ya vioo.Kama unamfahamu vema Mzee Malecela basi jitahidi kuepuka kuzungumzia ishu za ndoa au infidelity.Nilishakutahadharisha awali kuwa katika jitihada zako za kumtetea baba yako unaweza kuishia kumuumbua zaidi.

Kuna tunaomwelewa Malecela kabla hata ya akina Hawa Ngulume na huyu mpare Anne Kilango (na walivyomfanyizia 2005)!
 
Kwa kweli Slaa anatia huruma, nilimsikiliza jana alivyokuwa anahaha na Kigwangalla (MB) tu nikasema sasa huyu Mkuu akianza kunishughulikia mimi, nani atamshughulikia Rais wa CCM, nikajiuliza au mimi MB wa CCM ni sawa na mgombea URAIS wa CDM aliyegaragazwa? Kwa kweli Slaa hana jipya yule Mzee, labda ma-think tank wa CDM (kama hata mpo!) mtafute agenda nyingine, na siyo ufisadi, kwa ajili ya kuibeba CDM la sivyo itapotea kabla ya 2015. yaani ameishiwa sera na hoja. Kwa mtindo huu basi kasi ya kuporomoka kwa CDM, na Slaa itakuwa kubwa mno. Slaa - hadi kufikia 2015 atakuwa amepoteza prospects za kuingia Ikulu kwa kiasi kikubwa mno!

Una Tabia Za Uongo na Umbeya, so watu kukuamini wewe ni kupoteza Muda.
 
Kwa kweli Slaa anatia huruma, nilimsikiliza jana alivyokuwa anahaha na Kigwangalla (MB) tu nikasema sasa huyu Mkuu akianza kunishughulikia mimi, nani atamshughulikia Rais wa CCM, nikajiuliza au mimi MB wa CCM ni sawa na mgombea URAIS wa CDM aliyegaragazwa? Kwa kweli Slaa hana jipya yule Mzee, labda ma-think tank wa CDM (kama hata mpo!) mtafute agenda nyingine, na siyo ufisadi, kwa ajili ya kuibeba CDM la sivyo itapotea kabla ya 2015. yaani ameishiwa sera na hoja. Kwa mtindo huu basi kasi ya kuporomoka kwa CDM, na Slaa itakuwa kubwa mno. Slaa - hadi kufikia 2015 atakuwa amepoteza prospects za kuingia Ikulu kwa kiasi kikubwa mno!

VIPI MBONA HUPENDI KUWAELEZA WATU NAMNA ULIVYOFUKUZWA KAZI PALE MUHIMBILI KWA KOSA LA KUKODI GAR LENYE SEBENE NA KUWAFURUMISHIA WAGONJWA WAKIWEMO WAMOYO MUZIKI MZITO?????......IKIWEMO PIA KUMZOMEA WAZIRI MKUU PALE DENTAL.....SUMAYE AKAWAFURUMUSHA ....MLIKUWA WATATU ....?????
PAMOJA NA HAYO NATAMBUA USINGEWEZA KUWA DAKTARI MZURI....MUNGU AMBARIKI SUMAYE NA MWAKYUSA KWA KUWAFUKUZA KAZI.....BUT NAKUPONGEZA KWA JUHUDI ZAKO KWENYE BIASHARA....NA NAPENDA KUKUTIA MOYO.........USIJALI FITNA ZA WASWAHILI AMBAO WANAWAACHA WAGENI WANAANZA KUHARIBIA WAZAWA....

