Tabia za Kitanzania zinazonikera...

Tabia za Kitanzania zinazonikera...

Hahahahaha mie nna zero tolerance na hiyo aisee. Nitamuambia kabisa kama hauna headphones zima hiyo makitu. Yaani aisee!
Nyingine hii, mko kwenye usafiri wa puplic basi anatokea mtu anaweka loud speaker kwenye simu yake, simu yenyewe mchina na music hata haujulikani ni dogoli ama segere.... Wakati huo ndo muwe mnarudi home... mmechoka akili, mwili na damu. Huwa natamani nimwambie azime kha!!!!!
 
Wambea wa JF nao wanakera sana.

Unakuta jitu halikujui lakini kwa kujifanya linakujua ni bingwa. Kila mtu linamwambia 'aah yule Ngabu mi namjua sana yule'

Umenijulia wapi wewe mburula?

Halafu linaeneza umbea wake eti limekutana na wewe sehemu fulani wakati hata jinsi ufananavyo halijui.

Sasa mmekutania wapi kama mtu hata humjui zaidi ya kumsoma tu hapa JF?

Mazafacka hunijui sikujui, acha kujifanya unanijua. Kunijua siyo ujiko.

Au we ulidhani mashori watakushobokea ukijifanya unanijua?

Dah! Pole sana kumbe wahanga ni wengi.
 
Kwani ukiwa mliberali ni lazima kila.mada uhusianishe na hobby yako???

Unachokoza watu halafu muandamane kuwa mnanyimwa haki zenuuu!!!!!!!

Ukweli utabaki kuwa ukweli mwanaume utanukiaje bana? wanawake na mashoga wanapaswa kunukia
 
Afu kuna tabia unakuta mtu anafanya afu hajistukii kabisa. Kuna siku nilikuwa na rafiki yangu kwenye ji-international airport. Kuna que ya maana, nikampa chewing gum. Yaani nilitaka kuzimia alipoifungua na kutupa kikaratasi hapo chini! Niliinama tu kukiokota bila kuongeza neno! Na alivyo mrembo na msomi!

Dah.... pole sana. Vipi aliona aibu au hata kukwambia asante ya uongo na kweli???
 
Tabia ya mtu kujidai anamfahamu flani kisa ni superstaa....

Utakuta mnaongelea jambo flani kuhus mtu huyo, mf. Juma Kaseja. Mtu anadakia yule nimesoma naye primary yule, mara Wema Sepetu mie alikuwa jirani yangu. Mara Ali Choki yule mshikaji wangu nilikuwa naye maskani wakati naishi Dar.

Wengine huwa wana tabia ya kuwaponda. Utasikia Juma Kaseja hana lolote yule, mie kipindi nasoma naye alikuwa mbulula kweli, Mara Wema Sepetu usimuone hapo hajui hata kupika.

Ilhali hajawahi hata kumuona. Anachotaka yeye ni kuwa ujue anafahamiana na mastaa au watu maarufu.
 
Afu kuna tabia unakuta mtu anafanya afu hajistukii kabisa. Kuna siku nilikuwa na rafiki yangu kwenye ji-international airport. Kuna que ya maana, nikampa chewing gum. Yaani nilitaka kuzimia alipoifungua na kutupa kikaratasi hapo chini! Niliinama tu kukiokota bila kuongeza neno! Na alivyo mrembo na msomi!


hapa najikutaga nazunguka na uchafu muda mrefu mjini kutafuta pa kuutupa , lol
 
Je mnaekaa siti moja kwenye daladala kisha anakuzungushia mkono kwenye siti uliyoegemea?
Au anasinzia halafu anakuegemea? Natamani nimtie konzi


halafu ukute kikwapa kinatema ,,,,,, huwa nawatolea uvivu , ikishindikana namkula bega la meno.
 
Acha hizo kuna hii pia.
Unasafiri na mtu kwenye basi la kwenda mkoa hadi mkoa (dar to mbeya, mfano) mara kaagiza machungwa, mara ndizi, mara mahindi ya kuchemshwa, mara karanga mbichi, mua,na anamalizia na mayai ya kuchemsha. baada ya muda watu hawakai hapo! full tantalizing smell!


hii tabia ni maarufu sana kwa wale ndugu zetu waishio maeneo ya simiyu , shinyanga na mwanza...... usiombe ukae naye siti moja hasa yule primitive kutoka interior unaweza tembeza kichapo.
 
Misipendi tabia ya kunong'onezana hasa kipindi hiki cha mfungo
 
hii tabia ni maarufu sana kwa wale ndugu zetu waishio maeneo ya simiyu , shinyanga na mwanza...... usiombe ukae naye siti moja hasa yule primitive kutoka interior unaweza tembeza kichapo.

Umesahau wasafiri wa Dodoma - Iringa kupitia mtera........yaani hadi nyama mbichi na kuku wanatundikwa kwenye carrier na ukiuliza gari zima wanakutukana.
 
Back
Top Bottom