SUALA LA JINA ..WEWE UNAUJUWA UKWELI....LAKINI LAZIMA UKUBALI ULIKOSEA..MIMI NIMESOMA NA WATU WENYE TATIZO KAMA LAKO...KUANZIA o LEVEL...LAKINI WENGI WALIKUWA WAJANJA ...WALIFANYA AFFIRDAVIT KUYAKANA MAJINA YA SHULE MARA TU WALIPOINGIA CHUO KIKUUU.....UNGETAKIWA KUELEWA KUWA KWENYE SIASA HII ISSUE NI KUBWA SANA NA ITAKUHARIBIA NDOTO .....PENGINE HATA IMESHAKUKOESHA UWAZIRI KWENYE VETTIN YA JAMAA ZETU....,UNAWEZA KUENDELEA KUWA MBUNGE LAKINI HUTAKAA UPATE PRESIDENTIAL NOMINATION .....ULITAKIWA ULIVYOJUWA TU UNAINGIA KWENYE SIASA ....USAFISHE MAMBO YAKO NA SIMPLY UNGEENDA MAHAKAMANI KURUDIA JINA LAKO.......UKITAKA HATA SASA HUJACHELEWA .......YOU CAN DO IT.......
CHADEMA WALIKUWA HAWAIJUI HII ISHU BALI IMEPEKEKWA MEZANI KWA SLAA NA HASIMU WAKO NDANI YA CHAMA KUPITIA KWA MWANACHAMA WA KAWAIDA WA CHADEMA....NA FOR SURE HE IS SO FAR AHEAD OF YOU KUELEKEA 2015.....ILE KAULI KUWA WEWE NI HOUSE BOY UNAEMUANGALIZIA NYUMBA YAKE ITATIMIA ....I FEEL SO SORRY!!!
 
Tunamushukuru slaa kwa kuwataja mafisadi ccm na serikalini ,lakini lengo lake ni nini??

Mimim nashanga hata ccm nao wanaanza kutaja mafisadi jambo linalo kiondolea sifa ccm kuwa chama tawala!!!

Nadhani lengo hasa la slaa kuwataja mafisadi ni serikali ya kikwete kuwafikisha mahakamani!!!

Tunataka kikwete asiendelee kutaja mafisadi kwa kuwa kazi hiyo imefanywa na slaaa, sasa kazi aliyobaki nayo ni kuwapeleka mahakamani.


Ni wapumbavu wachache ambao watasema kikwete hana sifa ya kuwafukuza akina rostom kwa kuwa nayeye ni fisadi!!

Hata kama kikwete ni fisadi ,bado jukumu la yeye kama rais ni kutenda mema sawasawa na katiba ya nchi!!


Katika serikali ya kikwete bado kuna watu wamepelekwa mahakamani na wengine wamehukumiwa kunyongwa ,sasa hilo watu hawajalalamika.


Kikwete kaamuru wakati wa kura za maoni wakakamtwa akina mwakalebela na mungai katika ufisadi mbona watu hawakulalamika.



Bado serikali ya kikwete inatoa ruzuku kwa vyama vya upinzani pamoja na kwamba kikwete ni fisadi!!!




Upo mtego mkubwa kwa chadema endapo mafisadi watafukuzwa na kuamua kuhamia chadema , je watapokelewa ????




Maana rostam aziz ,lowasa na chenge wakihamia chadema , vita ya ufisadi chadema itakufa.!!!!



Ni bora chadema wakaacha kutumika na siasa za mafisadi za kuhoji uhalali wa kikwete kuwafukuza akina rostam. Ikumbukwe kuwa chadema walihoji uhalali wa kura zilizo mwingiza kikwete madarakani na sasa wameacha hilo wanataka mabadiliko ya katiba jambo ambalo ni jema
 
ww ni mnafiki na umetumwa na ccm cha msingi rudi kwao ukawambie mziki wa chadema au uingiliki
 
Kazi ya upinzani ni kukosoa serikali na kazi ya chama tawala ni kujikosoa!!!


Sasa hivi ccm kupitia kwa nape wamebadili vita ya ufisadi ,wanataka kuwashughulikia mafisadi serikalini !!!


Hii ndiyo faida ya upinzani sasa slaa angenyamaza kimya ccm wangeendelea kutunyonya!!!

Mimi napendekeza vita ihamie kwa wahasibu wa serikali ambao wamekuwa wakiiba fedha na kuandika uongo!!!


Riport ya cag inaonyesha wizi mkubwa unaofanywa na wahasibu wa serikali lakini sheria zinawlinda!!!



Tunataka sheria zibadilishwe ili wahasibu wanao iba wakamatwe mara moja.

Uingereza mwasibu akiiba ananyang'nywa cheti
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom